STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 8, 2013

Omar Omar mkali wa Mchiriku afariki dunia Dar

MSANII  nyota wa miondoko ya Mnanda a.k.a Mchiriku, Omari Omar amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Habari zilizoifikia MICHARAZO, asubuhii zinasema kuwa, Omar Omar aliyetamba na nyimbo mbalimbali ukiwemo ule maarufu wa 'Kupata ni Majaliwa' alifariki nyumbani kwao Temeke, saa chache baada ya kurejeshwa toka hospitali ya temeke alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.
Taarifa hizo zinasema kuwa mara baada ya kurejea nyumbani, msanii huyo alizidiwa na hatimaye kufariki na kwamba msiba wake upo nyumbani kwao Temeke Mikoroshini kwa ajili ya mipango ya mazishi.
Msiba wa msanii huo umekuja siku chache baada ya tasnia ya sanaa na burudani kumpoteza Juma Kilowoko 'Sajuki' msanii nyota wa filamu aliyefariki pia kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya muda mrefu.
MICHARAZO inawamuombea kila la heri Omar Omar na wengine waliotangulia mbele ya haki mapumziko mema katika safari yao ya Ahera. Innallillah Waina Illah Rajiun.
Taarifa zaidi tutakuwa tunawaletea kujua mkali huyo wa mduara aliyewafanya wasanii wengine kufuata mkondo wake akiwemo Dogo Mfaume, Ferouz, Easy Man na wengine.

Mayweather Jr, kuvaana na Guerrero Mei 4

BONDIA Floyd Mayweather Jr anatarajia kupanda jukwaani katika ukumbi wa MGM Grand, Las Vegas, Nevada, USA kuwania taji la WBC welterweight title May 4 ,2013 kuzipiga na Robert Guerrero bondia huyo ambaye ajawai kupigwa tangia angie katika uwanja wa masumbwi ya kulipwa tarehe 11-10-1996 bondia huyo alichezo mpambano wake wa mwisho May 5 mwaka jana na kutumikia kifungo cha Miezi mitatu kwa kosa la kumshambulia aliyekuwa mpenzi wake mama watoto wake kwa sasa yupo katika maandalizi ya mpambano huo wa tarehe hiyo katika mchezo wake wa mwisho aliocheza na Miguel Cotto alipata ushindi mwembamba kwa kuibuka kumtwanga kwa point
www.superdboxingcoach.blogspot.com    BONDIA Floyd Mayweather Jr  anatarajia kupanda jukwaani katika ukumbi wa MGM Grand, Las Vegas, Nevada, USA kuwania taji la    WBC welterweight title May 4 ,2013 kuzipiga na Robert     Guerrero bondia huyo ambaye ajawai kupigwa tangia angie katika uwanja wa masumbwi ya kulipwa  tarehe 11-10-1996 bondia huyo alichezo mpambano wake wa mwisho May 5 mwaka jana na kutumikia kifungo cha Miezi mitatu kwa kosa la kumshambulia aliyekuwa mpenzi wake mama watoto wake kwa sasa yupo katika maandalizi ya mpambano huo wa tarehe hiyo katika mchezo wake wa mwisho aliocheza na Miguel Cotto alipata ushindi mwembamba kwa kuibuka kumtwanga kwa point

LIONEL MESSI TENA MWANASOKA BORA WA DUNIA

Lionel Messi akifurahi baada ya kupokea tuzo yake ya nne mfululizo ya Ballon d'Or ya kwenye Ukumbi wa Convention Centre mjini Zurich Uswisi jana.
Lionel Messi akiwa kwenye tuzo za FIFA jana
Ronaldo, Iniesta na Messi wakiwa kwenye tuzo.
Kikosi XI cha FIFA kilichotangazwa jana. Kutoka kushoto mstari wa nyuma Cristiano Ronaldo, Marcelo, Sergio Ramos, Gerard Pique, Dani Alves, Iker Casillas. Mstari wa mbele kutoka kushoto: Radamel Falcao, Lionel Messi, Andres Iniesta, Xavi Hernandez na Xabi Alonso
Winga wa Fenerbahce, raia wa Slovakia, Miroslav Stoch akishukuru kwa tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka wakati wa sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.
Vicente del Bosque akishukuru baada ya kupokea tuzo ya Kocha Bora wa Dunia wa Mwaka 2012
Mwanasoka Bora wa Dunia wa zamani, Fabio Cannavaro wa Italia akionyesha jina la mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia wa Mwaka 2012, Lione Messi
Straika wa timu ya taifa ya Marekani, Abby Wambach akishukuru baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike wa Dunia

Mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama (kushoto) na mchezaji wa zamani wa Uholanzi, Ruud Gullit wakati wa kukabidhi tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka.

Mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama akisoma jina la mshindi wa tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka.

Fuleco, kikatuni cha fainali za Kombe la Dunia 2014 za nchini Brazil kikimkumbatia mwanasoka bora wa zamani Ronaldo stejini wakati wa sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.

Kocha wa timu ya taifa ya Brazi, Luiz Felipe Scolari na mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama wakipozi kwa picha

Straika wa Real Madrid, Mreno Cristiano Ronaldo na rafikiye wa kike Irina Shayk wakiingia kwenye sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.

Rais wa FIFA, Joseph Blatter akiambatana na muigizaji wa Kirafansa, Gerard Depardieu wakati akiwasili kabla ya kuanza kwa kwenye sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.
Waongozaji wa sherehe ya tuzo za FIFA Ballon d'Or, Ruud Gullit (kushoto) na Kay Murray wakiwa mzigoni

NYOTA wa Barcelona, Lionel Messi (25) jana aliweka rekodi ya kipekee ya kuwa mwanasoka wa kwanza duniani kutwaa tuzo ya Ballon d'Or ya Mwanasoka Bora wa Dunia kwa miaka minne mfululizo baada ya kuwashinda wapinzani wake Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Andres Iniesta wa Barcelona.
Muargentina huyo amekuwa mtu wa kwanza katika historia ya miaka 61 ya tuzo hiyo kuibeba mara nne mfululizo.
Johan Cruyff (1971, 1973, 1974) na Marco Van Basten (1988, 1989, 1992) wa Uholanzi, na Michel Platini wa Ufaransa walishinda tuzo ya Ballon d'Or mara tatu.
Mwanadada Abby Wambach wa Marekani alishinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike, wakati tuzo ya kocha bora wa kiume ilienda kwa Vicente Del Bosque wa timu ya taifa ya Hispania baada ya kuwashinda, Jose Mourinho wa Real Madrid ambaye alishasema mapema kwamba hatahudhuria sherehe hizo nchini Uswisi na Pep Guardiola.
Tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka
ilienda kwa winga wa Fenerbahce, raia wa Slovakia, Miroslav Stoch ambaye alifunga goli lake kwa kuunganisha moja kwa moja bila ya kutua chini mpira wa kona uliomfikia akiwa nje ya boksi. Stoch aliwaangusha Radamel Falcao aliyefunga goli la 'tik-taka' na Neymar aliyefunga goli katika mazingira magumu.
Kikosi cha wachezaji bora "First Eleven" wa dunia chote kimeundwa na nyota wanaocheza katika Ligi Kuu ya Hispania, huku Radamel Falcao pekee akitokea nje ya Barcelona na Real Madrid.
Real Madrid na Barcelona zimetoa wachezaji watano kila moja.

Kikosi Bora cha Dunia XI cha FIFA kilichotangazwa jana ni:

Kipa

Iker Casillas
Mabeki
Dani Alves, Marcelo, Sergio Ramos na Gerard Pique
Viungo
Xabi Alonso, Xavi Hernandez na Andres Iniesta
Washambuliaji
Cristiano Ronaldo, Radamel Falcao na Lionel Messi

Monday, January 7, 2013

SIMBA YATINGA NUSU FAINALI MAPINDUZI CUP, 'YAJITOA'

Kikosi cha Simba kilichotinga Nusu Fainali jana

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
PAMOJA na kufuzu hatua ya Nusu Fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi jana, Simba SC italazimika kuiachia timu yao ya pili, maarufu kama Simba B iendelee na michuano hiyo hata kama ikiingia fainali, ili kikosi cha kwanza kiende Oman keshokutwa.
Kocha Mkuu wa Simba SC, Mfaransa Patrick Liewig aliiambia BIN ZUBEIRY jana kwamba, anataka kwenda Oman na kikosi kamili ili aweze kuwajua wachezaji wote na kuweza kuipanga vyema timu yake.
Kuhusu wachezaji wa timu ya taifa, ambayo Januari 11 itacheza mchezo wa kirafiki na Ethiopia, Liewig alisema suala hilo linashughulikiwa na viongozi wa klabu hiyo. “Najua viongozi walikuwa wana kikao na viongozi wa shirikisho (TFF).
Sijui wamekubaliana vipi, lakini naweza kuwavumilia wachezaji hao wajiunge na timu Oman baada ya mechi na Ethiopia,”alisema.
Simba jana ilifuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, licha ya kutoka sare ya 1-1 na Bandari ya hapa katika mchezo wa mwisho wa Kundi A, kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Hadi mapumziko, timu hizo zilikuwa zimekwishafungana bao 1-1, Bandari wakitangulia kupata bao kwa penalti, mfungaji Haitham Juma dakika ya sita kabla ya Kiggi Makassy kuisawazishia Simba SC dakika ya 16.
Refa aliwapa penalti Bandari baada ya Haruna Shamte kumchezea rafu Fauzi Ally katika eneo la hatari na Haitham akaenda kupiga penalti, ambayo ilipanguliwa na kipa Dhaira na mpira kumkuta tena mpigaji, aliyeukwamisha nyavuni.
Kiggi alifunga kwa mpira wa adhabu kutoka upande wa kulia wa Uwanja, umbali wa mita 20, baada ya Abdallah Seseme kuangushwa.    
Kipindi cha pili, Simba walianza kwa kuimarisha kwa kikosi chao wakiwaingiza kwa mpigo, Mwinyi Kazimoto, Haruna Chanongo na Jonas Mkude kuchukua nafasi za Mussa Mude, Salim Kinje na Ramadhani Singano ‘Messi’, wakati Bandari walimtoa kipa wao Hassan Hajji na kumuingiza Ahmad Suleiman.
Kwa matokeo hayo, Simba SC imeungana na Tusker ya Kenya kufuzu Nusu Fainali ya michuano hiyo. Tusker ni kinara wa kundi kwa pointi zake saba na Simba imeingia kama mshindi wa pili kwa pointi zake tano.
Wachezaji wa Simba SC walioitwa Stars ni kipa Juma Kaseja, mabeki Amir Maftah na Shomari Kapombe, viungo Amri Kiemba na Mwinyi Kazimoto na mshambuliaji Mrisho Ngasa.
Katika wachezaji wote hao walioitwa Stars, walio kwenye kikosi cha Simba kinachocheza Kombe la Mapinduzi ni Kapombe na Mwinyi Kazimoto pekee. Kaseja, Ngassa, Kiemba ni majeruhi, wakati Amir Maftah imeelezwa ana madai yake anayosubiri alipwe ndipo ajiunge na timu.  

Imehamishwa Bin Zubeiry

Sepp Blatter apinga kitendo kilichofanywa na Boateng, AC Milan

Rais wa FIFA, Sepp Blatter

RAIS wa Shirikisho wa Soka Duniani, FIFA, Sepp Blatter ameponda kitendo cha nyota wa AC Milan, Kevin Prince Boateng kuamua kususa pambano lao la kirafiki la wiki iliyopita dhidi ya timu ya daraja la chini ya Pro Patria, akidai haiwezi kuvumiliwa.
Blatter alinukuliwa jana akiwa Dubai kwenye zira ndefu ya Mashariki na Kati, akisema kuwa kilichofanywa na Boateng na timu yake ya Milan haiwezi kusaidia kumaliza ubaguzi zaidi ya kuongeza tatizo, iwapo kila timu au kila mchezaji watakuwa wakiamua kususa mechi kwa kufanyiwa vitendo kama hivyo.
"Sidhani kama kuondoka uwanjani ndio suluhisho la tatizo, inaweza kutumiwa vibaya na timu nyingine hasa kama timu imefungwa katika pambano hilo," alinukuliwa Bletter.
Alisema wanasubiri taarifa toka Shirikisho la Soka la Italia kujua kitu gani kilichotokea, ingawa alisisitiza kuwa pamoja na kwamba FIFA inapinga vitendo vya ubaguzi, lakini pia haiungi mkono tabia ya kususia mechi vinapotokea vitendo kama hivyo wakati wa mechi.
Kevin Prince Boateng kiungo wa AC Milan

Boateng nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Ghana, Black Stars, aliamua kutoka uwanjani baada ya kufanyiwa vitendo vya kibaguzi na mashabiki wa Pro Patria katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Alhamis iliyopita ambapo licha ya kubembelezwa aligoma kufuta msimamo wake na kusababisha mechi hiyo kuvunjika.
Jana Jumapili wachezaaji wa timu hiyo ya Milan, walitinga uwanjani katika pambano lao la Seria A wakiwa na jezi zenye maandishi ya kupinga ubaguzi wa rangi ambapo timu hiyo ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Siena.
Vitendo vya kibaguzi dhidi ya wachezaji wenye asili ya Afrika kwa mataifa ya Ulaya vimekuwa vikizidi kushamiri kwa siku za karibuni, baadhi vikifanywa na wachezaji wenyewe kwa wenyewe na wakati mwingine vikifanywa na mashabiki kama ilivyotokea kwa Boateng.


Wachezaji wa AC Milan wakiwa wamevaa jezi zinazopinga ubaguzi wa rangi kabla ya mechi yao ya Seria A dhidi ya Siena jana
Hata hivyo pamoja na FIFA na FA za nchi mbalimbali kuvipinga vitendo hivyo na kutoa adhabu kwa wahusika bado havijaleta tija hasa kutokana na adhabu zake kuonekana nyepesi kuliko ukubwa wa jambo hilo.

TAFF YAWAONYA WASANII WALIOHARIBU MSIBA WA SAJUKI


Rais wa TAFF, Simon Mwakifwamba


SHIRIKISHO la Filamu Tanzania (TAFF) limekemea baadhi ya wasanii walioonyesha utovu wa nidhamu katika msiba wa  aliyekuwa msanii wa filamu nchini, Juma Kilowoko ‘Sajuki’.

Pia limesisitiza kuwa msanii atakaeripotiwa katika vyombo vya habari kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu atafungiwa kuigiza.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Rais wa TAFF, Simon Mwakifwamba alisema amesikitishwa na kitendo cha wasanii kuacha msiba na kwenda kunywa pombe wakati msiba huo ni wa dini.

Alisema baadhi ya wasanii kuonyesha utovu wa nidhamu katika msiba wa marehemu Kanumba na wengine katika msiba wa Sajuki.

“Nasikitika kuona msanii hajitambui hata kidogo, yani anaacha msiba anakwenda kunywa pombe tena jirani na mahala pa msiba, jamani huu msiba ni wa dini, hivyo atakayeripotiwa vibaya katika misiba TAFF tutamfungia” alisema Mwakifwamba.

Katika hatua nyingine alisema msiba huo ulitawaliwa na utani hali ya kwamba umewakutanisha watani wa makabila.

Msiba huo ulitawaliwa na utani baada ya kuwepo kwa wasanii wachekeshaji kama vile, Steven Mengele ‘Steve Nyerere’ ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya fedha, Lucas  Mhuvile ‘Joti’ na wengineo wengi.

Tuzo za wakali wa filamu 2012 kutolewa Februari



MBIVU na mbichi ya nani mkali katika fani ya filamu kwa mwaka 2012 zinatarajiwa kufahamika mwezi ujao wakati wa hafla ya kutangaza washindi itakapofanyika jijini Dar es Salaam.
Tuzo hizo za Wasanii Bora wa Filamu 2012 zilizoandaliwa na Mtandao wa filamucentral zinatarajiwa kutolewa kwa washindi mwezi Februari katika tarehe na ukumbi utakaotajwa na waratibu wake.
Mratibu wa tuzo hizo, Myovela Mfaiswa, aliiambia MICHARAZO kuwa maandalizi kwa ujumla ya hafla hiyo inaendelea vema huku wadau wa filamu wakiendelea kuwapigia kura washiriki wanaochuana katika kinyang'anyiro hicho.
Mfaiswa alisema vipengele vinavyowaniwa katika tuzo hizo zinazofanyika kwa mara ya pili baada ya kufanyika mara ya mwisho mapema mwaka jana kwa wasanii bora wa 2010 ni pamoja na cha Muigizaji Bora wa Kike inayowaniwa na Yvonne Cherry 'Monalisa', Jacklyne Wolper, Wema Sepetu, Jennifer Kyaka 'Odama' na Elizabeth Michael 'Lulu'.
Tuzo nyingine ni ya Mchekeshaji Bora inayowaniwa na wasanii Haji Salum 'Mboto', King Majuto, Sharo Milionea, Kitale na Kinyapi, huku Muigizaji Bora Chipukizi ikiwaniwa na Mariam Ismail 'Mammy', Abdallah Ambua 'Dulla', Slim Omary 'Mdudu Kiu', Jose Mteme 'Baga' na Halima Ali.
Tuzo ya Muigizaji Bora wa Kiume inawaniwa na Jacob Stephen 'JB', Vincent Kigosi 'Ray', Steven Kanumba, Hisani Muya 'Tino' na Single Mtambalike 'Richie', wakati tuzo za Mwandishi Bora wa Mswada inawaniwa na Octavian Natalis, Ali Yakuti, F Kanuti, Elizabeth Chijumba na Kimela Bila.
------

KUMEKUCHA MISS UTALII TANZANIA


KAMBI ya warembo watakaoshiriki fainali za shindano la urembo la Utalii, Miss Utalii Tanzania, inatarajiwa kuanza rasmi Jumamosi ijayo ikishirikisha warembo walioshika nafasi mbili za juu ya mashindano ya ngazi ya mkoa.
Rais wa Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo 'Chipps' aliiambia MICHARAZO kambi hiyo itakuwa ya siku 21 kabla ya kufanyika kwa kinyang'anyiro hicho mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es Salaam.
Chipps aliwataja warembo watakaoingia kambini tayari kuwania taji hilo la Tanzania na tuzo nyingine 28 zitakazowaniwa kuwa ni pamoja na Rose Godwin (Arusha), Irene Thomas, Sophia Yusuph na Ivon Stephen wote wa Dar.
Wengine ni Erica Elibariki (Dodoma), Jamia Abdul (Geita), Debora J. Mwansepeta (Iringa), Anna Pogaly (Kilimanjaro), Zena Sultan (Kigoma), Asha Ramadhani (Katavi), Joan John (Lindi), Doreen Bukoli (Mara), Dayana Joachim (Mbeya) na Jessica Rugalabamu wa Mwanza.
Warembo wengine ni Halima Suleman (Mtwara), Hadija Saidi (Morogoro), Mary Rutta (Manyara), Paulina Mgeni (Njombe), Anganile Rogers (Rukwa), Furaha Kinyunyu (Ruvuma), Neema Julius (Singida), Flora Msangi (Simiyu), Lightness Kitua (Shinyanga), Magreth Malale (Tabora) na Sarafina Jackson wa Tanga.
Wawakilishi wa vyuo wakaoshiriki kinyang'anyiro hicho ni Irene Richard Makoye na Hawa Nyange.
Tuzo zitakazowaniwa na warembo hao mbali na taji litakalompa mshindi uwakilishi wa nchi katika shindano la kimataifa ni pamoja na tuzo za heshima za Jamii, Elimu ya Jamii, Afya ya Jamii, Utalii, Utamaduni, Uchumi, Miundo Mbinu ya Utalii, Uwekezaji, Madini na maliasili mbalimbali za taifa.

Suarez afunga bao la utata na kuivusha Liverpool Kombe la FA

HATUA KWA HATUA YA BAO LA UTATA LA SUAREZ JANA
Suarez akijitengenezea vizuri mzuri kwa mkono
Amefanikiwa na sasa anaelekea kufunga bao

Akimtoka kipa aliyejaribu kumzuia
Kazi imekuwa nyepesi anafunga kilainii..huku Mansfield wakiinua mikono wakilalamikia bao hilo

Anashangilia na wenzake

Anaubusu mkono wake kwa kazi nzuri uliofanya

 

NYOTA wa timu ya Liverpool, Luis Suarez, jana akitokea benchi alitengeneza bao kwa mkono kisha kufunga na kuivusha timu yake kwenye michuano ya Kombe la FA nchini England.

Bao hilo ambalo tukio la kutengenezwa na mkono halikuonwa na mwamuzi wa pambano hilo la raundi ya tatu ya michuano hiyo iliisaidia kuipa Liverpool ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya

Mansfield Town.
Raia huyo wa Uruguay ambaye anakumbukwa na Waafrika kwa kulizuia bao la Ghana katika Fainali za Kombe la Dunia 2010, alifunga bao hilo katika dakika ya 59 dakika tano tangu aingie dimbani kuchukua nafasi ya Daniel Sturridge, aliyetangulia kufunga bao la mapema.
Wenyeji Mansfield waliolalamikia tukio hilo, walipata bao la kufutia machozi dakika ya 80 kupitia Matt Green, ambalo halikuwasaidia kutong'oka kwenye michuano hiyo ambayo pia jana ilishuhudiwa Arsenal wakilazimishwa sare ya 2-2 ugenini na Swansea City.
Arsenal ilielekea kushinda pambano hilo baada ya kutoka nyuma ya bao 1-0 mara kipindi cha pili kilipoanza baada ya dakika 45 za kwanza kwenda mapumziko bila kufungana na kufunga mabao mawili dakika 10 za mwisho wa mchezo huo kabla ya kujisahau na Swansea kusawazisha zikiwa zimesalia dakika tatu.
Michu alianza kuiandikia Swansea bao dakika ya 51 kabla ya Lucas Podolski kusawazisha dakika ya 81 na Kieran Gibbs kufunga bao la pili dakika mbili baadae na wakati wengi wakiamini Arsenal imepita kwa raundi ya nne,  Danny Graham kusawazisha bao hilo na kuzifanya timu zao sasa kurudiana tena ili kufuzu hatua ijayo itakayoanza Januria 26.

Amefanikiwa na sasa anaelekea kufunga bao

TUZO BALLON D'OR LEO, AGUERO ATAKA MESSI APEWE

Aguero  akiwa na Lionel Messi

NYOTA wa timu ya Mamchester City ya England ambaye pia ni mchezaji wa timu ya taifa ya Argentina, Sergio 'kun' Aguero, amesema kwamba tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia ya Ballon d'Or inapaswa kwenda kwa Lionel Messi. 
Sherehe za kumtangaza mwanasoka bora wa dunia wa mwaka 2012 zitafanyika leo kwenye Ukumbi wa Zurich Convention Centre nchini Uswisi.

Aguero akihojiwa na gazeti la Argentina la 'Ole', alisema Muargentina mwenzake huyo anayeichezea Barcelona ya Hispania anastahili kupewa tuzo hiyo.
"Anastahili tuzo hiyo kwa yote aliyoyafanya akiwa na Barcelona na timu ya taifa ya Argentina," alisema Muargentina huyo, ambaye pia ana ndoto za kuja kuwa mchezaji bora wa dunia siku moja.
 "Si jambo rahisi, lakini kama utafanya mambo yako vizuri huwezi kujua (unaweza kushinda tuzo). Unajua daima unapaswa kuota kuwa mchezaji bora duniani," aliongeza.
Aguero pia alizungumzia kiwango cha timu yake cha sasa. "Hatujacheza kama ambavyo tulikuwa tukicheza msimu uliopita, lakini tuko katika nafasi nzuri. Tunaongezeka ubora na katika mechi mbili zilizopita tulicheza vizuri sana. Tuna kikosi kizuri na tuna uwezo wa kurejea katika kiwango kama cha msimu uliopita. Kutolewa kwenye Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ilikuwa pigo kubwa kwa sababu tulikuwa na matumaini makubwa katika michuno ile. Tulikuwa katika kundi gumu. Taji la Ligi ya Klabu Bingwa ni jambo tunaloliota pia. Tutafanya vyema siku zijazo," alisema.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina pia alijumuisha mwaka wake 2012 akisema: "Ulikuwa ni mwaka mzuri katika maisha yangu ya soka. Ulikuwa muhimu katika kujijenga kwenye klabu ya Man City na kutwaa ubingwa wa England. Na kikubwa ni kufunga goli lile lililoamua bingwa katika dakika za lala salama. Ilikuwa ni ndoto iliyogeuka kwa kweli," aliongeza Aguero.
Mshambuliaji huyo pia alizungumzia timu ya taifa ya Argentina, akisema: "Jambo muhimu zaidi ni kwamba tufuzu kwa Kombe la Dunia 2014 mapema iwezekanavyo. Kama ukipoteza mechi mbili katika michuano hii migumu ya kuwania kufuzu timu nyingine zinakufikia. Ulikuwa ni mwaka mzuri kwa timu ya taifa. Tumeanza kuzoeana na kufanya mambo sahihi uwanjani," alisema.

Saturday, January 5, 2013

Machini aibuka kumtetea Balotelli, adai hawatamfukuza

Kocha Mancini na Balotelli
MANCHESTER, England
KOCHA wa Manchester City, Roberto Mancini amesema atampa Mario Balotelli "nafasi nyingine 100 zaidi" za kujirekebisha baada ya kusisitiza kuwa malumbano yake na mshambuliaji huyo hayakuwa ni ngumi.
Picha zinaonyesha wawili hao wakitenganishwa wakati wa mazoezi yao ya jana.
Lakini Mancini alisema kuhusu tukio hilo kwamba kilichotokea na Muitalia mwenzake huyo: "Si ngumi, siyo kweli. Picha zinaelezea vibaya tukio.
"Nitampa nafasi nyingine 100 kama nadhani inawezekana akabadilika. Nampa nafasi nyingine, hakika, kwa sababu ana umri wa miaka 22 na anaweza kufanya makosa."
Tukio hilo jipya zaidi katika mfululizo wa matukio ya utata yanayomhusisha mshambuliaji huyo, limemuonyesha Balotelli katika picha akikunjana na kocha wake.
Picha zinaonyesha Mancini akimbwatukia mchezaji wake huyo, ambaye amefunga magoli matatu katika mechi 21 msimu huu.
Picha moja inawaonyesha wawili hao wakiangaliana uso kwa uso, nyingine Mancini akivuta jezi ya Balotelli, wakati katika picha nyingine mshambuliaji huyo anaonekana akivutwa pembeni na wafanyakazi wa uwanjani hapo.
Lakini Mancini amedai kwamba tukio hilo limekuzwa mno na kusisitiza kwamba Balotelli anahitaji klabuni hapo.
"Haikuwa mbaya," alifafanua. "Tulikuwa tunacheza mechi, Mario akampiga teke mwenzake nikamwambia 'nenda ndani (kwenye vyumba vya kuvalia), ondoka uwanjani'.
"Alisema 'hapana' hivyo nikamvuta shati lake na kumsukuma nje ya uwanja. Hicho ndicho kilichotokea. Hakuna cha zaidi."
"Mario yuko hivi lakini mtazamo wangu (kuhusu hatma yake) hautabadilika, hii siyo muhimu. Tatizo litakuwa yeye mwenyewe. Kama hatabadilika, kwake itakuwa ngumu sana huko baadaye, Kwake, si kwangu.
"Mario anaweza kubaki nami siku moja, mwezi mmoja, miaka mitano. Ana miaka 22. Anahitaji kubadilika. Tatizo lake ni yeye mwenyewe."
Alipoulizwa kama ni yeye ndiye aliyepandisha hasira katika tukio hilo, Mancini alijibu: "Hapana. Kwa sekunde mbili za kwanza, ndiyo, lakini baada ya sekunde tatu ama nne hakutaka kuondoka uwanjani. Kwangu alipaswa kuondoka."

BURIANI SAJUKI, NDIVYO ALIVYOZIKWA NA MAELFU JIJINI DAR

Hili ndilo kaburi ambalo Sajuki amezikwa  katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam Januari 4, 2013.

Rais Kikwete naye alikuwepo katika kumzika Sajuki Januari 4, 2013.
Hallooo... hapa ndo tunakaribia kumzika mshkaji wetu Sajuki...!

Hapa ni maandaalizi ya mapeeema kabla jeneza la sugu halijaletwa na mwili wa msanii huyo kuzikwa Januari 4, 2013. 



Na mie nipishe nichukue ukumbusho wa kaburi la Sajuki...!



Tafakuri makini kabla ya mazishi ya Sajuki  Januari 4, 2013.

Steve Nyerere mwenye kanzu mbele, Tino (nyuma ya Steve) na waombolezaji wengine wakitafakari kabla mwili kufikishwa kwenye makaburi ya Kisutu na kuzikwa jijini Dar es Salaam Januari 4, 2013.

Kwaheri jembe letu Sajuki... msanii Ray akitafakari kabla ya kuzikwa kwa Sajuki  Januari 4, 2013.

Tangulia mwana... sote tuko nyuma yako Sajuki! Jotti akitafakari kabla ya mazishi ya Sajuki  Januari 4, 2013.
Single Mtambalike 'Richie' (kushoto) naye aliibuka 'kisheikh' kumsindikiza Sajuki  Januari 4, 2013. 
Chuzi naye alikuwepo na mtoko wake wa Kisheikh


Kwaheri mwanangu Sajuki... msanii nyota wa filamu, Mzee Chillo naye alikuwapo kumzika Sajuki Januari 4, 2013.

Hivi ni kweli umeondoka Sajuki? Siamini!

Mtangazaji Benny Kinyaiya hakubaki nyuma kumsindikiza Sajuki  Januari 4, 2013.
Msanii Jimmy Mponda a.k.a Jimmy Master alikuwa akimuaga Sajuki kwa staili yake.
Mhe. Zitto Kabwe (wa pili kushoto) akitafakari jambo na wasanii na waombolezaji wengine katika makaburi ya Kisutu kabla ya kuzikwa kwa Sajuki  Januari 4, 2013.

Kwaheri kijana wangu....! Msanii nyota wa filamu, Mzee Magali (kulia) akionekana mwenye majonzi tele kabla ya kuzikwa kwa mwenzao Sajuki  Januari 4, 2013.  (Picha zote: Shafii Banzi)
Said Fella (kushoto) na Chege pia walikuwapon
Ni huzuni kubwa kwa kifo cha mpendwa wetu Sajuki... Mungu amlaze pema! Mbunge wa Kinondoni, Mhe. Iddi Azzan.




Hapa kabla ya kuwasili kwa mwili kwenye makaburi ya Kisutu  Januari 4, 2013.








RAIS Dk Jakaya Kikwete jana aliongoza maelfu ya waombolezaji katika mazishi ya msanii Juma Kilowoko 'Sajuki' aliyefariki juzi jijini Dar es Salaam.
Mazishi ya msanii huyo yalifanyika katika makaburi ya Kisutu na kuhudhuriwa na watu maarufu nchini wakiwemo viongozi wa Serikali, Wabunge, wanamichezo na wasanii mbalimbali wa filamu na muziki.
Mwili wa Sajuki uliwasili makaburini katika gari maalum la kubebea wagonjwa saa 8:47 mchana, dakika tatu baada ya Rais Kikwete kuwasili na msafara wake.
Mwili huo uliingizwa kaburini saa 8:53 na baada ya hapo baba wa marehemu, Mzee Said Kilowoko alitupia udongo kwenye kaburi la mwanae na kufuatiwa na Rais Kikwete na kisha Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba na kufuatiwa na waombolezaji wengine.
Akiongea katika makaburi ya Kisutu, Dk. Kikwete alisema serikali inasikikitishwa na kifo cha msanii huyo kijana aliyekuwa na ndogo za kuendeleza tasnia ya filamu nchini na kuitaka familia kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki cha maombolezo.
Naye baba wa marehemu, Mzee Juma Kilowoko, aliishukuru serikali, wasanii na watanzania kwa ujumla kwa namna walivyoshiriki tangu kifo cha mwanaye kitokee mpaka walipompumzisha jana kwa heshima zote na kudai hana cha kuwalipa zaidi ya kulipwa na Allah SW.
Baadhi ya viongozi waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe, Mbunge wa Kinondoni, Idd Azan, Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye, Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa na wengineo wengi.
Sajuki alifariki dunia juzi asubuhi katika hospitali ya Muhimbili alipolazwa kwa matatizo ya upungufu wa damu.
Baadhi ya waombolezaji akiwemo Meneja wa kundi la TMK wanaume Family Said Fella,  Wanamuziki Banana Zoro na Kassim Mapili wamesema kifo cha Sajuki ni pigo sio tu kwa familia yake bali tasnia nzima ya sanaa nchini.
Wasanii mbalimbali pamoja na wachezaji wa mpira wa miguu wa zamani walijitokeza katika mazishi ya msanii huyo, aliyeanza kufahamika mwaka 2005 alipojiunga Kaole kabla ya kuanza kujitegemea akizalisha filamu mbalimbali zilizompatia umaarufu mkubwa.
Marehemu Sajuki ameacha mke na mtoto watoto wawili.