STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

Ommy Lax achekelea video yake kupokewa vema

MSANII anayekuja kwa kasi nchini, Iman Omari 'Ommy Lax' amesema amefurahi namna mashabiki wa muziki walivyoipokea video yake mpya ya wimbo uitwao 'Mimi na Wewe' ambao inaendelea kutamba kwa sasa katika vituo mbalimbali vya runinga.
Ommy anasema jambo hilo limemtia nguvu na kujipanga kuandaa kazi nyingine mpya ili kuzidi kuwapa burudani mashabiki wake, sambamba na kulitangaza jina lake.
Video hiyo mpya ya Ommy Lax imetengenezwa na Zolla D, na 'audio' yake imetengenezwa katika studio za Bokaz Entertainment chini ya Man DVD.
Kabla ya video hiyo msanii huyo aliyejitumbukiza kwenye sanaa hiyo mwaka 2006 alitamba na video za nyimbo za 'Kioo Changu' alioimba na Matonya na 'Wapotezee' aliyomshikisha PNC.

No comments:

Post a Comment