STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

Yacine Brahimi ndiye Mwanasoka Bora wa Afrika wa BBC 2014

 
http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Yacine+Brahimi+Algeria+v+Armenia+International+DPgMxDsahSgl.jpgNYOTA wa Algeria anayeichezea Porto ya Ureno, Yacine Brahimi ndiye mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika 2014.
Brahimi alitangazwa kushinda tuzo hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Yaya Toure wa Manchester City jana.
Tuzo hizo uandaliwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza,BBC na Brahimi, 24, anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka Algeria kushinda tuzo hiyo ambayo hupigiwa kura na mashabiki kutoka pande mbalimbali za bara la Afrika. 
Akihojiwa mara baada ya kukabidhiwa tuzo yake Brahimi amesema ni heshima kubwa kwake kushinda tuzo hiyo muhimu na anawashukuru watu wote nchini kwake na popote pale ambao walimpigia kura. 
Brahimi alikuwa akichuana na Yaya Toure na Gervinho kutoka Ivory Coast, Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Gabon na Vincent Enyeama kutoka Nigeria.

No comments:

Post a Comment