STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 9, 2014

Arsene Wenger apata mtetezi Arsenal

http://i3.mirror.co.uk/incoming/article4568785.ece/alternates/s615/Arsenal-v-Anderlecht.jpg
NYOTA wa zamani wa Uingereza, Gary Lineker amewaponda mashabiki wa Arsenal ambao wanamzomea meneja wa timu hiyo Arsene Wenger.
Kuna picha za video zilizotoka zikionyesha Wenger mwenye umri wa miaka 65 akizomewa na mashabiki wakati akipanga treni kufuatia Arsenal kuchapwa mabao 3-2 na Stoke City Jumamosi iliyopita.
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuwa Mfrungaji Bora wa Kombe la Dunia, ambaye kwasasa ni mtangazaji wa michezo wa BBC aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii akiwaponda mashabiki hao kwa kukosa heshima pamoja na matokeo hayo baada ya kuona picha hizo za video.
Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Britania Arsenal walikuta wakiwa nyuma kwa mabao 3-0 mpaka kufikia muda wa mapumziko.
Kocha huyo pia alijikuta katika wakati mgumu mbele ya mashabiki wa Arsenal kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya West Bromwich Albion.

No comments:

Post a Comment