STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 30, 2013

HATIMAYE MSANII LULU AACHIWA KULA RAHA USWAHILINI

Lulu akifurahi baada ya kuachiwa kwa dhamana jana
Lulu akijibu maswali ya waandishi baada ya kuachiwa kwa dhamana

Lulu akilia baada ya kuachiwa kwa dhamana  huku akisaidiwa na muigizaji mwenzake, Dokta Cheni, ambaye alikuwa mstari wa mbele kuwezesha kutoka kwake kwa kipindi chote cha miezi tisa aliyokaa rumande binti huyo

Lulu akijibu maswali ya waandishi baada ya kuachiwa kwa dhamana jana

Lulu akimkumbatia mama yake mzazi Lucrecia Kalugila

Lulu akimkumbatia mama yake mzazi Lucrecia Kalugila

Mungu mkubwa... mama wa Lulu akifurahi baada ya mwanae kuachiwa kwa dhamana jana

Lulu akianza safari ya kwenda uswahilini jana






Sitaki kupigwa picha bana!






Lulu akisaidiwa na Dk Cheni kuanza safari yake ya uswahili, kulia mmoja wa wanahabari


MSANII Elizabert Michael 'Lulu' alionekana akicheka kwa furaha ya kuachiwa huru kwa dhamana kwa dakika chache jana alasiri akiwa na mama yake Lucrecia Kalugila, lakini muda mrefu baadaye wakajikuta wakibubujikwa na machozi bila kikomo ikiwa ni matokeo ya kuzidiwa na hisia za furaha hiyo. pia wakionekana kutoamini juu ya kile kilichotokea.
Msanii huyo nyota wa filamu nchini, ameachiwa kwa dhamana hatimaye baada ya kutimiza masharti aliyiopewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam katika kesi inayomkabili ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa msanii mwenzake nyota, marehemu Steven Kanumba.
Awali, mama huyo wa Lulu, ndugu, jamaa, marafiki na wasanii mbalimbali wa filamu nchini walionekana mahakamani tangu saa 2:30 asubuhi juzi, lengo likiwa ni kujua hatma ya mpendwa wao ambaye amekuwa akisota mahabusu tangu Aprili mwaka jana.
Baadaye, mama huyo alionekana kujawa na hisia kali kiasi cha kumwaga machozi yatokanayo na furaha aliyokuwa nayo baada ya mahakama kumuachia binti yake kwa dhamana na wote wawili kuonekana wakikumbatiana; kama watu wasioamini juu ya kile kilichotokea.

ILIVYOKUWA
Lulu mwenye miaka 18, anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya bila kukusudia ya msanii mwenzake, Kanumba (28), aliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti aliyopewa.
Msanii huyo alifikishwa saa 7:50 mchana akitokea mahabusu ya gereza la Segerea, akiwa katika ‘deffender’ jeupe la Magereza lenye namba za usajili STK 2823.
Mawakili wa pande zote walihakiki nyaraka za dhamana. Ilipofika saa 9:10 alasiri, Lulu alipandishwa kizimbani akiwa na wadhamini wake.
Mbele ya Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Francis Kabwe, Lulu aliwawakilisha na wadhamini wawili, James Mboneka kutoka Wizara ya Afya na Florian Mutafungwa wa Wizara ya Ardhi.
Saa 9:20, Lulu alikamilisha taratibu za mahakama na kuachiwa huru hatimaye ambapo mama yake (Lucrecia), ndugu, jamaa na marafiki zake walijikuta wakiangua kilio cha furaha.
Akizungumza baada ya kuwa huru kwa dhamana, Lulu alisema anamshukuru Mungu pamoja na watu wote walio pamoja naye katika kipindi chote kigumu.
"Sina la kusema... nawashukuru wote waliokuwa pamoja na mimi tangu nilipopata kesi hii. Ila bado nawaomba waendelee kuniombea kwa sababu nimepata dhamana tu, bado nina safari ndefu. Kesi  bado mbichi, niombeeni jamani," alisema Lulu huku akilia kabla ya kuondoka kwenye viunga vya mahakama hiyo akiwa ndani ya
gari lenye namba za usajili T 480 CFX, Toyota Land Cruser (V8) la rangi ya kijivu.
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala alisema dhamana ni mchakato wa kisheria unaotakiwa kufuatwa katika mahakama na kwamba mteja wao amefanikiwa kupata dhamana na sasa wanasubiri wito wa mahakama wakati itakapopanga tarehe kwa ajili ya kusikiliza ushahidi wa Jamhuri wa kesi ya msingi.
Mapema Juzi, Jaji Zainabu Mruke alitoa masharti ya dhamana kwa mshtakiwa huyo baada ya wakili wa utetezi Peter Kibatala kuwasilisha maombi ya dhamana kwa hati ya dharula chini ya kifungu cha 148 kidogo cha (1) na cha (2) cha Mwenendo wa Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA).
Jaji Mruke alisema kosa linalomkabili  mshakiwa lina dhamana kisheria na kwamba mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa kufuata masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa serikali watakaosaini  hati ya dhamana ya Sh. milioni 20 kila mmoja.
Alitakiwa pia awasilishe hati zake za kusafiria, kuripoti kila tarehe Mosi ya mwezi kwa Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na asitoke nje ya mkoa wa Dar es Salaam bila kibali cha msajili huyo.
Katika kesi ya msingi, Lulu anadaiwa kuwa  Aprili 7, 2012, katika eneo la Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam, alimuua Kanumba bila kukusudia.

ZAMBIA WAVULIWA TAJI AFRIKA, NIGERIA HAOO ROBO FAINALI

Victor Moses wa Nigeria akikimbilia mpira wakati wa mechi yao dhidi ya Ethiopia leo, Nigeria walishinda 2-0 magoli yote yakifungwa na Moses kwa penalti.

Tumewavua ubingwa... Wachezaji wa Burkina Faso wakishangilia baada ya sare yao ya 0-0 dhidi ya Zambia iliyowavua ubingwa wa Afrika watetezi hao jana.

MABINGWA watetezi wa AFCON, Zambia 'Chipolopolo', wamevuliwa ubingwa kufuatia sare ya 0-0 dhidi ya Burkina Faso, huku Nigeria wakivuka hadi robo fainali kwa magoli mawili ya penalti dakika za lala-salama na kuishinda Ethiopia waliomaliza 10 uwanjani.
Nigeria ambao walimaliza wakiwa wa pili nyuma ya Burkina Faso, watawakabili Ivory Coast katika mechi ya robo fainali inayotarajiwa kutazamwa kama fainali.
Kocha wa Nigeria, Stephen Keshi alisema baada ya mechi hiyo kwamba ushindi wa jana aliusubiri kwa siku nyingi sana na anaamini utawapa faraja Wanigeria kote duniani.
"Kila mechi ina mbinu zake. Tutaingia kuwakabili Ivory Coast kwa mbinu tofauti na tulizotumia kuwakabili Ethiopia au hata tulizotumia katika mechi mbili zilizotangulia," alisema mchezaji huyo wa zamani wa Nigeria wakati akijibu swali la mwandishi aliyetaka kujua wanajiandaaje kwa mechi ya ya robo fainali na mbinu gani watakazotumia. "Kuhusu mbinu tutakazotumia siwezi 'kushea' na wewe. Hizo nitashea na wachezaji wangu."
Zambia ambayo ilimuacha nje nahodha wao mhamasishaji, Chris Katongo, aliyewapa ubingwa wao wa kwanza wa Afrika mwaka jana, ilicheza kwa kiwango cha chini huku ikikosa makali katika umaliziaji huku straika wao Collins Mbesuma "akimpasia" kipa wa Nigeria, Vincent Enyeama, kwa kishuti "mtoto" katika nafasi ya wazi zaidi waliyopata Chipolopolo.
Kocha Mfaransa, Herve Renard, aliyewapa ubingwa mwaka jana, alimuacha nje Katongo kutokana na madai ya kucheza chini ya kiwango katika mechi zao mbili za awali, maamuzi ambayo atayajutia.
Burkina Faso iliyocheza kwa kujilinda zaidi ikihitaji sare tu ili kusonga mbele, ilipata pigo la mapema baada ya kinara wa mabao wa fainali hizi, Alain Traore, kuumia katika dakika ya 10 na kutolewa kwa machela. Traore amefunga magoli matatu yakiwamo mawili katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Ethiopia katika mechi yao ya pili.
Zambia pia walipata pigo dakika chache baadaye baada ya nyota wao Davis Nkausu kuumia 'enka' kufuatia kukanyagwa vibaya na nahodha wa Burkina Faso, katika tukio ambalo lilistahili kadi nyekundu lakini halikutoka hata onyo. Nafasi ya Nkausu ilichukuliwa na Joseph Musonda.
Burkina Faso wamemaliza vinara wa kundi hilo kwa kuwa na pointi tano, sawa na Nigeria walio katika nafasi ya pili kutokana na kuzidiwa magoli.
Hii ni mara ya kwanza kwa Burkina Faso kutinga raundi ya pili tangu walipoandaa michuano hiyo mwaka 1998.
Zambia "imefia" katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi tatu baada ya sare tatu. Mabingwa hao walikuwa na maandalizi mabovu kwa kuchapwa mechi tatu, ikiwamo dhidi Tanzania kupitia goli pekee la Mrisho Ngassa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, na sare moja katika mechi zao nne za kujipima kabla ya michuano hiyo.
Mabingwa kutolewa katika hatua ya awali, ni mara ya kwanza tangu mwaka 1992 wakati Algeria walipotolewa katika hatua ya makundi.
Winga wa Chelsea, Victor Moses, ndiye aliyekuwa shujaa wa Nigeria baada ya kufunga penalti mbili za dakika za lala salama na kuipeleka timu yake hatua ya robo fainali ambayo kama matokeo yangebaki ya 0-0 ingeaga mashindano.
Moses aliangushwa mara mbili ndani ya boksi na akafunga penalti zote mbili, ya pili langoni akiwa amesimama kiungo, Addis Hintsa, aliyelazimika kuvaa jezi ya kipa baada ya mlinda mlango wa Ethiopia, Sisay Bancha, kutolewa kwa kadi ya pili ya njano huku wakiwa tayari wameshamaliza orodha yao ya wachezaji wa kuwabadilisha uwanjani. 

BALOTELLI AKUBALI MIAKA MINNE NA NUSU AC MILAN

Balotelli

KLABU ya AC Milan wameafiki dili la kumsajili mshambuliaji Manchester City, Mario Balotelli kwa mkataba wa miaka minne na nusu, mkurugenzi wa klabu hiyo ya Italia, Umberto Gandini, amethibitisha.
Mfumania nyavu huyo wa zamani wa Inter Milan, Balotelli (22) atafanyiwa vipimo vya afya mjini Milan leo (Jumatano) kabla ya kusaini mkataba wake.
Ada ya awali ya uhamisho inaaminika kuwa ni paundi milioni 19 ambayo inasemekana imeshalipwa na huenda ikaongezeka kufikia paundi milioni 22.
Mchezaji huyo mwenye vituko ndani na nje ya dimba, ataondoka Manchester City huku akiwa ameweka gumzo baada ya mwishoni mwa mwaka jana kukwidana na kocha wake, Roberto Mancini wakati wa mazoezi, mbali na matukio mengine ya utata aliyowahi kuyafanya klabu hapo.
Mchezaji huyo

Thursday, January 24, 2013

Simba kuonyesha makali ya Oman leo Taifa

Kikosi cha Simba kinachotarajiwa kushuka dimbani leo


MABINGWA wa soka nchini, Simba iliyorejea jana kutoka Oman ilipokuwa kwenye kambi ya mazoezi, inatarajiwa kushuka dimbani leo kuonyesha mambo ya umangani itakapovaana na Black Leopards ya Afrika Kusini katika pambano la kirafiki la kimataifa.
Pambao hilo litakalopigwa majira ya jioni kwenye dimba la Taifa, jijini Dar es Salaam itakuwa pambano la mwisho kwa Simba kabla ya kuanza kwa duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Jumamosi.
Simba inatarajiwa kuanza duru hilo kwa kuvaana na African Lyon kwenye uwanja wa Taifa.
Black Leopards inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini, ipo nchini kwa ziara ya kujipima nguvu wakisubiri kuendelea na ligi yao iliyosimama kwa sasa kupisha michuano ya AFCON-2013 inayofanyika nchini mwao.
Timu hiyo jana iliendelea kuwa mnyonge kwa Yanga kwa kulazwa mabao 2-1 ikiwa ni siku chache tangu ichezee kichapo cha kukandikwa mabao 3-2.
Simba iliyoenda moja kwa moja kambini mara baada ya kuwasili jana mchana, imetamba kuwapa raha mashabiki wake ambao walimaliza duru la kwanza la ligi kuu kwa masononeko.
Mabingwa hao hiyo itakuwa mechi yao ya nne ya kujipima nguvu baada ya awali kucheza mechi tatu ughaibuni nchini Oman ikishinda mechi moja na kupoteza mbili.

Mashabiki wa soka wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi katika pambano hilo la leo ili kutaka kushuhudia makali ya timu yao, baada ya watani zao Yanga waliokuwa Uturuki, walivyokonga nyoyo za mashabiki wao kwa kuisasambua Blac Leopards mara mbili.

Wanachama Yanga waanza kugeukana, kisa...!

Ramadhani Kampira, mmoja wa wanachama wa Yanga



BAADHI ya wanachama wa Yanga wameibuka na kuelezea hofu waliyonayo juu ya kupitishwa kwa vipengele vya katiba inayowapa madaraka makubwa Mwenyekiti na Makamu wake klabu hapo.
Wanachama hao walisema kupitishwa kwa vipengele vinavyowapa viongozi hao uwezo wa kumfuta uanachama mwanachama yeyote wa Yanga ni sawa na kuruhusu udikteta pamoja na kuivuruga Yanga.
Mmoja wa wanachama hao, Ramadhani Kampira, alisema japo wanachama wenzake waliafiki vipengele hivyo katika mkutano mkuu ulioitishwa mwishoni mwa wiki, lakini ukweli hakubaliani navyo.
Kampira aliyewahi kuichezea timu hiyo na kung'ara na TAMCO Kibaha na Sifa United, alisema kuruhusu hali hiyo inaweza kutumiwa vibaya na viongozi katika suala la chuki binafsi.
"Mtu anaweza kuamka usingizi au kutoka nyumbani akiwa kagombana na mkewe kisha kuamua kumfukuzisha mtu uanachama kwa chuki na kusiwepo wa kuwahukumu kwa vile lipo kwenye katiba," alisema Kampira.
Naye Mwinjuma Muumini, ambaaye ni mmoja wa waimbaji nyota wa muziki wa dansi, alisema hakubaliani na maamuzi hayo japo alikiri hajui kitu gani kilichowakumba wanachama wenzake na kuafiki jambo hilo.
Muumini, anayefahamika kama 'Kocha wa Dunia' au 'Mzee wa Chelsea' alisema kuwa maamuzi hayo ni kurejesha ukoloni na kuruhusu udikteta katika Yanga kwani haikubaliki hata kwa sheria ya nchi.
"Sijajua ajenda za mkutano huo zilikuwa zipi, lakini kilichofanywa na wanachama wenzetu ni msiba ambao utakuja kuigharimu na kuivuruga Yanga mbele ya safari, huo ni udikteta,:" alisema.
Juu ya suala la kutimuliwa kwa wanachama wenzao waliokuwa waajiriwa wa klabu hiyo, Louis Sendeu na Celestine Mwesigwa, Kampira yeye alisema taratibu na sheria za kazi zizingatiwe na zisiingizwe katika masuala ya michezo.
"Wale walikuwa waajiriwa na kama walitimuliwa kazi bila kuzingatiwa taratibu au kulipwa haki zao stahiki, walikuwa na haki ya kutafuta jasho lao mahali pengine, hivyo suala hilo lisitumiwe kuwaonea watu waliotendwa sivyo ndivyo,": alisema Kampira.
Wanachama wa Yanga waliafiki kwa kauli moja kuwatimua uanachama akina Sendeu kwa madai ya kosa la kukimbilia mahakamani ya usuluhishi kudai haki zao za malimbikizo na misharaha.
Pia mkutano huo uliafiki kubadilishwa kwa vipengele vya katiba yao kwa kuwaruhusu viongozi hao wa juu kuwatimua wanachama mara watakapobainika kufanya makosa bila kusubiri maamuzi ya wengi.

Irene Paul amuibua Kalunde

Msanii Irene Paul


BAADA ya kutumikishwa katika kazi za wasanii wengine, mwanadada mkali wa Bongo Movie, Irene Paul 'Brown Eyes', amefyatua filamu yake binafsi ya kwanza kupitia kampuni binafsi aliyoianzisha hivi karibuni.
Msanii huyo, aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa, filamu hiyo mpya inafahamikwa kwa jina la 'Kalunde' na ipo njiani kuachiwa mtaani ikiwa imewashirikisha wasanii kadhaa nyota nchini.
Irene aliwataja wasanii hao walioshiriki filamu hiyo inayozungumzia masuala ya ndoa za utotoni na changamoto zake, ni pamoja na Grace Mapunda 'Mama Kawele', Hemed Suleiman 'PHD', Ahmed Olotu 'Mzee Chillo', yeye na Richard Mshanga 'Masinde'.
"Kwa mara ya kwanza nimeibuka na filamu yangu binafsi iitwayo 'Kalunde' ambayo mbali na kuigiza mie mwenyewe pia imewashirikisha wasanii kadhaa mahiri nchini kama akina Mzee Masinde, Mzee Chillo, Mama Kawele, Hemed na wengineo," alisema Irene.
Irene alisema kwa sasa anamalizia mambo fulani kabla ya kuitoa hadharani kuwapa mashabiki wake burudani ambayo wamekuwa wakimshuhudia katika kazi za watu wengine.
Muigizaji huyo aliyewajio kuwa mtangazaji na pia mwanamitindo, alisema filamu hiyo imezalishwa na kampuni yake binafsi iitwayo Krema Production na kazi hiyo ni mwanzo wa kudhihirisha kwamba yeye hajabahatisha kuingia katika fani hiyo.

Kabla ya kuipakua kazi hiyo binafsi, mwanadada huyo alishacheza filamu kama Shujaa, I Hate My Birthday, Unpredictable, The Shell, Handsome wa Kijiji, Triple L, Fikra Zangu na nyingine zinazozidi 15 tangu atumbukie kwenye fani hiyo mwaka juzi.

Zola D ana Swahili Hip Hop


Zola D katika pozi
MSANII nyota wa muziki wa hip hop nchini, David Mlope 'Zola D' anajiandaa kupakua albamu yake ya kwanza tangu atuimbukie kwenye fani hiyo itakayokuwa na nyimbo 21.
Akizungumza na MICHARAZO, Zola D, alisema albamu hiyo itafahamikwa kwa jina la 'Swahili Hip Hop' ambayo imekusanya nyimbo zake zote alizozifyatua tangu aingie kwenye fani hjiyo mwaka 1995.
Zola D alisema, baadhi ya nyimbo zitakazokuwa katika albamu hiyo ni pamoja na kibao kilichompa ujiko miaka kadhaa iliyopita cha 'Moto wa Tipper', 'Jana Sio Leo', 'Sipati Mchongo', 'What Going On', 'Hustler King', 'Unde', 'Msela Sana', Rap Gangster' na 'Rudi'.
Nyingine ni nyimbo zake mbili za hivi karibuni ambazo zinaendelea kutamba katika vituo vya redio na runinga za 'Coast to Coast' na 'Knockout' alioimba na P Funk.
"Nimeshakamilisha kila kitu kabla ya kuitoa hadharani albamu yangu itakayokuwa ya kwanza tangu nitumbukie katika fani hii miaka karibu 20 iliyopita, itakuwa na nyimbo za zamani na mpya ambazo baadhi zinaendelea kutamba nchini na nje ya nchi," alisema.
Msanii huyo ambaye pia ni bondia wa ngumi za kulipwa wa uzito wa juu akiwa pia amesilimu kutoka dini ya Ukristo akifahamika kwa jina la Daud, alisema mashabiki wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiuulizia juu ya albamu hiyo waondoe shaka.

MBUNIFU ALLY REMTULLAH KUIPEPERUSHA BENDERA MAREKANI


Meneja Masoko wa Kampuni ya Tanzania Hair Industry ltd James Walwa – Jimmy akimkabidhi mbunifu wa mavazi nchini Ally Rehmtullah tiketi kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha Afrika Mashariki katika mkutano wa ‘The Economics of the Africa Fashion Industry’ utakaofanyika nchini Marekani mwezi wa Februari. Tanzania Hair Industry ltd ambao ndio watengenezaji wa nywele maarufu aina ya Darling ndio wadhamini wa safari ya mbunifu huyu kwenye mkutano huo wa kihistoria utakaofanyika katika Kikuu cha Havard nchini Marekani.
 
Mbunifu mahiri wa mavazi nchini Tanzania Ally Remtullah amechaguliwa kuiwakilisha Africa Mashariki katika ‘East Africa Fashion Industry’ kuongea katika mkusanyiko wa Afrika Business Conference utakaofanyika Harvard Business School nchini Marekani.
 
Akizungumza na Lenzi ya Michezo  jijini Dar es Salaam jana, Mbunifu huyo Remtullah amesema shughuli hiyo itakayofanyika katika Chuo Kikuu cha Marekani cha Harvard ambacho ni kikubwa kuliko vyote duniani itafanyika Februari tarehe 15 mwaka 2013.
 
Akifafanua amesema kuwa kila mwaka Chuoni hapo kunafanyika mikutano ya ‘Africa Business Conference’ ikiwa na kauli mbiu tofauti na sasa mwaka huu yeye amechaguliwa kuwa mmoja wa wazungumzaji kuhusiana na ‘The Economic of Africa Fashion’.
 
Ally Remtullah amesema kwa ujumla anaiwakilisha Afrika Mashariki katika kategori hiyo ambapo anatarajiwa kuzungumzia changamoto zinazoikabili na fursa zinazopatikana katika tasnia ya fasheni Afrika Mashariki, ikiwemo tatizo la umeme na gharama za manunuzi ya vitambaa vya Pamba ambayo kimsingi huzalisha katika ukanda huu.
 
Amesema anafurahi kuchaguliwa na wandaaji hao kuziwakilisha nchi za Afrika Mashariki na sasa si kwenda tena kuonyesha mavazi, bali ni kuzungumza mbele ya wadau wakubwa wa kidunia kuhusu nafasi ya masuala ya ubunifu na uchumi.
Wazungumzaji wengine katika mkutano huo ni pamoja na mbunifu maarufu wa Afrika Magharibi Ituen Basi kutoka Nigeria.
 
Katika maandalizi hayo Ally amesema pamoja na kusoma vitu vingi kuhusiana na uchumi katika tasnia ya fasheni na gharama za uzalishaji za viwanda vya nguo, pia amekutana na wafanyabiashara wakubwa wa viwanda vya kutengeneza nguo hasa za kiafrika akiwemo Mfanyabiashara Mkubwa nchini Mh. Mohammed Dewji ambaye kwa namna moja ama nyingine amempa ushirikiano wa kutosha.
 
Safari hiyo ya mbunifu wa mavazi nchini Ally Remtullah katika mkutano mkubwa wa kihistoria wa Boston nchini Marekani, imedhaminiwa na kampuni ya Tanzania Hair Industry Ltd, ambao ni wazalishaji wa nywele maafuru aina ya Darling.

YANGA YAILIZA TENA BLACK LEOPARDS CCM KIRUMBA-MWANZA



Wachezaji wa timu Yanga wakifurahia goli la pili lililofungwa na Jerry Tegete kipindi cha pili mnamo dakika ya 54 kwa njia ya penati.


Golikipa wa timu ya Black Leopards,Posnett Omony akisota kuokoa mpira uliotinga wavuni kutoka kwa mchezaji wa timu ya Yanga Jerry Tegete kwa njia ya penati mnamo dakika ya 54.Timu ya Yanga imeibuka kifua mbele mpaka dakika 90 kwa kuinyuka goli 2-1 timu ya Black Leopards kwenye mchezo wao wa marudiano wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa CCM-Kirumba jijini Mwanza.Picha na JICHIE BLOG-jijini Mwanza.


Mchezaji wa timu ya Yanga David Luhende akitaka kumchomoka mchezaji wa timu ya Black Leopards, Moses Kwena, kwenye mchezo wao wa marudio uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jioni ya leo.


Pichani ni Golikipa wa Black Leopards Posnett Omony akijitahidi kuokoa mpira uliopigwa kwa kichwa na mchezaji wa Yanga, Said Bahanuzi na hatimaye kutinga kimiani mnamo dakika ya saba.


Mchezaji Hamis Kiza wa Yanga akifanya jitihada za kumtoka beki wa timu ya Black Leopards,Victor Kamhuka.


Mchezaji wa wa timu ya Yanga David Luhende akitaka kumtoka mchezaji wa timu ya Black Leopards, Moses Kwena, kwenye mchezo wao wa marudio uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.






Baadhi ya mashabiki wa Mpira wakiwa wamepanga mstari kwa ajili ya kununua tiketi na kujionea kandanda safi kabisa kati ya timu ya Yanga na Black Leopards ya Afrika kusini.


Kikosi cha Yanga kikiwa katika picha ya pamoja.


Sehemu ya umati wa watu waliokuwa wakishuhudia mchezo huo,ambapo timu ya Yanga imetoka kifua mbele goli 2-1 dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini, mchezo huo umechezwa leo kwenye uwanja wa CCM-Kirumba jijini Mwanza.


Mtanange ukikaribia kuanza.


Kikosi cha timu ya Black Leopards.


Benchi la ufundi la timu ya Yanga


Ilikuwa ni patashika nguo  kuchanika, mchezaji wa timu ya Yanga, Jerry Tegete akiwatoka baadhi ya mabeki wa timu ya Black Leopards, Jerry alifanikiwa kufunga goli la pili mnamo dakika ya 54 kipindi cha pili.





Nginja nginja tuu


Makocha wakipongezana mara baada ya mpira kuisha.


Sehemu ya Umati wa mashabiki wa timu ya Yanga.


Mashabiki wakiwa kwenye mstari kwa ajili ya kuingia uwanjani.

Wednesday, January 23, 2013

Kinyambe aufungua mwaka na mpya

KInyambe akiwa katika pozi zake
MCHEKESHAJI anayezidi kutamba nchini kwa sasa, Mohammed Abdallah 'Kinyambe' ameufungua mwaka 2013 kwa kuachia filamu yake mpya iitwayo 'Urithi wa Kinyambe'.
Akizungunza na gazeti hili, Kinyambe anayefahamika pia kama James, alisema filamu hiyo tayari imeshaingia sokoni akiwa ameigiza na wasanii kadhaa maarufu nchini.
Kinyambe mwenyeji wa Mbeya, alisema baadhi ya wasanii alioigiza nao filamu hiyo ya vichekesho ni pamoja na Chrispin Masele 'Masele Chapombe' na Erick Ivyoivyo.
"Nimeuanza mwaka mpya kwa kuachia sokoni filamu yangu mpya ya komedi iitwayo 'Urithi wa Kinyambe' ambayo nimeigiza na wakali kadhaa akiwemo Masele na Erick Ivyo ivyo ninaotamba nao kwenye 'Vituko Show'," alisema Kinyambe.
Kinyambe alisema kazi hiyo mpya ni mwanzo wa raha alizojiandaa kuwapa mashabiki wake, kwani pia anajipanga kuwapa burudani katika muziki.
"Mashabiki wangu wakae tayari kupata vitu vizuri, kwani baada ya Urithi wa Kinyambe pia nakamilisha nyimbo zangu kadhaa ili niikamilishe albamu yangu," alisema.
Msanii huyo, alisema nyimbo mpya hizo zinakuja baada ya kuachia vibao vitatu tofauti kama 'Maumivu' alioimba na Baguje, 'Maimuna' alioimba na Leila Tot na Erick Ivyo ivyo na kile cha 'Kiduku Mpapaso' aliomshirikisha Kesse.

Baby J ataka ubunifu zaidi Bongofleva

Msanii Baby J
MSANII anayezidi kuja juu katika muziki wa kizazi kipya nchini, Jamila Abdullah 'Baby J', anayejiandaa kuachia hadharani wimbo wake mpya uitwao 'Nimempenda Mwenyewe' alioimba na Diamond, amewataka wasanii wenzake kuwa wabunifu na kulinda asili yao.
Baby J, alisema ubinifu na kulinda mila na asili ya kitanzania inaweza kuwa njia rahisi ya kujitambulisha kimataifa kuliko tabia ya kuiga kazi za watu na tamaduni za kigeni.
Akizungumza na MICHARAZO katika mahojiano maalum, msanii huyo anayetoka visiwani Zanzibar, Baby J alisema tabia ya kuiga kazi za wasanii wa nje au kuuiga utamaduni wa wa kigeni unawafanya wasanii wa Tanzania kushindwa kujitangaza kimataifa.
Baby J, alisema ni vema wasanii wakaumiza vichwa vyao kubuni vitu vyao wenyewe pamoja na kuhakikisha katika kazi zao zinaegemea katika mila na tamaduni za kitanzania ili hata zikishindanishwa nje ya nchi iwe rahisi kutambulika kuliko ilivyo sasa.
"Kwa kuwa muziki wetu umepiga hatua kubwa kwa sasa kulinganisha na siku za nyuma ni vema sasa wasanii wakabadilika na kubuni kazi zao wenyewe wakizingatia mila na asili ya Tanzania ili kujitambulisha kwa urahisi kimataifa," alisema.
Kuhusu mipango yake, Baby J, alisema kwa sasa yu mbioni kuachia hadharani wimbo wake wa nane uitwao 'Nimempenda Mwenyewe' aliomshirikisha Diamond.
"Wimbo umeshakamilika na utakuwa wimbo wangu wa nane baada ya awali kutoa nyimbo saba nilizoshirikisha wasanii kadhaa nyota kama Chid Benz, Pasha, Ally Kiba na Banana Zorro na wengine," alisema Baby J.
Msanii huyo ambaye ni mke wa mtu alianza kufahamika kwenye ulimwengu wa muziki mwaka 2006 alipotoka na wimbo uitwao 'Mpenzi wa Moyo' alioimba na Taqwa.

YANGA-MBIWA ASAINI MIAKA 5 NEWCASTLE

Mapou Yanga-Mbiwa

NEWCASTLE United wamemsajili beki Mapou Yanga-Mbiwa kutoka katika klabu ya Ufaransa ya Montpellier kwa ada isiyotajwa, inayoaminika kuwa ni paundi milioni 6.7.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23 amesaini mkataba wa miaka mitano na nusu klabuni St James' Park.

Na mshambuliaji wa Bordeaux, Yoan Gouffran amebainisha kwamba pia anajiandaa kutua Newcastle leo.

Aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter:  "Kesho (leo) nitakuwa mchezaji mpya wa Newcastle na najivunia. Shukrani kwa kila mmoja."

Newcastle, ambao tayari wamemsajili beki wa kulia wa Ufaransa, Mathieu Debuchy katika kipindi hiki cha usajili cha Januari, pia wanakaribia kumsajili beki Massadio Haidara kutoka klabu ya Nancy ya Ufaransa pia.

Yanga-Mbiwa alikuwa nahodha wa Montpellier wakati wakitwaa taji lao la kwanza la Ligi Kuu ya Ufaransa, Ligue 1, msimu uliopita aliichezea klabu hiyo zaidi ya mechi 200.

"Ni heshima kutua katika klabu ya Newcastle United na kuwa na nafasi ya kucheza katika Ligi Kuu ya England," alisema. 


CHANZO:STRIKAMKALI

Arsene Wenger amvulia kofia Diame


LONDON, England
KOCHA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amemwagia sifa kiungo wa West Ham na ambaye wanamfukuzia kumnasa katika kipindi hikicha usajili wa dirisha dogo la Januari, Mohamed Diame.
Arsenal wamekuwa wakihusishwa mara kwa mara na usajili wa kiungo huyo mwenye miaka 25, anayeaminiwa kuwa na kipengele katika mkataba wake kinachomruhusu kuondoka ikiwa zitalipwa paundi za England milioni 3.5 (Sh. bilioni 9)
Diame ameonyesha kiwango cha juu na kuibuka kuwa mmoja wa wachezaji nyota wa klabu hiyo msimu huu, akifunga mabao mawili, yakiwamo dhidi ya Arsenal  katika mechi yake ya 18 tangu aanze kuichezea timu hiyo inayoongozwa na kocha Sam Allardyce.
Wenger ameongeza uvumi kuhusiana na kiungo huyo mwenye mwili 'jumba' wa timu ya taifa ya Senegal, akiwaambia waandishi wa habari: "Anafanya vitu vikubwa katika mechi, nimemuona akionyesha kiwango cha juu."
Arsenal ilifungwa 2-1 katika mechi yao dhidi ya Chelsea Jumapili, hivyo kuambulia pointi moja tu katika mechi tatu zilizopita za Ligi Kuu ya England ambazo zinawafanya waachwe kwa pointi saba na mahasimu wao katika kuwania nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England, Tottenham na pia kulingana na Liverpool na West Brom ambao wote wana pointi 34.
Hata hivyo, kuna habari njema kwa Arsenal kufuatia taarifa za kupona kwa kiungo wao Mikel Arteta aliyekuwa nje kutokana na majeraha.

Azam yarejea nchini kamili gado

Kikosi cha Azam

MABINGWA wa Kombe la Mapinduzi, Azam Fc wanatarajiwa kurejea leo usiku Dar es Salaam, wakitokea Nairobi, Kenya walipokwenda kwa ziara ya wiki moja hya michezo ya kujipima nguvu kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
AZAM FC yenye maskani yake Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, ilihitimisha vema ziara yake hiyo jana, baada ya kuifunga timu ya Benki ya Biashara Kenya, KCB bao 1-0 kwenye Uwanja wa City, Nairobi jioni hii.
Bao pekee la ushindi la Azam jioni ya jana lilifungwa na kiungo Ibrahim Mwaipopo kwa shuti la mpira wa adhabu katika dakika ya pili ya muda wa nyongeza, baada ya kutimu kwa dakika 45 za kawaida za kipindi cha kwanza.
Hata hivyo, Azam ingeweza kuondoka na ushindi mnene zaidi jana, kama si kiungo wake mwingine Abdulhalim Humud ‘Gaucho’ kukosa penalti dakika ya 83 baada ya shuti lake la kudakwa na kipa wa KCB.
Huo unakuwa ushindi wa pili katika mechi zake tatu za kujipima nguvu nchini humo, kwani awali bao pekee la Gaudence Exavery Mwaikimba kwa penalti dakika ya 58 liliipa Azam FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Sofapaka ya Kenya kwenye Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
Katika mchezo wake wa kwanza, mabingwa hao wa Kombe la Mapinduzi walifungwa mabao 2-1 na AFC Leopard kwenye Uwanja huo huo wa Nyayo.
Pamoja na kufungwa na Leopard, Azam watajilaumu wenyewe, kwani walipoteza penalti mbili kupitia kwa Joackins Atudo na Khamis Mcha ‘Vialli’.
Mabao ya Leopard katika mchezo huo, yalifungwa na Paul Were na Mike Barasa, wakati la Azam lilifungwa na Sammih Hajji Nuhu kwa penalti.
Azam ilimaliza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ikiwa katika nafasi ya pili kwa pointi zake 24, nyuma ya vinara Yanga waliomaliza na pointi 29, wakati Simba walimaliza nafasi ya tatu kwa pointi zao 23.
Pamoja na Ligi Kuu, Azam pia itacheza Kombe la Shirikisho la Soka Afrika na itaanza na Al Nasir Juba ya Sudan Kusini mjini Dar es Salaam kati ya Februari 15 na 17 mwaka huu.
Mechi hiyo itachezeshwa na marefa wa Kenya, katikati Davies Omweno na atakayesaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Peter Keireini, mwamuzi msaidizi namba mbili Gilbert Cheruiyot wakati mwamuzi wa mezani Anthony Ogwayo.
Kamisaa wa mechi hiyo atakuwa Hassan Mohamed Mohamud kutoka Somalia, wakati marefa wa mechi ya marudiano itakayochezwa mjini Juba wiki mbili baada ya mechi ya kwanza watatoka Rwanda, wakiongozwa na Gervais Munyanziza.


CHANZO:BIN ZUBEIRY

Simba yamalizana na akina Ochieng

Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji iliyokutana Januari 19 mwaka huu chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa, imeliondoa shauri lililokuwa mbele yake dhidi ya klabu ya Simba lililowasilishwa na wachezaji Pascal Ochieng na Daniel Akuffor baada ya pande hizo kufikia makubaliano.
Wachezaji hao kutoka Kenya na Uganda waliwasilisha malalamiko mbele ya kamati wakipinga kukatizwa mikataba yao bila kulipwa stahili zao. Hata hivyo, pande zimefikia makubaliano ya kuvunja mikataba nje ya kamati, na wachezaji hao kulipwa stahili zao.
Simba imekiri vilevile kudaiwa na wachezaji Shija Mkina, Swalehe Kabali, Victor Costa na Rajab Isiaka na kuahidi kuwalipa wachezaji hao wakati Coastal Union na mchezaji wake Mohamed Issa wamefikia makubaliano ya malipo, hivyo kuvunja mkataba kati ya pande hizo mbili.

Wakati huo huo kikosi cha timu hiyo ya Simba kilichokuwa Umangani kinatarajiwa kutua leo na kesho kikitarajiwa kushuka dimba la Taifa, Dar es Salaam kuvaana na Black Leopards ya Afrika Kusini.
Simba na Loepards watapambana katika mechi ya kirafiki ya kimataifa, ikitarajiwa kutambulisha mbinu walizojifunza wakiwa Oman.
Black Leopards leo wanatarajiwa kuvaana na Yanga katika pambano la marudiano litakalofanyika jijini Mwanza.
Pascal Ochieng
Katika mechi yao ya awali Yanga iliwalaza Waafrika Kusini haoa mabao 3-2, jijini Dar na pambano hilo la leo linatarajiwa kuwa na upinzani kila upande ukitamba kufanya kweli.

Masilahi yampeleka Kambi Msondo Ngoma

Muimbaji Athuman Kambi (wa pili toka kulia) akiwa na waimbaji wenzake wa Msondo Ngoma. Kutoka Kushoto ni Hassan Moshi , Eddo Sanga na Juma Katundu

MWANAMUZIKI mpya wa bendi ya Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki', Athuman Kambi amesema kusaka masilahi na kujifunza zaidi muziki ndiko kulikomhamisha kutoka Mlimani Park 'Sikinde'.
Aidha muimbaji huyo anayeshabihiana sauti na mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Hassani Rehani Bitchuka, amewaomba mashabiki wa Msondo kuwa na subira kabla ya kupata vitu adimu kutoka kwake.
Akizungumza na MICHARAZO, Kambi alisema hakuna kitu chochote kilichomtoa Sikinde na kutua Msondo zaidi ya kutafuta masilahi zaidi na pia kujifunza kwa wakongwe waliopo ndani ya bendi hiyo mpya aliyonayo.
Kambi alisema ameondoka Sikinde kwa amani na urafiki bila kugombana na mtu yeyote na kwamba hata kama mambo yatamshinda Msondo iwe rahisi kwake kurejea katika bendi hiyo iliyomtangaza hasa kwa kuweza kuimba kwa ufasaha sauti ya Bitchuka.
"Sijaondoka kwa ugomvi Sikinde, kilichonipeleka Msondo mbali na kusaka masilahi zaidi, lakini naamini nitaongeza ujuzi kwa kujifunza kutokwa wanamuziki waliopo ndani ya bendi hiyo," alisema.
Kambi aliongeza hana cha kuwaahidi kwa sasa Msondo zaidi ya kuomba wampe muda aweze kujipanga ili kuwapa vitu adimu ambavyo hawajawahi kuvipata.
"Wanipe muda nizoee mazingira kisha waone nitawapa kitu gani, ila nimejipanga kuwapa fadhila kwa namna walivyonipokea," alisema.
Muimbaji huyo alijiunga na Msondo wiki mbili zilizopita na tayari ameshaanza mazoezi na kushiriki maonyesho ya bendi hiyo.
-------