STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

Ajali Mlima Kitonga, basi latumbukia mtaroni na kuziba njia

 
Basi liitwalo Easy Bus lenye namba za usajili T 298 BLZ lililokuwa likitokea Lilongwe Malawi likiwa katika mtaro wa Mlima Kitonga.
 
 
Foleni kubwa iliyosababishwa na basi hilo baada ya kuingia mtaroni na kuziba njia.
BASI la abiria la Easy Bus lenye namba za usajili T 298 BLZ  linalofanya safari zake kati ya Malawi na Tanzania limepata ajali katika Mlima Kitonga, mapema leo baada ya kutumbukia kwenye mtaro.
Hata hivyo jambo la kushukuru Mungu ni kwamba hakuna mtu aliyepoteza maisha yake, japo ajali hiyo imesababisha foleni kubwa katika barabara hilo inayosifika kwa kona zake katika mlima huo.
Kwa mujibu wa mashuhuda, chanzo cha gari hilo kutumbukia mtaroni ni kufuatia kupata hitilafu na hatimaye uamuzi wa kuliegesha kando ukafanyika kisha abiria wote wakashuka ili kusubiri marekebisho hayo. 
Haikupita muda mrefu baada ya abiria kushuka gari lilikosa balansi, likaanza kurudi kinyumenyume na kisha kuingia mtaroni. 

No comments:

Post a Comment