STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 4, 2014

Taifa Stars kuingia kambini keshokutwa kuwasubiri Benin Taifa

Kocha Mart Nooij akizungtumza huku Nahodha Nadir Haroub Cannavaro akisikiliza kwa makini
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/1728070/highRes/480649/-/maxw/600/-/eoklao/-/stars.jpgKIKOSI cha wachezaji 26 walioitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa (Taifa Stars) kwa ajili mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) dhidi ya Benin itakayochezwa Oktoba 12 mwaka huu jijini Dar es Salaam wataingia kambini keshokutwa Jumatatu.

Kocha Mart Nooij aliyetangaza kikosi akiwa mjini Cairo, Misri kwenye kongamano la makocha la Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), alisema kikosi hicho kinachodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kitaingia kambini Jumatatu.
Wachezaji watakaoingia kambini keshokutwa ambao waliitwa kwenye kikosi hicho ni pamoja na;
Makipa: Deogratias Munishi (Yanga), Aishi Manula (Azam), na Mwadini Ali (Azam).
Mabeki:Said Moradi (Azam), Shomari Kapombe (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Aggrey Morris (Azam), Miraji Adam (Simba), Charles Edward (Yanga) na Emmanuel Simwanda (African Lyon).
Viungo: Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji: Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DR Congo), Mbwana Samata (TP Mazembe, DR Congo), Mrisho Ngasa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City), na Juma Liuzio (Zesco, Zambia).

No comments:

Post a Comment