STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 8, 2014

Thomas Muller aibeba Ujerumani Euro

Easy does it: Thomas Muller remained composed in the area to side-foot the ball into the roof net to put Germany back in front with twenty minutes remainingMSHAMBULIAJI nyota wa Ujerumani,  Thomas Muller aliendeleza rekodi yake ya mabao wakati alipoisaidia nchi yake kupaa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Scotland katika mechi ya kwanza ya kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Ulaya mwaka 2016 (Euro 2016).
Muller alifunga bao la kwanza katika dakika ya 18 ya mchezo, kabla ya  Ikechi Anya akaisawazishia Scotland katika dakika ya 66.
Baada ya matokeo kuwa 1-1, Ujerumani ambao ni mabingwa wa kombe la dunia chini ya kocha Joachim Low walifanya mashambulizi kadhaa langoni kwa Wascotish na katika dakika ya 70, Muller aliandika bao la pili na la ushindi.
Mabao hayo yamemfanya Muller kufikisha jumla ya  25 katika mechi 58 alizoichezea timu ya Taifa ya Ujerumani.
Katika mchezo huo Scotland walipata pigo katika dakika za majeruhi baada ya Charlie Mulgrew kutolewa nje kwa kadi nyekundu.

No comments:

Post a Comment