STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 13, 2013

Waziri Mulugo aahidi Mil 2 kwa Mbeya City wakiitungua Yanga kesho

http://kifltd.files.wordpress.com/2012/01/01_12_enn75u.jpg
Naibu Waziri Philipo Mulugo

Kikosi cha Mbeya City
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiSJsNsHjk8oZes4gIRZJMglBDLy-cqJ__Id6KV6ouVjbXYivTnjTaWyCOanYX5Ih6OyrwPaHjkzm8Gxz-fLOi_cbctliSDX9r5rqi82IUo5V_Wg7As77JRaNzSAHzEH_bs5dPA0IN52NbE/s1600/IMG_8317.JPG
Kikosi cha Yanga

NAIBU Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo ametanga kutoa dau la Sh Milioni 2 kwa kikosi cha Mbeya City iwapo watafanikiwa kuifunga Yanga katika pambano lao la Ligi Kuu Tanzania Bara linalochezwa kesho kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
Aidha Waziri huyo ameamua kufunga safari kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea mkoani Mbeya kwa ajili ya kuipa sapoti timu hiyo ya Mbeya City katika mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa kandanda mkoani humo.
Waziri Mulugo alisema amefunga safari hiyo ili kuhakikisha timu hiyo ya Mbeya City inapata ushindi dhidi ya mabingwa watetezi hao, Yanga ambao wameshatangaza vita dhidi ya timu hiyo wakitamba wameenda mkoani humo kuzoa pointi sita zikiwamo tatu za mechi ya leo.
Mechi nyingine ambayo Yanga imetangaza kuipigia hesabu ni ile ya Jumatano dhidi ya Prisons Mbeya iliyoanza ligi hiyo vibaya.
Waziri Mulugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songwe  mkoani humo, alisema kwa vile anaamini Mbeya City ni timu nzuri na iwapo ikipata sapoti itafanya maajabu katika mechi hiyo ya kesho na nyingine za ligi hiyo iliyokuw amesimama kwa wiki mbili mfululizo.
Alisema kutokana na hilo ndilo maana amefunga safari kwenda Mbeya kuisapoti timu hiyo na kuahidi kuwapa Sjh Mil 2 iwapo watafanikiwa kuifunga Yanga, aliyokiri ni moja ya timu kubwa yenye uzoefu, lakini bado haamini kama inaweza kufua dafu kwa Mbey City katika mechi hiyo.
"Naifahamu Yanga ni timu nzuri yenye wachezaji wazuri, lakini katika mchezo wa Jumamosi naamini kabisa watabugizwa mabao mengi ya Mbeya City, iliyonilazimu kufunga safari kuja kuisapoti ili ishinde na wakifanya hivyo nitawapa Sh. Mil 2 taslim kama zawadi yao," alisema.
Mbeya City inayonolewa na kocha mzoefu, Juma Mwambusi inashiriki ligi hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kupanda daraja ikiwa na timu nyingine mbili za Rhino Rangers ya Tabora na Ashanti United ya Dar es Salaam na mpaka sasa ina pointi nne kutokana na mechi mbili ilizocheza.
Ilianza kwa kutoka sare ya bila kufungana na Kagera Sugar kabla ya kuicharaza Ruvu Shooting kwa mabao 2-1 katika mechi yao ya mwisho zote zilizochezwa uwanja wa Sokoine kabla ya ligi kusimama kupisha pambano la kimataifa la Taifa Stars dhidi ya Gambia.

ROCK CITY MARATHON 2013 KUZINDULIWA SEPT 19

 Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi, akikata utepe kuzindua Mbio za Rock City Marathon 2012, katika hafla iliyofanyika mwaka jana katika Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.
Wadhamini wa Mbio za Rock City Marathon 2012, pamoja na Mwenyekiti wa BMT, Dioniz Malinzi (wa tatu kulia), wakiwa katika picha ya pamoja katika hafla ya uzinduzi wa mbio hizo mwaka jana uliofanyika katika Hoteli ya New Africa Dar. 

DAR ES SALAAM, Tanzania

UZINDUZI wa msimu wa tano wa mbio za Rock City Marathon 2013 zilizoanza mwaka 2009, zikiwa na lengo la kukuza Utalii wa Ndani kupitia michezo, unatarajia kufanyika Septemba 19, kwenye Hoteli ya New Afrika, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa mbio hizo, Mathew Kasonta, alisema kuwa pamoja na mambo mengine, mbio za mwaka huu za Rock City Marathon, zitakuwa kubwa na bora zaidi kulinganisha na miaka minne iliyotangulia.

“Tuko tayari kwa mbio za Rock City Marathon 2013, zitakzofanyika Oktoba 27. Kamati ya Maandalizi imeweka mikakati mizuri ili kuhakikisha mbio za mwaka huu zinakuwa bora na zenye mafanikio kulinganisha na misimu iliyopita,” alisema Kasonta.

Rock City Marathon zinaandaliwa na Kampuni ya Capital Plus International (CPI), kwa ushirikiano na Chama cha Riadha Tanzania (RT), pamoja na Chama cha Riadha mkoa wa Mwanza (MRAA), ambazo zimewavutia washiriki wengi wa ndani na nje ya nchi.

Kasonta aliongeza kwamba, mbio hizo zitakuwa na vipengele vitano kwa msimu huu, ambavyo ni mbio za kilometa 21 (wanawake na wanaume) na zile za kilometa tano kwa wakimbiaji kutoka makampuni mbalimbali.

Kategori nyingine za mbio hizo ni kilometa tatu kwa watu wenye ulemavu, kilometa tatu kwa watu wazima (zaidi ya miaka 55) na kilometa mbili kwa watoto walio kati ya miaka 7 mpaka 10.

Bw. Kasonta alisema kutokana na uzoefu wa mwaka jana kwa wanariadha wengi kujitokeza kushiriki, kamati ya maandalizi imeongeza idadi ya waongozaji watakaosaidia katika kuzifanikisha mbio hizo.

“Tunatarajia watu wengi kujitokeza mwaka huu, kwa kuwa tuna vitu vizuri kwa msimu huu. Tumejifunza kupitia mbio za mwaka jana, hivyo Kamati ya Maandalizi imekuja na mpango madhubuti utakaoboresha mbio zetu kwa mwaka huu,” alisema Kasonta.

Kivumbi cha FDL kuanza kesho, Kawawa Stadium kutumika Kigoma

JKT Kanembwa wakikaguliwa kwenye michuano ya Miaka 50 ya JKT jijini hivi karibuni jijini Dar
PAZIA la Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL) linatarajiwa kufunguliwa rasmi kesho katika viwanja tofauti, huku uwanja wa nyumbani wa  Kanembwa JKT ya Kigoma sasa utakuwa Uwanja wa Kawawa badala ya ule wa Lake Tanganyika.

Uamuzi wa kuhamishia mechi hizo Uwanja wa Kawawa ulioko Ujiji umetokana na Uwanja wa Lake Tanganyika kutumiwa na Serikali katika Operesheni Ondoa Wahamiaji Haramu inayoendelea nchini kwa sasa. Uwanja huo hivi sasa unatumika kuhifadhi wahamiaji hao.
 

Kanembwa JKT inaanzia nyumbani kwa kuikaribisha Polisi Tabora. Mechi hiyo itachezwa Jumamosi (Septemba 14 mwaka huu).

Mechi nyingine za kufungua dimba za ligi hiyo kuwania nafasi tatu za kucheza Ligi Kuu msimu wa 2014-2014 ni Burkina Faso na Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro, Mkamba Rangers na Lipuli ya Iringa kwenye Uwanja wa CCM Mkamba, Majimaji na Mlale JKT kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea na Kimondo na Kurugenzi kwenye Uwanja wa CCM Vwawa katika mechi za kundi B.
Mechi nyingine kwa kesho ni Tessema na Green Warriors zitaoneshana kazi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Siku inayofuata (Septemba 15 mwaka huu) Transit Camp na Polisi Dar (Mabatini mjini Mlandizi) wakati mechi nyingine za kundi hilo la A zitakuwa kati ya Villa Squad na African Lyon (Karume) na Ndanda FC na Friends Rangers (Nangwanda Sijaona, Mtwara).

Kundi C ni Polisi Mara na Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT na Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United na Mwadui (Kambarage, Shinyanga) wakati Pamba na Toto Africans zitamenyana Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mzee Gurumo kuagwa rasmi Oktoba 11 Diamond Jubilee

 
 
 
Mwenyekiti wa kamati ya kumuenzi Muhidin Maalim Gurumo, Asha Baraka, akizungumza jambo katika kutambulisha onyesho maalum la Gurumo litakalofanyika Oktoba 11 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.Anayefuata upande wa kushoto wa Asha ni mzee Muhdini Gurumo, Juma Mbizo, na Said Kibiriti.
Asha Baraka na wanakamati katika kutambulisha onyesho maalum la Gurumo litakalofanyika Oktoba 11 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam. Anayefuata upande wa kushoto wa Asha ni mzee Muhdini Gurumo, Juma Mbizo, Cosmas Chidumule na Said Kibiriti. Kulia ni Katibu wa kamati Saidi Mdoe
Juma Mbizo, mratibu wa shoo hiyo, akionyesha mfano wa CD itakayouzwa ikiwa ni juhudi za kumuwekea mazingira mazuri mwanamuziki Muhdini Gurumo, baada ya kutangaza kustaafu muziki. Picha zote na Kambi Mbwana
MWANAMUZIKI mkongwe aliyestaafu muziki akiwa na bendi ya Msondo Ngoma, Muhidini Maalim Gurumo, ameandaliwa shoo mbili za kumuaga, moja wapo ikipangwa kufanyika Oktoba 11, ikiwa ni VIP, katika Ukumbi wa Diamond Jubilee. 
Shoo nyingine kwa wapenzi wote itafanyika Novemba Mosi mwaka huu katika Ukumbi wa TCC Sigara Chang’ombe, jijini Dar es Salaam, zote zikiwa na lengo la kumuaga kwa heshima mwanamuziki huyo na kumpa nafasi ya kuyamudu maisha yake baada ya kuachana na muziki. 
 Akizungumza leo na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa shoo hiyo iliyopewa jina la (Gurumo 53), Asha Baraka, alisema kuwa ni heshima kuwa na mwanamuziki kama Gurumo, hivyo wadau wameamua kuandaa shoo hizo za kumtafutia fedha mkali huyo. 

 Alisema wazo hilo limefanyiwa kazi kwa pamoja, akiwa na wadau kadhaa, akiwamo Said Mdoe Katibu wa Kamati hiyo, Richard Sakala mjumbe, Cosmas Chidumule, Waziri Ally, Said Kibiriti na Juma Mbizo, ambaye ndio mratibu wa Kamati hiyo. 

 ”Lengo si kumpa karatasi za kuthamini mchango wake katika tasnia ya muziki wa dansi Tanzania, ila kuhakikisha kuwa anapata mwangaza wa maisha yake baada ya kuachana na muziki. 

 ”Huyu ni mwanamuziki mwenye uwezo wa juu wakati huo, hivyo kwa sasa lazima sisi wadau tuhakikishe anajiweka katika ramani nzuri, ikiwa ni kutambua ataishi vipi nje ya muziki,” alisema.

Naye Gurumo aliwaambia waandishi wa habari kuwa ameamua kuachana na muziki kwa sababu umri na afya yake hairuhusu kufanya kazi hiyo, hivyo asitokee mtu wa kupotosha ukweli wake huo. 

 ”Nasikia watu wanasema naachana na muziki Msondo nikiwa na lengo la kurudi tena Sikinde, jambo ambalo si kweli kwa kuwa sioni nitamuimbia nani wakati nimechoka. 

 ”Naomba kwa sasa kuwapa nafasi watu waliojitolea kunisaidia hasa kwa kuunda kamati hii ambayo nitapanda jukwaani kuimba mara ya mwisho, ukizingatia kuwa kazi yangu inahitaji kuagana na mashabiki wangu jukwaani na si mahali pengine,” alisema. 

 Katika hatua nyingine, mwanamuziki Cosmas Chidumule, alisema kuwa licha ya kuwa ameokoka, ila atapanda jukwaani kuimba na mzee Gurumo kama sehemu ya kutambua mchango wake.

”Nimeokoka lakini si sababu ya kunifanya nishindwe kumheshimu mwanamuziki ambaye nina uhakika mchango wake ulinifanya niwe juu katika muziki wa dansi Tanzania,” alisema.

 Kwa mujibu wa Kamati hiyo ambayo Mdoe ndio Katibu wake, taratibu zote zinaendelea ikiwa ni kuandaa nyimbo alizowahi kuimba na kuziweka katika mfumo wa kibiashara, ikiwamo mpango wa kuuza nyimbo zake katika makampuni ya simu za mikononi.

SGM ruksa kukipiga Ashanti Utd, wawili waombewa ITC

Said Maulid 'SMG'
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa Watanzania wawili kucheza mpira wa miguu nchini Afrika Kusini.

Wachezaji hao; Robert Kobelo na Mohamed Ibrahim wamepewa hati hizo baada ya kuombewa na Chama cha Mpira wa Miguu Afrika Kusini (SAFA) kama wachezaji wa ridhaa ili wajiunge na klabu ya Cacau United ambayo timu yake inacheza Ligi Daraja la Pili katika Wilaya ya Cacau.

Naye mchezaji Said Maulid aliyejiunga na Ashanti United akitokea nchini Angola msimu huu amepata ITC ambayo sasa inamwezesha kuchezea timu hiyo katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inayoingia mzunguko wake wa tatu keshokutwa (Septemba 14 mwaka huu).

TEMEKE, MJINI MAGHARIBI KUCHEZA NUSU FAINALI COPA COCA COLA LEO

TEMEKE na Mjini Magharibi zinapambana leo (Septemba 13 mwaka huu) katika mechi ya nusu fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 itakayofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam.

Timu hizo zimetinga hatua hiyo baada ya kushinda mechi zao za robo fainali ya michuano hiyo zilizochezwa jana (Septemba 12 mwaka huu) asubuhi kwenye uwanja huo huo.

Wakati Temeke imetinga hatua hiyo baada ya kuilaza bao 1-0 Iringa lililofungwa dakika ya 18 na Ramadhan Mohamed, Mjini Magharibi imeing’oa Mtwara kwa ushindi wa bao 1-0.

Robo fainali nyingine zinachezwa leo (Septemba 12 mwaka huu) jioni kwa Kilimanjaro kuvaana na mabingwa watetezi Morogoro huku Arusha ikioneshana kazi na Ilala.

Thursday, September 12, 2013

Bondia Afa ghafla mazoezini, ni 'Tembo Mtoto'

BONDIA Yohana Mathayo 'Tembo Mtoto' amefariki dunia jioni ya jana akiwa mazoezini kwake eneo la Kigogo Mburahati Dar es Salaam.
Kifo hicho kilimkuta ghafla wakati akifanya mazoezi ya kujiandaa na mpambano wake wa ubingwa uliopangwa kufanyika hivi karibuni.
Taarifa za kifo cha bondia huyo aliyekuwa akizidi kupanda chati nchini miongoni mwa mabondia vijana, zilitolewa na kocha wake Kwame Mkuruma, aliyedai mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwao Manzese na huenda akasafilishwa kwenda kuzikiwa kwao mkoa wa Tanga.
Mungu ametoa na Mungu ndiye aliyetwaa. Roho yake ilale mahali pema ila Yohana Mathayo 'Tembo Mtoto' utakumbukwa daima na wadau wenzako wa ngumi umetangulia nasi tu nyuma yako.
Bondia huyo mwenye rekodi ya kucheza michezo 7 ya ngumi za kulipwa akiwa ameshinda mara 4 na kupigwa mara moja na  droo mara mbili.  Marehemu huyo enzi za uhai wake  alijiunga na ngumi za kulipwa mwaka 2011 ambapo mchezo wake wa kwanza kacheza na Seba Temba wa Morogoro ambapo alitoa nae droo na mchezo wake wa mwisho kucheza ni Agosti 9 mwaka huu ambapo alishinda kwa TKO ya raundi ya pili dhidi ya Shujaa Keakea.

SHIWATA YAANZA KUKABIDHI NYUMBA KWA WANACHAMA WAKE< YATOA SHUKRANI MKURANGA

Mchezaji na Kepteni wa zamani wa Timu ya  Taifa Stars, Jella Mtagwa (kushoto) akipokea cheti cha nyumba aliyokabidhiwa na SHIWATA na eneo la robo ekari ambalo anatarajia kujenga nyumba kubwa
Mwanachama huyu wa SHIWATA kulia ameamua kujijengea nyumba yake pole pole hapa akikabidhiwa cheti chake
Mmoja wa wanachama wa SHIWATA, Emmanuel Ntumbii na mkewe wakipokea cheti cha kumilikishwa nyumba yake akishuhudiwa na wanachama wenzake.
Mwandishi wa Habari, Josephine Joseph akionesha cheti alichokabidhiwa na SHIWATA mbele ya nyumba yake katika sherehe ya kukabidhi nyumba za wasanii,Mkuranga.
Mkuu wa wilaya mstaafu, Bw. Henry Clemence akizungumza katika sherehe ya kukabidhi nyumba 38 za wasanii wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) katika kijiji cha Mwanzega, Mkuanga.


BAADA ya kukabidhi nyumba kwa wanachama 38, SHIWATA inatoa shukurani kwa viongozi wa kijiji cha Mwanzega Kata ya Mbezi, Tarafa ya Shungubweni,wanavijiji pamoja na viongozi wa wilaya ya Mkuranga akiwepo Mkuu wa wilaya, Mercy Silla kwa kufanisha sherehe ya ugawaji nyumba na vyeti.

Wanachama zaidi ya 70 wamejitokeza kuchangia ujenzi wa nyumba ili wakabidhiwe Desemba 28, 2013 katika sherehe nyingine ya kukabidhi nyumba ambayo inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali ambao waliomba udhuru sherehe ya awali.

SHIWATA inawahimiza wanachama wake wasifanye mzaha na kudharau mpango wa kuchangia ujenzi kwani utawanufaish na kuwamilikisha nyumba zao wenyewe kwa gharama nafuu.

Mtandao wa wasanii unatoa bure viwanja baada ya mwanachama kulipa gharama zote za kujiunga uanachama ambaye ataruhusiwa kujenga mwenyewe au kuchangia ujenzi wa nyumba kwa pamoja.

SHIWATA  inakusudia kujenga Shule ya Msingi, Sekondari na vyuo vya fani za utamaduni, Uandishi wa Habari na michezo mbalimbali ikiwemo soka kwa malengo ya kupata wachezaji bora ambao watanyanyua viwango vya michezo hiyo ndani na nje ya nchi ili kuwapatia vipato zaidi.

Pia inawahitaji wasanii, wanamichezo, wanahabari wenye vipaji na elimu ya juu katika fani zao wajiunge na SHIWATA ili waweze kuwa walimu wa sanaa na michezo mbalimbali ambayo itaanza kufundishwa kutoka ngazi ya Shule ya Msingi, Sekondari hadi Chuo katika kijiji cha Mwanzega.

Shule ya msingi itakapoanzishwa itatoa kipaumbele kwa masomo ya sanaa na michezo ili kupata wasanii na wanamichezo bora katika taifa letu.
SHIWATA pia inatarajia kujenga viwanja vya michezo, kumbi za Maonesho na Studio za kurekodia muziki na filamu zenye ubora ambazo zitauzwa ndani na nje ya nchi.

Wednesday, September 11, 2013

Walimu wajiandaa kugoma tena, kisa deni lao la Sh Bil 33

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgLy8pkk8A5UEzHJnD7gZMhQ25ia2Z2aWm3mWxyySq1BfXEhznl2nxMyd3ae2xtH8Zp78t_p5qDcFAJvzos2YCXtMVmmm_cWM8NLFz25_QgYOtKbEyqhKG8ZOOG_Agk1Wg4xJHaTmpR_0hq/s640/1.jpg
WALIMU nchini wameipa serikali muda wa mwezi  mmoja kabla ya kuingia tena kwenye mgomo kwa ajili ya kushinikiza walipwe malimbikizo ya madeni yao yanayofikia Sh. Bilioni 33.
Tishio hilo limetolewa na uongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ambapo kimesema kinatoa muda wa mwezi mmoja tu kwa serikali kuweza kulipa fedha hizo la sivyo wataingia kwenye mgomo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Rais wa chama hicho, 
Gratian Mukoba, alisema wamechoka kupewa ahadi hewa na serikali ndio maana wamefikia hatua hiyo.

‘Tumetoa mwezi huu wa tisa uwe wa mwisho kuililia serikali, baada ya hapo tutaamua hatua gani tufanye, maana tumekutana na makatibu wakuu wa wizara zinazowahudumia walimu lakini bado tunaishia kupewa ahadi hewa,” alisema Mukoba.

Mukoba aliongeza kuwa Agosti 14, mwaka huu, walikutana na makatibu wakuu wanaowahudumia walimu pamoja na Katibu Mkuu ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma, wakatakiwa kuwasilisha madai yao yote.

“Tulikutana na makatibu, katika kikao hicho, tuliwafahamisha kuwa walimu wanaidai serikali zaidi ya sh bilioni 33 na mwisho wa kikao hicho tulikubaliana CWT iwakilishe madai hayo ndani ya wiki mbili,” aliongeza Mukoba.

Mukoba alisema wiki mbili zilipofika, walienda kuonana tena na Katibu Mkuu, ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na kuwasilisha vitabu vyenye madai mbalimbali ya walimu.

“Madai hayo tuliyaambatanisha kwenye barua Na CWT/004/UTMS/VOL.11/94 na madai hayo sasa yamefikia sh bilioni sita,” alisema Mukoba.

Mukoba aliishangaa serikali kuanzisha Mpango wa Matokeo Makubwa sasa “Big Result Now”, huko walimu ambao ndio watekelezaji wakubwa wa mpango huo, wana maisha magumu kutokana na mishahara kuwa midogo na kuzidi kwa malikimbizo ya madeni yao.

“Walimu ambao ndiyo watelekezaji wakuu wa mpango huu japo hawaelewi au hawajapewa semina elekezi, lakini ndio watekelezaji wakubwa.

Naishangaa serikali kuwadharau walimu na nakuhakikishia mpango huo hautafanikiwa kama walimu hawapati haki zao,” alisema Mukoba.

Mukoba aliionya serikali ikamilishe madai ya walimu ili wafanye kazi kwa moyo tofauti na sasa ambapo wengi wamekata tamaa.

‘‘Walimu wa nchi hii wamekata tamaa. Mioyo yao imekufa ganzi kwa sababu serikali imekataa kuwalipa malimbizo yao.

Kwa nini serikali imeamua kuwatendea jeuri walimu kiasi hiki?” alihoji Mukoba.

Kombe la Chalenji kupigwa Kenya Nov.

Musonye (kushoto) mbele ya Kombe la Chalenji
MICHUANO ya Kombe la Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati mwaka huu imepangwa kufanyika kuanzia Novemba 22 hadi Desemba 8 nchini Kenya.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu kutoka Nairobi, katibu mkuu wa Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye, alisema kuwa tayari maandalizi ya mashindano hayo ya kila mwaka yameanza.

Musonye alisema kuwa anaamini nchi wanachama zitatumia mashindano hayo kuandaa timu zao kwa ajili ya michuano ijayo ya Kombe la Mataifa ya Afrika itakayofanyika mwaka 2015.
"Tumeshaanza maandalizi ya mashindano ya Chalenji na kwa asilimia mwenyeji atakuwa ni Kenya, taarifa zaidi tutaendelea kuzitoa," alisema Musonye.

Alisema kuwa sekretarieti ya shirikisho hilo imeshaanza kuwasiliana na nchi wanachama ili kuandaa timu na kutuma majina ya waamuzi watakaokwenda kuchezesha michuano hiyo.

Rais wa KFF, Sam Nyamweya, alikaririwa akizungumza jijini Nairobi mwishoni mwa wiki akisema kwamba Kenya imejiandaa kuwa wenyeji wa michuano hiyo na wanaamini watafanya vizuri kuliko miaka iliyopita.
Nyamweya alisema kuwa michuano hiyo inatarajiwa kufanyika katika miji miwili ambayo ni Nairobi na Kisumu.

"Ila bado Kisumu hawajathibitisha kuwa wenyeji," alisema rais huyo ambaye mwaka jana alishuhudia Harambee Stars ikilala dhidi ya wenyeji, Uganda (The Cranes) katika mechi ya fainali kwenye uwanja wa Mandela uliopo Namboole.

Mara ya mwisho Kenya kuandaa mashindano hayo ilikuwa ni mwaka 2009 na michuano hiyo ilifanyika Nairobi na Kakamega.

Timu ya taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) mwaka jana ikiongozwa kwa mara ya kwanza na kocha Kim Poulsen, ilimaliza katika nafasi ya nne baada ya kufungwa na 'ndugu zao' Zanzibar Heroes kwenye mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu.

CHANZO: NIPASHE

Wanafunzi Darasa la Saba waanza mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjT7UvQDBDmuLVn_p3H5eug8q68KSNsJew7-nXPZkWNTWzV8chyEsYyyTgkkoX7Su7X1IdCkfX0iTVkVnqrH3Pvz3j10-7TZD7kyYljop9BsIP9k4rtKp37uvPfTkzjBeVrTH9u8L9CgKc/s640/MITIHANI+YA+DARASA+LA+SABA+MORO+2.jpg
Kazi itakuwa kama hivi, wengine wanajaza wengine wakitafakari kwa kina katika mitihani iliyoanza leo kwa wahitimu wa darasa la 7 nchini

JUMLA ya wanafunzi 868,030 wa Darasa la Saba nchini, leo na kesho wanatarajia kufanya mtihani wa kuhitimu elimu yao ya msingi katika  michepuo miwili, wa Kiswahili na Kiingereza.

Mitihani hiyo imeanza asubuhi ya leo katikma shule mbalimbali nchini, ambapo kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, mtihani huo utakaojumlisha masomo matano, utafanyika kwa siku mbili kuanzia leo na kesho Alhamisi.

Kati ya idadi hiyo ya wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani huo, wavulana ni 412, 105 sawa na asilimia 47, na wasichana 455, 925 sawa na asilimia 52.52. Jumla ya masomo matano yanatarajiwa kutahiniwa na wanafunzi hao ambayo ni pamoja na Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii.

Kwa mujibu wa Mulugo, wanafunzi 844, 810 wanatarajia kufanya mtihani huo kwa lugha ya Kiswahili, ambao kati yao wavulana ni 400, 335 na wasichana 444,575, huku 22, 535 watafanya kwa lugha ya Kiingereza, ambao wavulana ni 11, 430 ma wasichana 11, 105.

Mulugo alitaja kundi lingine la wanafunzi ambao wanakwenda kufanya mtihani kuwa ni pamoja na lile la wasioona ambao idadi yao ni 88, wavulana 56 na wasichana 32, huku wale wenye uoni hafifu na ambao wanahitaji maandishi makubwa ni 597.

Kati ya watahiniwa hao wenye uoni hafifu, wanaotarajia kufanya mtihani huo kwa lugha ya Kiswahili ni 546, wavulana 263 na wasichana 283, na wale watakaofanya kwa Kiingereza ni 51, wavulana 21 na wasichana 30.

Alisema maandalizi yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa fomu maalumu za OMR za kujibia mtihani na nyaraka zote muhimu huku akiwaagiza maafisa elimu wa mikoa na halmashauri kuhakikisha mazingira yanakuwa tulivu na kuzuia mianya yote ya udanganyifu wa mitihani.

Mulugo pia aliwataka wasimamizi  kusimamia kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu.

Sambamba na hilo, aliwaasa wanafunzi wote kutojihusisha na vitendo vyovyote vya udanganyifu wa mtihani kwani watakaobainika kufanya hivyo watafutiwa matokeo yao yote ya mtihani.
MICHARAZO inawatakia kila la heri wanafunzi hao katika mitihani yao ili waweze kuifanya kwa amani na utulivu na ahatimaye wafaulu Inshallah.

Ajiua akijifanyia operesheni ya kujiondoa uvimbe tumboni

MKAZI mmoja wa kijiji cha Sadoto, Kata ya Sengarewa wilaya Ukerewe, amefariki dunia baada ya kujifanyia upasuaji wa kujiondoa uvimbe tumboni mwenyewe.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka wilayani humo, zinasema kuwa, Sitta Manoni mwenye umri wa miaka 44 alikuwa akisumbuliwa kwa muda mrefu na uvimbe tumboni, lakini hakuwa na uwezo wa kwenda kujitibia hospitalini na hivyo juzi aliamua kuchukua kiwembe na kujipasua uvimbe huo.
Hata hivyo mashuhudu wa tukio hilo wamedokeza kuwa mara baada ya kujifanyia operesheni hiyo ya 'kienyeji' majirani zake waliamua kumkimbiza hospitalini baada ya kumuona yupo kwenye hali mbaya na kufariki njiani.

Serikali yamkumbuka Mzee Gurumo

IMG_6952Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni, Bibi. Lilly Beleko kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo akimkabidhi Mzee Muhidini Gurumo barua kama ishara ya Serikali kutambua mchango wake uliotukuka katika tasnia ya Muziki nchini pamoja na kumpongeza kwa kustaafu kazi kazi hiyo, hivi karibuni nyumbani kwake Makuburi, Jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia nyuma ya Mkurugenzi ni Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Bw. Addo Mwasongwe na kulia pembeni ya Mzee Gurumo ni Mkewe, Bibi. Pili Said Kitwana.IMG_6981Nguli wa Muziki wa Dansi, Mzee Muhudini Gurumo (aliyevaa shati la drafti) akiwa na watumishi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, walipomtembelea nyumbani kwake Makuburi Jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Serikali kupitia Wizara hiyo ilimkabidhi barua rasmi Mzee huyo kutambua mchango wake katika tasnia ya Muziki na kumpongeza kwa kustaafu kazi hiyo. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni, Bibi Lilly Beleko, wa pili ni mke wa Mzee Gurumo, Bibi. Pili Said Kitwana na wa Pili Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Wizara Upande wa Sanaa, Bibi. Joyce Hagu. Picha zote na Concilia Niyibitanga Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
………………..
Na Concilia Niyibitanga- WHVUM
SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imempongeza Mzee Muhidini Gurumo kwa mchango wake uliotukuka katika tasnia ya Muziki nchini pamoja na kumpongeza kwa kustaafu kazi hiyo.
Akiwasilisha barua ya Serikali ya kutambua mchango wa nguli huyo juzi nyumbani kwake Makuburi Jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bibi. Lilly Beleko amesema kuwa Serikali inatambua na kuthamini  mchango wake katika muziki wa Dansi hapa nchini.
‘Serikali inathamini mchango wako katika Muziki hapa nchini na itaendelea kuzienzi kazi hizo na inakupongeza kwa kazi nzuri ulioifanya ya kuelimisha, kuhamasisha na kuburudisha jamii’. Amesema Bibi. Beleko.
Naye Rais wa Shirikisho la Muziki nchini, Bw. Addo Mwasongwe, amesema kuwa Shirikisho linampongeza kwa kazi zake nzuri na litaendelea kumtumia katika kazi za muziki ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri katika tasnia hiyo.
Nguli huyo wa muziki wa dansi nchini katika enzi zake za uimbaji ametunga nyimbo za kuelimisha jamii kufanya kazi kwa bidii, kudumisha usawa, amani na kuwakumbusha wazazi kutimiza wajibu wao wa kuwalea watoto katika maadili mema.
Mzee Gurumo ambaye ameanza kazi ya muziki mnamo miaka ya 1960 na kustaafu kazi hiyo mwaka huu amesema kuwa anaishukuru Serikali kwa kutambua kazi yake na amefarijika kwa kukabidhiwa barua ya kumtambua na kumpongeza kwa kustaafu kazi hiyo.

Kili Music Tour 2013 kuhitimishwa kwa kishindo Dar J'Mosi


 Hitimisho la Kili Music Tour 2013.
 Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusiana na tamasha kubwa la "Kili Music Tour litakalofanyika siku ya Jumamosi katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam, ambapo kiingilio kitakuwa sh. 2500 pamoja na  bia moja ya bure. (Picha na Francis Dande)
 Ben Pol akizungumza kuhusu tamasha hilo.
 Nasib Abdul 'Diamond Platinum'
Kala Jeramiah

Tuesday, September 10, 2013

TMK yaifumua Rukwa Copa Coca Cola


TIMU Temeke imejiweka katika nafasi nzuri ya kucheza robo fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 baada ya leo (Septemba 10 mwaka huu) asubuhi kuizamisha Rukwa mabao 5-1.

Hadi mapumziko katika mechi hiyo ya kundi B hatua ya Fainali za Taifa iliyochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam, washindi walikuwa mbele kwa mabao 3-0.

Mabao ya washindi yalitiwa wavuni na Constantine Katepa aliyefunga dakika ya 28, Patrick Ambrose dakika ya 36 huku Hamisi Kajole akipiga mawili dakika ya 43 na 71. Bao la nne lilifungwa dakika ya 46 na Ramadhan Juma.

Rukwa ambayo kwa matokeo hayo imeshatolewa ilipata bao lake dakika ya 51 kupitia kwa Francisco Nkanga. Timu nyingine katika kundi hilo ni Geita na Ilala.

Robo Fainali ya michuano hiyo itaanza keshokutwa (Septemba 12 mwaka huu). Kila kundi linatoa timu mbili kucheza hatua hiyo katika mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Coca-Cola.

TFF yamfungia Pondamali, refa wa Yanga na Coastal

Juma Pondamali (kushoto) akimlisha ujuzi Kaseja Taifa Stars
Na Boniface Wambura
KAMATIi ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imempiga faini ya sh. milioni moja na kumfungia miezi mitatu kocha wa makipa wa timu ya Coastal Union Juma Pondamali kwa kuwatukana washabiki wanaominika kuwa wa Simba.
Pondamali alifanya kosa hilo katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya timu yake na Yanga iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Mwamuzi Martin Saanya na mwamuzi msaidizi namba moja Jesse Erasmo waliochezesha mechi kati ya Yanga na Coastal Union nao wamefungiwa mwaka mmoja kila mmoja kwa kutoimudu mechi hiyo.

Nayo Yanga imepigwa faini ya sh. milioni moja (sh. 500,000) kwa kila kosa kutokana na washabiki wake kuwarushia waamuzi chupa za maji baada ya Coastal Union kusawazisha bao katika mechi hiyo. Pia waliwarushia chupa waamuzi hao wakati wakirejea vyumbani baada ya pambano hilo.

Vilevile Coastal Union imepigwa faini ya sh. 100,000 baada ya kuchelewa kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting). Timu hiyo ilichelewa kwa dakika 23. Kikao kinatakiwa kuanza saa 4 kamili asubuhi.

Kivumbi cha FDL kuanza Jumamosi, Kimondo Kurugenzi kuvaana Mbozi


Na Boniface Wambura
Timu za Kimondo SC ya Mbeya na Kurugenzi ya Mafinga zitatumia viwanja vya Mbozi na Mafinga kwa ajili ya mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoanza Jumamosi (Septemba 14 mwaka huu).

Kimondo SC sasa itatumia Uwanja wa CCM Vwava ulioko wilayani Mbozi badala ya Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine wa jijini Mbeya. Nayo Kurugenzi itatumia Uwanja wa Wambi ulioko Mafinga mkoani Iringa badala ya Uwanja wa Makambako ulioko mkoani Njombe.

Mechi za fungua dimba FDL msimu huu zitakuwa kati ya Burkina Faso na Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro, Mkamba Rangers na Lipuli ya Iringa kwenye Uwanja wa CCM Mkamba, Majimaji na Mlale JKT kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea na Kimondo na Kurugenzi kwenye Uwanja wa CCM Vwawa katika mechi za kundi B.

Septemba 14 mwaka huu Tessema na Green Warriors zitaoneshana kazi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Siku inayofuata (Septemba 15 mwaka huu) Transit Camp na Polisi Dar (Mabatini mjini Mlandizi) wakati mechi nyingine za kundi hilo la A zitakuwa kati ya Villa Squad na African Lyon (Karume) na Ndanda FC na Friends Rangers (Nangwanda Sijaona, Mtwara).

Kundi C ni Polisi Mara na Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT na Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United na Mwadui (Kambarage, Shinyanga) wakati Pamba na Toto Africans zitamenyana Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mademu toka Kenya, Nigeria kuvaana Okt

DAR ES SALAAM, TANZANIA - You can easily liken her with a PIII student or a fresh model who happen to put on gloves but, there is more to this affably pretty and shy Kenyan boxing star Sarah Achieng than you can chew. To start with, she is known as the defender of the underprivileged in her area and she takes no cue from anybody who want to undermine those close to her. The beautiful paid ranked slugger known for her hard hitting ferocity punches. Her fury in the ring is not easily contained.

sarah achieg
The Beautiful Goddess Sarah Achieng from KENYA 
 
Sarah Achieng derive from  the Western Kenyan city of Kisumu. She was raised by a fish mongering family and to her; fish diet is what made her skin health, soft and beautiful. She was once a finalist to the beauty parget. Sarah is BLACK, sweet, warm, soft and strong AFRICAN whose only purpose in the ring is to dispatch her opponents as fast as she can.
 
Now she has to wait until October 4, 2013 when her fury and ferocity punches may be properly utilized but, alas to whom other than the Princess Royal of African boxing Helen Joseph, the one and only "IBF Intercontinental Female Featherweight Champion".
This may be an ominous task for beautiful Sarah who want to emulate her heroines Conjestina Acheing better known as Conje to her friends and Kenyan public at large. Sarah Achieng (not  related to Conje) is an astute beautiful woman who happen to take a different turn in life and embrace boxing. She is the cutest of all the female boxers that Kenyan has ever had and a darling of the media as would the public.
 
Helen Joe 
Princess Royal of African boxing Helen Joseph from NIGERIA
 
Together with Conjestina Achieng they have feminizing Kenyan boxing fraternity with the tonic of their beauties! This is perhaps why most Kenyans identify with the name "Achieng"
 
Sarah's journey and her comfortable life in the SHOW BIZ would be majored by how far she can contain the amazingly punching power of the Ghanaian based Nigerian Princess Royal of African boxing Helen Joseph. Now the duo will meet in October 4, 2013 at the Accra National Sports Stadium. They would join other Ghanaian boxing luminaries the like of Issa Samir and Aryee Ayittey as they hassle each other for the "IBF World Youth Jr. Middleweight Title".
 
The two beautiful sluggers would be inline for the "IBF Intercontinental Female Featherweight Title" which Princess Royal of African boxing Helen Joseph won against the beautiful Hungarian slugger Mariana Guyas on May 3rd, 2013. Helen has promised her fans to spit fires and defend her title with all what she has. She will welcome Sarah with her open arms but, reminded her of the consequences that comes with her heroine attempt!
 
This would be yet another epic battle for Ghana that is reeling from recent breathtaking and star studded IBF competitions and this one would surely give boxing spectators their money worth.
 
Discussing the strategies used to enlist so many star boxers in his stable, Henry Manly-Spain who is the CEO of the Golden Concept Business Group tells the story of nationalism and business acumen. Manly-Spain's only interests is to equip Ghanaian boxing fraternity with several world acclaimed boxers who would promote the great nation of Ghana to the international scene.
 
"Boxing is tourism. It is business. It is economy. It is life."  said Manly-Spain. "We would use boxing to promote this great nation which Osagyfo Kwame Nkrumah made it Paradise for all those who are seeking freedom and prosperity" concluded this major businessman who is known as the Muttest (Godfather) to his friends.
 
The questions in the minds of many boxing fans is who would emerge the winner between these two beautiful sluggers? This one billion dollars question will be answered on October 4, 2013 as the two African beauties KISS the face of "SWEET SCIENCE"
 
Watch this space for more news on Helen Joseph and Sarah Achieng's rumble for October 4, 2013  
 
Congratulations TEAM Helen/Sarah: Henry Manly-Spain, Kofi Dukku-Rackets and Micahel Tetteh. Africa is proud of you!   

"Nothing else like IBF/AFRICA as it advances African interests to the Global professional boxing fraternity"   

They Call it AFRICA...! We Call it HOME. 
 
The United States Boxing Association (USBA) and International Boxing Federation (IBF) continental body to Africa, Middle East & Persian Gulf

Mesut Ozil akandia Real Madrid

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4ofh6d-gXibmGvc2xSsD8UfdtNJEaoqFh5VR-k8V5ZtbFQkA38OgBh_eW2UhZjNmxZJun5lUreGf6kmv9B3JxAoWcDyI6DqafsqZSqnXRzd4hrsJsA7mPvEmI-S1M0stt-cf073BC4981/s640/Mesut+Ozil+2013_1.jpg
MESUT Ozil amedai kwamba angejiunga Arsenal hata bure  na amebainisha kwamba "uwazi, kuaminiwa na kuheshimiwa" vilipotea Real Madrid.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani alikamilisha uhamisho wake wa siku ya mwisho ya usajili na kutua katika kikosi cha Arsene Wenger kwa dau la uhamisho la paundi milioni 40, akisaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo.
Ozil alibainisha kuwa mazungumzo na kocha huyo wa Arsenal yalimshawishi kupima hali yake ndani ya Real Madrid na kumvutia kuhamia kwenye Ligi Kuu ya England.
“Kwa namna fulani, mazungumzo yale yalinivutia kuhama na kunifanya nitambue kuwa nilichokipoteza Madrid: uwazi, kuaminiwa, kuheshimiwa," Ozil aliliambia gazeti la Die Welt.
"Yeye (Wenger) aliniambia vile anavyoniona, namna anavyonihitaji, na kile anachotarajia kutoka kwangu.
"Siwezi kufanya chochote kuhusu ada ya uhamisho. Ningeweza kuja hata bure."
Ozil, mchezaji aliyenunuliwa kwa ada iliyovunja rekodi ya uhamisho kwa Arsenal, alifunga ama kutoa pasi za magoli 108 katika mechi 159 katika michuano yote akiwa na Madrid.

Kumekucha tamasha la wanafunzi la Mtakuja J'mosi hii


BAADA ya kimya kirefu tangu kufanyika kwa mara ya mwisho kwa tamasha  wanafunzi hasa wa shule za Sekondari, uongozi wa Mtakuja Secondary School iliyopo Kunduchi kwa kushirikiana na mtangazaji maarufu Allan Lucky 'Rais wa Wanafunzi' wa kipindi maarufu cha Skonga ambacho hurushwa kupitia televisheni ya vijana ya EATV umeandaa tamasha la wanafunzi linalotarajiwa kuhudhuriwa na wanafunzi zaidi ya 3000 kutoka shule zaidi ya 20 za jijini Dar.
 
Tamasha hilo lenye lengo la kuwakutanisha wanafunzi wa shule mbali mbali za Dar-es-salaam kwa pamoja na kupata changamoto kimawazo na kiburudani, pia kuwakutanisha wadau mbali mbali wa elimu katika kufanikisha uboreshwaji wa elimu na kusaidia katika kutekeleza mpango wa 'Matokeo Makubwa Sasa', linatarajiwa kufanyika Jumamosi  katika viwanja vya shule hiyo.

Miongoni mwa shule ambazo zitashiriki ni: Mtakuja, Kondo, Jordan, St. Gasper, Mbezi Beach, Boko, Goba, Twiga, Maendeleo, Mwambao, Kisauke, Kinzudi, londa, Makongo, Kawe Ukwamani, Tegeta, Mbweni, Teta, Hananasif na Mtongani, zote ni za sekondari.

Tamasha hilo linatarajiwa kuhusisha wadau mbali mbali wa elimu watakaokutana katika kubadilishana mawazo na kupata burudani kwa kushuhudia vipaji lukuki walivyo navyo wanafunzi kutoka shule mbali mbali.

Miongoni mwa shughuli zitakazoendeshwa ni pamoja na maswali na majibu, fashion show, uimbaji, ufokaji, na wanafunzi wenye vipaji mbali mbali maalum watapewa nafasi.

Msemaji wa tamasha hilo ambaye pia ni mwalimu wa michezo wa Mtakuja Beach Sekondari Bw Misonji Charles amewataka wadau mbali mbali wa elimu kuhudhuria na kushuhudia vipaji vya wanafunzi mbali mbali na pia amewataka waandishi wa habari kujitokeza kwa wingi katika kuchukua habari na matukio mbali mbali yatakayojitokeza. Pia amewaomba wadau mbali mbali wenye uwezo wa kuchangia katika kufanikisha tamasha hili wajitokeze, kwa kuwa linaandaliwa kwa nguvu za shule na kamati maalum ya maandalizi pekee.

Kwa maelezo na kama unataka kushiriki, tafadhali wasiliana na Msemaji wa Tamasha Bw Misonji Charles kupitia 0714642442.