STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 20, 2014

Wiki 2 ngumu kwa Simba na Yanga VPL, kipimo cha Maximo, Phiri

Simba na Yanga zilipokuatana zenyewe siku ya Jumamosi na kushindwa kutambiana uwanja wa Taifa
Makipa wa Simba na Yanga, Peter Manyika na Deo Munishi 'Dida' wakipongezana
Kazi tumeimaliza kati yetu sasa tuangalie mechi zetu zijazo, makocha Marcio Maximo na Patrick Phiri wakisalimiana
BAADA ya kumalizana wenyewe kwa wenyewe, Watani wa Jadi wa Soka Tanzania, Simba na Yanga zinaanza wiki mbili ngumu kwao katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara wakati wakatapokabiliwa na mechi ngumu ambazo zinaweza kubadili muelekeo wa klabu hizo.
Yanga wanaokamata nafasi ya nne kwa sasa katika msimamo itakuwa na mechi ngumu mbili mfululizo kuanzia Jumamosi hii kwa kuumana na Stand United mjini Shinyanga kabla ya kuvaana tena na Kagera Sugar ambao wamekuwa wakiwatesa mara kadhaa wakiwafuata uwanja wa Kaitaba.
Iwapo Yanga itashinda mechi hizo za ugenini au kumaliza salama bila kupoteza itakuwa imevuka kikwazo cha mbio zake za ubingwa msimu huu.
Stand United licha ya kuwa ni timu ngeni katika ligi baada ya kupata msimu huu, lakini haitabiriki kwani iliwabania Simba uwanja wa Taifa kwa kutoka nao sare ya 1-1, kadhalika Kagera Sugar haitabiriki kabisa.
Wakati Yanga wakiwa na kibarua hicho, watani zao wenyewe wataanza wiki hii kwa kucheza ugenini kama Yanga kwa kuwafuata Prisons-Mbeya ambayo imekuwa ikisumbua kwenye uwanja wa Sokoine.
Baada ya kibarua hicho Simba itasafiri hadi Morogoro kuwafuata Mtibwa Sugar ambao wamekuwa wakiwajeruhi kwenye uwanja wa Jamhuri kila wakikutana.
Simba yenye pointi nne kama Prisons haijaonja ushindi katika ligi ya msimu huu, hivyo watakuwa na kazi ngumu kuhakikisha wanavunja mwiko wa kucheza mechi 10 za ligi tangu msimu uliopita bila kushinda.
Hata hivyo tayari benchi la ufundi na viongozi wa klabu hiyo ya Msimbazi imekuwa ikisisitiza kuwa mambo yanaelekea kutengemaa na kwamba mashabiki wao watarajie faraja ya kuonja ushindi katika mechi zijazo
Baada ya mechi za mwishoni mwa wiki MICHARAZO inakuletea msimamo kamili wa sasa wa ligi hiyo sambamba na mechi zitakazofuata katika ligi hiyo inayozidi kuchanja mbuga.

MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                              P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Azam               04  03  01  00  06  01  +5   10
02. Mtibwa Sugar   04  03  01  00  06  01  +5   10
03.Coastal Union    04  02  01  01  06  04  02    07
04.Yanga                04  02   01  01  04  04  00   07
05. Kagera Sugar   04  01  02   01  03  02 +1   05
06. Mbeya City       04  01  02  01  01   01  00   05
07.Stand Utd         04  01  02   01  03   05  -2   05
08.Prisons             04  01  01   02  04   04  00   04
09.Simba               04  00  04   00  04    04  00  04
10. JKT Ruvu         04  01  01  02   03   05   -2  04
11. Ruvu Shooting 04  01  01   02  03   05   -2  04
12. Ndanda Fc       04  01  00   03  07    09  -2  03
13. Polisi Moro       04  00  03  01   03    05   -2  03
14. Mgambo JKT    04  01  00  03   01    04  -3  03
RATIBA

Okt 25, 2004
Stand United v Yanga (Kambarage-Shinyanga)
Azam  v JKT Ruvu (Chamazi-Dar es Salaam)
Prisons-Mbeya vs Simba (Sokoine-Mbeya)
Ndanda v Mgambo JKT (Nangwanda Sijaona-Mtwara)
Kagera Sugar v Coastal Union (Kaitaba-Bukoba)
Ruvu Shooting v Polisi Moro (Mabatini-Mlandizi)

Okt 26, 2014
Mbeya City v Mtibwa Sugar (Sokoine-Mbeya)
 

Nov 1, 2014 
Kagera Sugar v Yanga (Kaitaba-Bukoba)
Coastal Union v Ruvu Shooting (Mkwakwani-Tanga)
JKT Ruvu vs Polisi Moro (Chamazi-Dar es Salaam)
Ndanda Fc Azam (Nangwanda Sijaona-Mtwara)
Stand Utd v Prisons-Mbeya (Kambarage-Shinyanga)
Mtibwa Sugar v Simba (Jamhuri-Morogoro)
 

Nov 2, 2014
Mgambo JKT vs Mbeya City (Mkwakwani-Tanga)

No comments:

Post a Comment