STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

Ronaldo, Messi, Neuer wapambanishwa Ballon d'Or 2014

 
SHIRIKISHO la Soka Duniani, FIFA limetangaza orodha ya wachezaji watatu watakaogombea tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Dunia, Ballon d’Or. Wachezaji hao waliopenya katika mchujo wa wachezaji 23 ni mtetezi wa tuzo hiyo nyota wa Ureno na klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo, Lionel Messi wa Argentina na klabu ya Barcelona na Manuel Neuer wa Ujerumani na timu ya Bayern Munich. Sherehe za utoaji tuzo inatarajiwa kufanyika Januari 12 mwakani huku Ronaldo akiwa ndio mshindi wa mwaka jana. Kwa upande wa wanawake walioteuliwa kugombea tuzo hiyo ni pamoja na Nadine Kessler wa Ujerumani, Marta wa Brazil na Abby Wambach kutoka Marekani. Kwa upande wa makocha walioteuliwa kugombea tuzo ni pamoja na Carlo Ancelotti wa Real Madrid, Joachim Loew aliyeiwezesha Ujerumani kunyakuwa Kombe la Dunia na kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone.

No comments:

Post a Comment