STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

RT kuamua hatma yao Desemba 6

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgF-lOhMYrCVlKenUdlFeY7QpbkcfwIJuaSC7FRgOrlXV1EJeCdVq0X8PHDRiN_zLwblmyeveKZjHa8mlDA2bS2ynAPJPiO9n0eTW0O5zXJ3aS4QS-pNbzMwCxd3_BYkbSpnr_Oyf4Eadk/s1600/IMG_9856.JPG
Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui
SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT) linatarajiwa kufanya kikao cha Kamati ya Utendaji ambacho kitapitia na kujadili maoni ya mikoa wanachama wao kwa ajili ya Rasimu ya Katiba Mpya ya shirikisho hilo.
Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui aliiambia MICHARAZO kuwa, awali kikao hicho kilikuwa kifanyike juzi Jumapili ila kilisogezwa mbele kwa sababu ya kutoa fursa kwa mikoa kuwasilisha maoni yao.
Nyambui alisema ni mikoa saba tu ambayo ilikuwa imewasilisha maoni yao tofauti na idadi ya mikoa wanachama wa shirikisho hilo ambayo ni 25.
"Kikao cha Kamati ya Utendaji cha RT kilichokuwa kifanyika Novemba 30 kimesogezwa mbele hadi Desemba 6 na ajenda zake zitakuwa ni kupitia na kujadili maoni ya mikoa juu ya Rasimu ya Katiba Mpya," alisema Nyambui.
Nyambui alisema ajenda nyingine ni kujadili maendeleo ya jumla ya mchezo huo na namna ya kuukwamua ili kuweza kufanya vema kwenye mashindano ya kimataifa yaliyopo mbele yao. Mikoa iliyowasilisha maoni yao mpaka sasa ni Dar es Salaam, Arusha, Mara, Mbeya, Majeshi, Tanga na Morogoro.

No comments:

Post a Comment