STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

Kocha Manchester Utd akerwa ratiba kuelekea X-mass Mwaka Mpya

http://www.nerdoholic.com/wp-content/uploads/2014/07/Van-Gaalmoyes1.jpg
Kocha Luis Van Gaal
RATIBA ya Ligi Kuu na michuano mingine nchini England kuelekea Sikukuu ya Krismasi inaonyesha kumkera Kocha wa Manchester United, Louis Van Gaal.
KOcha huyo ameonyesha kutofurahishwa na ratiba ya Ligi Kuu itakavyokuwa katika kipindi cha sikukuu hiyo na ile ya Mwaka mpya.
Kuna uwezekano mkubwa United ikacheza mechi nne ndani ya siku tisa katika kipindi cha kati ya Desemba 29 mpaka Januari 3 kutegemeana na ratiba ya Kombe la FA itakavyokuwa. 
Ratiba katika Ligi Kuu inaonyesha kuwa watakuwa wenyeji wa Newcastle United Desemba 26, kabla ya kucheza wa ugenini dhidi ya tottenham Hotspurs siku mbili baadae na siku ya mwaka mpya watapepetana na Stoke City. 
Akihojiwa Van Gaal amesema ana mke, watoto na wajukuu na hawezi kuwaona katika kipindi cha krismasi lakini alitaka kufanya kazi katika Ligi Kuu hivyo anapaswa kuzoea hali iliyopo. 
Van Gaal amesema hafurahishwi na suala hilo lakini hawezi kubadilisha na hadhani kama ni jambo zuri kwa wachezaji pia.

No comments:

Post a Comment