STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 25, 2014

Real Madrid yaizamisha Barcelona 3-1, Suarez aanza vibaya

Karim Benzema scores Real Madrid's third in the win over Barcelona
Benzema akifunga bao la tatu la Real Madrid
Neymar gave Barcelona the lead after just four minutes with Suarez providing the assist at the Bernabeu
Neymar akishangilia bao lake la mapema kabla ya Real  Madrid kuwageuzia kibao
Ronaldo takes his penalty in the 35th minute to bring Real Madrid level in the El Clasico tie against Barcelona on Saturday
Ronaldo akifunga penati yake
Real Madrid players react after Pepe gave them the lead against Barcelona on Saturday evening at the Bernabeu
Real wakishangilia bao la pili lililofungwa na Pepe
Pepe (right) was able to gift Real Madrid an important lead against Barcelona in the El Clasico showdown on Saturday
Piga Keleleeee Pepe akishangilia bao lake
Real Madrid's Ronaldo and Benzema celebrate sealing the El Clasico win at the Bernabeu in front of their own fans against Barcelona
Benzema akipongezwa na Ronaldo kwa bao lake la tatu
Barcelona held the lead until the 35th minute after Neymar's early goal in the El Clasico tie against Real Madrid
Messi akimpongeza Neymar kwa bao la mapema lililokuwa la kufutia machozi kwao
Lionel Messi (right) looks frustrated during the El Clasico match as Real Madrid's Ronaldo (left) beat his Barcelona opponent on Saturday
Messi hoi mbele ya Ronaldo
REAL Madrid wakiwa uwanja wa nyumbani wa Santiago Bernabeu wameizamisha wapinzani wao wa jadi, Barcelona iliyoshuka dimbani kwa mara ya kwanza wakiwa na nyota wao Luis Suarez kwa mabao  3-1 katika pambano la La Liga.
Barcelona walianza kwa mkwara kwa kuandika bao la kuongoza katika dakika ya nne kupitia kwa Neymar akimalizia kazi nzuri ya Suarez aliyekuwa akicheza kwa mara ya kwanza katika Ligi Kuu ya Hispania akitokea kifungoni.
Hata hivyo Cristiano Ronaldo aliendeleza rekodi yake ya kufunga mabao katika ligi hiyo kwa kufunga bao la kusawazisha katika dakika ya 35 kwa mkwaju wa penati na kufikisha bao la 16 katika mechi 9 za ligi hiyo.
Mabao mengine ya Real Madrid yalifungwa na Pepe katika dakika ya 50  kwa kichwa akimalizia mpira uliopigwa na Tom Kroos kabla ya Karim Benzema kuongeza bao la tatu lililowanyong;onyesha Barcelona na kuvunja rekodi yao ya kutopoteza katika ligi ya msimu huu.
Benzema alifunga bao hilo katika dakika ya 61 akimalizia kazi nzuri ya James Rodriguez na kuwapa Real Madrid ushindi uliowafanya wafikishe jumla ya pointi21 na kushika nafasi ya pili wakitofautiana pointi moja na Barcelona wenye pointi 22.

No comments:

Post a Comment