STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 9, 2014

Stars Maboresho yanyolewa 2-1 Taifa


Furaha ya kupata bao la kuongoza
hekaheka katika lango la Burundi
Kosakosa langoni mwa vijana wa Intamba Murugamba
Burundi wakiwakimbiza Stars Maboresho
Stars wakiokoa hatari langoni mwao
KIKOSI cha timu ya Taifa Stars Maboresho kimeendeleza unyonge wa Tanzania mbele ya Burundi baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 katika pambano la kirafiki na kimataifa lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa kama sehemu ya kusherehekea siku ya Uhuru wa Tanganyika.Stars Maboresho walianza kuandika bao dakika ya 11 kupitia Yusuf Rashid kabla ya Burundi kucharuka na kurejesha bao hilo dakika ya 25 kupitia Fabrice Mimimahanzwe na kwenda mapumziko wakiwa 1-1 na kipindi cha pili kuruhusu wageni kupata bao la ushindi lililovuruga 'pilau' la Uhuru.
Bao hilo liliwekwa kimiani na Nassor Niyonkulu aliyemalizia krosi pasi ya kutoka kushoto mwa uwanja na kupiga mpira uliosindikizwa wavuni na kipa Aishi Manula.

No comments:

Post a Comment