STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 9, 2014

Taifa Stars, Intamba Murugamba leo Taifa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhifuz9t7Y3fbFlEsJWzFqquZ1aaF6_DUgm80KzOToI2ybRZAe6rXvGp40l3lPx2b6wFjAX8t80WU09bbJP6u_98sEzq8jTp0ELUwy7n6DJO5jf-PqyqOqBZcfDI5qQsfTv9QtOYBznCZc/s1600/Staz.jpg
Kikosi hiki cha Taifa Stars Maboresho kilinyukwa mabao 3-0 na Burundi katika sherehe kama hizi za Uhuru mwaka jana
KIKOSI  cha Taifa Stars Maboresho kimerejea Dar es Salaam kutoka Bulyanhulu mkoani Shinyanga ambapo kiliweka kambi kwa ajili ya mechi ya kimataifa dhidi ya Burundi itakayochezwa leo. Timu hiyo ambayo jana asubuhi ilifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ilitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) juzi kwa ndege ya Fastjet saa 12.30 jioni na kwenda moja kwa moja kambini hoteli ya Tansoma. Nayo timu ya Taifa ya Burundi ilitua nchini jana saa 10 jioni kwa ndege ya RwandAir. Kikosi hicho kitafikia hoteli ya Tiffany Diamond kitakwenda moja kwa moja Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo kitafanya mazoezi kuanzia saa 11 jioni. Kiingilio cha mechi kati ya Tanzania na Burundi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni kitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya raungi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C ni sh. 5,000 tu.
Katika mechi mbili zilizopita baina ya timu hiyo kwenye michezo ya kirafiki ya kimataifa Stars imeshindwa kufurukuta baada ya awali kupigwa 3-0 uwanja wa Taifa kwenye sherehe kama hizi za Uhuru kupitia Maboresho na kisha 2-0 Stars yenyewe mjini BUnjumbura, Burundi.
Je, Stars Maboresho imeimarika kuweza kulipa kisasi kwa Intamba Murugamba? Tusubiri!

No comments:

Post a Comment