STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 20, 2014

Liverpool yashinda ugenini, Stoke yaua, Man U kazi leo






KLABU ya Liverpool imepata ushindi wa kushangaza ugenini baada ya kuilaza QPR mabao 3-2, huku mabao yake mawili yakitokana na kujifungwa kwa mabeki wa timu wenyeji.
Vijana hao wa Brendan Rodgers, walianza kutangulia kufunga baada ya beki wa QPR Richard Dunne kujifunga katika dakika ya 67 kabla ya mtokea benchi  Vargas kuisawazishia wenyeji katika dakika ya 87 na kuongeza la pili dakika 90.
Hata hivyo Coutinho wa Liverpool aliiandika timu yake bao la pili na Steven Caulker akajifunga kwenye dakika za nyongeza na kuwapa LIverpool ushindi huo muhimu.
Katika pambano jingine la ligi hiyo timu ya Stoke City ikiwa nyumbani iliinyoosha Swansea City kwa kuilaza mabao 2-1. Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea leo Jumatatu wakati Manchester United wastakapokuwa ugenini kuwakabiliWest Bromwich Albion kusaka pointi tatu zitakazowaingiza kwenye Nne Bora kwa mara ya kwanza msimu huu.

No comments:

Post a Comment