STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 9, 2014

Robin van Persie aipeleka Man Utd katika 3 Bora

Kitu! Van Persie akifunga bao la pili kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu ndogo
Vijana wa Van Gaal wakishangilia bao lao
Kuna maswali tena jamaniiiii!
Van Persie akifunga bao la kwanza
MSHAMBULIAJI wa Kiholanzi, Robin van Persie usiku wa jana aliiwezesha klabu yake ya Manchester United kukwea hadi nafasi ya tatu baada ya kuisambatarisha Southampton nyumbani kwao kwa kuwafunga mabao 2-1 katika Ligi Kuu ya England.
Van Persie aliandika mabao hayo katika dakika ya 12 na 71 na kuifanya Mashetani Wekundu hao kufikisha pointi 28 na kuziengua timu za Southampton na West Ham United na kuzipa presha Manchester City na Chelsea waliopo kileleni kwa sasa.
Bao la wenyeji liliwekwa kimiani na Pelle dakika ya 31 ambalo lilikuwa la kusawazisha kabla ya 'Vijana Watakatifu' kutepeta kipindi cha pili kwa bao la pili la van Persie.


No comments:

Post a Comment