STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 8, 2014

Waliokufa ajali ya Airbus ni wanne tu


AJALI mbaya iliyotokea mjini Gairo ikihusisha basi la Airbus lililokuwa likitokea Dar kuelekea Tabora imedaiwa kusababisha vifo vya watu wanne tu na wengine kadhaa kujeruhiwa tofauti na taarifa za awali toka kwa waliokuwa kwenye tukio hilo kuwa zaidi ya watu 10 walikuwa wamekata roho.
Ajali hiyo ambayo imekuja siku chache baada ya roho za watu 39 kupotea kwenye ajali ilitokea mkoani Mara ikihusisha magari matatu, ilielezwa ilitokea majira ya asubuhi baada ya basi la Airbus kupinduka mara kadhaa na kuharibika huku baadhi ya abiria wakijeruhiwa vibaya na kutupwa nje na kuleta hofu kubwa.
Hata hivyo jeshi la Polisi la Morogoro limethibitisha waliokufa ni abiria wanne tu na siyo zaidi ya idadi hiyo na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali mbalimbali mjini Dodoma na Morogoro.

No comments:

Post a Comment