STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 25, 2014

Enyeama aitahadharisha CAF kuhusu AFCON 2015

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Mali+v+Nigeria+2013+Africa+Cup+Nations+Semi+afU4DoYXKi0x.jpg
Vincent Enyeama
NAHODHA na kipa tegemeo wa timu ya taifa ya Nigeria 'Super Eagles', Vincent Enyeama amelitaka Shirikisho la Soka la Afrika, CAF kusitisha michuano ya Mataifa ya Afrika, AFCON 2015.
Michuano hiyo ilitarajiwa kufanyika Januari mwakani nchini Morocco kabla ya wenyeji hao kuchomoa kwa hofu ya ugonjwa wa Ebola.
Enyeama anayekipiga katika klabu ya Lille, alifafanua kuwa michuano hiyo inapaswa kusitishwa kutokana na wasiwasi juu ya ugonjwa wa Ebola kuongezeka. 
Enyeama,32, ameeleza woga wake kuwa ugonjwa huo ambao umeshaua zaidi ya watu 4,500 mpaka sasa utasambaa zaidi kufuatia mkusanyiko wa watu watakaokuwepo viwanjani. 
Nyota huyo aliongeza kuwa hatari ni kubwa kama AFCON itaandaliwa wakati huu ambapo bado ugonjwa huo haujadhibitiwa, lakini amesema atashiriki kama nchi yake itafuzu michuano hiyo pamoja na hatari iliyopo.

No comments:

Post a Comment