STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 22, 2015

HUYU NDIYE KOCHA MKUU MPYA WA SIMBA

SIMBA SC imeingia Mkataba wa miaka mwaka mmoja na kocha Dylan Kerr (pichani) mzaliwa wa Malta na mchezaji wa zamani wa England kwa ajili ya kuinoa klabu hiyo kuanzia Julai 1 mwaka huu. BIN ZUBEIRY inafahamu kocha huyo aliyezaliwa Januari 14 mwaka 1967 mjini Valletta amefikia makubaliano ya kuingia Mkataba wa mwaka mmoja na Simba SC wenye kipengele cha kuongezewa mmoja mwingine, iwapo atafanya kazi nzuri. Uongozi wa Simba SC wakati wote unakiri kuleta kocha Muingereza, lakini umekuwa ukigoma kutaja jina, ingawa BIN ZUBEIRY baada ya uchunguzi wa kina, imefanikiwa kumbaini mwalimu mpya wa Wekundu wa Msimbazi.
DYLAN KERR NI NANI NA AMETOKEA WAPI? Kerr anakuja Simba SC akitokea klabu ya Ligi Kuu ya Vietnam, Hai Phong aliyojiunga nayo Januari mwaka 2014. Huyo ni beki wa zamani wa kushoto aliyeibukia klabu ya Sheffield Wednesday mwaka 1984. Hakucheza mechi yoyote ya Ligi Kuu katika miaka yake minne ya kuwa na klabu hiyo ya Hillsborough hivyo akahamia Arcadia Shepherds ya Afrika Kusini mwaka 1988. Mwaka mmoja baadaye akarejea England kujiunga na Leeds United, ambako alicheza mechi 13 tu za Ligi Kuu katika miaka yake minne Elland Road kabla ya kutolewa kwa mkopo katika klabu mbili, kwanza Doncaster Rovers alikofunga bao lake la kwanza katika ligi, kisha Blackpool.  Katika miezi yake mitatu ya kuwa na Blackpool msimu wa 1991–1992, alifunga moja ya mabao katika ushindi wa 5-2 ugenini dhidi ya Lancashire na mabingwa wa Daraja, Burnley Uwanja wa Bloomfield Road. Mwaka 1993, Kerr akahamia Mortimer Common kujiunga na Reading, ambako alicheza mechi nyingi zaidi za ligi katika historia yake (89) na kufunga mabao matano.  Alikuwemo kwenye kikosi cha Royals kilichotwaa ubingwa wa Ligi Daraja la Pili, na wakati timu hiyo inashika nafasi ya pili katika Daraja la Kwanza msimu uliofuata alikuwepo kikosini. Mwaka 1996, Kerr akasaini Kilmarnock ya Scotland, ambako alicheza mechi 61 za ligi Killie katika miaka minne. Mwishoni mwa msimu wake wa kwanza katika klabu hiyo, alishinda Kombe la Scotland, kabla ya kuumia nyonga na kuwa nje kwa zaidi ya mwaka.
Dylan Kerr enzi zake anacheza Ligi Kuu England
Mwonekano wa sasa wa kocha Dylan Kerr
Kerr akatemwa Kilmarnock, na baada ya mechi moja ya kucheza kwa mkopo Carlisle United akajiunga na Slough Town Oktoba mwaka 2000, kabla ya Septemba mwaka huo kujiunga kwa muda na Kidderminster Harriers, lakini Mkataba wake wa mwezi mmoja ukasitishwa kwa utovu wa nidhamu. Akarejea Scotland kujiunga na Hamilton Academical Januari mwaka 2001 na miaka mitatu iliyofuata akacheza timu za Exeter City kwa miezi mitatu, Greenock Morton, Harrogate Town, East Stirlingshire na Hamilton Academical kwa mara nyingine kabla ya kustaafu akiwa na Kilwinning Rangers mwaka 2003. Baada ya kutungika daluga zake, Kerr akaenda kufundisha Marekani klabu ya Phoenix, Arizona ambako baada ya kukosa viza ya kuishi nchini humo akalazimika kurejea Scotland, ambako alifanya kazi kama Ofisa Maendeleo wa Argyll na Bute kati ya mwaka 2005 na 2009. Septemba mwaka 2009, Kerr akasaini Mkataba wa kuwa kocha Msaidizi wa Mpumalanga Black Aces ya Afrika Kusini hadi Juni mwaka 2010 alipohamia Thanda Royal Zulu kama Kocha Msaidizi pia, 2011 akaenda Nathi Lions (Msaidizi), 2012 akaenda Khatoco Khanh Hoa (Msaidizi) na mwaka 2012 akasaini Mkataba wa kuwa kocha wa mazoezi utimamu wa mwili (feetness) wa timu ya taifa ya Vietnam. Mwaka 2013 akahamia Hai Phong kama Kocha Msaidizi pia, kabla ya mwaka 2013 kuwa Kocha Mkuu wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 21 ya Hai Phong na mwaka 2014 akawa kocha Mkuu wa Hai Phong, ambayo aliipa ubingwa wa Taifa wa nchi hiyo. Kocha huyo kijana, anakuja Simba SC kurithi mikoba ya Mserbia, Goran Kopunovic ambaye baada ya miezi sita ya kufundisha klabu hiyo akashindwana na uongozi juu ya dau la Mkataba mpya. 
Credit:BIn Zubeiry

Sunday, June 21, 2015

Kamara, Ngoma watua Jangwani kilaini, Azam Mmh!

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/05/donald-ngoma.jpg
Ngoma
http://api.ning.com/files/-hwEeqCyyzcUDSa8niMV*j4Gexh4YMQlbQbOpDDsm5bj8CsNc1iWuShfdoofoJoxVS3yme2QGbewS7taPYct0Vd6GrOaJlx*/2.JPG
Kamara mwenye jezi nyeusi akiwa na wachezaji wenzake wa Yanga
KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limebariki ongezeko la wachezaji wa kigeni kutoka watano hadi saba na kwa maana hiyo imetoa fursa kwa wachezaji waliokuwa wakiwaniwa na Yanga, Donald Ngoma wa Fc Platimuz ya Zimbabwe na Lansana Kamara toka Sierra Leone kuwa na nafasi kubwa ya kukipiga Jangwani.
Kadhalika ongezeko hilo ambalo hata hivyo limeenda kinyume na maombi ya Umoja wa Klabu ya kutaka wachezaji wa kigeni wafikie 10, litazinufaisha Azam na Simba zilizokuwa zikiipigia debe ongezeko hilo. 
Ebu isome mwenyewe taarifa ya TFF juu ya maamuzi yao ya Kamati ya Utendaji iliyokutana jana visiwani Zanzibar

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - RELEASE NO. 101
TAREHE 20 JUNI, 2015
MAAMUZI YA KAMATI YA UTENDAJI
Kamati ya Utendaji ya TFF imefanya kikao chake cha kawaida leo tarehe 20/06/2015 katika ukumbi wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo kisiwani Zanzibar,

Baadhi ya maamuzi yake ni haya yafuatayo:

  1. TUNZO ZA VODACOM.
Baada ya kuzingatia  mapungufu yaliyojitokeza katika uteuzi wa tuzo za ligi kuu ya Vodacom msimu wa 2014/15, Kamati ya utendaji imeagiza Rais wa TFF aunde kamati maalum ya kusimamia mchakato wa utoaji wa tuzo za Vodacom. Kamati hii itazingatia umuhimu wa kuhusisha idara za ufundi za TFF katika zoezi hilo na wadhamini na ligi watahusishwa kwa ukaribu katika zoezi hili.

  1. KANUNI ZA LIGI 2015/16.
Kamati ya utendaji ilipitia rasimu ya kanuni za ligi kuu, FDL na SDL za msimu ujao wa 2015/16.
Mabadiliko makubwa yaliyofanywa ni kwenye maeneo yafuatayo:

  1. LESENI ZA VILABU.
Kamati ya utendaji imesisitiza kuwa hakuna klabu itakayopitishiwa usajili wake kama kupewa leseni ya klabu ya msimu.( Club Licencing).

  1. WAAMUZI.
Kamati ya utendaji imeridhia wazo la kamati ya maamuzi kuwa kuanzia msimu 2015/16 kutakuwa na jopo maalum ya waamuzi ( Elite referees) litakalochezeshwa mechi zote za ligi kuu.

Waamuzi hawa watakuwa ni 16 wa kati, 32 wa pembeni na 4 wa akiba. Hii itasaidia kuongoza ufanisi katika uamuzi. (refereeing).

  1. MGAWANYO WA MAPATO YA MILANGONI.
Vilabu vimeongezwa mgawanyo wa mapato  ya milangoni na sasa vitakuwa vinachukua asilimia 60% ya mapato ya mlangoni, makato mengine ni 18% VAT na 15% gharama za uwanja.

  1. UDHIBITI WA WACHEZAJI.
Kanuni ilikuwa inatoa fursa timu ya kuamua mechi ipi mchezaji asicheze baada ya kuwa na kadi tatu za njano imefutwa.

  1. KUSAJILI MIKATABA YA WACHEZAJI.
Kuanzia sasa mikataba kati ya wachezaji na klabu itakayotambuliwa na TFF itakuwa ni ile ambayo ni nakala halisi zilizopigwa muhuri na lakiri ya TFF  na kusajiliwa kwenye kumbukumbu ya TFF. Vilabu na mwachezaji watapewa nakala hizi baada ya  kusajiliwa na TFF.

  1. WACHEZAJI WA KIGENI.
Kamati ya utendaji imeamua kuwa kuanzia msimu 2015/16 idadi ya wachezaji wa kigeni watakaosajiliwa na klabu ya ligi kuu itakuwa 7 (saba) wachezaji wote hawa, wote wataruhusiwa kucheza kwa wakati wote.

Mikakati ya kusajiliwa wachezaji hawa ni haya yafuatayo:
  1. Mchezaji awe ni mchezaji wa timu za Taifa za nchi yake ( Senior, U23, U20, U19, U17 nk) au
  2. Mchezaji awe anacheza katika ligi kuu ya nchi yake au nchi nyingine wakati anasajiliwa.

  1. Kila mchezaji wa kigeni atakayesajiliwa atalipia ada ya maendeleo. Mpira wa vijana ya dola 2,000 kwa kila msimu atakyocheza hapa nchini. Fedha hizi zitapelekwa katika mfuko wa maendeleo ya mpira (Football Development Fund).

Pia imeamriwa kuwa mikataba ya vilabu na wachezaji iliyo hai itaendelea kutambuliwa na TFF. Na kwa wale ambao tayari wapo nchini wataruhusiwa  kuuhisha (to renew) mikataba yao iwapo watakubaliana na vilabu vyao.

4. LESENI ZA MAKOCHA
Kamati ya utendaji imeamua kuwa kuanzia msimu huu, Kocha wa timu ya ligi kuu sharti awe na leseni B ya CAF au itakayolingana nayo kutoka katika mashirikisho mengine duniani na kocha msaidizi awe na leseni C ya CAF, hii ni kwa misimu mitatu.
Kuanzia msimu wa 2018/2019 kocha wa Ligi Kuu atatakiwa kuwa na leseni A ya CAF au inayolingana na hiyo kutoka katika mashirikisho mengine duniani.

Aidha Kamati ya Utendajji ya TFF imemteua Meshack Bandawe kuwa mjumbe wa bodi ya mfuko wa  maendeleo ya mpira wa miguu - TFF (FDF), Bandawe ni meneja wa PPF kanda ya ziwa.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


Argentina yaifumua Jamaica kidude, yatinga robo fainali

Argentina
Safi sana kijana, Higuain (kulia) akipongezwa na Messi na Di Maria baada ya kufunga bao la mapema

Argentina 4
Messi akikikusanya kijiji kama kawaida yake
Argentina 5
Gonzalo Higuain akishangilia bao lililoivusha Argentina robo fainali za Copa America
BAO la dakika 11 ya Gonzalo Higuain kutokana na pazi murua ya Angel di Maria imeiwezesha Argentina kusonga mbele katika kundi lake kwenye michuano ya Copa America, huku Chile ikiitafanua Bolivia 5-0 na Uruguay na Paraguay wakitoshana nguvu katika mechi nyingine.
Argentina kwa ushindi huo imeongoza kundi lake la B kwa kufikisha pointi saba mbili zaidi ya Paraguay na zote zimesonga mbele hatua ya robo fainali.
Bolivia licha ya kupigwa mkono na Chile, lakini timu hizo mbili zimefuzu hatua ya robo fainali kutoka kundi A, huku kundi C likitarajiwa kutua washindi wao leo sambamba na timu mbili zitakazoungana na zilizofuzu moja kwa moja. Timu tatu za Uruguay, Venezuela na Ecuador zinawania nafasi ya Best Looser katika michuano hiyo.

Utukutu wamponza Neymar, afungiwa mechi nne Copa America

Mshikemshike baada ya Neymar kuzua tafran kwa kupiga mpira ulio 'mbabua' mgongoni mchezaji wa Colombia
Neymar (10) akizozana na wachezaji wa Colombia huku akizuiwa na wenzake wa Brazil
Neymar vurugu
Kwani we unataka nini? Neymar akizozana na wachezaji wa Colombia huku mwamuzi akiteta naye
AMA kweli hasira hasara! Straika tegemeo na nahodha wa timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr anatarajiwa kuikosa michuano ya Copa America inayoendelea nchini Chile baada ya kufungiwa kucheza mechi nne. 
Mshambuliaji huyo wa Barcelona mwenye umri wa miaka 23 alionyeshwa kadi nyekundu kwa kuzozana na wachezaji wa Colombia kufuatia kipigo cha bao bao 1-0 walichopata Brazil katika mchezo wao wa makundi. Mbali na kadi ya moja kwa moja, lakini inadaiwa kuwa Neymar alimtolea lugha ya matusi mwamuzi wa pambano hilo na ndiyo sababu ya kuadhibiwa kukosa mechi nyingine za ziada badala ya moja tu ya kadi aliyopewa.
Nyota huyo tayari anatumikia adhabu ya kutocheza mechi moja hivyo kumfanya kutokuwepo katika mchezo wa mwisho wa makundi dhidi ya Venezuela utakaochezwa usiku wa leo.
Lakini Shirikisho la Soka la Amerika Kusini sasa limepitia tukio hilo na kuongeza adhabu kwa nyota huyo baada ya kudaiwa ripoti ya mwamuzi ilitaarifa kumtusi. 
Mchezaji wa Colombia Carlos Bacca ambaye pia alipewa kadi nyekundu katika tukio hilo naye amepewa adhabu ya kutocheza mechi mbili huku wachezaji wote wakipewa nafasi ya kukata rufani kama hawakuridhika na adhabu.

The Cranes yamfukuzisha kazi kocha Nooij Taifa Stars

Bechi la ufundi
Kocha Stars na wenzake wakati wa wimbo wa Taifa kabla ya kuvaana na Uganda The Cranes
Kocha Nooij akisindikizwa na Polisi mara baada ya filimbi ya mwisho ya mchezo wa timu yake dhidi ya Uganda The Cranes am,bapo Stars ilichapwa mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Na Mwandishi Wetu Zanzibar

SAFARI ya Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeifikia tamati baada ya Kamati ya Utendaji ya TFF, kutangaza kulipiga chini benchi nzima baada ya timu hiyo kucharazwa mabao 3-0 na Uganda The Cranes.
Stars ilitandikwa mabao hayo katika mchezo wa kwanza wa kuwania fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani Rwanda, uliochezwa kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani hapa.
Mara baada ya pambano hilo ambalo lilikuwa la 18 kwa Stars chini ya Kocha Nooij ikiwa imeshinda mechi tatu tu, moja likiwa la mashindano Kamati ya Utendaji ya TFF ilikutana na kutoa taarifa ya kumtimua kocha huyo na wasaidizi wake na taarifa za chini chini zinapasha kuwa Charles Boniface Mkwasa na Abdallah Kibadeni huenda wakapewa timu.

TFF ilimpa kocha Mart Nooij mtihani wa mwisho na endapo atashindwa kuipeleka Taifa Stars, basi atafute njia ya kuondoka baada ya wapenzi wa soka nchini kuchoshwa na ipigo ya timu hiyo.


Wiki iliyopita, Taifa Stars ilipokea kichapo cha idadi kama hiyo cha mabao kutoka kwa Misri katika mchezo wa kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) zitakazofanyika mwaka 2017 nchini Gabon.


Katika mchezo huo ambao Stars ilicheza kama isiyo na mwalimu ilijikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0. bao hilo liliwekwa kimiani na Sekisambo Erisa ambaye alikuja kufunga bao jingine na kufanya aitungie Stars mara mbili na lingine lilifungwa na Miya Farouk.

Kabla ya kuanza mchezo huo, Taifa Stars ilipata pigo baada ya mchezaji wake Oscar Joshua kuugua ghafla na kuukosa mchezo huo.


Kwa mara ya mwisho Stars ilifuzu kwa fainali hizo za Chan mwaka 2009 zilipofanyika kwa mara ya kwanza nchini Iory Coast na ilitolewa katika hatua ya makundi ikiwa chini ya Mbrazil Marcio Maximo.


Mara baada ya pambano hilo mashabiki wenye hasira walitaka kumtandika kocha Nooij kabla ya askari Polisi waliokuwa uwanjani kumuokoa.
Tangu mapema mara baada ya kufungwa bao la kwanza, mashabiki waliibadilika Stars na kuanza kuizomea na kuwafanya wachezaji kupoteza kujiamini na kusababisha kufungwa mabao mengine yaliyoiweka timu hiyo katika wakati mgumu kusonga mbele kwenye michezzo hiyo ya Chan.
Stars na Uganda zitarudiana wiki mbili zijazo na mshindi atakayesonga mbele ataumana na Sudan katika raundi inayofuata.
Chini ni taarifa ya TFF juu ya kusitisha kibarua cha Kocha Nooij.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 20 JUNI, 2015
KAMATI YA UTENDAJI YASITISHA AJIRA YA NOOIJ
Kamati ya utendaji ya Shirikishi la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Katika kikao chake cha leo pamoja na mambo mengine ilipitia mwenendo wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mchezo kati ya Tanzania na Uganda, kama sehemu ya tathmin ya mwenendo wa timu.

Kamati ya utendaji kwa kauli moja imeamua yafuatayo:

1.Ajira ya Kocha Mkuu Maart Nooij inasitishwa mara moja kuanzia  tarehe 21/June/2015.

2.Benchi lote la ufundi la Taifa stars limevunjwa kuanzia tarehe 21/06/2015.

3.Uongozi wa TFF utatangaza punde benchi jipya la ufundi la timu ya Taifa.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Wednesday, June 17, 2015

Boateng kurejea tena San Siro

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/06/26/article-2670725-1F2594FC00000578-295_634x645.jpgTENA? Aah haiwezekani! Wakala wa Kevin-Prince Boateng amethibitisha kuwa kiungo huyo anaweza kujiunga tena na AC Milan katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ghana alikaa San Siro kwa miaka mitatu na kufanikiwa kushinda taji la Serie A katika msimu wake wa kwanza kabla ya kuondoka kwenda Schalke ya Ujerumani Agosti mwaka 2013. 
Hata hivyo, Boateng anataka kuondoka Schalke baada ya kusimamishwa na klabu hiyo Mei 11 mwaka huu kufuatia kichapo walichopata dhidi ya Koln. 
Wakala wa Boateng, Federico Pastorello amesema kwa sasa wanasubiri ofa, lakini akakiri kuwa uwezekano wa kurejea Milan ni mkubwa. 
Milan baada ya kumtimua kocha Filippo Inzaghi 'Pippo' na kumuajiri Sinisa Mihajlovic, inategemewa kutenga fungu kubwa kwa ajili ya usajili kiangazi hiki ili kurejesha makali yao baada ya kumaliza msimu wa Serie wakiwa nafasi ya 10.

Man City yaongeza dau kwa Sterling

http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2014/1002/soc_g_sterling_jv_1296x1296.jpg&w=1500&h=1500&scale=crop&site=espnfcBAADA ya kukaushiwa kimtindo na Liverpool, klabu ya Manchester City imeongeza ofa yao kufikia Pauni Milioni 35.5 kwa ajili ya kumwania Raheem Sterling,
Ofa ambayo kuna uwezekano pia wa kukataliwa na Liverpool kwani klabu hiyo wanamthaminisha mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza kuwa thamani ya ya Pauni Milioni 50. 
Wiki iliyopita Liverpool walikataa ofa ya Pauni Milioni 25 iliyotolewa na City kwa ajili ya nyota huyo. 
Sterling alijiunga na Liverpool akitokea Queens Park Rngers mwaka 2010 na bado ana mkataba na Liverpool unaomalizika mwaka 2017 pamoja na kukataa mkataba mpya ambao ungemuwezesha kulipwa kitita cha Pauni 100,000 kwa wiki. 
Meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers amesema mwezi uliopita kuwa anategemea Sterling kubakia Anfield mpaka atakapomaliza mkataba wake.

Copy and WIN : haundi milioni 35.5 kwa ajili ya kumuwania Raheem Sterling, ofa ambayo kuna uwezekano pia wa kukataliwa na Liverpool. Liverpool wanamthaminisha mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza kuwa thamani ya ya paundi milioni 50. Wiki iliyopita Liverpool walikataa ofa ya paundi milioni 25 iliyotolewa na City kwa ajili ya nyota huyo. Sterling alijiunga na Liverpool akitokea Queens Park Rngers mwaka 2010 na bado ana mkataba na Liverpool unaomalizika mwaka 2017 pamoja na kukataa mkataba mpya ambao ungemuwezesha kulipwa kitita cha paundi 100,000 kea wiki. Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amesema mwezi uliopita kuwa anategemea Sterling kubakia Anfield mpaka atakapomaliza mkataba wake.

 and WIN : h

RATIBA YA LIGI KUU YA ENGLAND 2015-2016 HII HAPA



http://www.hdwallpapersinn.com/wp-content/uploads/2014/08/chelsea-football-club-full-team-celebrations-hd-wallpapers.jpg
Watetezi wa Ligi Kuu ya England

http://www.totalsportek.com/wp-content/uploads/2015/03/Premier-League-Fixtures.jpgRATIBA ya awali ya Ligi Kuu ya England, msimu wa 2015-2016 imetolewa ambapo watetezi wa taji hilo Chelsea wataanzia nyumbani dhidi ya Swansea City na itakuwa ni ukaribisho mzuri wa Andre Ayew Pele.
Mchezaji huyo wa Ghana amesajiliwa na Swansea na pambano hilo litakuwa kipimo tosha kwake kuonyesha kama anahimili ligi hiyo ya EPL.
Mashetani Wekundu wenyewe wataanzia pia nyumbani dhidi ya vijogoo vya London Kaskazini, Tottenham Hotspur, huku Arsenal nao wataanza kwa kupepetana na West Ham United na Liverpool na Manchester City zote kila mmoja zitaanzia ugenini katike mechi zao za kwanza Agopsti 8.

Ratiba kamili ya awali ya ligi hiyo imekaa hivi:



Jumamosi, Agosti 8, 2015

AFC Bournemouth   v Aston Villa

 Arsenal          v West Ham

 Chelsea          v Swansea City

 Everton          v Watford

 Leicester City   v Sunderland

 Man United       v Tottenham

 Newcastle v Southampton

 Norwich City     v Crystal Palace

 Stoke City       v Liverpool

 West Brom  v Man City



Jumamosi, Agosti 15, 2015

Aston Villa       v Man United

Crystal Palace    v Arsenal

Liverpool         v AFC Bournemouth

Man City          v Chelsea

Southampton       v Everton

Sunderland v Norwich City

Swansea City      v Newcastle

Tottenham  v Stoke City

Watford           v West Brom

West Ham    v Leicester City



Jumamosi, Agosti 22, 2015

Arsenal           v Liverpool

Crystal Palace    v Aston Villa

Everton           v Man City

Leicester City    v Tottenham

Man United v Newcastle

Norwich City      v Stoke City

Sunderland v Swansea City

Watford           v Southampton

West Brom   v Chelsea

West Ham    v AFC Bournemouth



Jumamosi, Agosti 29, 2015

AFC Bournemouth   v Leicester City

Aston Villa       v Sunderland

Chelsea           v Crystal Palace

Liverpool         v West Ham

Man City          v Watford

Newcastle   v Arsenal

Southampton       v Norwich City

Stoke City        v West Brom

Swansea City      v Man United

Tottenham   v Everton



Jumamosi, Septemba 12, 2015

Arsenal           v Stoke City

Crystal Palace    v Man City

Everton           v Chelsea

Leicester City    v Aston Villa

Man United v Liverpool

Norwich City      v AFC Bournemouth

Sunderland v Tottenhamr

Watford           v Swansea City

West Brom   v Southampton

West Ham    v Newcastle





Jumamosi, Septemba 19, 2015

AFC Bournemouth   v Sunderland

Aston Villa       v West Brom

Chelsea           v Arsenal

Liverpool         v Norwich City

Man City          v West Ham

Newcastle   v Watford

Southampton       v Man United

Stoke City        v Leicester City

Swansea City      v Everton

Tottenham   v Crystal Palace





Jumamosi, Septemba 26, 2015

Leicester City    v Arsenal

Liverpool         v Aston Villa

Man United v Sunderland

Newcastle   v Chelsea

Southampton       v Swansea City

Stoke City        v AFC Bournemouth

Tottenham   v Man City

Watford           v Crystal Palace

West Brom   v Everton

West Ham    v Norwich City





Jumamosi, Oktoba 3, 2015

AFC Bournemouth   v Watford

Arsenal           v Man United

Aston Villa       v Stoke City

Chelsea           v Southampton

Crystal Palace    v West Brom

Everton           v Liverpool

Man City          v Newcastle

Norwich City      v Leicester City

Sunderland v West Ham

Swansea City      v Tottenham





Jumamosi, Oktoba 17, 2015

Chelsea           v Aston Villa

Crystal Palace    v West Ham

Everton           v Man United

Man City          v AFC Bournemouth

Newcastle  v Norwich City

Southampton       v Leicester City

Swansea City      v Stoke City

Tottenham  v Liverpool

Watford           v Arsenal

West Brom   v Sunderland



Jumamosi, Oktoba 24, 2015

AFC Bournemouth   v Tottenham

Arsenal           v Everton

Aston Villa       v Swansea City

Leicester City    v Crystal Palace

Liverpool         v Southampton

Man United v Man City

Norwich City      v West Brom

Stoke City        v Watford

Sunderland v Newcastle

West Ham    v Chelsea



Jumamosi, Oktoba 31, 2015

Chelsea           v Liverpool

Crystal Palace    v Man United

Everton           v Sunderland

Man City          v Norwich City

Newcastle   v Stoke City

Southampton       v AFC Bournemouth

Swansea City      v Arsenal

Tottenham   v Aston Villa

Watford           v West Ham

West Brom   v Leicester City



Jumamosi, Novemba 7, 2015

AFC Bournemouth   v Newcastle

Arsenal           v Tottenham

Aston Villa       v Man City

Leicester City    v Watford

Liverpool         v Crystal Palace

Man United v West Brom

Norwich City      v Swansea City

Stoke City        v Chelsea

Sunderland v Southampton

West Ham    v Everton



Saturday, November 21st, 2015

Chelsea           v Norwich City

Crystal Palace    v Sunderland

Everton           v Aston Villa

Man City          v Liverpool

Newcastle  v Leicester City

Southampton       v Stoke City

Swansea City      v AFC Bournemouth

Tottenham   v West Ham

Watford           v Man United

West Brom   v Arsenal



Jumamosi, Novemba 28, 2015

AFC Bournemouth   v Everton

Aston Villa       v Watford

Crystal Palace    v Newcastle

Leicester City    v Man United

Liverpool         v Swansea City

Man City          v Southampton

Norwich City      v Arsenal

Sunderland v Stoke City

Tottenham   v Chelsea

West Ham          v West Brom



Jumamosi, Desemba 5, 2015

Arsenal           v Sunderland

Chelsea           v AFC Bournemouth

Everton           v Crystal Palace

Man United v West Ham

Newcastle  v Liverpool

Southampton       v Aston Villa

Stoke City        v Man City

Swansea City      v Leicester City

Watford           v Norwich City

West Brom   v Tottenham



Jumamosi, Desemba 12, 2015

AFC Bournemouth   v Man United

Aston Villa       v Arsenal

Crystal Palace    v Southampton

Leicester City    v Chelsea

Liverpool         v West Brom

Man City          v Swansea City

Norwich City      v Everton

Sunderland v Watford

Tottenham  v Newcastle

West Ham    v Stoke City



Januari, Desemba 19, 2015

Arsenal           v Man City

Chelsea           v Sunderland

Everton           v Leicester City

Man United v Norwich City

Newcastle   v Aston Villa

Southampton       v Tottenham

Stoke City        v Crystal Palace

Swansea City      v West Ham

Watford           v Liverpool

West Brom   v AFC Bournemouth



Jumamosi, Desemba 26, 2015

AFC Bournemouth   v Crystal Palace

Aston Villa       v West Ham

Chelsea           v Watford

Liverpool         v Leicester City

Man City          v Sunderland

Newcastle   v Everton

Southampton       v Arsenal

Stoke City        v Man United

Swansea City      v West Brom

Tottenham   v Norwich City



Jumatatu, Desemba 28, 2015

Arsenal           v AFC Bournemouth

Crystal Palace    v Swansea City

Everton           v Stoke City

Leicester City    v Man City

Man United v Chelsea

Norwich City      v Aston Villa

Sunderland v Liverpool

Watford           v Tottenham

West Brom   v Newcastle

West Ham    v Southampton



Jumamosi, Januari 2, 2016

Arsenal           v Newcastle

Crystal Palace    v Chelsea

Everton           v Tottenham

Leicester City    v AFC Bournemouth

Man United v Swansea City

Norwich City      v Southampton

Sunderland v Aston Villa

Watford           v Man City

West Brom   v Stoke City

West Ham    v Liverpool



Jumanne, Januari 12, 2016

AFC Bournemouth   v West Ham

Aston Villa       v Crystal Palace

Liverpool         v Arsenal

Swansea City      v Sunderland



Jumatano, Januari 13, 2016

Chelsea           v West Brom

Man City          v Everton

Newcastle   v Man United

Southampton       v Watford

Stoke City        v Norwich City

Tottenham   v Leicester City



Jumamosi, Januari 16, 2016

AFC Bournemouth   v Norwich City

Aston Villa       v Leicester City

Chelsea           v Everton

Liverpool         v Man United

Man City          v Crystal Palace

Newcastle   v West Ham

Southampton       v West Brom

Stoke City        v Arsenal

Swansea City      v Watford

Tottenham   v Sunderland



Jumamosi, Januari 23, 2016

Arsenal           v Chelsea

Crystal Palace    v Tottenham

Everton           v Swansea City

Leicester City    v Stoke City

Man United v Southampton

Norwich City      v Liverpool

Sunderland v AFC Bournemouth

Watford           v Newcastle

West Brom   v Aston Villa

West Ham    v Man City



Jumanne, Februari 2, 2016

Arsenal           v Southampton

Crystal Palace    v AFC Bournemouth

Leicester City    v Liverpool

Man United v Stoke City

Norwich City      v Tottenham

Sunderland v Man City

Watford           v Chelsea

West Brom   v Swansea City

West Ham    v Aston Villa



Jumatano, Februari 3, 2016

Everton           v Newcastle



Jumamosi, Februari 6, 2016

AFC Bournemouth   v Arsenal

Aston Villa       v Norwich City

Chelsea           v Man United

Liverpool         v Sunderland

Man City          v Leicester City

Newcastle  v West Brom

Southampton       v West Ham

Stoke City        v Everton

Swansea City      v Crystal Palace

Tottenham   v Watford



Jumamosi, Februari 13, 2016

AFC Bournemouth   v Stoke City

Arsenal           v Leicester City

Aston Villa       v Liverpool

Chelsea           v Newcastle

Crystal Palace    v Watford

Everton           v West Brom

Manchester City   v Tottenham

Norwich City      v West Ham

Sunderland v Man United

Swansea City      v Southampton



Jumamosi, Februari 27, 2016

Leicester City    v Norwich City

Liverpool         v Everton

Man United v Arsenal

Newcastle   v Man City

Southampton       v Chelsea

Stoke City        v Aston Villa

Tottenham   v Swansea City

Watford           v AFC Bournemouth

West Brom   v Crystal Palace

West Ham          v Sunderland





Jumanne, Machi 1, 2016

AFC Bournemouth   v Southampton

Arsenal           v Swansea City

Aston Villa       v Everton

Leicester City    v West Brom

Liverpool         v Man City

Man United v Watford

Norwich City      v Chelsea

Sunderland v Crystal Palace

West Ham          v Tottenham



Jumatano, Machi 2, 2016

Stoke City        v Newcastle



Jumamosi, Machi 5, 2016

Chelsea           v Stoke City

Crystal Palace    v Liverpool

Everton           v West Ham

Man City          v Aston Villa

Newcastle   v AFC Bournemouth

Southampton       v Sunderland

Swansea City      v Norwich City

Tottenham   v Arsenal

Watford           v Leicester City

West Brom   v Man United



Jumamosi, Machi 12, 2016

AFC Bournemouth   v Swansea City

Arsenal           v West Brom

Aston Villa       v Tottenham

Leicester City    v Newcastle

Liverpool         v Chelsea

Man United v Crystal Palace

Norwich City      v Man City

Stoke City        v Southampton

Sunderland v Everton

West Ham    v Watford



Jumamosi, Machi 19, 2016

Chelsea           v West Ham

Crystal Palace    v Leicester City

Everton           v Arsenal

Man City          v Man United

Newcastle   v Sunderland

Southampton       v Liverpool

Swansea City      v Aston Villa

Tottenham   v AFC Bournemouth

Watford           v Stoke City

West Brom   v Norwich City



Jumamosi, Aprili 2, 2016

AFC Bournemouth   v Man City

Arsenal           v Watford

Aston Villa       v Chelsea

Leicester City    v Southampton

Liverpool         v Tottenham

ManUnited   v Everton

Norwich City      v Newcastle

Stoke City        v Swansea City

Sunderland v West Brom

West Ham    v Crystal Palace





Jumamosi, Aprili 9, 2016

 Aston Villa      v AFC Bournemouth

 Crystal Palace   v Norwich City

 Liverpool        v Stoke City

 Man City         v West Brom

 Southampton      v Newcastle

 Sunderland       v Leicester City

 Swansea City     v Chelsea

 Tottenham  v Man United

 Watford          v Everton

 West Ham   v Arsenal



Jumamosi, Aprili 16, 2016

 AFC Bournemouth v Liverpool

 Arsenal          v Crystal Palace

 Chelsea          v Man City

 Everton          v Southampton

 Leicester City   v West Ham

 Man United       v Aston Villa

 Newcastle v Swansea City

 Norwich City     v Sunderland

 Stoke City       v Tottenham

 West Brom v Watford





Jumamosi, Aprili 23, 2016

AFC Bournemouth   v Chelsea

 Aston Villa      v Southampton

 Crystal Palace   v Everton

 Leicester City   v Swansea City

 Liverpool        v Newcastle United

 Man City         v Stoke City

 Norwich City     v Watford

 Sunderland       v Arsenal

 Tottenham v West Brom

 West Ham   v Manch United





Jumamosi, Aprili 30, 2016

Arsenal           v Norwich City

Chelsea           v Tottenham

Everton           v AFC Bournemouth

Man United v Leicester City

Newcastle   v Crystal Palace

Southampton       v Man City

Stoke City        v Sunderland

Swansea City      v Liverpool

Watford           v Aston Villa

West Brom   v West Ham





Jumamosi, Mei 7, 2016

AFC Bournemouth   v West Brom

Aston Villa       v Newcastle

Crystal Palace    v Stoke City

Leicester City    v Everton

Liverpool         v Watford

Man City          v Arsenal

Norwich City      v Man United

Sunderland v Chelsea

Tottenham   v Southampton

West Ham    v Swansea City

 

Jumapili, Mei 15, 2016

Arsenal           v Aston Villa

Chelsea           v Leicester City

Everton           v Norwich City

Man United v AFC Bournemouth

Newcastle   v Tottenham

Southampton       v Crystal Palace

Stoke City        v West Ham

Swansea City      v Man City

Watford           v Sunderland

West Brom   v Liverpool