STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 1, 2013

Bandari yaonja kipigo, Gor Mahia, Sofapaka ziking'ara KPL

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Kenya, Tusker




BAADA ya ushindi mfululizo, vijana wa Bandari Kenya mwishoni mwa wiki waliisherehekea vibaya sikukuu ya Pasaka baada ya kunyukwa na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Kenya (KPL)  Tusker kwa mabao 2-1, huku Gor Mahia na Sofapaka zikipata ushindi katika mechi zao zilizochezwa jana.
Kipigo ilichopewa Bandari inayochezwa na watanzania wanne waliowahi kutamba na klabu za Simba na Yanga imeipomosha timu hiyo kwa nafasi moja nyuma toka ya tano hadi sita ikizimwa na kasi yake ya kutoa vipigo kwa wapinzani wake baada ya kushinda mara mbili mfululizo na hivyo kusaliwa na pointi zake nane.
Bandari waliokuwa ugenini ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao kwea kuwashtua vijana wa Tom Olaba kocha aliyewahi kuinoa Mtibwa Sugar kwa bao lililofungwa na Eric Okoth kabla ya Jesse Were na Mganda, Andrew Ssekyayomba kuzima matumaini ya Bandari kupata ushindi wa tatu mfululizo.
AFC Leopard wakiwa ugenini walikiona cha mtema kuni siku ya Jumamosi baada ya kunyukwa mabao 2-1 na Muhoroni Youth, huku vijana wa KCB jana walirejea kileleni mwa msimamo baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya mabingwa wa 2010 Ulinzi Stars na kuwaengua Thika United waliokuwa wamekalia kiti hicho kwa saaa 24 baada ya Jumamosi kuicharaza Chemelil 2-1.
Mabao ya vijana hao watunza fedha wa benki ya biashara ya nchini, yaliwekwa kimiani na Jacob Keli na Edward Mwaura na kuifanya timu yao irejee kileleni kwa kujikusanyia pointi 14, mbili zaidi ya Thika.
Nao mabingwa wa zamani wa Kombe la Shirikisho Afrika, Gor Mahia jana ilizinduka katika ligi hiyo kwa kuidonyoa Mathare United kwa bao 1-0 baada ya wiki iliyopita kuzimwa na Ulinzi kwa kulazwa mabao 2-0.
Ushindi huo umeifanya Gor Mahia inayochezwa na kipa wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ivo Mapunda kukwea hadi nafasi ya 10 ikiwa mbele ya mabingwa watetezi Tusker waliopata ushindi wake wa kwanza katika mechi tatu ilizocheza msimu huu.
Mabingwa wa zamani wa Kenya, Sofapaka nao jana walitoa kipigo kitakatifu kwa Karuturi Sports kwa kuikong'ota mabao 4-2 katika mfululizo wa mechi za ligi hiyo ya Kenya.
Matokeo kamili ya mechi za ligi hiyo ya jirani zilizochezwa mwishoni mwa wiki ni kama ifuatavyo;

Nairobi City Stars v Sony Sugar (2-1)
Thika United v Chemelil (2-1)
Western Stima v Home Boys (1-0)
Muhoroni Youth v Leopards (2-1)
 Tusker  v Bandari (2-1)
KCB v Ulinzi Stars (2-0)





Sofapaka v Kurituri Sports (4-2)






Gor Mahia v Mathare United (1-0)







































Sikinde yachekelea ujio wa Mbinga

Adolph Mbinga (kulia) akicharaza gitaa kando ya Hassan Rehani BItchuka
UONGOZI wa bendi ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde' umesema kutua kwa  Adolph Mbinga kumeiongezea nguvu bendi yao ambayo leo inamalizia shamrashamra  za Sikukuu ya Pasaka eneo la Mivinjeni, Dar es Salaam.
Mbinga, nyota wa zamani wa bendi kadhaa ikiwamo African Stars, Mchinga Sound na  Levent Musica, ametua Sikinde wakati bendi hiyo ikimpoteza muimbaji wao nyota,  Athuman Kambi aliyekimbilia Msondo Ngoma.
Katibu Mkuu wa Mlimani, Hamis Mirambo alisema wanaamini kwa uzoefu alionao  Mbinga utaisaidia Sikinde kuzidi kusimama imara na kuwakimbiza wapinzani wao katika  muziki wa dansi.
Mirambo alisema uzuri wa Mbinga mbali na kucharaza magita, pia ni mtunzi na  muimbaji kitu ambacho kitaisaidia Sikinde baada ya kuondokewa na wanamuziki wake  kadhaa wakiwamo waliofariki au kutimkia kwa mahasimu wao Msondo Ngoma.
Mirambo alisema bendi hiyo baada ya kumtambulisha Mbinga mwishoni mwa wiki, leo  watamalizia zoezi hilo katika siku ya Jumatatu ya Pasaka eneo la Mivinjeni, Kurasini.
"Tutamalizia kumtambulisha Mbinga na nyimbo zetu mpya," alisema  Mirambo.

---------

Bessa alia wasanii kunyonywa jasho lao


Salim Mbwana 'Bessa' a.k.a Madhira
MCHEKESHAJI Salim Mbwana 'Bessa' amedai kuwa sanaa ya maigizo nchini bado haijanufaisha wadau wake kulingana na ukubwa wa kazi wanayofanya kutokana na kuwapo kwa unyonyaji na wizi unaofanywa na watu wachache waliohodhi soko la fani hiyo.
Bessa ambaye ni mlemavu wa miguu, alisema kwa namna wadau wa sanaa hiyo wanavyochapa kazi, ni wazi kwamba wangekuwa mbali sana kiuchumi akitolea mifano wasanii wa Nigeria.
"Bado sanaa haijaleta mafanikio kama jasho linalovuja kwa wasanii, kuna haja ya  kuongezwa juhudi za kunusuru fani hii ili wadau wanufaike kama wasanii wenzao wa  kimataifa," alisema Bessa anayejiita 'Madhira'.
Alisema hata yeye mwenyewe pamoja na kujivunia umaarufu mkubwa alionao, tangu aanze kuuza sura kwenye filamu na vichekesho mbalimbali, bado hawezi  kutembea kifua mbele kujisifia mafanikio kwani yupo 'choka mbaya'.
"Sanaa haijaninufaisha ipasavyo, sina cha kujivunia kwa vile kuna hali ya ubabaishaji mkubwa kwa wasanii nchini kunyonywa na kuibiwa jasho lao," alisema Bessa.
Mkali huyo aliyewahi kutamba na utunzi wa riwaya katika gazeti hili, kwa sasa ndiye  mtunzi mkuu katika kampuni iliyompa ajira ya kudumu ya ASl Riyamy.

Irene Paul Hofu filamu ya Kanumba

Irene Paul aliyecheza kama mhusika mkuu katika filamu ya Love & Power

MUIGIZAJI kinara wa filamu ya mwisho ya nyota wa zamani wa fani hiyo nchini, Steven Kanumba iitwayo "Love and Power', Irene Paul amedai anahofia kufufua upya majonzi ya kifo cha Kanumba kilichotokea Aprili mwaka jana.
Irene alinukuliwa wiki hii akisema kutoka kwa filamu hiyo kutaamsha majonzi yake na ya mashabiki wakubwa wa marehemu Kanumba anayetimiza mwaka mmoja  tangu afikwe na mauti ghafla nyumbani kwake Sinza Vatican.
"Kwa kweli sitamani hata kuiona filamu hiyo, naamini itafufua upya majonzi ya  kumpoteza Kanumba ambaye kwangu ni mmoja wa wasanii wakubwa zaidi kuwahi kutokea nchini," alisema  Irene.
Filamu hiyo inatarajiwa kuachiwa rasmi Aprili 12 ikiwahusisha washiriki watatu ambao wametangulia mbele ya haki bila wenyewe kuishuhudia kazi hiyo.
Wasanii hao waliofariki ni Husseni Mkiety 'Sharo Milionea' na John Stephano Maganga waliofariki kwa nyakati tofauti mwishoni mwa mwaka jana.
Kwa mujibu wa taarifa za wasambazaji wa filamu hiyo, inatarajiwa kuzinduliwa rasmi  siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kanumba Aprili 6 kabla ya kuingizwa sokoni wiki  inayofuata.
Inaelezwa kuwa simulizi la filamu hiyo linashabihiana na tukio halisi lililosababisha kifo cha Kanumba.

Kava la filamu ya mwisho ya Marehemu Kanumba

IBF Afrika sasa yahamia Botswana


 
Rais wa IBF Africa, Onesmo Ngowi (kushoto)
RAIS wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi amewasili katika jiji la Gaborone, Botswana kupromoti ubingwa wa IBF wa Kimataifa katika uzito wa Bantam.  
Bondia wa Botswana Lesley Sekotswe na bondia mwenzake kutoka nchini Namibia Immanuel “Prince” Naidjala walitoka sare wakati wakishindania ubingwa huo katika pambano lililofanyika katika jiji la Windhoek, Namibia tarehe 20 Mei  mwaka huu.  
Ujio wa Rais Ngowi ulikuwa unangojewa na wadau wengi wa ngumi katika nchi hii tangu aitembelee Botswana mwaka 2002 wakati wa mpambano kati ya bondia wa Botswana Thuso Kubamang na Peter Malinga kutoka nchini Afrika ya Kusini.  
Rais Ngowi atakutana na viongozi wa serikali ya Botswana pamoja na wadau mbalimbali wa ngumi na safari yake itaanzia jiji kuu la Gaborone mpaka jiji la pili kwa ukubwa la Francistown ambako wadau wengi wa ngumi wanamsubiri kwa hamu.  
Nchi ya Botswana ni nchi yenye msingi mzuri sana wa ngumi za ridhaa lakini tatizo kubwa limekuwa ni namna ya kuwaendelza wanapofikia kikomo kwenye ridhaa. Kikao cha Ngowi na viongozi wa serikali wa Botswana kitaweka msingi mzuri wa namna ya kuwaendeleza mabondia wa Botswana. 
Botswana ni nchi inayopakana na Namibia kwa hiyo mpambano wa Sekotswe na Naidjala unategemewa kuwa na wapenzi wengi wa ngumi kutoka katika nchi hizi mbili.

Picha, Promota Kinda Nangolo wa Namibia akimwaga Rais wa IBF/Africa Onesmo Ngowi wakati akiondoka nchini humo kuelekea Botswana!

Sunday, March 31, 2013

Liverpool yazinduka EPL, yaifumua Aston Villa kwao

http://cache.images.globalsportsmedia.com/news/soccer/2013/3/31/315082header.jpg
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard akishangilia bao la jioni ya leo

MABINGWA wa zamani waUlaya, Liverpool jioni ya leo imezinduka tena kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kupata ushindi wa mabo 2-1 ugenini mbele ya wenyeji wao Aston Villa.
Mkwaju wa penati iliyopigwa na nahodha Steven Gerrard katika dakika ya 60 ndiyo iliyoihakikisha Liverpool ushindi wa pointi tatu muhimu baada ya kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa bao 1-0 lililotupiwa kambani na Mbelgium mwenye asili ya DR Congo, Christian Benteke.
Benteke alifunga bao hilo katika dakika ya 31, akimaliza kazi nzuri ya Gabriel Agbonlahor.
Wageni waliingia kipindi cha pili kwa kasi na iliwachukua dakika mbili tu kusawazisha bao kupitia Jordan Henderson na dnipo kwenye dakika ya 60 Gerrard akatupia mpira wavuni kwa penati  baada ya Luis Suarez kuangushwa langoni mwa Aston Villa alipokuwa akienda kumsalia kipa wa Brad Guzan.
Hata hivyo ushindi huo wa leo umeiacha Liverpool katika nafasi ya saba, ikiwa imecheza mechi 31, ikiwa nyuma ya wapinzani wao, Everton walioishinda jana bao 1-0 dhidi ya  Stoke City.