STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 5, 2014

NI DIAMOND PLATNUMZ TENA! CHANNEL O YAMTEUA X4 ORODHA HII HAPA

http://larrybway91.files.wordpress.com/2014/04/diamond-platnumz.jpg?w=594SUPASTAA Diamond ameendelea kutusua anga la kimataifa baada ya Channel O ya Afrika Kusini kumteua katika vipengele vinne kuwania tuzo ya CHAOMVA 2014.
Diamona aliyetwaa tuzo ya AFRIMMA hivi karibuni na kushindwa kiduchu kunyakua tuzo za MTV na BET ameteuliwa kwenye vipengele vya Most Gifted Video of the Year, Most Gifted New Comer, Most Gifted Afro Pop na Most Gifted East Africa.
Tumpigie kura za kutosha na tumuombee Mungu hata kama HUPENDI ilimradi tu ashinde!
ORODHA KAMILI HII HAPA:
MOST GIFTED MALE
CASSPER NYOVEST – DOC SHEBELEZA
DAVIDO – AYE
RIKY RICK FT OKMALUMKOOLKAT – AMANTOMBAZANE
K.O. FT KID X – CARACARA
SARKODIE – ILLUMINATI

MOST GIFTED FEMALE
THEMBI SEETE – THUNTSHA LEROLE
BUCIE FT HEAVY K – EASY TO LOVE
LIZHA JAMES FT UHURU – QUEM TI MANDOU
TIWA SAVAGE FT DON JAZZY – EMINADO
SEYI SHAY – IRAWO

MOST GIFTED NEWCOMER
DREAM TEAM FT TAMARSHA, AKA & BIG NUZ – TSEKEDE
CASSPER NYOVEST – DOC SHEBELEZA
EMMY GEE FT AB CRAZY & DJ DIMPLEZ – RANDS AND NAIRAS
DIAMOND – NUMBER ONE
PATORANKING – GIRLIE O (REMIX)


MOST GIFTED DUO, GROUP OR FEATURING
UHURU FT OSKIDO & PROFESSOR – Y-TJUKUTJA
DJ CLOCK FT BEATENBERG – PLUTO (I REMEMBER)
R2BEES FT WIZKID – SLOW DOWN
K.O. FT KID X – CARACARA
KCEE FT WIZKID – PULL OVER

MOST GIFTED DANCE
UHURU FT OSKIDO & PROFESSOR – Y-TJUKUTJA
DAVIDO – SKELEWU
DJ CLOCK FT BEATENBERG – PLUTO (I REMEMBER)
P SQUARE – PERSONALLY
BUSISWA FT VARIOUS – NGOKU

MOST GIFTED RAGGA DANCEHALL
BUFFALO SOULJAH – BASAWINE
OREZI – RIHANNA
JESSE JAGGZ FEAT WIZKID – BAD GIRL
PATORANKING – GIRLIE O (REMIX)
SHATTA WALE – EVERYDOBY LIKES MY TING

MOST GIFTED AFRO POP
DAVIDO – AYE
MAFIKIZOLO FT MAY D – HAPPINESS
DIAMOND – NUMBER ONE
FLAVOUR ADA ADA
IYANYA – JOMBOLO

MOST GIFTED KWAITO
UHURU FT OSKIDO & PROFESSOR – Y-TJUKUTJA
CHARACTER FT MONO T & OSKIDO – INXEBA LENDODA
BIG NUZ FT KHAYA MTHETHWA – INCWADI YOTHANDO
DJ VETKUK VS MAHOOTA – KHABA LENJA
DJ CNDO – YAMNANDI INTO

MOST GIFTED R&B
2FACE FT T PAIN - RAINBOW
JIMMY NEVIS FT KWESTA – BALLOON
GB COLLECTIVE FT BRIAN TEMBA & REASON – CHOCOLATE VANILLA
DONALD – CRAZY BUT AMAZING
NIYOLA – TOH BAD

MOST GIFTED HIP HOP
CASSPER NYOVEST – DOC SHEBELEZA
KHULI CHANA FT DA L.E.S & MAGESH – HAPE LE HAPE 2.1
PHYNO – ALOBAM
K.O. FT KID X – CARACARA
AKA – CONGRATULATE

MOST GIFTED SOUTHERN
DJ CLOCK FT BEATENBERG – PLUTO (I REMEMBER)
CASSPER NYOVEST – DOC SHEBELEZA
AKA – CONGRATULATE
ZEUS – PSYCH
K.O. FT KID X – CARACARA

MOST GIFTED WEST
R2BEES FT WIZKID – SLOW DOWN
DAVIDO – AYE
BURNA BOY FT D’BANJ – WON DA MO
OLAMIDE – TURN UP
DR SID FT DON JAZZY – SURULERE


MOST GIFTED EAST
SAUTI SOL – NSHIKE
DIAMOND – NUMBER ONE
NAVIO – NO HOLDING BACK
EDDY KENZO – SITYA LOSS
ELANI – KOOKOO

MOST GIFTED VIDEO OF THE YEAR
EMMY GEE FT AB CRAZY & DJ DIMPLEZ – RANDS AND NAIRAS
DAVIDO – AYE
K.O. FT KID X – CARACARA
BURNA BOY – RUN MY RACE
TIWA SAVAGE FT DON JAZZY – EMINADO
DR SID FT DON JAZZY – SURULERE
RIKY RICK FT OKMALUMKOOLKAT – AMANTOMBAZANE
CASSPER NYOVEST – DOC SHEBELEZA
SARKODIE – ILLUMINATI
DJ CLOCK FT BEATENBERG – PLUTO (I REMEMBER)
AKA – CONGRATULATE
DIAMOND – NUMBER ONE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPfsySjCulA6nI6NANBb-74R99q6AlmjsTTFY7BlaqovuPWEvH2mhvXvzyDq1BU8sDFB0DD3SKugGwn0zuH7qjboNOhAs1fttc8Xy_dzLSEdlqV2DgoVa8Ku_EhdAFbQBqCeRHduQ8cvE/s640/532cebddf6210a2e0b489f323059cc1a.jpeg

van Persie atatahadharisha Falcao Old Trafford

http://i4.eurosport.com/2014/09/03/1306699-28127090-640-360.jpgRADAMEL Falcao hajahakikishiwa namba katika kikosi cha kwanza cha Manchester United, kwa mujibu wa mshambuliaji wa Mashetani Wekundu, Robin van Persie.
Mchezaji wa kimataifa wa Colombia, Falcao (28), alijiunga na Man  U kwa mkopo wa mwaka mmoja uliowagharimu paundi milioni 6.
"Nakaribisha ujio wake, anatufanya tuwe bora zaidi," Van Persie aliiambia Fox Sports NL.
"Katika klabu kubwa daima unahitaji wachezaji bora, ambao pia wanafiti katika falsafa. Falcao ni lazima apiganie namba, kama ilivyo kwangu mimi."
Falcao alifunga magoli 11 katika mechi 20 alizochezea klabu ya Monaco ya Ligi Kuu ya Ufaransa msimu uliopita, kabla ya kuumia goti Januari, maumivu yaliyomweka nje ya Kombe la Dunia nchini Brazil.
Kulikuwa na uvumi kwamba ameletwa Man U ili kuchukua nafasi ya Van Persie (3)1, ambaye amevumishiwa kuhitaji kufanyiwa upasuaji wa goti.
"Nimevutiwa kwamba watu wamefikiria kitu kama hicho," alisema Mholanzi huyo, ambaye alitua Old Trafford akitokea Arsenal kwa paundi milioni 24 mwezi Agosti 2012 na alifunga magoli 26 ya ligi katika msimu wake wa kwanza na kuisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa.
"Sijui yametokea wapi hayo na naweza kusema huku mkono wangu nikiwa nimeuweka kwenye moyo wangu kwamba sitakuwa hospitalini kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji."

Taifa Stars yaifuata Burundi ikiwa na hasira ya 3-0

http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/stars%20jezi.jpg?itok=YI5JETByhttp://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/field/image/team-stars.jpg?itok=qYvzIZN8KIKOSI chenye wachezaji 20 cha timu ya taifa (Taifa Stars) kimeondoka nchini leo alfajiri kwenda Bunjura, Burundi huku kocha wa timu hiyo, Mholanzi Mart Nooij akiahidi kulipa kisasi cha kufungwa 3-0 dhidi ya taifa hilo katika mechi yao ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya 'Etamba Murugamba' itakayopigwa nchini humo Jumapili.
Katika mechi iliyopita ya kirafiki iliyozikutanisha timu hizo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Aprili 26, mwaka huu, kikosi cha Taifa Stars kilichokuwa "kimefinyangwafinyangwa" na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kulazimisha waanze wachezaji watano wa 'maboresho', kililala 3-0 dhidi ya Warundi na kuharibu pilau la sherehe zilizokuwa zimefana za Miaka 50 ya Muungano.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kuagwa kwa Taifa Stars, Nooij alisema amekiandaa vyema kikosi chake kuhakikisha kinaibuka na ushindi ili kulipa kisasi cha kufungwa nyumbani na pia kujihakikishia kinapanda katika viwango vya soka vya kimataifa vinavyotolewa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).
"Ninatambua Burundi ina wachezaji wazuri na wa kimataifa kina (Amisi) Tambwe, (Pierre) Kwizera na (Didier) Kavumbagu lakini kwa kikosi tunachokwenda nacho, tuna uhakika wa kushinda ugenini na kulipa kisasi maana walitufunga kwetu," alisema Nooij.
Aliwataja wachezaji 20 anaokwenda nao Bunjumbura kuwa ni pamoja na makipa Mwadin Ally (Azam FC) na Deogratias Munishi 'Dida' (Yanga).
Wengine ni Shomari Kapombe (Azam FC), Oscar Joshua (Yanga), Said Morad (Azam FC), Nadir Haroub 'Canavaro' (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Joram Mgeveke (aliyesajiliwa Simba kutoka kikosi cha maboresho ya Taifa Stars), Simon Msuva (Yanga), Erasto Nyoni (Azam FC), Himid Mao (Azam FC), Amri Kiemba (Simba), Haruna Chanongo (Simba), Salum Abubakary 'Sure Boy' (Azam FC), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya ya Qatar), Hamis Mcha (Azam FC), Juma Luizio (Zesco FC ya Zambia), Mrisho Ngasa (Yanga), Mbwana Samata na Thomas  Ulimwengu (wote TP Mazembe ya DRC).
Nooij alisema mshambuliaji na nahodha wa Azam FC, John Bocco 'Adebayor', beki kisiki Agrrey Morris na kipa Aishi Manula wameachwa katika msafara wa Burundi kwa sababu mbalimbali zikiwamo majeraha na kutokuwa na uhakika wa kucheza Jumapili.
Alisema Bocco na Morris ni majeruhi huku akieleza kuwa makipa Dida na Mwadini wanatosha kwa mechi hiyo, hivyo haoni sababu ya kwenda na Manula.
Stars itaingia uwanjani mwishoni mwa wiki ikiwa na kumbukumbu ya kutolewa na Zimbabwe kwenye mbio za kuwania kushiriki fainali zijazo za Mataifa ya Afrika (Afcon) zitakazofanyika Morocco mwakani.
Naye Somoe Ng'itu anaripoti kuwa washambuliaji wawili wa kimataifa wa Simba, Amissi Tambwe, Pierre Kwizera na Didier Kavumbagu wa Azam, waliondoka nchini jana na kuelekea kwao Burundi kwa ajili ya kujiunga na timu yao ya taifa inayojiandaa kuivaa Taifa Stars keshokutwa.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, kocha msaidizi wa Simba, Selemani Matola, alisema kuwa Tambwe, Kwizera na nyota wengine wa Taifa Stars walipewa ruhusa jana kwa ajili ya kujiunga na timu zao za taifa.
Matola alisema kuwa hata hivyo, kuondoka kwa nyota hao hakutaharibu programu ya mazoezi kwa sababu huko wanapokwenda pia wanakwenda kucheza mechi ya kimataifa.
"Kwa upande wetu tuko vizuri, kikosi kimeiva na msimu ujao tutatoa ushindani kwa kila tutakayekutana naye," alisema Matola.
Taifa Stars na Burundi zinakutana katika mchezo unaotambuliwa na kalenda ya FIFA.
Tayari wachezaji wanaocheza nje ya nchi, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Mwinyi Kazimoto anayecheza klabu ya Al Markhiya ya Qatar wameshawasili nchini.
Awali Stars ilitarajia kucheza dhidi ya Morocco lakini Waarabu hao waliikacha wakidai kwamba wamewakosa nyota wao wanaocheza nje ya nchi hiyo.

Uhaba wa walimu Elimu ya Dini tatizo kubwa nchini-IEP

http://www.educatedanxiety.com/wp-content/uploads/2014/08/quran-2.jpgNA SULEIMAN MSUYA
JOPO la Elimu la Waislam (IEP) limesema pamoja na mafanikio yanayopatikana katika kuhakikisha kuwa elimu ya dini inapatikana nchini kote bado wanakabiliwa na changamoto kubwa ya uchache wa waalimu wenye taaluma hiyo.
Hayo yamebainishwa Afisa Mwandamizi wa (IEP) Suleyman Daud wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam.
Daud alisema tangu utaratibu huo wa kutoa elimu ya dini uanze wamepata mafanikio makubwa jambo ambalo linawapatia hamasa ya kuendelea kuboresha ili uweze kutoa tija kwa vijana wa Kiislaam hapa nchini.
Alisema jitihada zao zimejikita katika kuwapatia elimu ya dini vijana wakiislam ambao wanamaliza vyuo mbalimbali hapa nchini kuanzia ngazi ya cheti, stashahada na shahada ili waweze kutoa elimu kwa vijana wa shule za msingi.
“Napenda kuwaambia Watanzania jamii ya Kiislam kuwa juhudi zetu zinaenda vizuri za kuwapatia vijana wao elimu ya dini ila changamoto kubwa ni uchache wa walimu wenye elimu hiyo kuwafundisha” ,alisema.
Afisa Mwandamizi huyo wa (IEP) alisema pamoja na changamoto hiyo ya uchache wa waalimu mafanikio yamekuwa yakiiongezeka kwa shule nyingi kuongezeka katika kufanya mitihani hiyo ambayo haina athari yoyote katika matokeo ya darasa la saba.
Daud alisema katika mtihani wa mwaka jana mikoa 26, wilaya 94 na shule 2,100  ya Tanzania Bara na Visiwa zilishiriki watahiniwa walikuwa 68,096 ambapo ufaulu ulikuwa asilimia 38.04.
Aidha Afisa alisema kwa matokeo ya mwaka huu wa 2014  mtihani ambao ulishirikisha mikoa 26, wilaya 115, shule 2559 na wahitimu 74192 na ufaulu ni sawa na asilimia 46.45 ambao ni ongezeko la asilimia 8.
Alisema mitihani hiyo itakuwa ikifanyika kila mwaka kwa wanafunzi wa wakiislam wanaomaliza la saba  ambapo lengo lao ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2017 mitihani hiyo iwe inatambulika kwenye Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).
Daud alisema pamoja na ukweli kuwa mitihani hiyo kutotambulika katika baraza la mitihani bado vijana wa kiislaam wamekuwa wakishiriki bila kuleta pingamizi hasa katika shule ambazo zinaendeshwa kwa taratibu za kiislaam.
Afisa Mwandamizi huyo alisema katika kufikia malengo hayo juhudi zinahitajika kutoka kila pande hasa kwa wazazi kwani ni wazi kuwa elimu hiyo inawajengea uadilifu na upendo vijana hao.
‘Unajua kwa muda mrefu elimu ya dini imekuwa ikitolewa kwa wanafunzi wa sekondari pekee jambao ambalo imeifanya NECTA kulitumia somo hilo katika kutafsiri matokeo ya mwanafunzi hivyo lengo letu ni kuhakikisha elimu hiyo inakuwa rasmi katika elimu ya msingi”, alisema.

Nigeria kitanzini mbele ya FIFA

http://goodlife.com.ng/uploads/Sanni-Azeez_87_dream-team.jpg 
NIGERIA imejiweka matatani mbele ya Shirikisho la Soka Duniani, FIFA kutokana na mgogoro mkubwa wa uongozi uliopo katika Shirikisho lao la soka la NFF.
Kutokana na hali hiyo FIFA limeipa Nigeria muda wa mpaka Septemba 8 kwa kiongozi wa NFF Chris Giwa awe amejiuzulu au wafungiwe. 
Katika barua yake iliyotumwa kwa katibu mkuu wa NFF Musa Amadu, FIFA wameeleza kuwa kamati yake ya dharura imeamua kuisimamisha nchi hiyo mpaka mtajwa atapoachia madaraka na katibu mkuu aweze kuendelea na majukumu yake bila kubughudhiwa. 
FIFA pia ilifafanua kuwa kamati ya utendaji NFF iliyoteuliwa Agosti 25 mwaka huu ikiwa chini ya Rais Aminu Maigari itatakiwa kuitisha mkutano mkuu haraka ili kuchagua wajumbe wa kamati ya uchaguzi kabla ya kuitisha mkutano mwingine wa uchaguzi kwa ajili ya viongozi wapya wa shirikisho hilo. 
FIFA imeweka wazi katika barua yake hiyop iliyosainiwa na kamtibu mkuu wake Jerome Valcke kuwa mara NFF itakapofungiwa nchi hiyo haitapata nafasi ya kushiriki michuano yoyote ya kimataifa ikiwemo hata ile ya kirafiki. 
Hata hivyo uamuzi huo wa FIFA kusogeza mbele muda huo umetoa ahaueni kwa mchezo wao wa kufuzu Mataifa ya Afrika dhidi ya Congo utakaofanyika Jumamosi hii huko Calabar lakini kuna wasiwasi wa mchezo wao dhidi ya Afrika Kusini unaotarajiwa kufanyika Septemba 10 usifanyike kama maagizo hayo hayatazingatiwa.

Thursday, September 4, 2014

Aisha Bui atupa Mshale wa Kifo mtaani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEia3UxHjhFQAOtMelt-HNeHnCq8_8wf46ChclxFiV2yd_QvEl8doJA8VY0-uwmtjMvo2485UzpHaf1mBS6BXhx2VtKIuhIJGQ7MOGFqX5s0a2QX8Qz0bozYXluvp6KZ6mcuSwwpQhDKvLI2/s1600/20+MSHALE+WA+KIFO.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3XcWgG-PIr5TS48iUJEtAv8TdXlMJat1wUJ0RmV_smA6QE96gEkWhXQH3-lx2guv25uPB77I5gzaKn1_hPEWpfiEObyIwSH4_IW6gqJUS383iB30pwku-hktxmQo1QPqKYI4tV2pOL9s/
FILAMU mpya ya mwanadada Aisha Bui iitwayo 'Mshale wa Kifo' imeachiwa rasmi huku muigizaji huiyo akijipanga kwa ajili ya kutengeneza kazi nyingine mpya.
Akizungumza na MICHARAZO, Aisha Bui alisema filamu hiyo inatoka leo na kwa sasa yeye na 'crew' yake ya Bad Girl 'Film's wapo katika matayarisho wa kuandaa kazi mpya ili kuendelea kuwapa burudani mashabiki wao.
Filamu hiyo ya Mshale wa Kifo ni ya kwanza kiwa mwanadada huyo anayetamba na filamu mbalimbali na ndani ya kazi hiyo ameigiza yeye mwenyewe, Ahmed Olotu 'Mzee Chillo', Salim Ahmed 'Gabo' na wengine.
"Ile filamu ya 'Mshale wa Kifo' imetoka leo baada ya kukwama Agosti 25, kwa sasa Bad Girl Film's tunaanza maandalizi ya kuandaa kazi nyingine mpya, tunataka kuwapa burudani mashabiki wetu mwanzo mwisho sambamba na kuleta mapinduzi ya kuondokana na filamu za 'sebuleni' na ufukweni," alisema Aisha Bui mama wa mtoto mmoja.
Kabla ya kutoa filamu hiyo mwanadada huyo, alitamba na filamu kama Saturday Morning, Better Days, Not Without My Son, Continous Love, Revenge of Love, Mirathi, Pain of Love, Crazy Love na The Second Wife.








Sikinde waachia mbili za uhamasishaji Gesi mikoa wa Kusini

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgyQvJbNPmPY9Zp7MmXibkXD186MC54L8sZ79WM1IZ_KxdV5R5Wh9ZWSAd3-nx1OZIXAfVweaIncxaslL1wDR3VQuRmdKX2u7M6swKmwLhBJ4W2tcShvII75vxkD5IjN7HNy3v0uowGg6s/s1600/sikinde.JPGBENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Sikinde' imefytua nyimbo mbili mpya maalum kwa ajili ya kuwahamasisha wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kwa neema walizojaliwa.
Kwa mujibu wa Katibu wa Sikinde, Hamis Mirambo nyimbo hizo ni 'Fursa Zimefunguliwa' na 'Neema Kubwa ya Gesi' ambazo tayari zimeshasambazwa ili kurushwa hewani.
Mirambo aliiambia MICHARAZO nyimbo hizo zimetungwa maalum kwa ajili ya kuwahamasisha na kuwaelimisha wakazi wa mikoa hiyo juu ya neema zilizogundulika katika mikoa yao ikiwamo Gesi.
"Ni nyimbo ambazo za kuhamasisha na kuelimisha juu ya wakazi wa mikoa hiyo ya Kusini mwa Tanzania kuitumia vyema neema na fursa  zilizopo katika mikoa yao kujiletea maendeleo," alisema.
Mirambo aliongeza kuwa bendi yao tayari imekamilisha nyimbo za albamu yao mpya na wanajipanga kwa ajili ya kuzizidua sambamba na kuzitengenezea video zake.
Albamu hiyo itakayofahamika kama 'Jinamizi la Talaka' itakuwa na nyimbo saba badala ya sita ilivyozoeleka kwa albamu za bendi za muziki wa dansi.
Pia, alidokeza kuwa kuanzia sasa siku ya Jumamosi watakuwa wakitoa burudani kwenye ukumbi wa Wipes Bar Bandari, Kurasini huku siku ya Ijumaa kama kawaida wanakamua Break Point, Posta Mpya na Jumapili uwanja wa nyumbani wa DDC Kariakoo.

Hatari! Kim Kardashian akubali kuvua nguo kupamba jarida la GQ

Kim-Kardashian-Naked-GQ

Kim-Kardashian-Naked-GQ-2
Kim-Kardashian-Naked-GQ-3

MWANADADA nyota wa Marekani, ambaye ni mke wa nyota wa muziki duniani, Kanye West, Kim Kardashian anataka uache kujiuliza maswali inakuwaje awapo bila ya nguo baada ta kukubali kupigwa picha ili kupambana Jarida ya GQ.

Kim atatokelea kwenye Jarida hilo toleo la nchini Uingereza. Tayari Kim ameshinda tuzo ya mwanamke wa mwaka kutoka GQ , akiwa ndio kwanza ana miaka 33. Dah! Hii ni Hatareeee

Rooney aibeba England afunga bao pekee dhidi ya Norway











BAO pekee la kipindi cha pili la mkwaju wa penati uliofungwa na Nahodha mpya wa England Wayne Rooney iliisaidia kuipa ushindi timu hiyo dhidi ya Norway katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa usiku wa jana.
Rooney alifunga bao hilo katika dakika ya 68 kwenye pambano lililochezwa uwanja wa Wembley na kuhudhuria na watazamaji zaidi ya 40,000.

Lahm, Klose watunukiwa Ujerumani ikilala 4-2 kwa Argentina

http://content4.promiflash.de/article-images/w500/philipp-lahm-per-mertesacker-und-miroslav-klose-werden-aus-dfb-team-verabschiedet.jpg 







04 Sep 2014 BAADA ya kazi nzuri waliyoifanyia nchi ya Ujerumani, wachezaji wakongwe Miloslav Klose, Philipp Lahm na Per Mertesacker wamepewa tuzo za heshima jana kabla ya mchezo wa kirafiki kati ya Ujerumani na Argentina Uwanja wa Esprit Arena ambao ulishuhudiwa Ujerumani ikinyukwa mabao 4-2.
Watatu hao waliichezea Ujerumani katika fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 dhidi ya Argentina kabla ya kuamua kustaafu soka ya kimataifa.
Klose, ambaye ni mfungaji bora wa kihistoria wa Ujerumani kwa mabao yake 71, ametungika daluga baada ya kuwa mfungaji wa mabao mengi zaidi katika historia ya Kombe la Dunia.
Hata hivyo furaha yao ya kupokea tuzo hizo ziliingia shubiri baada ya kuishuhudia Ujerumani ikifa mbele ya Argentina.
Winga mpya wa Manchester United,  Angel di Maria ametengeneza mabao matatu na kufunga moja katika mchezo huo uliochezwa mjini Dusseldorf, Ujerumani.
Mchezaji huyo ghali zaidi kusajiliwa Manchester United na Uingereza nzima alipika mabao ya Sergio Aguero, Erik Lamela na Federico Fernandez kabla ya kufunga na lake mwenyewe siku 52 tangu bao la Mario Gotze katika muda wa nyongeza liipe Ujerumani ubingwa wa dunia nchini Brazil. 
Ujerumani walipata mabao yao kupitia Andre Schurrle Gotze aliyefunga la pili kwa mabingwa hao wa dunia.

Yanga yawanyoa Wakenya, Maximo we acha tu!

Simon Msuva akionyesha makali yake. Juu kikosi cha Yanga (Picha zote kwa hisani ya Bin Zubeiry
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Yanga, Mbrazil Genilson Santos 'Jaja' ameendelea kuwapa raha wana Yanga baada ya kuifungia bao pekee lililowapa vijana wa Jangwani ushindi wao wa nne mfululizo ikiwa chini ya kocha Marcio Maximo katika pambano la kirafiki la kimataifa dhidi ya Thika United ya Kenya.
Mechi hiyo iliyochezwa jana kwenye uwanja wa Taifa, ilishuhudia Jaja akiifunga bao hilo katika kipindi cha pili na kuwafanya mashabiki waliokuwa wakitaka mchezaji huyo atolewe dimbani kunyamaza kimyaa.
Jaja alifunga goli hilo akimalizia kwa kuugusa kidogo tu mpira wa krosi murua ya dakika ya 58 kutoka kwa winga Simon Msuva ambaye jana alichezeshwa kama straika wa kati.
Goli hilo liliibua shangwe kwa mashabiki wa Yanga ambao walikuwa kimya katika kipindi cha kwanza kutokana na ubovu uliooneshwa na safu yao ya ushambuliaji ikiongozwa na Mbrazil huyo katika kipindi hicho.
Yanga waliokuwa wameweka kambi ya siku 10 visiwani Zanzibar wakicheza mechi za kirafiki tatu na kushinda zote dhidi ya Chipukizi FC, Shangani FC na KMKM zote za Ligi Kuu ya Zanzibar, walianza mechi hiyo kwa mpira wa polepole uliochagizwa na pasi fupifupi za mfumo wa Kibrazil wa kocha Marcio Maximo.
Kikosi cha kwanza cha Yanga kilichoanza na wachezaji wawili wapya kutoka Brazil, Andrey Coutinho na Genilson Santos 'Jaja' kilimaliza kipindi cha kwanza kikiwa hakijafunga goli hata moja, sawa na wageni wao Thika United waliomaliza msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Kenya wakiwa nafasi ya tano.
Katika kipindi hicho cha kwanza, kiungo wa kimataifa wa Yanga kutoka Rwanda, Haruna Niyonzima 'Fabregas' alionyesha kiwango cha juu hasa katika dakika 30 za mwanzo akifuatwa na Coutinho ambaye alionekana wazi kuwa kivutio kikubwa cha Wanayanga kutokana na chenga zake za Kibrazil zilizojaa kila aina ya fedheha.
Kabla ya mechi hiyo kuanza, Maximo aliyekuwa anaingia kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa akiwa kocha wa Yanga baada ya kuiongoza kwa mafanikio timu ya taifa (Taifa Stars), aliwanyanyua vitini wapenzi na mashabiki wa Yanga baada ya kuonyesha ishara ya ngumi ambayo ilitafsiriwa kama amedhamiria kurudisha magoli 5-0 ambayo Yanga ilipokea kutoka kwa watani wao wa jadi, Simba misimu mitatu iliyopita.
Maximo, kocha wa zamani wa Stars, aliendelea kuwa kivutio zaidi pale alipojishika kifuani na kutoa ishara kwamba 'anaweza' kuipa mafanikio zaidi timu ya Yanga.
Mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Hashim Abdallah kutoka Dar es Salaam ambaye ana daraja la kwanza la uamuzi, ilishuhudiwa Maximo akibadilisha wachezaji kadhaa kipindi cha pili akiwatoa Jaja, Dilunga, Niyonzima, Coutinho na Msuva na kuwaingiza Hamis Thabit, Omega Seme, Said Bahanunzi na Nizar Khalfan ambao walibadilisha kwa kiasi kikubwa mechi hiyo na kuifanya iwe kivutio kwa Wanayanga.
Kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki hasa wa Yanga waliofurika upande wa Magharibi na Kusini mwa Uwanja wa Taifa huku baadhi ya mashabiki wa Simba wakikaa kwenye jukwaa lao la Kaskazini mwa uwanja huo na kuendelea upinzani wao wa jadi dhidi ya Yanga kwa kuipa sapoti timu ngeni ya Thika United.
ilikuwa ni mechi ya nne ya kirafiki ya Yanga chini ya Maximo na ya kwanza kwa kocha huyo Mbrazil kwenye Uwanja wa Taifa tangu aanze kuifundisha klabu hiyo.
Kocha Maximo alisema baada ya mechi hiyo jana kuwa timu yake inapaswa kubadilika na kutumia nafasi zinazopatikana huku pia akiisifu Thika United akisema ilicheza vizuri kuliko wao licha ya Wanajangwani kuibuka na ushindi.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga alisema jana kuwa baada ya kushinda mechi zao zote nne za kirafiki wanaangalia uwezekano wa kucheza mechi nyingine moja ya kujipima kabla ya kuwavaa Azam FC katika pambano lao la kuwania Ngao ya Jamii la kuashiria ufunguzi wa pazia la Ligi Kuu ya Tanzania Bara Septemba 13.
Vikosi:
Yanga: Deogratius Munishi 'Dida', Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub 'Cannavaro', Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima/ Hussein Javu (dk 73), Hassan Dilunga/ Hamis Thabiti (dk. 46), Genilson Santos 'Jaja' (Said Bahanunzi (dk 75), Simon Msuva/ Omega Seme (dk 73) na Andrey Coutinho/ Nizar Khalfan (dk. 70).
Thika United: Hamza Muwonge, Simon Mbuguo, Sammy Meja, Tonny Kizito, Dirkir Glau, Dennis Odhiambo, Moses Odhiambo, Wyclif Opondo, Michael Olunga, David Kingatua na Joseph Kulia.

Falcao adai kutimiza ndoto, baba yake akifichua mbio za usajili wake

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj50uj4azVYQV9K1swq8oLz1YdrwmF3ZCcWreW8jp-zesvohIn_fLQqgBZCSLLyz0w0_zU4bmENmfRK_4D2v5EmRWci16t2fMdxHuG0FTNrAj5fIjiVp26G-db_N5JNK7hB3nQ3mRPdr0vu/s1600/Radamel+FALCAO%27s+father+with+his+son+in+Venezuela.png
Baba na mwana

WAKATI baba yake Radamel Garcia, akibainisha kuwa Arsenal, Liverpool, Manchester City na Juventus, zilikuwa zikipigana mkumbo kumsajili kabla ya kuhamia Manchester United, mshambuliaji nyota wa Colombia aliyekuwa As Monaco ya Ufaransa, Radamel Falcao amebainisha kuwa ametimiza ndoto zake baada ya kukamalisha usajili wa mkopo kwenda kwa Mashetani Wekundu.  Falcao aliiambia runinga ya Manchester Utd, MUTV kuwa alikuwa na ndoto za siku nyingi kukipiga katika Ligi Kuu nchini Uingereza kutokana na ushindani uliopo. 
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa ametua katika klabu ambayo ni bora kabisa nchini humo na sasa kila kitu kinakwenda sawa. 
Falcao, 28 alisafiri kwenda jijini Manchester kwa ajili ya vipimo vya afya Jumatatu jioni huku United wakithibitisha dili hilo baada ya kupita saa mbili na nusu toka dirisha la usajili lifungwe. 
United wameilipa Monaco kitita cha paundi milioni sita ili kupata huduma ya Falcao kwa msimu mmoja huku wakiwa na chaguo la kumsajili moja kwa moja wakitoa kitita kingine cha euro milioni 55.
Hata hivyo baba yake mzazi amebainisha kabla ya kutua Old Trafford, Falcao alikuwa akiwindwa na klabu nne tofauti zikiwamo tatu za England ili kunasa saini yake kabla mshambuliaji huyo hajaamua kutuma Manchester United kwa mkopo akitokea Monaco. 
Mzee huyo Ramadel Garcia alinukuliwa na The Mirror kuwa alisema Real Madrid waliamua kutomfuatilia Falcao, tofauti na Juventus, Arsenal, Manchester City na Liverpool.

Odemiwngie kupasuliwa, van Persie akwepa 'kisu'


WAKATI mshambuliaji nyota wa Manchester United anayetokea Uholanzi, Robin van Persie akinusurika kupigwa 'kisu', mshambuliaji was kimataifa wa Nigeria, Peter Odemwingie amebainisha kuwa sasa anahitaji kufanyiwa upasuaji kutokana na majeraha ya goti aliyonayo. 
Odemwingie sasa anategemewa kukosa sehemu ya msimu wa Ligi Kuu kufuatia kuumia katika mchezo ambao Stoke City waliitandika Manchester City kwa bao 1-0 Jumamosi iliyopita. 
Taarifa zinadai kuwa mchezaji huyo anaweza kuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi 10 au zaidi. 
Odemwingie mwenye umri wa miaka 33 alithibitisha hayo jana katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kwa kudai kuwa atakosa mechi nyingi za ligi msimu huu. 
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa atafanya kila awezalo kuhakikisha anarejea tena uwanjani akiwa fiti zaidi na kuendelea kuisaidia timu yake ya Stoke.
Majeruhi ya Odemwingie ambaye anachukuliwa kama mchezaji muhimu katika kikosi cha Stoke yamemlazimisha meneja Mark Hughes kumsajili winga wa kimataifa wa Morocco Oussama Assaidi kwa mkopo kutoka Liverpool katika siku ya mwisho kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili majira ya kiangazi.
Hali ikiwa hivyo kwa Odemwingie, Robin van Persie ameiambia Fox Sports NL kuwa hatafanyiwa upasuaji wa goti na kwamba kwa sasa anajipanga kuwania namba dhidi ya mshambuliaji mpya Radamel Falcao ambaye alijiunga na Manchester United Jumatatu.
Wakati United ikimsajili kwa mkopo mshambuliaji huyo raia wa Colombia akitokea klabu ya Monaco, iliripotiwa kuwa Mholanzi huyo atafanyiwa upasuaji hivyo kuwa nje kwa muda mrefu.
Lakini Van Persie, ambaye amekuwa akisumbuliwa na goti mapema katika wasifu wake kisoka, alipuuzia taarifa hizo: "Ninashangaa watu hao kutengeneza hisia kama hizo.
"Sijui yanatokea wapi na ninaweza kusema ukweli kutoka moyoni sitakuwapo hospitali kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji."
Falcao aliigharimu Monaco Euro milioni 60 miezi 12 iliyopita na amefunga mabao 155 katika mechi 200 za mwisho akiwa Porto, Atletico Madrid na klabu hiyo ya Ligue 1. 

Ngumi! Said Yazidu, Mualgeria kuzipiga YMCA-Moshi

MABONDIA wa Tanzania Said Yazidu na Ally Ramadhani 'Alibaba' wanatarajiwa kupanda ulingoni wiki ijayo kwa ajili ya kupeperusha bendera ya Tanzania katika mapambano mawili tofauti ya kimataifa dhidi ya mabondia kutoka nchi za Malawi na Algeria.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa PST, Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania, Anthony Rutta, Yazidu atazipiga na Djamel Dahou wa Algeria katika pambano la kuwania ubingwa wa Dunia wa WBO la raundi 12 na Alibaba atapigana na Alick Mwenda wa Malawi kuwania ubingwa wa UBO Afrika litakalokuwa la raundi 10.
Michezo yote pamoja na ile ya utangulizi ipatayo 10 itachezwa siku ya Septemba 12 kwenye ukumbi wa YMCA, Moshi mkoani Kilimanjaro chini ya kampuni ya Green Hill Promotion na kusimamiwa na PST.
Rutta alisema maandalizi ya michezo hiyo imekamilika na kuwataka wakazi wa Moshi na mikoa ya jirani kujiandaa kupata burudani ikiwa ni kwa mara ya kwanza kushuhudia ngumi za kulipwa katika hadhi ya kimataifa kama hiyo.
Katibu huyo alisema mbali na michezo hiyo ya kimataifa ya kuwania mataji ya UBO, siku hiyo kutakuwa 'vita' vingine kwa mabondia wa mikoa tofauti ikiwamo wenyeji Kilimanjaro  katika michezo ya utangulizii ya kuwasindikiza akina Yazidu na Alibaba.
Rutta aliyataja mapambano hayo ni lile la wanadada Fatuma Yazidu wa Dar atakayepigana na Joyce Adam wa Dodoma, Emmanuel Alex wa Kilimanjaro dhidi ya Ali Bugingo wa Dar, Pascal Bruno wa Kilimanjaro dhidi ya Cosmas Kibuga wa Arusha, George Allen wa Kilimanjaro atayepigana na Ssebo Husseni wa Dar na Raymond Muabwango wa Kilimanjaro watakayenyooshana na Fadhil Mkinda wa Dar.
"NI burudani isiyopaswa kukoswa na mashabiki wa mchezo wa ngumi kwani mabondia wote watakaoumana ni wenye viwango na wanaoujua mchezo huo," alisema Rutta.

Azam nouma yanasa udhamini wa miaka miwili NMB

 
MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Azam wameingia mkataba wa miaka miwili na Benki ya NMB  jana
Kwa mujibu wa Mweyekiti wa Azam Said Mohamed alisema mkataba huo utakuwa ikiisadia timu hiyo mambo mbalimbali ikiwemo vifaa vya michezo kama Jezi, Viatu na nauli ya kusafiria wakati wa mechi za mikoani.
“Udhamini wetu na NMB utakuwa  ukihusisha vifaa vyote vya michezo ikiwemo Jezi, Viatu na vifaa vingine na hatuwezi kusema gharama yake kwa sababu ni makubaliano yetu sisi na NMB ,” alisema Mohamed.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Mark Wiessing alisema mafanikio ya Azam FC pamoja na uongozi bora ndivyo vilivyo wavutia kuingia nao mkataba huo ambao anaamini utakuwa na manufaa kwa pande zote mbili.
Hiyo siyo mara ya kwanza kwa NMB kujiingiza katika udhamini wa michezo mara ya kwanza iliwahi kuidhamini timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars,mwaka 2007 hadi 2010 na imekuwa ikitoa mchango katika kuendeleza soka la vijana nchini.

Wednesday, September 3, 2014

Mpya! Diamond afunguka kilichomponza vurugu za Ujerumani

Diamond Platnumz

Screen Shot 2014-09-01 at 12.16.12 AM

KUANZIA siku tatu zilizopita stori kubwa kwenye kiwanda cha burudani Tanzania imehusu fujo zilizotokea Ujerumani kwenye show aliyokwenda kufanya Diamond Platnumz huko Stuttgart.
Kilichotokea ni kwamba saa kumi alfajiri ndio promota alimpeleka Diamond kwenye ukumbi kunakofanyika show. 
Kwa nini ilitokea akamchelewesha? nini kilitokea baadae? hizi hapa chini ni kauli za Diamond mwenyewe kama alivyohojiwa na mtandao huu.

1. ‘Mpaka sasa hivi nashindwa kuelewa tatizo lilikua nini, siamini kama tatizo lilikua ni hela, balance iliyokua imebaki ni balance ndogo kama EURO 3500 hivi ambazo ni zaidi ya milioni 7 za Tanzania, ninavyojua Mapromoter wengi wa nje wakifanya show huwa wanauza na vinywaji wenyewe na wanapata hela nyingi sana kwenye vinywaji kuliko hata viingilio so nahisi labda walivuta muda ili waendelee kuuza vinywaji zaidi’
2. ‘Walichelewa kunipeleka kwenye show, walinifata kwenye mida ya saa tisa usiku na wakawa hawana hela yangu iliyobaki, nikawaambia siendi kokote mpaka wamalize kunilipa, walikua na EURO 1500 wakati nilikua nawadai 3500 nikawaambia lazima wanipe hela yote, wakaifata ndio tukaenda kwenye show’
Screen Shot 2014-09-01 at 12.16.38 AM 
3. ‘Tukafika kwenye show saa10 kasoro, kweli hata ningekua mimi shabiki ningekasirika ningefanya vurugu, wengine walilipa zaidi ya laki moja na wametoka kwenye miji na nchi jirani, niliwaambia wanipeleke nikafanye show ndani ya ukumbi japo tulikuta watu wengi sana nje lakini Mapromota walikua waogawaoga kunipeleka ndani’
4. ‘Nikakuta watu wengi na vurugu nje, nikamwambia promota atupeleke ndani tungefika kwenye stage ingetulia baada ya sisi kuimba manake ni vitu tunakutana navyo kwenye muziki lakini promota walikua waogawaoga, askari wa Ujerumani karibu gari 7 wakaja pale lakini mtiti ukawa mkubwa’
5. ‘So dakika ya mwisho tukaona hapashukiki ndio wakaturudisha hotelini, kiukweli nimesikitishwa sana manake nilikua nimejipanga vizuri na ilikua ni mara yangu ya kwenda kuperform pale Stuttgart, imenisikitisha manake watu walikua kuniona alafu mwisho ikashindikana kuwafikishia walichokitarajia’
Screen Shot 2014-09-01 at 12.16.59 AM 
6. ‘Nafikiri October tutakua na show nyingine na itafanyika kulekule, nilikua nazungumza na uongozi wangu kwamba wanataka show nyingine na tayari wameshatuma hiyo hela ya show nyingine’ 
Millardayo.com

Majanga! Mwandishi Mwingine wa Marekani achinjwa

Mwandishi aliyechinjwa na IS Steven Sotloff
Wapiganaji wa dola ya Kiislam IS wamesambaza picha za video katika mitandao kwa lengo la kuonyesha kuchinjwa kwa mwandishi wa habari raia Marekani Steven Sotloff ambaye ni mmoja wa mateka wanaoshikiliwa na wapiganaji hao.

Mwandishi huyo Sotloff, mwenye umri wa miaka 31 ambaye alitekwa na wapiganaji hao mwezi August mwaka jana. 
Wapiganaji hao wa katika picha hizo pia wameonekana wakimtishia kumuua mateka mwingine anayedhaniwa kuwa ni raia wa Uingereza.Mwezi uliopita Sotloff alionekana mwishoni katika picha za video zilizoonyeshwa kuhusiana na kuchinjwa kwa mwandishi mwingine wa Marekani James Foley.
Baada ya mauaji ya mwandishi wa awali Foley, mama mzazi wa mwandiashi wa Sotloff alitoa ombi maalumu kwa kiongozi wa wanajeshi hao Abu Bakr al-Baghdadi kutoa muua mtoto wake. 
Msemaji wa Ikulu ya White House Josh Earnest amesema kuwa maofisa wa Marekani wanaendelea na uchunguzi wa ripoti hiyo.
Marekani hivi karibuni ilifanya mashambulizi ya anga dhidi ya IS nchini Iraq. 
Mwandishi wa masuala ya usalama wa BBC Frank Gardner amesema hatua hiyo ya wapiganaji wa IS ni kulipa kisasi kwa Marekani

David Beckham asikitishwa na Welbeck kwenda Arsenal

https://pbs.twimg.com/media/Bwi2sE9CYAAExQt.jpg
Danny Welbeck katika uzi mpya wa Arsenal
Tom Cleverley aliyehamia Aston Villa
UHAMISHO uliochelewa wa Kiungo wa Manchester United Tom Cleverley kwenda Aston Villa kwa Mkopo wa Msimu mmoja umebarikiwa hii jana wakati nyota wa zamani wa Man United David Beckham amesikitishwa kuondoka kwa David Welbeck kutoka Man United kwenda Arsenal.
Dirisha la Uhamisho lilifungwa rasmi juzi usiku lakini Uhamisho wa Cleverley ulichelewa lakini hivi sasa Bodi ya Ligi Kuu imeubariki.
Makubaliano kati ya Man United na Aston Villa yana vipengele kwamba Cleverley, mwenye Mkataba na Man United hadi 2015, anaweza kurudi Old Trafford Mwezi Januari au Villa imsaini kwa kudumu katika Kipindi hicho cha Usajili.
Cleverley, mwenye Miaka 25, amekulia toka Vyuo vya Soka vya Man United tangu akiwa mdogo na kuichezea Klabu hiyo Mechi 79.
David Beckham amesikitishwa na kuondoka kwa Danny Welbeck na kuhamia Arsenal.
Beckham amesema Arsenal wamepata dhahabu kwa kumnunua Welbeck na kuonyeshwa kusikitishwa kwake kumpoteza Mchezaji aliekuzwa kipaji toka Chuo cha Soka cha Man United tangu akiwa na Umri wa Miaka 8.
Beckham amesema: “Ni wazi kumwona Danny kuondoka, kwa mimi Shabiki wa Man United, kunasikitisha lakini mie si Meneja!”

Gari la Rais wa Kenya lililoibwa lapatikana Uganda

MAAFISA wakuu kutoka Shirika la Polisi wa Kimataifa, Interpol amethibitisha kuwa gari la ulinzi wa Rais Uhuru Kenyatta lililoibwa mjini Nairobi wiki jana limepatikana nchini Uganda.
Kwa sasa gari hilo limepelekwa mjini Kampala.
Mkurugenzi wa polisi wa kimataifa Interpol nchini Uganda Assab Kasingye aliambia BBC kuwa gari hilo litarudishwa Nairobi.Gari hilo aina ya BMW liliibwa siku ya Jumatano usiku mjini Nairobi. Watu watatu wamekamatwa kuhusiana na wizi huo.
Gari hilo liliibwa na watu waliokuwa wamejihami Jumatano wiki jana.
Hata hivyo msemaji wa serikali Manoah Esipisu alikanusha habari hizo akisema kuwa gari lililoibwa halikuwa na ulinzi wa Rais Kenyatta bali lilikuwa gari kuu kuu la polisi.
Lakini lilikuwa linaendeshwa na afisa wa polisi aliyeripoti kuwa gari hilo ni mmoja ya magari ya ulinzi wa Rais.Afisa huyo wa polisi pia alisemekana kuwa mmoja wa maafisa wa polisi wa ulinzi wa Rais.
Tukio la wizi wa gari hilo, lilisababisha taharuki miongoni mwa maafisa wa ulinzi kwa sababu magari ya ulinzi wa Rais yenyewe yanapaswa kuwa na ulinzi mkali.
Takwimu za polisi zinaonyesha kuwa visa vitatu vya wizi wa magari huripotiwa mjini Nairobi kila siku.
Hiki ni kisa kimoja kati ya vingi vya wizi wa magari ambapo mtu yeyote anaweza kuathirika.
BBC