STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, April 27, 2013

Ruvu Shooting walalamikia gharama, lakini yaionya Simba

Kikosi cha Ruvu Shooting Stars
UONGOZI wa Ruvu Shooting umesikitishwa na gharama ulizobebeshwa na serikali na shirikisho la soka, TFF, kufuatia kuahirishwa kwa pambano la ligi kuu ya Bara dhidi ya Simba juzi.
Lakini uongozi huo umesisitiza kuwa kipigo kwa 'mnyama' kipo palepale timu hizo zitakapokutana katika tarehe mpya - Mei 5.
TFF ilitangaza kuahirisha pambano hilo lililokuwa lichezwe kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam saa chache kabla ya kufanyika kwake na kupanga lifanyike Mei 5.
Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire aliimbia MICHARAZO jana kuwa wamekerwa na kusikitishwa na kitendo hicho kilichowatia hasara kubwa ya kuweka kambi, kufanya maandalizi na kusafiri kutoka Mlandizi mpaka Dar Es Salaam na kukaa siku kadhaa kisha kuahirishwa mechi.
Bwire alisema licha ya TFF kuwaomba radhi na kujitetea kuwa haihusiki na kuzuiwa kutumiwa kwa Uwanja wa Taifa kutokana na kupisha maandalizi ya sherehe za Muungano, lakini inastahili lawama kwa kitendo hicho kwani walipaswa kulifahamu hilo mapema na kuzipunguzia gharama timu husika.
"Tumeumizwa sana na kilichofanyika, tulifanya maandalizi yenye gharama kwa ajili ya mechi hiyo, hata hivyo hatuna mpango wa kudai fidia yoyote kwani TFF imeshajitetea kwetu na sasa tunafikiria mechi yetu ya Mei Mosi dhidi ya JKT Oljoro," alisema.
Bwire alisema pamoja na kuiwaza mechi hiyo ya Oljoro, lakini Simba wasifikirie tayari wameshaepuka kipigo kutoka kwao, kwani hata Mei 5 wakikutana lazima wakutane nacho kwa maandalizi waliyofanya na kiu yao ya kumaliza kwenye 'Nne Bora'.
"Kipigo kwa Simba kipo pale pale wameahirishiwa tu, tunataka kuonyesha kuwa Ruvu ni timu nzuri na tunataka tumalize katika Tatu au Nne Bora msimu huu, kwani kwa mechi zilizosalia tuna uwezo wa kufikisha pointi 42," alitamba Bwire.
Timu hiyo ipo katika nafasi ya saba ikiwa na pointi 30 ikiwa na michezo minne kabla ya kumaliza msimu wa 2012-2013.

Simba yatishiwa Polisi, Machaku aapa Mnyama lazima akae


Kikosi cha Simba
Machaku Salum 'Balotelli' wa Polisi Moro
LICHA ya kuhitaji miujiza ili kubaki kwenye ligi kuu ya Bara msimu ujao, wachezaji wa Polisi Morogoro wana imani ya kujikwamua na janga hilo kwa kuanzia na kuifunga Simba katika mchezo baina ya timu hizo kwenye Uwanja wa Taifa kesho.
Polisi Morogoro ni ya pili toka mkiani katika ligi ambayo zitashuka timu tatu za mwisho, ikiwa na pointi 19.
Ili kubaki kwenye daraja hilo la juu zaidi Polisii nahitaji kushinda mechi zake tatu zilizobaki ili kufikisha pointi 25 na kupunguza tofauti ya magoli ya -10 iliyonayo.
Bahati mbaya kwa Polisi, hata hivyo, jumla hiyo imeshafikiwa na ama kupitwa na timu zote zilizo katika eneo la salama la kubaki kwenye ligi kuu na zikiwa si tu na michezo iliyobaki bali pia uwiano bora wa magoli.
African Lyon na Toto Africa nazo zina uwezo wa kufikisha pointi 25 lakini kwa kubakiwa na michezo miwili na mmoja, kwa mpangilio huo, zipo katika mazingira magumu zaidi ya Polisi Morogoro.
Mmoja wa wachezaji wa Polisi Salum Machaku alisema licha ya timu yao kuwa katika eneo la hatari, lakini hawajakata tamaa.
Amedai wachezaji wote wamejipanga kufanya kweli katika mechi zilizosalia dhidi ya Simba, Kagera Sugar na Coastal Union.
"Hatujakata tamaa na wala hatuamini kama Polisi itarudi daraja la kwanza," alisema na kueleza zaidi, "tumejipanga kupigana kiume katika mechi zilizosalia ili kubaki na Simba wakae chonjo kwani tutakufa nao Uwanja wa Taifa."
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuichezea Simba na timu za Pan Africans, Azam na Mtibwa Sugar, alisema hakuna mchezaji wala mwana Polisi Moro anayetaka kusikia habari za kushuka daraja japo wamechelewa mno kuzinduka.
Machaku alisema ugeni wao katika ligi wakati wa duru la kwanza lililosababisha wapoteze mechi na pointi nyingi ndiyo iliyowagharimu kabla ya kuzinduka katika duru la pili wakiwa wamechelewa.

Machupa, Kisiga waibeba Golden Bush wakiipa kichapo Wahenga Fc

Shaaban Kisiga (Katikati) akiwatoka wachezaji wa Wahenga Fc

Nyota wa Wahenga Fc, Macocha Tembele akiwatok wachezaji wa Golden Bush

Yusuf (9) wa Wahenga, akitafuta mbinu za kumtoka Abuu Ntiro huku wachezaji wenzake wakiwa tayari kumpa msaada katika pambano lao lililochezwa jana na Wahenga kunyukwa mabao 2-1

Abuu Ntiro akimtoka Yusuf

Heka heka katika lango la Wahenga Fc

NYOTA wa zamani wa Simba na taifa Stars, Athuman Idd Machuppa na Shaaban Kisiga 'Marlon' jana waliisaidia Golden Bush Veterani kupata ushindi muhimu  wa mabao 2-1 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Wahenga Fc katika pambano maalum la kusherehekea  Miaka 49 ya Muungano.
Timu hizo zilipambana katika mchezo mkali na uliosisimua uliochezwa kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Darajani, ambapo Machuppa, Kisiga wakisaidiwa na nyota wa zamani wa Simba na Yanga walifunga mabao hayo katika muda wa dakika tano tu mara baada ya kurejea toka mapumziko timu zikiwa hazijafungana.
Machuppa ndiye aliyeanza kuifungia Golden Bush bao tamu katika dakika ya 68 akimalizia kazi nzuri ya Herry Morris kabla ya Kisiga kuongeza jingine dakika tano baadaye na kuzima matumaini na Wahenga Fc waliokuwa uwanja wa nyumbani kulipa kisasi ilichokutana nacho mwezi uliopita kwenye uwanja wa Kinesi.
Katika pambano hilo la Kinesi, Wahenga walinyukwa pia mabao 2-1 huku mvua ikiwanyeshea timu zote mbele ya aliyekuwa mgeni rasmi, Kamanda wa Polisi, Thobias Andengenye.
Golden Bush na kikosi kilichosheheni nyota waliowahi na wanaendelea kutamba nchini kama kipa Aman Simba, Abuu Ntiro, Godfrey Bonny 'Ndanje', Wisdom Ndlovu, Herry Morris, Said Sued, Salum Sued, Kisiga, Machuppa na wengine waliifanya Wahenga ishindwe kufuruka licha ya mara kadhaa kubisha hodi langoni mwa mwao.
Dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika huku kiza kikiwa kimeshaanza kutamba uwanjani, Wahenga walipata bao la kufutia machozi lililofungwa kwa mkwaju wa penati na nyota wa kikosi hicho, Macocha Tembele aliyekuwa akihaha uwanja mzima kuibeba timu yake.
Licha ya Wahenga kuendelea kushambulia lango la Golden Bush, mpaka kipyenga cha mwamuzi, Pondamali kulia walijikuta wakiendelea kuwa 'wateja' wa Wakali wa soka Dar es Salaam kwa kukubali kipigo kingine cha mabao 2-1.

Warembo 16 watemwa Miss Tabata



Warembo wa watakaoshiriki shindano la Miss Tabata 2013 wakiwa katika pozi tofauti kambi yao ya mazoezi Da West Park
 
JUMLA ya warembo 16 wametemwa katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Redds Miss Tabata ambao utafanyika Mei 31 Dar West Park.
Mratibu wa shindano hilo, Godfrey Kalinga, alisema jana kuwa warembo hao wametemwa kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo utoro, kukosa sifa za kushiriki na utovu wa nidhamu.
Kalinga aliwataja warembo waliyotemwa kuwa ni Sophia Claud (21), Lilian Mpakani (19), Lilian Msanchu (19), Rita Frank (20), Pasilida Mandali (21), Rachel Mussa (19), Jasmin Damian (18), Angelina Mkinga (19), Mercy Mwakasungu (20), Tunu Hamis (19), Ray Issa (22), Shamim Abass (22), Shan Abass (22), Amina Ally (18), Magdalena Bhoke (21)  na Zilpha Christopher (19)
Kalinga aliwataja warembo wanoendelea na mazoezi katika umbumbi wa Dar West Park, Tabata kila siku kuwa ni Hidaya David (22), Aneth Ndumbalo (19), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Kitereja (19),  Angela Fradius (19), Domina Soka (21), Rehema Kihinja (20) and  Glory Jigge (18).
Wengine ni Rachel Mushi (20), Caroline Sadiki (20), Kabula Juma Kibogoti (20), Blath Chambia (23), Suzzane Daniel Gingo (18), Upendo Lema (22), Pasilida Mandari (21) na Martha Gewe (19).
Washindi watano kutoka Tabata watafuzu kushiriki Redds Miss Ilala baadaye mwaka huu.
Anayeshikilia taji la Miss Tabata ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.
Redds Miss Tabata inaandaliwa na  Bob Entertainment na Keen Arts na chini ya Udhamini wa Redds, CXC Africa, Fredito Entertainment, Brake Points na Saluti5.
 

Cheka, Mashali patachimbika Mei Mosi


Reeling from the recent defeat in the hands of the German strongman Uensal Arik , TEAM Francis Cheka is back on the drawing board as it attempts to defuse negative impact of the loss in their forthcoming rumble against the man of the people and dreadlock Thomas MashaliThe duo is competing for the “IBF Continental Africa Super Middleweight Title” as optional defense for Cheka.
 
 
The tournament slated for 1st May, 2013 (May Day) has elicited a lot of excitements from thousands of boxing stakeholders in Tanzania and the whole of East African region. Thomas Mashali is the East & Central African Middleweight Champion and the biggest crowd puller in the region todate.

                                                                      Francis Cheka (right) and Uensal Arik (left)
 

Cheka’s recent defeat was kind of embarrassment as he took the fight as a warm up but alas, things turned bitter as the Germany strongman Uensal Arik sent him reeling to the floor before Thomas Mtua threw out the towel as SOS for the Tanzanian slugger! It was a defeat from “Manna”as this kind of taught Cheka a lesson or two about taking boxing serious as there is nothing as a small fight in boxing.


Adam Tanaka of Mumask Investment and Gebby Presure LTD, the man of the hour promoting this fight has been working over drive to have all the details finalized. Of the top priority is the arrival of the ring officials (all coming outside Tanzania) who have been summoned to preside over the rumble. This is so because Adam want to avoid complaints from either boxer should the decision goes against their expectations.

"The poster in Kiswahili language tells it all"

 
The man who has been charged with the responsibility to stand in as “the third man in the ring” is no other than the Zambian Army Officer, John Shipanuka who himself looks like a heavyweight boxer in refereeing uniform. Shipanuka’s body language and impatiality with boxers in the ring has illuminated his CV and make him one of the most sort-out ring officials in Sub Sahara Africa.

Arusha Mayor (left) and IBF/AFRICA' Onesmo Ngowi(right) crowing Cheka after his last defense 12/26/12

To assist him would be two Sedentary Generals of; Uganda Professional Boxing Commission (UPBC), master Simon Katogole and Daudi Chikwanje of Malawi Boxing Association (MBA). These two gentlemen would be in the company of one of the most experienced judges in East Africa Alhaj Ismail Sekisambu also from Uganda.


So, “the chickens have finally come home to roost" as any of the two has to face the consequences of his mistakes in the ring on that particular day.


So, as the clock ticks to the morning hours of May Day 2013, Dar Es Salaam landscape may turn into a “quicksand” for the two gladiators as fans from all walks of life jams the PTS Social Hall to witness yet another rumble of the year!
 
 
 Nothing has been left to chances as the World's premier professional boxing “top dog” the IBF has already given its blessing by sanctioning for the title!
 

Suarez akubali yaishe, aomba msamaha



LONDON, England
Mshmbuliaji wa Liverpool Luis Suarez ameomba msamaha baada ya kukubali adhabu ya kutocheza mechi 10 kwa kumng'ata Branislav Ivanovic wa Chelsea katika mechi ya ligi kuu ya soka ya Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita.
Muuruguay huyo alikuwa na muda mpaka mchana jana kupinga adhabu ya Chama cha Soka ya kuongeza mechi saba katika adhabu ya kawaida ya kukosa michezo mitatu kwa kosa la kufanya ukatili lakini akaamua kutobishia.
"Nataraji kuwa watu niliowaudhi Jumapili iliyopita watanisamehe na narudia tena kumuomba radhi binafsi Branislav," Suarez aliseka katika ukurasa wake wa Twitter.
"Ingawa ni wazi kwamba mechi 10 ni nyngi kuliko vifungo vilivyowahi kutolewa katika kosa kama hili huko nyuma ambapo wachezaji walijeruhiwa, nakubali kuwa kitendo changu kilikuwa hakikubaliki kwenye uwanja wa soka hivyo sitaki kuleta picha mbaya kwa watu kwa kukata rufaa."
Suarez, ambaye alimng'ata Ivanovic mkononi katika sare ya 2-2 kwenye uwanja wa Anfield wiki-endi iliyopita, hatoweza kuichezea Liverpool katika michuano ya ndani mpaka Septemba.
Liverpool, ambayo ilimpiga faini Suarez, ilisisitiza kusikitishwa kwake na uamuzi wa FA wa kumfungia Suarez kwa mechi 10.
"Adhabu dhidi ya Luis ilikuwa yake binafsi kuamua na ni lazima tuheshimu uamuzi wake wa kutokata rufaa kufungiwa mechi 10," mkurugenzi mtendaji Ian Ayre alisema.
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers aikilaumu chama cha soka kwa ukali wa adhabu ya Suarez na palikuwa na kuungwa mkono na makocha wa timu pinzani jana.
"Katika kesi hii, ukubwa wa adhabu na kosa vinaonekana kupishana mno kulingnaisha na makosa ambayo wachezaji wengine wamewahi kuadhibiwa nayo," kocha wa Arsenal Arsene Wenger aliwaambia waandishi wa habari.
"Nadhani kilichommaliza kabisa Suarez ni historia yake, ambayo ina makosa mengi.
"Ndiyo sababu ameadhiwa vikali sana, ndiyo sababu pekee ambayo naweza kuiona."
Kocha wa Manchester City Roberto Mancini alisema katika mkutano wake wa Ijumaa na waandishi wa habari: "Mechi tano au sita zilitosha, huu ndiyo mtazamo wangu lakini sifanyi kazi FA."
Ni mara ya pili kwa Suarez, 26, kufungiwa kwa kumng'ata mchezaji wa timu pinzani baada ya kumng'ata Otman Bakkal wa PSV Eindhoven kwenye shingo wakati akiichezea Ajax 2010, na kufungiwa mechi saba.
Suarez alifungiwa pia mechi nane msimu uliopita baada ya FA kumuona ana kosa la kumbagua kwa rangi ya ngozi Patrice Evra wa Manchester United Oktoba 2011.
Reuters

Suarez

Thursday, April 25, 2013

Simba yatoa msimamo kuahirishwa ghafla kwa mechi yao na Ruvu Shooting



Na Ezekiel Kamwaga
UONGOZI wa Simba umekubaliana na hatua ya serikali kuzuia kuchezwa kwa mchezo uliopangwa kuchezwa leo wa Ligi Kuu ya Tanzania baina ya Wekundu wa Msimbazi na Ruvu Shooting Stars.
Hata hivyo, uongozi wa Simba haujafurahishwa na namna uzuiaji huo ulivyofanyika. Taarifa imetolewa leo kwenye siku ya mechi yenyewe wakati maandalizi yote yakiwa yamefanyika na hivyo kusababisha matatizo katika sehemu kubwa tatu.
Mosi, uongozi wa Simba umeingia gharama kubwa ya kuweka timu kambini na kujiandaa na mechi. Pili, benchi la ufundi na wachezaji walikuwa tayari wamejiandaa na mechi kimwili na kiakili na kuahirishwa huku kwa mechi kumesaidia tu kuvuruga programu. Tatu, wapenzi na washabiki wa Simba wamepata usumbufu wa kwenda uwanjani na kukuta hakuna mechi.
Uongozi wa Simba unapenda kutumia nafasi hii, katika namna ya kipekee kabisa, kuwaomba radhi wapenzi na wanachama wake ambao walifika Uwanja wa Taifa kutazama mechi ambayo haikuwapo.
Washabiki ndiyo wanaoifanya Simba na mchezo wa mpira wa miguu nchini uwe na umaarufu ulionao na bila wao ligi yetu inaweza kupoteza nguvu na ushindani ilionao.
Simba SC inapenda kuwe na utaratibu unaojulikana wa kuahirisha mechi wa walau saa 48 kabla ya siku ya mechi. Hii itasaidia pande zote zinazohusika. Kama mechi imeshindikana kwa sababu za nje ya uwezo wa kibinadamau (Force de Majeure) kama vile mafuriko, tetemeko la ardhi na vimbunga, mechi inaweza kuahirishwa ghafla lakini si kwa mechi ambayo uwepo wake ulifahamika miezi kadhaa nyuma.
Tunashauri pia kwamba siku za mechi ambapo Ligi Kuu inachezwa (match days), inatakiwa kuwa zinafahamika na isiwe kila siku mechi zinachezwa. Simba ilikuwa na mechi wikiendi iliyopita na Ruvu ilikuwa na mechi Mbeya zaidi ya wiki moja iliyopita na hivyo mechi hii ingeweza kuchezwa hata jana (Jumatano) ambayo ni siku ya kawaida kwa mechi kuchezwa badala ya leo Alhamisi.
Ni matumaini yetu kwamba kuahirishwa kwa mechi hii kutakuwa fundisho kubwa katika upangaji wa ratiba na uahirishaji wa mechi ambao una faida kwa pande zote husika.


Poppe arejea Simba
MWENYEKITI wa Simba, Mhe, Ismail Aden Rage, amemshukuru aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu, Zacharia Hans Poppe, kwa kukubali kurejea kushikilia nyadhifa zake zote.
Poppe alitangaza kujiuzulu nyadhifa zake za uongozi ndani ya Simba Machi 7 mwaka huu, kutokana na hali ya migogoro iliyokuwapo wakati huo.
Hata hivyo, Rage alikataa kujiuzulu huko kwa Poppe na akasema atamshawishi abadili maamuzi kwa manufaa ya Simba.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaarifu wana Simba popote walipo kwamba Poppe amerejea na yuko tayari kuitumikia Simba kama Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba,” alisema Rage.
Kwa upande wake, Poppe alisema amerejea Simba kutokana na utulivu ulioanza kujitokeza klabuni na kwamba nia yake ni kuhakikisha klabu inafanya usajili mzuri na wa kiwango kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.

GHANA KUWAKA MOTO KWA MASUMBWI


By Onesmo Ngowi
GHANA, one of the boxing powerhouses in African continent is edging towards three biggest IBF tournaments next week on May 3rd, 2013 at the Accra Sports Arena in Ghana
Princess Hellen Joseph

GoldeMike Boxing Promotion Syndicate is at it again and this time Ghanaian boxing stakeholders and the whole of West Africa region will enjoy a thrilling moment which they all have been carving for.

This is one of the major IBF tournaments in Sub Sahara Africa and nothing is being left to chance as the promoters “Henry Many-Spain and Michael Tetteh” painstakingly deal with all the final details for this epic duel!
Albert Mensah (right)
Drawing the line of this epic boxing tournament is none other than two of the Ghanaian’s most fiercest opponents in Jr. Middleweight, Albert Mensah when he confront his archenemy Ben Odemattey.
 
The duo is battling for the “IBF Continental Africa Jr. Middle Weight Crown”. Came sun, come rain one of them would be the King of the Jr, Middleweight in Africa.
 
Following this epic bout, will be the Princessfrom Nigerian boxing royal family, Princess Helen Joseph when she goes toe to toe with another Princess from Austro-Hungarian Boxing Empire, Princess Marianna Gulyas.

The two beautiful Princesses who would pass in a beauty-parget are battling for the “IBF vacant Intercontinental Featherweight Female Crown”.

"We are definately going to get the crown" said Koffi Dakku-Ricketts,the man who is behind Princess Helen's success as a trainer. Ricketts boast of many similar success stories and make him one of the best trainers Ghana has ever had in years!
 
This has been “a seek and hide game” for the past two years but, this time around, no ground can hide any of the two as the moment of truth is about to come.
 
The man of the moment is none other than the Ghanaian ups and comings boxing star and Olympiad boxer “Issa Samir” in a duel of his life when he host the handsome Georgian true-nan and flamboyant “Robison Omshashavili” for the vacant “IBF World Jr. Middleweight Crown” in a 12 rounds epic battle.
 
The bout christened“The Battle of the Gold Coast” would rekindle the memory when one of the Ghanaian boxing king, Professor Azumah Nelson when hosted Sidnei Dal Rovere in a similar battle at the Accra Sports Stadium in 1988.
 
The ground can be “quicksand” for the two as they crave to prove to the whole world that they are indeed “pound for pound” gladiators and future world champions on the rise!
 
This is; in a matter of fact “a thumb up” for Ghana as it makes African continent proud once again after shining out during the last “World Cup tournament” in South Africa.

Hii kali! Sherehe za Muungano zakwamisha pambano la Simba na Ruvu Shooting Taifa

 
Viongozi wakuu wa TFF, Leodger Tenga na Angetile Osiah
Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeahirishwa mpaka Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Kisa cha kufanyika ghafla kwa mabadiliko ya pambano hilo imetokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo na ghafla. Ratiba ya mechi nyingine za VPL zinabaki kama zilivyo.

Kitendo hicho cha mechi hiyo kuahirishwa ghafla kinauonyesha umuhimu wa klabu na hata FA kumiliki uwanja wake ili kuondokana na matatizo kama hayo yanayolitia doa soka la Tanzania.

Hata hivyo pamoja na pambano hilo kupigwa 'dochi' hadi Mei 5, TFF imesisitiza kuwa ratiba nyingine za ligi hiyo inayopelekea ukingoni itaendelea kama ilivyo, ambapo kesho (Aprili 26 mwaka huu) Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Jumapili 'Mnyama' Simba itaikaribisha Polisi Moro kwenye pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa siku ya Jumapili (Aprili 28 mwaka huu).

Msondo Ngoma yapeleka mpya Magereza

Waimbaji nyota wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede 'Kamchape' na Juma Katundu 'JK wa Msondo'
BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma,  inatarajiwa kuwapelekea burudani mashabiki wao wa maeneo ya Mtoni kwa Aziz Ali na Magereza Ukonga.
Msemaji wa Msondo, Rajabu Mhamila 'Super D' aliiambia MICHARAZO kuwa, bendi yao imeongeza ratiba ya kutoa burudani wiki hii kwa mashabiki wa maeneo hayo.
Alisema Msondo inayojiandaa kupakua albamu mpya ya 'Suluhu' leo itatoa burudani Mtoni kwa Aziz Ali kabla ya kesho kwenda Magereza Ukonga.
"Jumatano na Alhamisi tutakuwa tukitoa burudani katika maeno hayo, na Ijumaa hadi Jumapili ratiba inabaki kama ilivyo," alisema.
Alisema kwa kuwakumbusha mashabiki wao, Ijumaa hufanya vitu vyao Leaders na Jumamosi  huwa TCC Chang'ombe na Jumapili watavuka bahari hadi Kigamboni.
"Jumapili tutakuwa G-Five Kigamboni, ambapo Msondo itapiga nyimbo za zamani na mpya zilizoifanya iitwe Baba ya Muziki," alisema.

CATHERINE FOUNDATION YATOA MSAADA DODOMA


Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda na Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige wakiwakikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Matumaini cha mjini Dodoma.

ASASI ya Kijamii ya Catherine Foundation jana imetembelea kituo cha kulelea wa watoto cha Matumaini Village kilichopo mkoani Dodoma ambapo walikwenda kutoa misaada mbalimbali wakiongozwa na Mkurugenzi wa Asasi hiyo, Catherine Magige.
Katika Hafla hiyo Mgeni Rasmi alikuwa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda ambapo asasi hiyo ilitoa vitu mbalimbali vikiwemo, Madaftari, Mafuta, Sabuni, Juice, miswaki na dawa zake, mchele, sukari, nguo za watoto, kanga za wakinadada wanaowalea watoto hao na vingine vingi.

 
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akihutubia katika hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akihutubia katika hafla hiyo jana.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akiwakikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akiwakiwapa zawadi mbalimbali kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.

Sikinde kutambulisha mpya wakielekea Mbeya kwenye Mei Day

Waimbaji wa Mlimani Park 'Sikinde' Hassani Kunyata, Abdallah Hemba na Hassani Bitchuka 'Stereo' watakaotoa burudani kwa wakazi wa jijini la Mbeya na vitiongoji vyake kuanzia kesho wakienda kwenye Mei Day

BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Sikinde' inatarajiwa kutambulisha nyimbo zake mpya katika miji kadhaa wakati wakielekea Mbeya katika sherehe za Mei Day.
Sikinde imealikwa kutumbuiza katika sherehe hizo ambazo kitaifa zitafanyikia kwenye mkoa huo wa Mbeya wiki ijayo.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo alisema wakati wakiwa njiani kuelekea Mbeya watafanya maonyesho kadhaa katika maeneo mbalimbali na nje na ndani ya mkoa huo.
Milambo alisema maonyesho hayo yataanza kesho Ijumaa watakapotambulisha nyimbo zao kwenye ukunbi wa Comfort Chamazi, kabla ya Jumamosi kuwa City Pub uliopo Mwanjelwa.

Sikinde itaendeleza makamuzi yake siku ya Jumapili eneo la Tunduma kabla ya siku ya Mei Mosi kutumbuiza kwenye sherehe za Mei Daya asubuhi kwenye uwanja wa Sokoine kabla ya usiku kufanya vitu vyao ukumbi wa Benjamini Mkapa mjini humo.
"Siku ya Mei Mosi tukishatoka kutumbuiza uwanja wa Sokoine tutafanya onyesho katika ukumbi maarufu mjini humo kisha kuanza safari ya kurejea Dar kuendelea na mengine," alisema.
Milambo anasema katika maonyesho yote watatambulisha nyimbo zao wanazoziandaa kwa ajili ya albamu mpya kama 'Jinamizi la Talaka', 'Kuvunjika kwa Dole Gumba', 'Nundule' na nyingine.
"Pia tutawapa burudani mashabiki kwa kuwakumbusha vibao vyetui vya zamani vilivyotufanya Sikinde kutambuliwa kama 'Mabingwa wa Muziki wa Dansi Tanzania," alisema Milambo.

Ally Mustafa 'Barthez' afichua siri nzito Yanga

Kipa Ally Mustafa 'Barthez' akiwa mazoezini

KIPA tegemeo wa vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ally Mustafa 'Barthez' amefichua siri akidai kung'ara kwake katika msimu wa kwanza ndani ya Yanga kumetokana na kuaminiwa na makocha pamoja na kuungwa mkono na wachezaji wenzake, wanachama na mashabiki wa klabu hiyo.
Barthez aliyeitwa kwenye kikosi cha pili cha timu ya taifa 'Young Taifa Stars', alisema pia kiu kubwa ya mafanikio aliyokuwa nayo na kutaka kuwadhihirishia Watanzania kwamba yeye ni mkali ndiyo iliyomfanya kujituma zaidi na kuipigania Yanga kufanya ilivyofanya msimu huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Barthez aliyetua Yanga akitokea Simba alikokuwa akisugua benchi nyuma ya kipa Juma Kaseja, alisema ameweza kung'ara kwa sababu makocha aliokutana nao Jangwani walimuamini na kumpa nafasi ya kuonyesha kipaji alichonacho.
Barthez, alisema ni vigumu kwa mchezaji yeyeote kuweza kuonyesha ubora wake kama hapewi nafasi na hata yeye hakuonekana bora mahali alipotoka kwa vile hakuamini na kupewa nafasi ya kucheza tofauti na tangu atue Yanga.
"Najisikia faraja kufanikiwa kuisaidia Yanga, pia kurejesha heshima yangu, lakini hii haikuja kimiujiza bali ni kutokana na makocha wangu kuniamini na kunipa nafasi sambamba na ushirikiano mzuri ninaopata kwa wachezaji wenzangu na sapoti kubwa ya wanachama na mashabiki," alisema.
Kipa huyo aliyewahi kutamba na timu mbalimbali za wilayani Ilala kabla ya kupanda daraja na Ashanti United kisha kunyakuliwa na Simba mwaka 2005, alisema bado hajaridhika na mafanikio aliyonayo akiota kuisaidia zaidi Yanga na hasa kwenye michuano ya kimataifa.
Barthez aliyetua Yanga na mguu mzuri kwa kuiwezesha kuibebesha taji la Kombe la Kagame kwa mara ya pili mfululizo Julai mwaka huu kisha kukaribia kuipa taji la 23 la Ligi Kuu Tanzania Bara, alisema anatambua changamoto inayomkabili kuendelea kubaki kuwa bora na atajituma zaidi.

Zahoro Pazi ajiandaa kutimkia Celtic ya 'Sauzi'

Zahoro Pazi (kulia) alipokuwa na kikosi cha Azam kabla ya kupelekwa kwa mkopo JKT Ruvu

MSHAMBULIAJI wa Azam FC anayecheza kwa mkopo katika klabu ya JKT Ruvu, Zahoro Pazi anatarajiwa kuondoka nchini kwenda Afrika Kusini kwa mara ya pili kujiunga na klabu ya Bloemfotein Celtic ya nchini humo.
Celtic inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo (PSL), ilimuita na kumfanyia majaribio mchezaji huyo mapema mwaka huu na kuelezwa kuwa alifaulu lakini kwa kuwa nafasi ilikuwa ni ya mchezaji mmoja tu, alichukuliwa Mzimbabwe Roderick Mutuma.
Hata hivyo, mara aliporejea nchini Pazi alisema aliahidiwa na klabu hiyo kuitwa tena mara baada ya msimu huu kumalizika ili kuendelea kujifua na timu hiyo kwa ajili msimu ujao na kwamba safari hiyo ingefanyika mwezi Mei.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Pazi alisema mapema wiki hii alipigiwa simu na kocha wa klabu hiyo, Clinton Larsen, na kumfahamisha kuwa ajiandae kwenda nchini humo mwezi Juni wakati mazoezi ya kusaka wachezaji wa msimu ujao utakapoanza.
"Ile safari yangu haitakuwa tena Mei, nimepigiwa simu na kocha wa Celtic na kunieleza kwamba mazoezi yao kwa ajili ya kujiandaa msimu mpya yataanza mwezi Juni, hivyo natakiwa niende wakati huo," alisema Pazi.
Alisema kusogezwa mbele kwa safari yake kumekuwa ni nafuu kwake akiamini kutamfanya ajifue zaidi ili atakapoenda awe katika kiwango kile kile kilichoivutia klabu hiyo iliyomuona kwenye michuano ya Kombe la Kagame na Kombe la Hisani nchini DR Congo.
"Ligi yao kama yetu itaisha mwezi ujao, na kwa vile safari itakuwa Juni naamini nitatumia muda uliosalia kujifua zaidi ili niendapo huko niwe katika kiwango kile kile na kufanya niweze kujiunga nao, naamini Mungu ataniwezesha kutimiza ndoto zangu kucheza soka la kulipwa," alisema Pazi.
Mchezaji mwingine wa Azam, Abdulhalim Humud 'Gaucho' naye amefaulu majaribio yake katika klabu ya Jomo Cosmos na atajiunga nao Julai mwaka huu kwa ajili ya msimu mpya.

Mbio za kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania zaanza rasmi


Mshindi wa Redd's Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred

HARAKATI za awali za kumsaka Redd’s Miss Tanzania zinaanza rasmi mwishoni mwa wiki hii wakati kutakapokuwa na kinyang’anyiro cha kuwapata warembo wa vitongoji katika maeneo mbalimbali nchini wakiwamo wa vyuo vya elimu ya juu (Redd’s Miss High Learning), imefahamika.
Taarifa kutoka kwa waandaaji wa shindano la Redd’s Miss High Learning mkoani   Morogoro, zinaeleza kuwa mwakilishi wao atasakwa mkoani humo kesho. Imefahamika vilevile kuwa Jumamosi, pia kutakuwa na kinyang'anyiro cha aina hiyo mkoani Dodoma wakati atakaposakwa mrembo wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), mwakilishi wa vyuo vya elimu ya juu kutoka mikoa ya Kagera na Mwanza.
Mratibu wa shindano la Redd’s Miss Morogoro High Learning, Verdian Kamugisha, alisema kuwa kila kitu kimekamilika na kutakuwa na burudani za kutosha wakati watakapokuwa wakimsaka mwakilishi wao.
“Tumekamilisha kila kitu na warembo wote wako katika hali nzuri na kutakuwa na burudani za kutosha. Wakazi wa Morogoro waje kuwaunga mkono warembo wetu ili hatimaye tupate mwakilishi atakayepeperusha vyema bendera ya mkoa huu," alisema Kamugisha.
Mratibu wa Shindano la Redd’s Miss UDOM, Rachel Matina, alisema vilevile kuwa wamekamilisha maandalizi wanaamini kwamba kazi iliyobaki ni kwa watu wa Dodoma kujitokeza keshokutwa kushuhudia namna washiriki kutoka Chuo Kikuu Dodoma walivyopania kulitwaa taji la Redd’s Miss Tanzania mwaka huu.
Joseph Rwebangira anayeratibu shindano la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wa mikoa ya Kagera na Mwanza, alisema mrembo wao atapatikana keshokutwa katika shindano litakalofanyika jijini Mwanza na wanachosubiri sasa ni kwa mashabiki wa mikoa hiyo kujitokeza kwa wingi ili kuwaunga mkono warembo wao na pia kupata burudani mbalimbali.
Katika hatua nyingine, shindano la kumsaka mrembo wa kitongoji cha Hai mkoani Kilimanjaro linatarajiwa pia kufanyika mjini humo mwishoni mwa wiki hii, kama ilivyo kwa kinyang'anyiro cha kuwasaka warembo wa kitongoji cha Tarime mkoani Mara.
Hivi sasa, shindano la Redd’s Miss Tanzania hudhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original. Mshindi wa shindano hilo ngazi ya taifa huiwakilisha nchi katika shindano la kumsaka mrembo wa dunia.

Lewandowski ainyanyasa Real Madrid Ligi ya Ulaya

Robert Lewandowski aliyeiua Real Madrid jana usiku
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Poland Robert Lewandowski usiku wa jana aliinyanyasa atakavyo Real Madrid baada ya kuwatungua mabao manne na kuiwezesha klabu yake ya Borussia Dortmund kuizabua timu hiyo ya Hispania kwa mabao 4-0 katika pambano la Nusu Fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Lewandowski aliyefunga bao mopja kipindi cha kwanza na mengine kipindi cha pili, ameiweka mabingwa wao zamani wa Ulaya kutoka Ujerumani ambao hivi karibuni walitemesha taji la Bundesliga, katika nafasi nzuri ya kufuzu fainali.
Mkali huyo anayefukuziwa na klabu mbalimbali za Ulaya ikiwamo Manchester United, alifunga bao la kwanza dakika ya nane, kabla ya nyota wa Madrid, Cristiano Ronaldo kusawazisha bao dakika mbili kabla ya mapumziko.
Akiwainyanyasa atakavyo ngome ya Madrid, Lewandowski alifunga mabao mawili ndani ya dakika tano mara baada ya kipindi cha pili kuanza akifunga la pili dakika ya 50 na kuongeza jingine dakika ya 55 kabla yua kumalizia udhia dakika ya 67 kwa bao la penati.
Kipigo hicho kimeiacha Madrid wakiwa hoi wakisubiri miujiza kupitia kocha wao Mreno Jose Mourinho kusaka ushindi katika mechi ya marudianoi itakayochezwa wiki ijayo nyumbani kwao ili kufuzu fainali wakihitajika kushinda mabao 3-0.
Pia kipigo hicho cha Madrid jana kimeongeza machunbgu ya Wahispania ambao walikuwa wakiota kushuhudia fainali ya El Classico Mei 25 kufuatia Barcelona juzi kugaragazwa na mabingwa wa Ujerumani na wanafainali wa mara tatu katika miaka miaka minne Bayern Munich kwea mabao 4-0 na kufifisha matumaini hayo.

Wednesday, April 24, 2013

Ruvu Shooting yaichimba mkwara Simba

Ruvu Shooting

Simba wanaotaka kulinda heshima

UONGOZI wa klabu ya soka ya Ruvu Shooting ya Pwani imeichimba mkwara Simba itakayovaana nayo kesho kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikitamba kuwa ni lazima 'mnyama' afe wakitaka kulinda heshima yao.
Akizungumza na MICHARAZO Afisa Habari wa klabu hiyo, Masau Bwire, kwamba mchezo huo kwao wanauchukulia kama fainali na hivyo watashuka dimbani kwa nia moja ya kusaka ushindi ili kudhihirisha kwamba wao ni bora kuliko wana Msimbazi.
"Tunahitaji kuutumia mchezo wa kesho (Alhamis) dhidi ya Simbaili kujenga heshima ya kisoka kwa timu yetu na kuwadhihirishia Watanzania kwambatimu yetu ni nzuri na ina vijana wenye vipaji na uwezo mkubwa wa soka, muhimu sheria 17 zizingatiwe," alisema Bwire.
Msemaji huyo alisema wanaiheshimu Simba kama klabu kongwe na timu yenye uwezo mkubwa kiuchumi na yenye kiu ya kutaka kulinda heshima yake angalau kuambulia nafasi ya tatu baada ya kulitema taji la ubingwa, lakini bado watashuka dimbani kwa dhamira moja tu ya kupata pointi tatu.
Bwire alisema kikosi chao kinachonolewa na kocha Charles Boniface Mkwara hawatakuwa tayari kuwa daraja la mafanikio ya Simba hiyo kesho na hivyo kuwaonya wanamsimbazi kwamba wakae chonjo na wasitarajie mteremko.
"Kocha katuhakikishia kwamba wachezaji wake wopte wapo vyema kwa ajili ya pambano hilo kitu ambacho kinatuma matumaini ya kuanya vyema mbele ya Simba," alisema Bwire.
Hata hivyo pambano hilo la kesho halitakuwa na maana yoyote kwa timu hizo kwani zote hazina matumaini ya ubingwa wala kupata nafasi ya uwakilishi wa mechi za kimataifa mwakani ambazo tayari zimeshachukuliw ana timu mbili za juu za Yanga na Azam.

JKT Ruvu yazishusha rasmi daraja Lyon, Toto African

JKT Ruvu waliozishusha daraja Lyon na Toto Africans

TIMU ya maafande wa JKT Ruvu wamezishusha rasmi timu za African Lyon na Toto African baada ya jioni ya leo kupata ushindi uliowavusha kwenye hatari ya kurudi Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao.
Maafande hao waliokuwa wakiuguza kipigo cha mabao 3-0 toka kwa vinara wa ligi hiyo Yanga, ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Lyon katika pambano lililofanyika kwenye uwanja wa Chamazi na kuifanya kufikisha pointi 26 ambazo haziwezi kufikiwa na timu za Toto na Lyon.
Lyon na Toto zikishinda mechi zao zilizosalia katika ligi hiyo zitazifanya zifikishe pointi 25 tu na hivyo kuwa vigumu kwao kupona kwenye timu tatu za kucheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao.
Lyon imesaliwa na mechi mbili ikiwa na pointi 19, ilihali Toto imesaliwa na mechi moja tu ikiwa na pointi zake 22, hali ambazo inazipa tiketi ya kurudi Ligi Daraja la Kwanza na kusubiri timu ya mwisho ya kuungana nao.
Miongoni mwa timu zilizopo katika janga hilo la kuzifuata klabu hizo ni Polisi Moro iliyosaliwa mechi tatu ikiwa na pointi 19, Mgambo Shootinmg yenye pointi 25 na kusaliwa na mechi mbili ikiwamo dhidi ya Simba.
Pamoja na ushindi huo wa bao 1-0 jioni ya leo bado haijaiweka salama JKT Ruvu kwani italazimika kupata ushindi kwa mechi zake mbili zilizosalia ili kuvuna pointi zaidi zitakazowatoa eneo hilo la hatari.
JKT Ruvu, Mgambo JKT, Polisi Moro na Prisons moja wapo inaweza kuungana na Lyon na Toto iwapo itazembea katika mechi zao zilizosalia.
Kipute cha ligi hiyo kitaendelea tena kesho kwa pambano moja kati ya Simba na Ruvu Shooting pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa, kabla ya Ijumaa kushuhudiwa kipute kingine ambacho kinaweza kutangaza bingwa mpya nchini iwapo Azam itachemsha mbele ya wenyeji wao Coastal Union ya Tanga.
Pambano la timu hizo litachezwa uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga ambapo Azam italazimika kupata ushindi iwapo itataka kuwatia presha Yanga wanaosubiri kulitwaa taji hilo.
Azam wana pointi 47 na kama itashinda mechi zake tatu zilizosalia itafikisha pointi ambazo tayari Yanga imeshazikusanya ikiwa ina michezo miwili mkononi ukiwamo dhidi yua mahasimu wao Simba.

KWA WADAU WA MASUALA YA SHERIA

Laws of Tanzania (CD-ROM) (Principal and subsidiary legislation revised edition 2002

Inline image 1
This is the first complete revision of the laws of Tanzania since 1966 and
comprises principal legislation and subsidiary legislation in force on 31
July 2002. The principal legislation consists of 415 chapters arranged
numerically. There are ten main volumes and a supplementary volume, which
contains the index, alphabetical and chronological tables and certain
omitted Acts which were not in force at the completion of the Law Revision
of 2002. The revised edition of the subsidiary legislation has been
arranged in a similar fashion and consists of ten volumes. The edition
consists of various tables of content; the Constitution (in Kiswahili); and
the ordinary laws of the country (Acts and subsidiary legislation), set out
in numbered chapters.

*Contents Include:*

   - Statutes of Tanzania, revised edition 2002
   - Principal legislation consisting of 415 Chapters in 10 volumes
   - Supplementary Volume with alphabetical and chronological Table of Acts
   - Subsidiary Legislation consisting of 10 volumes

Pricing for single-user, main work archive only). Publication not updated.
Multiple-user pricing available on request.

*Of Interest and Benefit to:*

   - Judicial officers
   - Prosecutors
   - Legal practitioners
   - Libraries
   - Academics

*Key Benefits:*

   - Powerful electronic searching allows for easy and rapid access to
   information
   - Handy hyperlinks facilitate easy navigation within the product

ORDER TODAY!

contacts : WIGO
Mob: +255 655 308308,
        +255 767 102102,
email: cerengeti@gmail.com


TAIFA STARS KUSHIRIKI MICHUANO YA COSAFA

Kocha Kim Poulsen kati
Na Boniface Wambura
TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itashiriki michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika Julai mwaka huu nchini Zambia.

Taifa Stars inashiriki michuano hiyo ya timu za Taifa za nchi wanachama wa COSAFA ikiwa timu mwalikwa. Nchi wanachama wa COSAFA ni Afrika Kusini, Angola, Botswana, Comoro, Lesotho, Madagascar, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Shelisheli, Swaziland, Zambia na Zimbabwe.

Michuano hiyo itafanyika kuanzia Julai 6 hadi 21 mwaka huu katika miji ya Lusaka, Ndola na Kabwe. Ratiba ya makundi ya michuano hiyo itapangwa Mei 3 mwaka huu jijini Lusaka.

Mara ya mwisho michuano hiyo ilifanyika miaka mitatu iliyopita. Hii itakuwa mara ya pili kwa Tanzania kushiriki michuano hiyo baada ya kucheza ya kwanza iliyofanyika mwaka 1996 nchini Zimbabwe.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inatarajia kuingia kambini mwishoni mwa mwezi ujao kujiandaa kwa mechi ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech.

Juni 16 mwaka huu Taifa Stars itacheza na Ivory Coast jijini Dar es Salaam katika mechi nyingine ya mchujo ya Kombe la Dunia wakati Juni mwishoni na Julai mwanzoni itacheza mechi ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Uganda.

Wakati huo huo, waandishi wa habari wanaotaka kuripoti michuano hiyo wanatakiwa kuwasilisha majina yao TFF kabla ya Aprili 27 mwaka huu ili maombi yao yatumwe COSAFA kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho (Accreditation).

AMCHINJA MAMA YAKE AKIMTUHUMU UCHAWI


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Diwani Athuman.

WATU wawili wameuawa katika matukio mawili tofauti mkoani Mbeya, likiwamo la kijana kumchinja mama yake kwa kutumia kisu kama kuku baada ya kumtuhumu kuwa ni mchawi aliyemloga mkwe wake.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Barakael Masaki, jana aliwaeleza waandishi wa habari kuwa tukio la kijana kumchinja mama yake mzazi limetokea juzi majira ya saa 1:00 jioni katika kijiji cha Chobwe wilayani Ileje.

Alimtaja mwanamke aliyetuhumiwa kuwa ni mchawi na kisha kuchinjwa na mwanae kuwa ni Anna Panja (60) mkazi wa kijiji cha Chobwe.

Akisimulia tukio hilo, Masaki aliema kijana huyo aitwaye Michael Panja akiwa na mwenzake ambaye bado hajafahamika, walimvamia mama huyo nyumbani kwake akiwa amelala na mumewe Basale Panja (76), wakamchukua mama huyo na kumchinja shingoni kwa kutumia kisu na kusababisha kifo chake papo hapo.

Alisema baada ya kutenda unyama huo, Michael na mwenzake walitoroka na kwenda kusikojulikana.

Alisema Jeshi la Polisi linaendelea kuwasaka watuhumiwa hao ili wakamatwe na kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya mauaji.

Aidha, alitoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake wajenge utamaduni wa kufikisha malalamiko na kero zao kwa vyombo husika ili yaweze kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Katika tukio la pili, kundi la wananchi wenye hasira wakitumia silaha za jadi walimuua Lufingano Nsinge (32), baada ya kumtuhumu kujihusisha na matukio ya mauaji ya watoto wadogo yaliyokuwa yakitokea katika kijiji chao.

Kamanda Masaki alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 3:00 usiku katika kijiji cha Ndala, kata ya Kandete kwenye kitongoji cha Katumba wilayani Rungwe.

Akisimulia tukio hilo, Masaki alisema marehemu Nsinge siku ya tukio aliingia ndani ya nyumba ya John Mwansamaleba (53) kwa nia ya kufanya uhalifu na ndipo alipokutwa na wananchi hao.

walioamua kuchukua sheria mkononi kwa kumshambulia kwa silaha za jadi kama vile mipini, shoka, kuni na mapanga na kusababisha kifo chake papo hapo.

Alisema Jeshi la Polisi linawashikilia watu wanne kuhusiana na tukio hilo.

Aliwataja watu hao kuwa ni John Mwasamaleba, Angolisye Mwakalinga (30), Lukas Mwasamaleba (40) na Leah Ndemange (45), wote wakazi wa kijiji cha Ndala.
 
CHANZO: NIPASHE

Kamati ya Utendaji Simba yamaliza mzozo wa makocha wao


Makocha wa Simba, Julio na Liewig waliosuluhishwa na kamati ya utendaji ya Simba
KAMATI ya Utendaji ya klabu ya Simba imemaliza mzozo uliokuwepo kati ya makocha Patrick Liewig na msaidizi wake, Jamhuri Kihwelu 'Julio' baada ya kuwakutanisha na kutoa maamuzi katika kikao chao kilichofanyika jana.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani za klabu hiyo zinasema kuwa haikuwa kazi rahisi kwa kamati hiyo kuliweka sawa benchi lake la ufundi kutokana na makocha hao kubwatukiana kwenye kikao kila mmoja akitaka kuwa juu ya mwenzie.
Chanzo cha habari ndani ya Simba kiliiambia MICHARAZO kuwa, licha ya majibizano yaliyoibuka kwenye kikao hicho, lakini mwishoe ilitolewa maamuzi kwamba Liewig ndiye anayepaswa kusikilizwa kama kocha mkuu na wasaidizi wake wakipaswa kumtii kwa manufaa ya klabu yao.
"Kikao kikubwa kizito kutokana na makocha hao kubwatukiana mbele yetu kabla ya kuwaweka sawa na kuwasuluhisha ambapo maamuzi yaliyofikiwa ni kwambna maamuzi yote katika timu yafanywe na kocha mkuu peke yake na wasaidizi ni kufuata baadaye ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima," chanzo kilisema.
Pia kikao hicho kiliamua kwa pamoja kwa kukubaliana na benchi lao la ufundi kuiingiza timu kambini huko Bamba Beach kwa ajili ya pambano lao la kesho dhidi ya Ruvu Shooting na kwa mechi nyingine zilizosalia kza Ligi Kuu Tanzania Bara inayoelekea ukingoni huku wenyewe wakiwa wameshatemesha ubingwa.
Makocha Mfaransa Patrick Liewig na Julio waliingia kwenye mzozo baina yao kutokana na kile kilichoelezwa kutofautiana na kusababisha kuigawa timu jambo lililohatarisha klabu yao ambayo ipo nafasi ya nne kwa sasa ikiwa na pointi zake 36 ikisaliwa na mechi tatu.