STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

Yaya Toure aongoza orodha ya mwisho Mwanasoka Bora Afrika 2014

http://www.football-marketing.com/wp-content/uploads/2012/01/PUMA-Yaya-Toure.jpg
KIUNGO nyota wa Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast, Yaya Toure ameongoza orodha ya wachezaji watano walioingia Fainali za kuwania Tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika 2014.
Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limetoa orodha ya mwisho ya wachezaji hao watano wanaowania tuzo hiyo ambayo awali ilikuwa na wachezaji 25.
Mtetezi wa tuzo hiyo anayetarajiwa kutwaa kwa marta ya nne anachuana na Wanigeria wawili, Mghana mmoja na Mgabon.
Orodha hiyo inaonyesha kuwa Toure anachuana na  Vincent Enyeama na Ahmed Musa wote wa Nigeria, Mghana Asamoah Gyan na Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon.
Toure alitwaa tuzo hiyo miaka mitatu iliyopita na kama akifanikiwa kuitwaa tena msimu huu, atakuwa amefikia rekodi ya Mcameroon Samuel Eto, ambaye ameitwaa mara nne.
Mshindi atatangazwa jijini Lagos, Nigeria Alhamis Januari 8, 2015

No comments:

Post a Comment