STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 9, 2014

Msafara wa viongozi CHADEMA watekwa nyara

http://www.gumzolajiji.com/wp-content/uploads/2014/09/SAM_7117.jpg
Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kahama, Juma Protas
MSAFARA wa viongozi na wanachama wa chama Demokrasia na Maendeleo Chadema wa Kanda ya ziwa Magharibi wametekwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wakitoka kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za serikali za Mitaa kata ya Bulyanhulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari,  Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kahama, Juma Protas alisema tukio hilo lilitokea  juzi katikati ya Kijiji cha  Kalagwe kata ya Ntobo na Kijiji cha Nyambula  Kata ya Ngongwa majira ya Saa 3:30 Usiku wakati wakitoka kwenye Kampeni  Kijiji cha Kakola.
Akizungumzia tukio hilo Protas alisema walipofika eneo la Daraja walikuta magari matatu  yamesimama pembeni ambayo ni Basi la Jordan ambalo lilikuwa linatoka mkoani Geita kuelekea Kahama,Roli aina ya Fuso na Gari ndogo inayomilikiwa na Kampuni ya TBL kupitia bia ya Balimi ambayo nayo yalikuwa yametekwa.
Alisema wakati wanajaribu kuyapita magari hayo ghafla waliona Mawe na Miti ambayo ilikuwa imetandazwa barabarani  na ndipo majambazi hao waliamuru Msafara huo ambao ulikuwa na magari mawili wenye watu 10 wasimame na watoe simu na fedha walizokuwa nazo.
“Tulisikia sauti  wakisema zimeni  taa za gari na muziki na hatuwezi kuwadhuru nyinyi Makamanda ila tunataka fedha na simu, na tupo kazini mnatakiwa kuwalaumu viongozi waliokula Pesa za Escrow  bila hiyo tusingefanya haya mnayoyaona”alifafanua Protas.
Aliwataja waliokuwemo kwenye msafara huo kuwa ni mratibu wa Kanda ya ziwa mashariki Renatus  Mzemo, Mwenyekiti wa Kamati ya Rasilimali Kanda ya ziwa Magharibi, Emmanuel Mbise na Mwenyekiti wa Kamati ya Uenezi wa chama hicho Kanda hiyo Juma Protas ambaye ndiye Mwenyeki wa Chadema.
Viongozi hao  wa Chadema walikuwa wamepanda gari aina ya Toyota  Prado yenye no. T 707  BBP ambayo hata hivyo ilivunjwa baadhi ya vioo.
“Tuliibiwa fedha  tathimini zaidi ya shilingi laki tisa pamoja na simu 11 ambazo hazikufahamika mara moja thamani yake na gari yetu moja ambayo ni ya mdau alyejitolea kutusaidia ilivunjwa vioo na ile ya M4C yenyewe walisema hawawezi kuivunja maana ni wananchi walichanga kuinunua”,aliongeza Protas
“Kulikuwa na magari mengi tuliyoyakuta yametekwa na abiria walinyang’anywa simu na fedha zao, pia kulikuwa na Mwalimu mmoja wa Shule ya Msingi Lunguya ambaye alitekwa akiwa na pikipiki na wakamfunga  Kwenye mti pamoja na ddugu yake  na baada ya kuchukua fedha walitoweka kusikujulikana”,AliongozeaMwenyekiti huyo.
Hata hivyo Jeshi la Polisi wilayani Kahama lilifika eneo hilo   baada ya kupewa taarifa na abiria waliokuwa kwenye basi ambalo lilitekwa  na kukuta majambazi hayo yakiwa yametokomea kusikojulikana  na kutoa msaada wa kiusalama kwa magari  yote na abiria waliotekwa.
MALUNDE

No comments:

Post a Comment