STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 11, 2012

NMB YAKABIDHI MADAWATI SHULE YA MSINGI VICTORIA


Meneja wa benki ya NMB tawi la NMB House Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akikabidhi madawati 25 yenye thamani ya shilingi milioni 5 kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Victoria Bw. Sufini Mbwambo iliyopo Dar es Salaam wiki iliyopita.Aanayeshuhudia tukio hilo ni Afisa wa tawi la NMB House Jane Mubezina pamoja na mmoja wa maafisa wa Elimu.
 
Meneja wa tawi la NMB House  Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akiwa pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria pamoja na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Sufini Mbwambo (kulia) wakati wa makabidhiano ya madati yenye thamani ya shilingi milioni 5, jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria wakiimba nyimbo kushukuru benki ya NMB kwa msaada wa madawati waliyotoa shuleni hapo

NMB YAKABIDHI MADAWATI SHULE YA MSINGI VICTORIA


Meneja wa benki ya NMB tawi la NMB House Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akikabidhi madawati 25 yenye thamani ya shilingi milioni 5 kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Victoria Bw. Sufini Mbwambo iliyopo Dar es Salaam wiki iliyopita.Aanayeshuhudia tukio hilo ni Afisa wa tawi la NMB House Jane Mubezina pamoja na mmoja wa maafisa wa Elimu.
 
Meneja wa tawi la NMB House  Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akiwa pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria pamoja na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Sufini Mbwambo (kulia) wakati wa makabidhiano ya madati yenye thamani ya shilingi milioni 5, jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria wakiimba nyimbo kushukuru benki ya NMB kwa msaada wa madawati waliyotoa shuleni hapo

JOKHA KASSIM Mwimbaji wa taarabu anayetamba na T-Moto


Jokha Kassim
 
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
UKIPATA bahati ya kuusikia wimbo wa Riziki Mafungu Saba, hakika utaanza kuupenda muziki wa taarabu, hata kama awali hujaupenda.
 
Ni wimbo mzuri. Wenye mashairi mazito na yenye ujumbe murua, unaoelezea jinsi riziki zinavyopangwa na Mungu na wala sio binadamu, wakiwamo wenye roho mbaya.
 
Wimbo huo umeimbwa na mwanamama Jokha Kassim, alipokuwa na kundi zima la Zanzibar Stars Modern Taarab.
 
Kwa sasa Jokha anafanya kazi katika kundi zima la Tanzania Moto Modern Taarab, maarufu kama T-Moto, lenye wakali wengine kibao.
 
Tayari Jokha amerekodi wimbo unaokwenda kwa jina la ‘Domo la Udaku’, ukiwa ni ujio mpya wa kundi hilo la taarabu nchini.
 
Mwimbaji huyo juzi alifanya mazungumzo na Fiesta Magazine na kusema kuwa muziki ni kipaji chake, alichobarikiwa na Mungu.
 
Cheche zake zilianza kuonekana tangu zamani, alipokuwa hodari sana wa kuimba nyimbo mbalimbali za taarabu.
 
“Muziki huu ni kipaji changu, tangu zamani niliweza kuimba kwa ufanisi na kushangaza wengi waliokuwa wakiona mahala popote.
 
“Nashukuru, leo hii nimeweza kufanya juhudi na kufika T-Moto, ikiwa ni baada ya kujulikana nilipofanya kazi na Zanzibar Stars kwa mafanikio makubwa,” alisema.
 
Licha ya kuanza zamani kuimba, lakini alianza kuingia kwenye kundi la muziki mwaka 2002, alipohitajiwa na uongozi wa Zanzibar Stars na kumtambulisha kimuziki.
 
Kilichomkwamisha kuingia mapema kwenye sanaa ni kukatazwa na wazazi wake, hivyo kusubiri hadi mwaka huo alipoanza kushika kipaza sauti na kurindimisha sauti yake.
 
Jokha alikuwa mke wa kwanza wa Mfalme, Mzee Yusuph, ila kwa sasa wameachana na kila mmoja anaishi kivyake.
 
Siku chache baada ya kuachana na mzee Yusuph, hamu ya kuimba ilimtesa, hivyo kuamua kufanya harakati za kuibua kipaji chake.
 
Jokha na Mzee Yusuph wamezaa mtoto mmoja, ambaye pia ni mwimbaji na Mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarab.
 
“Nilifanya kazi ya ziada kuingia kwenye muziki, maana baba yangu hakupenda suala hilo, hivyo kunipa wakati mgumu.
 
“Hata hivyo Mungu akipanga lake hakuna wa kuweza kutengua, ndio maana nimeweza kufika hatua hii na kujulikana sehemu kubwa kupitia soko la muziki wa taarabu,” alisema.
 
Mwimbaji huyo mwenye mvuto wa aina yake, anashindwa kubainisha chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yake na mume wake Mzee Yusuph.
 
Anasema riziki imekwisha kwa ndoa yao, huku akisema bado wanaheshimiana kwasababu wameachana bila kuwa na ugomvi, huku wakifanikiwa kupata mtoto mmoja, aliyepewa jina la Yusuph Mzee Yusuph.
 
Muziki wa taarabu unazidi kufanya vizuri kutokana na waimbaji wake wengi kuwa wabunifu.
 
Katika hilo anaamini kuwa mambo yatazidi kuwa mazuri, huku mashabiki wakipata vitu adimu kutoka kwao.
 
Mwimbaji huyo anavutiwa na mkali wa muziki huo nchini, Zuhura Shaaban.
 
Katika kundi lake la T-Moto, Jokha ameimba nyimbo zaidi ya tatu, ukiwamo wa ‘Unavyojidhani Haufanani’ ‘Mimi ni Star’ na ‘Aliyeniumba Hajanikosea’, ambao ulibeba jina la albamu ya kwanza.
 
Kwa albamu hii mpya inayoandaliwa, Jokha amesharekodi wimbo mmoja unaokwenda kwa jina la Domo la Udaku.
 
Katika hilo, ni wazi kuwa wao watakuwa juu zaidi, maana bendi nyingi zimekosa ubunifu na mikakati ya kimuziki.
 
“Kwenye muziki kumekuwa na ushindani, hivyo nadhani kinachotakiwa ni mipango, mikakati pamoja na nyimbo nzuri.
 
“Sisi tunavyo vitu hivyo, nadhani ni wakati wetu kuwa kileleni maana mashabiki wana kiu ya kuona mambo yetu yanakuwa mazuri,” alisema.
 
Jokha alizaliwa miaka kadhaa iliyopita, Zanzibar, katika Hospitali ya Mnazi Mmoja.
 
Elimu ya Msingi aliipata katika shule ya Darajani na kuhitimu mwaka 1995 ile ya Sekondari aliipata kwenye shule ya Haile Selasi.
 
Mbali na Jokha, wengine wanaopatikana kwenye kundi hilo ni pamoja na Nyawana Fundikira, Aisha Masanja, Shimuna Kassim, Amina Rashid, Hanifa Juma, Shaban Ramadhan, Mrisho Rajabu, Rahma Omari, Silver Mwandilee, Kasikile Msukule na wengineo.
You might also like:

Azam hatimaye yaiangukia Simba kuhusu Ngassa wakubali kugawa mgao wa usajili kwa wana Msimbazi


KLABU ya soka ya Azam imeuangukia uongozi wa klabu ya Simba wakiwaomba walimalize suala la nyota wao Mrisho Ngassa kwa njia ya amani mradi winga huyo awahi kwenda kufanyia vipimo kwa lengo la kutua rasmi katika klabu ya El Merreikh ya Sudan.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana jana jioni na kuthibitishwa na Katibu Msaidizi wa Azam, Twalim Suleiman 'Chuma' ni kwamba Azam imeuandikia barua uongozi wa Simba ukisema wapo tayari kuwapa sehemu ya fedha za usajili za Ngassa, mradi waondoe pingamizi lao lililopo TFF kabla ya saa 5 asubuhi ya leo.
Barua hiyo iliyosainiwa na Makamu Mwenyekiti wa Azam, Shani Cristom, imesema kuwa kwa vile muda wa usajili wa wachezaji kwa El Merreikh ni mfupi wangeomba Simba kutumia uungwana ili kumruhusu Ngassa aende Sudan kufanyiwa vipimo vya afya baada ya awali kusaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo.
Pia barua hiyo inasema Azam wapo tayari kuwapa Simba Dola za Kimarekani 25,000 na wapo (Azam) kusaliwa na Dola 50,000 katika Dola 75,000 za kumuuzia Ngassa, na kuutaka uongozi huo wa Simba kuhakikisha suala la mchezaji huyo ikiwemo kuondoa pingamizi lao TFF linafanyika kabla ya saa 5 asubuhi.
Katibu Msaidizi wa Azam, Twalib Chuma alikiri kuandikwa kwa barua hiyo na kutumwa kwa uongozi wa Simba na nakala kupelekwa TFF akisema lengo ni kuhakikisha Ngassa anapata fursa ya kujiunga na timu ya El Merreikh inayoshiriki Ligi ya Mabingwa wa Afrika mwakani.
"NI keli tumewaandikia barua Simba na kutuma nakala TFF kwa sababu ya kutaka kulimaliza suala la Ngassa kiungwana ili kumpa nafasi mchezaji huyo kwenda kucheza soka la kulipwa Sudan kwa manufaa ya taifa," alisema.
Twalib alisema anadhani jambo hilo la Ngassa litaisha kwa amani na kila upande kuridhia, japo walisema hawakuona sababu ya kulumbana na Simba ilihali klabu zote zipo kwa maendeleo ya soka la Tanzania.
Habari nyingine zilizotufikia asubuhi hii zinasema kuwa, pande mbili za klabu hizo wanatarajia kukutana kwa ajili ya kusaini makubaliano mapya juu ya uhamisho wa nyota huyo alioyeng'ara katika michuano ya Kombe la Chalenji iliyomalizika nchini Uganda hivi karibuni.





KIM POULSEN AWATAJA ASKARI WA KUWAVAA WAZAMBIA 

KOCHA wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 24 kitakachoingia kambini jioni ya Desemba 12 mwaka huu kuajianda kwa mechi ya kirafiki dhidi ya mabingwa wa Afrika, Zambia.

Katika kikosi hicho, wachezaji walioitwa kwa mara ya kwanza ni kipa Aishi Manula anachezea kikosi cha U20 cha Azam na timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes), beki wa kushoto wa Azam, Samih Nuhu, beki wa kushoto wa Mtibwa Sugar, Issa Rashid na mshambuliaji wa Azam, Mcha Khamis.

Pia kati ya wachezaji walioitwa, sita walikuwa kwenye kikosi cha Zanzibar (Zanzibar Heroes) kilichokamata nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Chalenji iliyomalizika Jumamosi jijini Kamapala, Uganda. Wachezaji hao ni Mwadini Ally, Nassoro Masoud Cholo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Samih Nuhu, Aggrey Morris na Mcha Khamis.

Kikosi kamili kilichoitwa ni makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally na Aishi Manula (Azam U20). Mabeki ni Shomari Kapombe (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Nassoro Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Samih Nuhu (Azam), Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga), Amir Maftah (Simba), Issa Rashid (Mtibwa Sugar) na Kevin Yondani (Simba).

Viungo ni Frank Domayo (Yanga), Athuman Idd Chuji (Yanga), Mrisho Ngasa (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Mcha Khamis (Azam), Salum Abubakar (Azam), Amri Kiemba (Simba) na Mbwana Samata (TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo- DRC).

Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC) na Mwinyi Kazimoto (Simba).

Monday, December 10, 2012

Peter Manyika: 'Straika' wa zamani anayefuata nyayo za baba yake









HANA muda mrefu tangu alipotumbukia katika soka, lakini kipaji kikubwa cha alichonacho cha soka kimeanza kumtabiria kuja kuwa nyota kama baba yake aliyewahi kung'ara na timu za Mtibwa Sugar, Yanga na Taifa Stars.
Peter Manyika, ndiye kipa namba moja kwa sasa wa timu ya taifa ya vijana ya U17 'Serengeti Boys' iliyozikosa kiduchu fainali za Afrika zitakazochezwa mwakani nchini Morocco baada ya kujikwaa kwa vijana wenzao wa Kongo.
Manyika, mtoto wa kwanza wa nyota wa zamani, Manyika Peter ndiye aliyekaa langoni katika mechi zote dhidi ya Kondo ikiwemo ile ya ushindi wa bao 1-0 nyumbani na kipigo cha mabao 2-0 ugenini wiki iliyopita.
Kipa huyo anasema mechi ya pili dhidi ya Kongo ndiyo mechi itakayobaki kichwani mwake kama tukio la huzuni kwa kushindwa kuisaidia Serengeti Boys kurejea tukio la mwaka 2004 kufuzu fainali za Afrika kabla ya kutolewa.
Manyika aliyeanzia kucheza kama mshambuliaji wa kati kabla ya kubadilishwa namba akiwa Shule ya Msingi, baada ya kipa wao kuumia na yeye kuhamishiwa langoni na kung'ara, anasema vurugu walizofanyiwa Kongo hatazisahau.
"Kwa kweli fujo na vitimbi tulivyofanyiwa Kongo ni mambo yanayonifanya nishindwe kuisahau mechi hiyo kwani hatukutarajia kama tungerudi salama kwa namna walivyotufanyia 'unyama' ndani na nje ya uwanja," anasema.
Manyika, anayetarajiwa kuibukia timu ya U20 ya Mgambo Shooting katika michuano ya Kombe la Uhai baada ya kuachana na  JKT Ruvu, anasema kwa tukio la furaha hakuna kama alipoitwa timu ya taifa na kuwa kipa namba moja.
"Sio siri kuitwa kwangu Serengeti Boys kulikuwa kwa kushtukiza sikutarajia na furaha zaidi ni kuwa kipa namba moja wa timu hiyo," anasema.
Manyika anasema japo anajiamini ana kipaji cha soka cha kuzaliwa na kurithi toka kwa baba yake, lakini hakutarajia mafanikio hayo ya mapema.

CASILLAS
Manyika anayemtaja mjomba wake, David 'Mzee wa Yeah' na Method kama walioibua na kukiendeleza kipaji chake kabla ya baba yake kutia nguvu, anasema alivutiwa kisoka na nyota wa zamani wa Brazil, Ronaldo de Lima na kujikuta akicheza kama mshambuliaji wa kati.
Anadai hata hivyo alipohamia kwenye ukipa amehamisha mapenzi kwa kipa Joe Hart na Ike Casillas aliyedai ndiyo kiigizo chake huku akimzimia pia Yew Berko wa Yanga.
Manyika anayependa kula ugali kwa dagaa na mlenda na kunywa Fanta, anadai japo Ronaldo kastaafu soka bado anaendelea kuwa mchezaji bora kwake kuwahi kumuona kutokana na umahiri wake wa kufumania nyavu.
Akiwa na ndoto za kucheza soka la kulipwa, Manyika anayesoma kidato cha tatu kwa sasa katika Shule ya Sekondari Kizuka iliyopo Morogoro, anasema kipindi kifupi alichokuepo katika soka amenufaika kwa mambo mengi.
Anadai kutumainiwa na taifa, kumudu maisha kwa kujinunulia vitu bila kutegemea wazazi na kusafiri sehemu mbalimbali ni baadhi ya mafanikio hayo.
Manyika anasema donge nono kulipata ni Sh 540,000 alizopata hivi karibuni na kutumia kununua godoro, runinga na deki yake na matumizi mengine.
"Nashukuru fedha hizo zimenifanya niwe kila kitu cha kuanzia maisha kwani mama yangu alinichongea pia kitanda. Huwezi amini awali hakupenda kabisa nicheze soka ila kwa sasa ananiunga mkono," anasema.

NDOTO
Manyika anayezishabikia Yanga, Barcelona na Real Madrid akiwazimia Dimitar Babatov na Ronaldo, anasema japo Serengeti Boys imeshindwa  kufuzu fainali za Afrika anadhani itafanya hivyo baadaye.
Pia anasema anaamini Taifa Stars chini ya Kim Poulsen ikijipanga vema inaweza kufuzu fainali za Kombe la Dunia na za Afrika kwa vile kocha huyo ni mjanja, mjuzi na mwenye malengo mazuri.
"Kim nimefanya naye kazi ni bonge la kocha na watanzania tunapaswa kumuunga mkono na kumkumbatia kwani anaweza kutupeleka mbali, hata fainali za Dunia, muhimu tujipange, japo watu wanaona ni ngumu."
Manyika anayemtaja John Bocco kama nyota anayemzimia Bongo, anadai wakati anaibukia katika soka hakutaka kabisa kutumia mgongo wa baba yake mpaka alipogundua kama amejitosa kwenye mchezo huo.
"Huwezi amini aliyenisaidia kufika hapa ni mjomba wangu Mzee Yeah, baba alikuja kuwa msaada wa kuninunulia vifaa baada ya kutambua nimejitosa kurithi kipaji chake."
Anaongeza kwa kuwashukuru wawili hao, pia mama yake kipenzi, Method na, ndugu, jamaa na rafiki wote wanaomuunga mkono.

KIPAJI
Peter Manyika 'Casillas' alizaliwa Agosti 13, 1996 jijini Dar es Salaam akiwa mtoto wa kwanza kati ya wawili wa familia yao, elimu yake ya Msingi aliisoma Shule ya Rutihinda kabla ya kujiunga na Kizuka Sekondari.
Kisoka, alianza makeke yake tangu shule ya msingi akicheza kama 'straika'  kabla ya kuhamia kwenye ukipa, timu yake ya kwanza ya kueleweka ikiwa ni Zaragoza ya Magomeni kabla ya kutua kituo cha soka cha Twalipo.
Anasema akiwa na kituoni hapo mwaka jana aling'ara katika michuano ya Airtel akiichezea Shule ya Jitegemee kisha kutua JKT Ruvu U20 na kuichezea katika Kombe la Uhai.
Baadaye Juni mwaka jana aliitwa Serengeti Boys na kumudu nayo mpaka sasa na hivi karibuni ameelekea Mgambo Shooting U20 atakaoicheza katika michuano ya Uhai 2012.
Akiowa na ndoto za kuja kuwa mfanyabiashara mkubwa, Manyika hutumia muda wake wa ziada kusikilia muziki, kuangalia muvi na anadai soka la Bongo  lipo juu hasa baada ya vijana kupewa nafasi ya kuonyesha vipaji vyao.
Anasema kama hali hiyo ikiendelea Tanzania itafika mbali, japo ametaka wadau wa soka kuwekeza zaidi na kudhamini klabu zote bila ubaguzi pia akitaka kuongezeka kwa michuano mingi zaidi ya ile ya ligi.
Juu ya Simba na Yanga, kinda hilo linalowasihi wachezaji wenzake kuzingatia mazoezi na kulitumaini soka kama ajira zao zinazoweza kuwatoa kimaisha anasema hana papara za kuzikimbilia kwa vile anataka kwanza kujenga jina.
"Simba na Yanga kwa sasa ni kubwa mno kwangu, labda baadaye tena kwa kuridhishwa na masilahi, napenda zaidi kucheza nje ya nchi au klabu isiyo na presha kubwa kama vigogo hao," anasema.

MESSI AVUNJA REKODI YA GERD MULLER, FALCAO NOMA

Asante Mungu nimempita Gerd Muller... mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi akishangilia goli lake la 86 msimu huu jana usiku dhidi ya Real Betis.
Messi akishangilia kuvunja rekodi ya mabao 85 iliyowekwa na Mjerumani Gerd Muller mwaka 1972. Messi alifunga mabao mawili dhidi ya Real Betis jana na kufikisha jumla ya mabao 86 mwaka huu 2012. Ana mechi tatu kabla ya kuumaliza mwaka huu.
Falcao wa Atletico Madrid akishangilia moja ya mabao yake matano dhidi ya Deportivo Coruna jana usiku. Atletico walishinda 6-0.
Shujaa wa mabao MATANO, Radamel Falcao wa Atletico Madrid akishangilia moja ya mabao yake dhidi ya Deportivo Coruna jana usiku. Atletico walishinda 6-0.

MADRID, Hispania
LIONEL Messi asiyezuilika ameweka rekodi mpya ya kufunga mabao mengi zaidi kwa mwaka mmoja wa kalenda katika historia ya soka duniani na kuwasaidia vinara ambao hawajapoteza mechi katika La Liga, Barcelona, kuendelea kuongoza kwa tofauti ya pointi sita juu ya Atletico Madrid kufuatia ushindi mgumu 2-1 ugenini dhidi ya Real Betis jana.

Mwanasoka Bora wa Dunia Messi alifunga goli lake la 85 na la 86 kwa mwaka 2012 katika mechi iliyojaa ushindani kwenye uwanja wa Benito Villamarin mjini Seville na kuipiku rekodi ya mabao 85 iliyowekwa na Mjerumani Gerd Mueller mwaka 1972.

Tukio hilo la kihistoria la Messi lilifunika mambo makubwa yaliyofanywa jana usiku na mshambuliaji Atletico, Radamel Falcao, ambaye mapema alifunga magoli matano peke yake wakati walipoisambaratisha timu inayoburuta mkia ya Deportivo Coruna kwa mabao 6-0 nyumbani.

Mshambuliaji huyo wa Colombia, anayefahamika kama 'the tiger' na ambaye anagombewa na klabu tajiri zaidi za Ulaya, alifikisha jumla ya mabao yake msimu huu kuwa 16 katika mechi 15 wakati Atletico ikidumisha tofauti ya pointi tano juu ya mahasimu wao wa mji mmoja Real Madrid.

Kikosi cha Jose Mourinho cha Real kililazimika kuzinduka kutoka nyuma mara mbili na kupata ushindi mgumu wa 3-2 ugenini dhidi ya Real Valladolid Jumamosi ambao uliwasaidia kupunguza pengo la pointi dhidi ya Atletico, ambao waliwafunga 2-0 wikiendi iliyopita, kuwa pointi mbili kwa usiku huo.

Hata hivyo, Atletico walijibu kwa kushinda mechi yao ya 12 katika 15 za ligi msimu huu dhidi ya timu iliyopanda daraja ya Depor ambayo iko hatarini kurejea moja kwa moja daraja la pili.

Barca wameshinda mechi zao zote msimu huu ukiacha sare ya 2-2 nyumbani dhidi ya Real Madrid Oktoba na magoli mawili ya Messi yaliwafanya wafikishe pointi 43, huku Atletico wakiwa na pointi 37 na Real wana pointi 32. Betis ni wa tano wakiwa na pointi 25, sawa na wanaoshikilia nafasi ya nne Malaga, ambao waliwasambaratisha Granada 4-0 Jumamosi.

"Inaonekana kama jambo lisilowezekana kwamba yeye (Messi) anaweza kufunga magoli mengi kiasi hiki ndani ya mwaka mmoja lakini kuna mechi tatu zimebaki na tunatumai kwamba ataendelea kuongeza jumla ya mabao yake," kocha wa Barca, Tito Vilanova, aliuambia mkutano na waandishi wa habari.

"Tunatumai kwamba atakwenda mbali sana katika maisha yake ya soka kwa sababu bado ni mdogo sana," aliongeza. "Sidhani kama tutaona mchezaji mwingine kama yeye."

BETIS WASIO NA BAHATI
Kikosi cha Vilanova kiliwatawala Betis kama ilivyotarajiwa katika kipindi lakini wakapoteza umiliki baada ya mapumziko na mwamba wa lango uliinyima timu hiyo goli mara tatu.

Messi aliifikia rekodi ya Mueller wakati alipochukua mpira katika eneo la katikati katika dakika ya 16 na akaiacha safu ya ulinzi ya Betis ikiwa imesimama kabla ya kufunga kwa shuti la pembeni chini kulia.

Pasi ya 'akili' ya kisigino ya Andres Iniesta ilimpikia Messi goli la pili dakika tisa baadaye kwa shuti kali kutokea katika eneo lile lile la kwanza ndani kidogo ya boksi na mpira ukatumbukia kwenye kona ile ile ya lango.

Ruben Castro alirudisha goli moja kwa wenyeji katika dakika ya 39 na kufanya kipindi cha pili kuwa kigumu zaidi kwa wageni.

Messi alikaribia kufunga 'hat-trick' dakika tano kabla ya mechi kumalizika wakati alipopiga 'tikitaka' ya jirani na lango lakini kipa wa Beti, Adrian alipangua mpira huo ambao ulimrudia Jordi Alba ambaye shuti lake liligonga 'besela' na mpira kutoka nje.

Kipigo kilikuwa kigumu kwa Betis, ambao waliwachapa Real 1-0 nyumbani mwezi uliopita na kuwapa Barca moja ya mitihani migumu zaidi kufikia sasa msimu huu ambao ulistahili japo pointi moja.

Mshambuliaji wa Atletico, Diego Costa alirekebisha makosa ya kadi nyekundu aliyopewa Alhamisi kwenye Ligi ya Europa wakati alipofunga goli la kuongeza kwenye Uwanja wa Calderon kwa kichwa kutokana na kona iliyopigwa na Koke katika dakika ya 23.

Kiungo wa Depor, Juan Valeron alipiga kichwa kilichogonga nguzo dakika nne baadaye lakini Atletico waliongeza la pili wakati Falcao alipoikimbilia vyema pasi ya Koke na kufumua shuti la chini lililotinga kwenye kona ya wavu.

Mpira uliorushwa haraka kutokea kushoto dakika tatu kabla ya mapumziko ulimpikia goli la pili mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 na akafumua shuti kali lililomshinda kipa Daniel Aranzubia kutokea kwenye kona ya eneo la penalti.

Falcao kisha akaangushwa ndani ya boksi na akafunga penalti hiyo katika dakika ya 64 na kukamilisha 'hat-trick' yake, akafunga kwa kichwa la nne na akakamilisha lake la tano katika dakika ya 71.

Yeye ni mchezaji wa kwanza kufunga magoli matano katika mechi ya La Liga tangu Fernando Morientes alipofanya hivyo kwa Real Madrid dhidi ya Las Palmas mwaka 2002.

MALLORCA AIBU
Real Mallorca waliendelea kuporomoka kuelekea kushuka daraja wakati walipofungwa 4-0 ugenini Levante, kikiwa ni kipigo cha nane katika mechi 10 walizocheza bila ya ushindi.

Obafemi Martins aliwafungia Levante goli la kuongoza kabla ya mapumziko na David Navarro, Ruben Garcia na Vicente Iborra walifunga katika kipindi cha dakika 10 katika kipindi cha pili.

Levante, ambao wamefuzu hatua ya 32-Bora ya Ligi ya Europa, wako katika nafasi ya sita wakiwa na pointi 24, huku Mallorca wakiwa katika nafasi ya 17 kwa pointi 13.

Timu inayochechemea ya Athletic Bilbao ilipata ushindi wa tano tu msimu huu wakati waliposhinda 1-0 nyumbani dhidi ya Celta Vigo.

Goli la kichwa la Aritz Aduriz katika dakika ya 33 liliamua mechi kwenye uwanja wa San Mames na kuiinua Bilbao hadi nafasi ya  13 wakiwa na pointi 18 points. Celta wako katika nafasi ya 15 kwa pointi 15.

Manyika Jr bado aliota pambano la Kongo



KIPA namba moja wa timu ya taifa ya vijana U17 'Serengeti Boys', Peter Manyika 'Casillas' amesema itamchukua muda mrefu kusahau matukio waliyofanyiwa na wenyeji wao Kongo katika pambano lao la marudiano la kuwania kucheza fainali za Afrika.
Manyika, alisema vitisho na fujo walizofanyiwa na wenyeji wao kabla na baada ya kuanza kwa pambano hilo, kwa kiasi kikubwa vilichangia timu yake kupokea kipigo cha mabao 2-0 na kung'olewa mashindano na kuzima ndoto za kufuzu fainali hizo za 2013.
Akizungumza na MICHARAZO katika mahojiano maalum nyumbani kwao, Kigogo jijini Dar es Salaam juzi, Manyika alisema ingawa hilo ndilo pambano lake la kwanza la kimataifa nje ya nchi, lakini hakuwaza kama angekutana na vitimbi kama hivyo ikizingatiwa michuano yenyewe ni ya vijana, pia wenzetu walipokewa vema hapa nchini.
"Kwa kweli niliingiwa na woga na hofu kubwa kwa namna wenyeji wetu walivyotufanyia vituko na fujo ambazo kwa kiasi fulani zilitupotezea umakini uwanjani, licha ya makocha kututia moyo kulipigania taifa," alisema.
Manyika, alisema anadhani kuna haja ya shirikisho la soka Afrika kuyaangalia matukio hayo waliyofanyiwa ikiwemo kupigwa kwa kocha wao msaidizi, Jamhuri Kihwelu 'Julio' ili kuyakemea yasiweze kurudia tena kwani yanaweza kujenga uhasama usio na maana.
Serengeti Boys, walishindwa kurejea rekodi iliyowekwa na wenzao mwaka 2004 walipofuzu fainali hizo za Afrika za U17 kabla ya kuenguliwa kwa kosa la kuchezesha 'kijeba' Nurdin Bakar na nafasi yao kupewa Zimbabwe waliokuwa wamewatoa.

Mwisho

Miyeyusho, mtwanga Nassib na kutwa taji la WBF






Bondia Fransic Miyeyusho akionesha ufundi wake kwa kumtupia masumbwi Nassibu Ramadhani wakati wa Mpambano wao wa kugombania ubingwa wa WBF uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Miyeyusho alishinda kwa T.K.O ya raundi ya kumi picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Mohamed Matumla  kulia  akimuhadhibi Doi Miyeyusho wakati wa mpambano huo usiku wa kuamkia  leo Matumla alishinda kwa K,O raundi ya pili Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Juma Fundi kushoto na Fadhili Majia wakioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki Majia alishinda kwa pointiPicha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Miyeyusho kushoto akimwazibu mpinzani wake Nassibu Ramadhani kwa kumtupia makonde mazito wakati wa Mpambano wao wa kugombania ubingwa wa WBF uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Miyeyusho alishinda kwa T.K.O ya raundi ya kumi picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Miyeyusho akionesha ufundi wake kwa kumtupia masumbwi Nassibu Ramadhani wakati wa Mpambano wao wa kugombania ubingwa wa WBF uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Miyeyusho alishinda kwa T.K.O ya raundi ya kumi picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mkangara kulia akimvisha mkanda wa ubingwa wa WBF bondia Fransic Miyeyusho baada ya kumtwanga Nassibu Ramadhani  kwa T.K.O raundi ya kumi kushoto ni promota wa mpambano huo Mohamed Bawaziri www.superdboxingcoach.blogspot.com
Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mkangara kulia akimpongeza Bingwa wa ubingwa wa WBF bondia Fransic Miyeyusho baada ya kumtwanga Nassibu Ramadhani  kwa T.K.O raundi ya kumi kushoto ni promota wa mpambano huo Mohamed Bawaziri www.superdboxingcoach.blogspot.com
bondia Fransic Miyeyusho akiwa amebebwa juu akiwa na mikanda miwili alioshinda baada ya kumtwanga Nassibu Ramadhani picha nwww.superdboxingcoach.blogspot.coma
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila  'Super D' kushoto akiwa na wadau waliojitokeza kuangalia mpambano huo
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Francis Miyeyusho juzi alifanikiwa kutetea taji lake la Mabara la UBO na kunyakua taji jipya pia la Mabara la WBF baada ya kumtwanga kwa TKO 10 mpinzani wake Nassib Ramadhani.
Miyeyusho alimtwanga Nassib TKO hiyo katika raundi ya 10 katika pambano kali lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam na ikuhudhuriwa na viongozi na wanamasumbwi mbalimbali nyota nchini.
Pambano hilo lililoandaliwa na mratibu Mohammed Bawazir na lililokuwa la kwanza kwa mabondia hao lilikuwa na jumla ya raundi 12 uzito wa bantam na lilianza kwa Nassib kumpeleka puta mpinzani wake kwa makonde makali.
Hata hivyo kadri raundi zilivyokuwa zikisonga mbele Nassib alianza kuonekana kuishiwa pumzi hasa kuanzia raundi ya nane na kumpa nafasi mpinzani wake nafasi ya kusimama imara kabla ya kusalimu amri katika raundi ya 10.
Mara baada ya Miyeyusho kutangazwa kuwa mshindi alikabidhiwa mataji yake mawili na aliyekuwa mgeni ramsi, Waziri wa Habari Utamaduni, Vijana na Michezo Dk Funella Mukangara na kuamsha hoi hoi ukumbini hapo.
Kabla ya pambao hilo, kulikuwa na mapambano mengine ya utangulizi ambapo Mohammed Matumla ' Snake Boy Jr' alimpiga kwa KO Doi Miyeyusho, Deo Samuel alitoka sare na Freddy Sayuni ,Fadhil Majiha alimpiga kwa pointi Juma Fundi na Ibrahim Classic alimpiga kwa pointi Said Mungi.
Baadhi ya mashabiki waliofurika kwenye ukumbi huo waliwapongeza waratibu wa pambano hilo sawia na kuwasifu mabondia wote waliopigana siku hiyo husuisani kumwagia sifa Nassib wakidai ni 'bonge' la bondia licha ya kupoteza mchezo huo.

Mwisho

Wednesday, December 5, 2012

YANGA YAZINDUA KALENDA YAKE KWA MBWEMBWE



YANGA walitumia burudani ya muziki na wanenguaji kujaza watu kwenye makao makuu ya klabu yao jijini Dar es Salaam wakati wakizindua Kalenda yao ya mwaka 2013.
Mabingwa hao wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) wameingia ubia wa mwaka mmoja na kampuni ya ‘Pecha Media & Health Promotion’ kutengeneza kalenda za klabu yao.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Nasib Limira alisema kuwa kampuni yake imeamua kutengeneza kalenda za Yanga ili kuisaidia klabu hiyo kukuza uchumi wake.
Alisema klabu hiyo inayojiandaa kwenda Uturuki kuweka kambi kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu huu, ina vyanzo vingi vya mapato, lakini inakosa fedha nyingi kutokana na kuwapo kwa ‘wajanja’ wanaotengenezaa bidhaa kwa jina la klabu hiyo na kuziuza kwa faida yao binafsi.
“Yanga ni klabu kubwa, lakini inakosa pesa nyingi kutokana na kuwapo kwa watu ambao wanajinufaisha kwa kutengeneza kalenda na bidhaa nyingine wakitumia jina la klabu hii. Tumeamua kuwasaidia kutengeneza kalenda hizi ikiwa ni sehemu ya mchango wetu katika kuwasaidia kuinua kipato chao,” alisema Limira.
Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema kuwa kutengenewa kwa kalenda hizo ni mwanzo mzuri kuonesha kwamba wamedhamiria kuinua kipato cha klabu hiyo na kudhibiti mianya ya watu kutengeneza bidhaa kwa jina la klabu hiyo huku pesa za mauzo zikiishia kwenye mifuko yao bila klabu hiyo kunufaika chochote.
“Huu ni mwanzo tu, tunataka kuwadhihirishia wapenzi wa Yanga kwamba tuko makini na mali za klabu. Tumeanza na Kalenda, zitafuata bidhaa nyingine kama jezi maana watu wengui wamekuwa wakituhujumu katika hili,” alisema Mwalusako.
Alisema kalenda hizo zinauzwa kwa Sh. 5,000 na katika kila kalenda Yanga itapata Sh.1,500 na kwamba kampuni hiyo imeanza kwa kuitengeneza nakala 100,000.
Hiyo ni mara ya kwanza kwa Yanga, ambao wamemaliza mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo wakiwa katika nafasi ya kwanza, kutengeneza kalenda maalum za klabu yao tangu ianzishe mwaka 1935.

Afisa Habari KIFA afia ofisini



AFISA Habari wa chama cha soka Manispaa ya Kinondoni (KIFA), Seif Mairo 'Saddam', alifariki dunia jana baada ya kuanguka ghafla akiwa kwenye ofisi za chama hicho.
Taarifa za kifo chake ziliwasilishwa na Mweka Hazina wa KIFA, Harid Kamguna.
Kamguna alisema Mairo aligundulika kuwa tayari amefariki baada ya kufikishwa katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
Alisema Afisa habari huyo mwenye umri wa miaka 76 anatarajiwa kuzikwa leo mchana katika makaburi ya Ndugumbi jijini Dar es Salaam.
Alisema marehemu alianza kazi hiyo tangu mwaka juzi na alisifiwa kwa ushirikiano wake mzuri na vyombo vya habari.
Enzi za uhai wake Mairo, aliyekuwa akifahamika zaidi kama Saddam, mbali na kuucheza mpira katika timu mbalimbali pia amewahi kuziongoza klabu kadhaa pamoja na soka la kuendeleza vipaji vya watoto na vijana kupitia chama cha Kinondoni, KIDYOSA na ni mmoja wa waasisi wa chama cha yosso cha Dar, DAYOSA aliyowahi kuwa Katibu Msaidizi kwa kipindi kirefu kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu wa chama hicho.
Kamguna alisema marehemu ameacha mke na mtoto mmoja. Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen.

Chanzo:NIPASHE

Tanzania kubeba maombi AFCON 2017



Na Sanula Athanas
RAIS wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), Leodegar Tenga amesema kuwa wamejipanga kutuma maombi ya kuandaa fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2017 huku akiipa nafasi kubwa Tanzania kuwa moja ya nchi zitakazoandaa.
Tenga, ambaye pia ni rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya shirikisho hilo jijjini Dar es Salaam jana.
"Kuna kitu ambacho tunakifanya kuhusu kuandaa michuano hiyo, kitakapokamilika tutawataarifu. Tanzania ina nafasi kubwa ya kuwa moja ya nchi zitakazoandaa michuano hiyo kutokana na miundombinu iliyopo na mapenzi ya soka miongoni mwa watu wake,” alisema Tenga bila kubainisha kitu kipi hasa wanakifanya.
Hata hivyo, taarifa kutoka Kenya zinaeleza Waziri wa Michezo na Vijana wa nchi hiyo, Ababu Namwamba alisema mwezi uliopita kuwa viongozi wa soka wa nchi za Uganda, Kenya na Tanzania walipanga kukutana Kampala, Uganda wakati wa michuano inayoendelea ya Kombe la Chalenji kuzungumza kutuma maombi ya kuandaa kwa pamoja AFCON 2017.
Waziri huyo alikaririwa na vyombo vya habari nchini humo akisema: “Tunasikitika kushindwa kutuma maombi ya kuandaa mashindano makubwa kutokana na miundombinu mibovu. Tunahitaji kuwekeza kwenye miundombinu ya michezo ili kuwa kwenye nafasi nzuri ya kuandaa mashindano makubwa,” alisema.
Kenya haijawahi kuandaa michuano mikubwa tangu iandae mashindano ya All African Games mwaka 1987. Tanzania yenye uwanja wa kisasa wa Taifa wa Dar es Salaa unaoweza kuchukua watu 60,000, ‘inazipiga fimbo’ nchi jirani za Kenya na Uganda.

UFAFANUZI WA WARAKA
Katika hatua nyingine, Tenga alisema sababu ya kuwaandikia wanachama wa TFF waraka wa kuwaomba wapitishe mabadiliko ya katiba ya shirikisho hilo badala ya kusubiri idhini hiyo kwenye Mkutano Mkuu wa Dharura, ni tatizo la ukosefu wa fedha.
Tenga alisema ni kweli kwamba walipaswa kuitishia mkutano wa dharura ili kupitisha mabadiliko hayo lakini TFF haina fedha ya kuitisha mkutano huo ambao hugharimu hadi Sh. milioni 110.
Alisema mabadiliko hayo ni maagizo ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na kwamba wasipoyatekeleza, Tanzania haitaruhusiwa kushiriki michuano yoyote ya kimataifa kuanzia mwakani.
Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa (Taifa Stars), alisema baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF wakiwamo wa mkoa wa Kagera wamepinga hatua hiyo huku Pwani wakihitaji ufafanuzi zaidi kabla ya kupitisha waraka huo.
“Tumetuma waraka kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF ili waturuhusu kufanya marekebisho ya katiba yetu. Tunatambua kwamba tulipaswa kuitisha Mkutano Mkuu wa Dharura ili wajumbe wakae na kupitisha, lakini hali yetu kiuchumi siyo nzuri,” alisema Tenga.
“Kwa miaka saba iliyopita tulikuwa tunatumia kati ya Sh. milioni 90 hadi 110 kuandaa kila Mkutano Mkuu wa TFF. Pesa iliyopo kwa sasa inatosha Mkutano Mkuu mmoja tu ambao ni wa Uchaguzi Mkuu.
“Endapo agizo hili la FIFA tungeliipata mapema, tungelizungumza katika mkutano uliopita, lakini tulipata taarifa Julai mwaka huu,” alisema.
Rais huiyo pia alizipongeza timu za taifa za Kilimanjaro Stars na Zanzibar Heroes kwa kuingia hatua ya nusu fainali katika michuano inayoendelea ya Kombe la Chalenji.

Chanzo: NIPASHE
   

SELCOM PAYPOINT YAANZA KUUZA VOCHA ZA ZUKU...!

Meneja wa matangazo na Masoko wa Kampuni ya SelCom wireless Paypoint Juma Mgori, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana wakati wa kutangaza rasmi Kampuni hiyo kuanza kuuza vocha za kulipia king’amuzi cha Zuku kupitia vituo mbalimbali vya Selcom Paypoint. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Zuku Tanzania, Fadhil Mwasyeba.

Meneja wa matangazo na Masoko wa Kampuni ya SelCom wireless Paypoint Juma Mgori , akifafanua jambo kwa wanahabari (hawapo pichani) juu ya huduma wanazotoa ikiwa ni pamoja na ulipiaji wa bili mbalimbali kama za simu za makampuni yote, Luku, Startime, tiketi za treni za jijini Dar es Salaam, kulipia ada za mitihani (NECTA), kuangalia matokeo na sasa Zuku.

Meneja Mkuu wa Zuku Tanzania Fadhil Mwasyeba  akizunguma na waandishi wa habari wakati wa makubaliano ya mkataba wa kujiunga na SelCom kwa ajili ya Malipo ya Zuku.

Meneja Mkuu wa Zuku Tanzania Fadhil Mwasyeba kushoto akizunguma na waandishi wa habari wakati wa makubaliano ya mkataba wa kujiunga na SelCom kwa ajili ya Malipo ya Zuku, wengine ni  Meneja wa matangazo na Masoko wa Kampuni ya SelCom wireless Paypoint Juma Mgori   na Meneja wa Bidhaa na uboreshwaji wa viwango Julio Batilia .

Waandishi wa Habari Rehema Kilagwa wa NIPASHE (mbele kulia), Mwasiti wa The Guardian (wa pili kulia) na wengine wakifuatilia maelezo kutoka kwa kina Mgori wa SelCom na Fadhili wa Zuku (hawapo pichani) wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari kuelezea namna wateja wanavyoweza kununua vocha za Zuku kupitia simu za mikononi jana Desemba 4, 2012.

Meneja Mkuu wa Zuku Tanzania Fadhil Mwasyeba (wa pili kushoto) akibadilishana hati ya makubaliano ya kulipia king'amuzi cha Zuku kwa njia ya mtandao na Meneja wa matangazo na Masoko wa Kampuni ya SelCom wireless Paypoint Juma Mgori,  makubariano hayo yamefanyika Dar es salaam jana kwa ajili ya kurahisisha hudumu hio. Wanaoshuhudia ni maofisa kutoka Selcom na Zuku.

UGANDA YAIFUATA KILI STARS NUSU FAINALI TUSKER CHALLENGE 

Chanzo BIN ZUBEIRY 

Wachezaji wa Uganda wakimpongeza Geoffrey Kizito (anayetazama kamera amekumbatiana na Kiiza), baada ya kufunga bao kwanza dakika ya nne dhidi ya Ethiopia katika Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala. Uganda ilishinda 2-0 bao lingine likifungwa na Robert Ssentongo dakika ya 60 na kwa ushindi huo, Uganda itamenyana na Tanzania Bara katika Nusu Fainali Alhamisi usiku, mchezo ambao utatanguliwa na Nusu Fainali nyingine kati ya Kenya na Zanzibar.
Ssentongo akisababisha

Kiiza mawindoni

Kipa Samson Asfaw Worku akiwa amedaka mpira, huku beki wake Girma Bekele Debele akimdhibiti Brian Umony kulia

Gotochi Panom Yietch akigombea mpira na Robert Ssentongo kulia

Robert Ssentongo anaondoka na mpira baada ya kumlamba chenga beki wa Ethiopia kulia

Hamisi Kiiza akimtoka Chala Deriba Debala wa Ethiopia

Kiiza, Walusimbi, Wasswa wakicheza na Ssentongo 

Kutoka kulia Hamisi Kiiza na Henry Kalungi wakimpongeza Robert Ssentongo kufunga bao la pili