STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 8, 2014

Sepp Blatter athibitisha kutetea kiti FIFA

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani,FIFA Sepp Blatter amethibitisha kuwa atakitetea kiti chake katika uchaguzi ujao wa shirikisho hilo. 
Akihojiwa jijini Manchester, Blatter 78 alithibitisha uamuzi wake japo alidai atatoa taarifa rasmi katika mkutano mkuu wa kamati ya utendaji ya FIFA utakaofanyika Septemba 25 na 26. 
Tayari rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA Michel Platini ameshatangaza kutogombea nafasi hiyo ya Blatter. 
Blatter ambaye amekuwa katika kiti hicho cha FIFA tangu mwaka 1998 amesema amechukua uamuzi huo kwa vile kazi alioianza anaona bado haijamalizika. 

No comments:

Post a Comment