STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 25, 2014

Mtibwa yarejea kileleni, Rama Salum, Okwi, Tegete 'ambeep' Kavumbagu

Rama Salim (kushoto) na Emmanuel Okwi ambao wameendelea kufunga mabao katika Ligi Kuu na kumbeep Didier Kavumbagu
WAKATI Mtibwa Sugar ikirejea kileleni bila kutoka jasho leo, Mgambo JKT imejinasua mkiani na kuiachia msala timu ya Polisi Moro, huku kiungo mshambuliaji nyota wa Coastal Union, Rama Salum akimwashia 'endketa' mshambuliaji wa Azam, Didier Kavumbagu baada ya kufikisha bao la tatu leo.
Rama alifunga bao la kusawazisha la Coastal na kumfanya kushika nafasi ya pili akilingana na Ally Shomar wa Mtibwa wakiwa na mabao matatu, moja pungufu dhidi ya manne ya Kavumbagu.
Kadhalika Jerry Tegete ameanza na moto baada ya magoli yake mawili aliyofunga leo Shinyanga yamemfanya kuingia kwenye orodha ya wanaowania Kiatu cha Dhahabu.
Mshambuliaji huyo ameungana na wachezaji wengine saba kushika nafasi ya tatu sambamba na Emmanuel Okwi aliyefunga jioni ya leo dhidi ya Prisons-Mbeya.
Wakati katika mbio za ufungaji bora ikiwa hivyo, Mtibwa itakayoshuka dimbani kesho ugenini ikiwa ni kati ya timu mbili ambazo hazijaonja machungu ya kipigo sambamba na Simba, itaumana na Mbeya City baada ya kurejea kileleni kutokana na uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Awali Azam waliwatangulia kwa faida ya herufi A wakiwa wamelingana kila kitu kabla ya leo kutibuliwa na JKT Ruvu waliowafumua bao 1-0 uwanja wa Chamazi na kushuka had nafasi ya pili licha ya timu kuwa na pointi 10 sawa na Yanga ambayo imerejea nafasi ya tatu.
Hata hivyo Mtibwa ina nafasi nzuri kwa vile ina mchezo mmoja mkononi kulinganisha na wenzake waliocheza mechi tano kila moja dhidi ya nne za Mtibwa.
Matokeo mengine ya ligi hiyo jioni ya leo imebadilisha msimamo maeneo ya kati na mkiani baada ya Mgambo kujinasua mkiani kwa kushinda 1-0 dhidi ya Ndanda na kufikisha pointi sita zilizowapeleka hadi nafasi ya nane wakilingana na Kagera Sugar waliolazimishwa sare ya 1-1 na Coastal.
Nazo timu za maafande wa JKT, Ruvu Shooting na JKT Ruvu zimefanikiwa kupanda hadi kwenye nafasi ya tano na sita kwa kufikisha pointi 7 baada ya kupata ushindi wa pili mfululizo timu zote hizo zikiwa zinalingana kwa kila kitu isipokuwa wakitenganishwa kwa herufi zao za mwanzo, JKT wakiitangulia Ruvu.
Unaweza kuuchungulia msimamo wa ligi hiyo na orodha ya wafungaji kujionea mwenyewe.

MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                              P    W    D   L    F    A   GD  Pts
01. Mtibwa Sugar    04  03  01  00  06  01  05  10
02. Azam                05  03  01  01  06  02  04  10
03. Yanga               05  03  01  01  07  04  03  10
04. Coastal Union   05  02  02   01  07  05  02  08
05. JKT Ruvu          05  02  01  02   04  05  -1  07
06. Ruvu Shooting  05  02  01   02  04  05  -1  07
07. Kagera Sugar    05  01  03   01  04  03  01 06
08.  Mgambo JKT    05  02  00  03   02  04  -2  06
09. Prisons              05 01  02   02  05  05  00  05
10. Simba               05  00  05   00  05  05  00 05
11. Mbeya City        04  01  02  01   01  01  00  05
12. Stand Utd          05 01  02   02  03   08  -5  05
13. Ndanda Fc         05  01  00  04   07  10  -3  03
14. Polisi Moro         05  00  03  02   03  06  -3  03

Wafungaji Bora:

4- Didier Kavumbagu(Azam)
3-
Ally Shomari (Mtibwa), Rama Salum (Coastal)
2-
Shaaban Kisiga, Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Ame Ally (Mtibwa), Rashid Mandawa, Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam), Jabir Aziz (JKT Ruvu), Jerry Tegete (Yanga)

No comments:

Post a Comment