STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 6, 2013

Aishi Manula achekelea ushindani Ligi Kuu

Kipa Aishi Manula
KIPA mahiri anayedakia timu ya Azam FC na timu ya soka ya Tanzania (Taifa Stars), Aisha Manula, amesema anafurahishwa na hali ya ushindani uliojitokeza mapema kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
Manula, miongoni mwa wachezaji chipukizi waliopo kikosi cha Kim Poulsen kinachojiandaa na mechi ya kukamilisha ratiba kati ya Tanzania na Gambia, alisema kwa mwendo ulianza kwenye ligi hiyo ni wazi msimu huu ni mgumu.
Kipa huyo aliyewahi kuwa kipa bora wa michuano ya Uhai Cup 2011, alisema matokeo ya kustaajabisha yaliyojitokeza katika mechi za raundi mbili za awali ni dalili za kuwa na msimu mgumu ulioweza kutabirika kirahisi.
"Nafurahishwa na namna ligi ilivyoanza, inaonyesha itakuwa ya aina yake msimu huu kwani timu zinaonyesha kupania kufanya vyema na ndiyo maana mechi mbili za awali za kila timu kumekuwa na matokeo yaliyostaajabisha, " alisema. Manula, alisema kwa upande wa klabu yake ya Azam anaamini huu utakuwa ni msimu wake wa kuweka rekodi kwa kunyakua ubingwa kwa mara ya kwanza baada ya miaka nenda taji hilo kuzunguka klabu za Simba na Yanga.
Kipa huyo aliyekuwa dimbani wakati Azam ikizamishwa bao 1-0 na Yanga katika mechi ya Ngao ya Hisani, alisema haoni kitakachoizuia Azam isitimize ndoto ya kutwaa taji la Ligi Kuu mwaka 2013-2014.
Azam washindi wa pili wa misimu miwili mfululizo, ilianza ligi hiyo kwa mechi za ugenini ikipata sare ya 1-1 kwa Mtibwa Sugar kabla ya kuilaza Rhino Rangers  2-0 mjini Tabora na mechi ijayo itakuwa Kagera kuvaana na Kagera Sugar.

Mauaji ya kinyama! Waendesha Bodaboda wazidi kuuwawa Iringa

Edger Lalika akiwa  wodini kabla ya  kufariki dunia
 Francis Godwin na  Kayanda Mnyanya,Iringa 
 
ZIKIWA  zimepita  siku  chache  toka  mmoja kati ya madereva boda boda mjini Iringa kutekwa kisha  kujeruhiwa vibaya kabla ya kuporwa  pikipiki  yake ,unyama huo dhidi ya madereva  boda boda  umeendelea kutikisa mji wa Iringa baada kijana mmoja mkazi wa kihodombi kutekwa kisha kuuwawa kinyama.
Tukio hilo la kinyama  limetokea  usiku  wa  leo baada ya kijana  huyo aliyetambulika kwa  jina la Edger Lalika kukutwa ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani .
Mashuhuda  wa  tukio hilo  wameueleza mtandao  huu wa matukio daima .com kuwa tukio la kuuwawa  kwa  dereva  boda  boda  huyo liletokea eneo la  Tosamaganga wilaya ya Iringa mkoani Iringa.
Hata  hivyo kijana  huyo anayekadiliwa  kuwa na umri wa miaka 20,ameuwa akiwa anafanya shughuli zake za bodaboda baada  ya  kukodiwa na mteja  wake huyo ambae aliamua  kuitoa roho yake kabla ya kumpokonya boda boda.
Kutokana na tukio  hilo  baadhi ya madereva bodaboda wamelaani vikali kitendo hicho na kuwataka madereva bodaboda wengine kuungana na kushirikiana na jeshi la polisi kufichua vitendo hivyo  vya utekaji na mauwaji  dhidi ya madereva  boda boda.
Mazishi ya kijana huyo yanafanyika leo katika makaburi ya mlolo Iringa mjini
Jeshi la  polisi mkoa  wa Iringa  limethibitisha  kutokea kwa mauwaji  hayo.

Matukio Daima

Mhe. Ndugai atupiwa lawama vurugu za jana bungeni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbR2CeEeeh8aIgUAxVg23rr5e1DG0s7zx41yhCH6ZY0ziYoTLNSlZ-GP5_9Ea0yd37vWfoS1hBkiDketxjf3x7RCdF75YebSxZRnTJ2pZrrF6f6fURo2Bm3aA0BXX6bHz5R5_eUhGDKMDI/s400/_MG_0724+MBILI.JPG

Wanabodi, 
Mwaka mmoja uliopita niliwahi kuleta hoja hii humu Wito: Wabunge Badilini Kanuni Kuondoa Udikteta wa Spika/N.Spika!
Leo nimeikumbuka kufuatia vurugu za jana bungeni!.
Chanzo cha vurugu zile ni "Ukosefu wa Busara Ndogo Tuu toka kwa Naibu Spika!".
Tangu tumepata uhuru, Tanzania imekuwa nchi ya chama kimoja kwa kipindi kirefu, tulipoingia mfumo wa vyama vingi ile 1992, tulifanya marekebisho tuu ya kanuni, ila hatukuweza kufanya mabadiliko ya "mind set" toka mfumo wa chama kimoja hadi mfumo wa vyama vingi, hivyo hali hii imeendelea mpaka sasa kwa CCM ambayo ndio chama tawala, kuendelea kuonekana ni chama dola kwa sababu ndiyo inayoongoza dola, na nafasi ya vyama vya upinzani kuonekana vipo vipo tuu kwa vile vimeanzishwa kwa mujibu wa sheria!.
Kufuatia hali hii ya "CCM Supremacy" kunapelekea viongozi wa mihimili mikuu ya nchi, Bunge, Mahakama na Serikali, kutimiza wajibu wake kwa mlengo wa heshima kwa CCM kwa sababu M/Kiti wa chama tawala ndie head of Executive, ambaye ndiye rais wa nchi anaeteua kila mtu!.
Huku kujikomba komba kwa CCM, kumepelekea hata Spika na Naibu Spika ambao walipaswa kutimiza majukumu yao independently, wanajikuta wakiifavour CCM, kwa lengo la kujikomba komba huku wakiliangamiza taifa bila wao kujijua kwa kisingizio kuwa kwa vile CCM ndio chama tawala!.
Kwa mujibu wa uendeshaji wa mabunge ya vyama vingi, Mkuu wa shughuli za serikali bungeni, ambaye ni Waziri Mkuu, na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, KUB, ambaye ni Mhe. Freeman Mbowe, wana hadhi sawa kabisa ndani ya bunge!. Hakuna mmoja ambaye ni mkubwa zaidi ya mwingine wala hakuna aliyebora zaidi ya mwenzake!. Wako sawa sawa kabisa!.
Vivyo hivyo, hadhi za mawaziri na mawaziri vivuli ndani ya bunge ni sawa kabisa, tofauti pekee ni mawaziri wana means zaidi kutokana na uwezeshaji kiliko hawa vivuli!. Mfano Waziri Magufuli, akishakagua barabara au kuizindua, waziri kivuli alipaswa aifanyie ukaguzi na kutoa mawazo yake kama ni chini ya kiwango etc, etc.
Haki zote za Waziri Mkuu bungeni ndizo pia haki za KUB!. 
Japo haijaandikwa kwenye kanuni yoyote kuwa Waziri Mkuu akisimama, "ni lazima spika ampe ruhusa ya kusikilizwa" no matter what!. Spika hana mamlaka yoyote ya kuamua kutomsikiliza Waziri Mkuu anaposimama kwa hoja yoyote!. Vivyo hivyo, spika au naibu spika, "hana mamlaka!" ya kumzuia KUB kuzungumza!. 
Naomba wale wenye mapenzi mema na nchi hii, hebu tuwe wakweli toka ndani ya nafsi zetu, hivi kweli pale bungeni jana, angesimama Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda, hivi kweli Naibu Spika angemwambia "Kaa Chini?!". Angeendelea kusimama hivi Naibu Spika angewaamuru askari wa bunge kumtoa nje?!.
Hadhi ya KUB ni sawa kabisa na Waziri Mkuu, kitendo cha Naibu Spika kumzuia KUB asizungumze, kumuamuru akae chini na kisha kuamuru atolewe nje, "that was provocation kwa wapinzani wote wa kweli!", kiliwatia hasira, na kilichofuata ni actions in provocation!. Chanzo ni ukosefu wa busara ndogo tuu wa Naibu Spika!.
Laiti Mhe. Naibu Spika, angelimruhusu KUB kuzungumza na kuisikiliza hoja yake!, naamini 100% kwa 100%, yote yaliyofuatia yasingetokea!.
Bungu letu lina mapungufu makubwa na ya msingi ya kikanuni za uendeshaji mabunge ya vyama vingi!. Kiukweli kila kunapotokea vurugu bungeni, mimi huwa namkumbuka sana Mhe. Samuel Sitta!.
Kiukweli huko nyuma nimewahi kulalamikia sana uendeshaji wa bunge wa Madam Spika, Mhe. Anna Makinda, lakini sasa sasa nakiri, pamoja na mapungufu yake yote ya kibinaadamu, Mhe. Anna Makinda is better of 100 times than Mhe. Job Ndugai!. This man is a disaster!. 
Wabunge tumieni kanuni namba 135-(1) Kutuondolea mtu huyu, japo najua wabunge wa CCM watautumia wingi wao vibaya kutoipitisha hoja hiyo, ile tuu process ya "kukataliwa!" ni funzo tosha!.
Mwaka mmoja uliopita nilitoa angalizo hili, na leo nalitoa tena! Wito: Wabunge Badilini Kanuni Kuondoa Udikteta wa Spika/N.Spika!

Wasalaam.
Pasco.

Chanzo : JamiiForums

Msikiti wa Answar Sunna wateketea kwa moto, kisa...!

 
MSIKITI mkubwa wa Answar Sunna  uliopo  barabara ya Saba mjini Dodoma  umewaka  moto  mchana  huu  ikiwa  ni  muda  mfupi  baada  ya  swala  ya  mchana  kumalizika.

Akiongea  kwa  njia  ya  simu  mmoja  wa  mashuhuda  walioshuhudia  tukio  hilo  amedai  kuwa  chanzo  cha  moto  huo  ni  moto wa  JIKO  la  wakazi  wa    ghorofa ya  juu  ya  jengo  la  msikiti  huo...

Hata  hivyo, shuhuda  mwingine  aliyeongea  na  mtandao  huu  amedai    kuwa  chanzo  cha  moto  huo  ni  hitilafu  ya  umeme  iliyoanzia  ghorofa  ya  juu  ya  jengo  hilo.

 
Kwa  mujibu  wa  mashuhuda  hao, moto  huo  umefanikiwa  kudhibitiwa  na  jeshi  la  zima  moto  na  kwamba  hakuna  mtu  aliyepoteza  maisha  kutokana  na  moto  huo.


  
MPEKUZI

Anko Kitime, Shigongo, Msama waula BASATA

Profesa Penina Mlama
Na Veronica Kazimoto – MAELEZO, Dar es Salaam
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Penina Mlama kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.  
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari - MAELEZO, Uteuzi huo wa Profesa Mlama unaanzia mwaka 2013 na unatarajia kumalizika mwaka 2016.
Prof. Mlama ni Profesa wa Sanaa na Sanaa za Maonyesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.  
Aidha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla watu 12 kuwa wajumbe wa BASATA kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka huu.
Walioteuliwa ni pamoja na wawakilishi wa Vyama na Asasi mbalimbali wa Baraza hilo ambao ni Dkt. Vincensia Shule, John Kitime, Angela Ngowi, Dkt. Herbert Makoye, Erick Shigongo na Alex Msama.
Alex Msama
Wawakilishi wengine ni pamoja na Juma Adam Bakari, Daniel Ndagala, Michael Kadinde na Joyce Fisoo.
Wanaoingia kwa mujibu wa nyadhifa zao ni Prof. Hermas Mwansoko na Katibu Mtendaji wa BASATA.
http://www.bongocelebrity.com/wp-content/uploads/2012/06/John-Kitime.jpg
John Kitime 'Anko'
 
Katika hatua nyingine Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara amemteua Bwana Ghonche Materego kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). 
Kabla ya uteuzi huo Materego alikuwa amemaliza muda wake kama Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa.
Wajumbe wa Bodi hiyo walioteuliwa na Waziri Mukangara ni Dkt. Herbert Makoye, Prof. Emanuel Mbogo, Dkt. Lucy Mboma, Prof. Hermas Mwansoko pamoja na Katibu Mtendaji wa BASATA.
Wakati huo huo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla ya watu 21 kuwa wajumbe wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka 2013 hadi 2015. 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjoeAYpD19CUAPAApd52dHguEu911uTkpaFXAq9066MauQU5HEOi7C5LkQMpYFJQ0CXHPoiVJTGw5pvzB3-YujazwtVwQPuZQWhh4elz789G570CD39Q2Vvf-E15sj7DMO2jURIUcZW5jJy/s1600/eric.jpg
Eric Shigongo
Wajumbe hao ni Dkt. Shani Omari, Prof. Yohana Msangila, Ester Riwa, Dkt. Issa Zidi, Khadija Juma na Dkt. Martha Qorro.
Wengine ni Mmanga Mjawiri, Razia Yahaya, Richard Mbaruku, Selina Lyimo, Keneth Konga, Amour Khamis, John Kiango, na Shani Kitogo. 
Wajumbe wengine ni Ally Kasinge, Ahmed Mzee, Rose Lukindo, Shabani Kisu pamoja na Edwin Mgendera.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo la BAKITA atachaguliwa na wajumbe watakapokutana kwenye kikao chao cha kwanza.

Zantel yamleta Azonto, kuwasha moto kesho Dar

Mwanamuziki anayetamba na wimbo wa Azonto kutoka Ghana, Fuse ODG (katikati), akionesha manjonjo yake  wakati wa mkutano na waandishi wa habari, kuhusiana na onesho lake litakalofanyika Jumamosi katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam. Katikati ni Ofisa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan. Mwanamuziki huyo ameletwa na Kampuni ya Simu za mkononi ya Zantel kwa kushirikiana na Times FM. (Picha na Francis Dande)
Mwanamuziki anayetamba na wimbo wa Azonto kutoka Ghana, Fuse ODG akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusiana na onesho lake litakalofanyika leo katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam. Wa pili kushoto ni Ofisa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan.

Wanaombeza bondia Francis Cheka someni hapa!

Francis Cheka (kulia) alipokuwa akimsulubu Mmarekani Phil Williams na kutwaa mkanda wa WBF
HIVI karibuni Mtanzania Francis Cheka ambaye alikuwa  bingwa wa IBF katika bara la Afrika uzito wa kati (Super Middleweight) alimshinda bondia kutoka Marekani Phil William na kutawazwa kuwa bingwa wa dunia anayetambuliwa na Shirikisho la Ngumi la Dunia (WBF). Ushindi wa Cheka sio tu kwa Tanzania bali na kwa bara la Afrika na dunia yote kwa ujumla.
 
Cheka ameungana na mabingwa wengine wa dunia wa uziro wa kati (Super Middleweight) wanaotambuliwa na vyama na mashirikisho kadhaa kama ifuatavyo:
 
IBF    -  Carl Froch kutoka nchini Uingereza
WBC -  Andre Ward kutoka nchini Marekani
WBA -  Andre Ward kutoka nchini Marekani
WBO -  Robert Stieglitz kutoka nchini Ujerumani
WBF -   Francis Cheka kutoka nchini Tanzania
IBO   -  Thomas Oosthuizen kutoka nchini Afrika ya Kusini

Kwa uchache hao ni mabingwa wa uzito wa uzito wa kati (Super Middleweight ) wanaotambuliwa na vyama/mashirikisho hayo niliyoyataja hapo juu. Kati ya mabingwa wa dunia wa mashirikisho/vyama sita vikubwa duniani Afrika imetoa mabindia wawili tu nao ni Francis Cheka kutoka nchini Tanzania na Thomas Oosthuizen kutoka nchini Afrika ya Kusini.
 
Ubingwa alioupata Francis Cheka ni wa dunia na hautakiwi upingwe na mtu yeyote yule nje ya ulingo bali wanaotaka kumpinga na kuukebehi wanatakiwa wapande naye ulingoni au wamtafutie mtu wao apande naye ulingino ili apigane na Francis Cheka.
 
Kwa bahati mbaya, taratibu na sheria za mchezo wa ngumi haziruhusu mtu yeyote ambaye hayuko kwenye viwango vya ubora wa ngumi agombee ubingwa wa aina yeyote ule.
 
Mashirikisho au vyama vya ngumi vimeweka utaratibu maalum wa mabondia watakaoweza kugombea ubingwa wa dunia na mara nyingi ni wale tu walio kwenye viwango vya juu kuanzia namba moja hadi namba tano.
 
Tanzania sasa tuna bingwa wa dunia katika uzito wa kati (Super Middleweight) na ni Francis Cheka. Tunachukua fursa hii kumfagilia na kumpongeza Francis Cheka kwa kulitangaza vyema jina la Tanzania na kuliweka kwenye chati duniani.
Onesmo Ngowi
Rais wa IBF Africa, Ghuba ya Uarabu na Uajemi na mashariuki ya Kati
 

Stars watua salama Banjui, Kaseja kukaa golini kesho

Juma Kaseja
Na Boniface Wambura
KIKOSI cha Taifa Stars kimewasili salama hapa Banjul, Gambia tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji itakayochezwa kesho (Septemba 7 mwaka huu).

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imewasili hapa jana (Septemba 5 mwaka huu) saa 11 jioni ikitokea Dakar, Senegal ambapo ilichelewa kuunganisha ndege, hivyo kuamua kutumia usafiri wa barabara kwa vile ni karibu na baadaye kupanda kivuko kuingia Banjul badala ya kulala na kuchukua ndege nyingine siku inayofuata.

Wachezaji wako katika hali nzuri na leo jioni wanatarajia kufanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Independence ulioko Bakau ambao utatumika kwa mechi ya kesho. Timu imefikia hoteli ya Seaview iliyoko kandokando ya Bahari ya Atlantic.

Mechi hiyo itaanza saa 10.30 jioni kwa saa za hapa ambapo nyumbani Tanzania itakuwa saa 1.30 usiku, na itachezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda Munyemana Hudu. Waamuzi wasaidizi ni Theogene Ndagijimana, Honore Simba na Issa Kagabo. Kamishna ni Andy Quamie kutoka Liberia.

Washabiki na vyombo vya habari vya hapa wanaizungumzia mechi hiyo ambayo ina umuhimu mkubwa kwa pande zote, huku Gambia ikiwa imeita wachezaji tisa wanaocheza barani Ulaya na Marekani. Gambia ambayo imepata uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Gambia (GFA) imepania kuhakikisha haimalizi mechi za mchujo ikiwa na pointi moja tu.

Kwa upande wa Tanzania, Kocha Kim Poulsen amesema nia ni kuona Stars yenye pointi sita inamaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Ivory Coast ambayo tayari imechukua tiketi pekee ya kucheza raundi ya mwisho kutoka kundi hili la C.

“Mechi hii ni muhimu kwetu kwa vile tunataka matokeo mazuri ugenini. Lakini kikubwa ni kuwa matokeo mazuri si tu yatatuweka katika nafasi ya kuwa wa pili, lakini vilevile yatatusaidia kuongeza pointi kwenye viwango vya ubora vya FIFA, na kikubwa zaidi hii ni sehemu ya maandalizi ya sisi kucheza Fainali za Afrika za 2015,” amesema Kim.

Stars inatarajiwa kupangwa hivi; Juma Kaseja, Vincent Barnabas, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Henry Joseph, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Amri Kiemba, Mrisho Ngasa, Simon Msuva na Khamis Mcha.

Yanga yafafanua sakata la Katibu Mkenya

Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga (kati) akifafanua jambo wakati wa mkutano wake na wanahabari leo kufafanua suala la ajira ya Katibu Mkuu wa klabu hiyo uliofanyika leo. (Picha:Francis Dande)
UONGOZI wa klabu ya Yanga kupitia Makamu Mwenyekiti wake, Clement Sanga ametoa ufafanuzi juu ya habari zilizokuwa zimeenea kuhusiana na taarifa za mabadiliko ya kaimu katibu mkuu Lawrence Mwalusako kuondolewa kwenye nafasi yake na kuchukukuliwa na mtu mwingine.
Akiongea na waandishi wa habari leo,  Sanga amesema taarifa hizo hazina ukweli kwamba tayari kuna mtu anachukua nafasi ya Mwalusako, bali kilichotokea ni kutokuwepo kwa mawasiliano mazuri katika suala hilo kati ya viongozi na wazee.
Kilichopo ni kwamba uongozi wa klabu ya Young Africans upo katika mchakato wa kuhakikisha unajaza nafasi zilizopo wazi za mkurugenzi wa ufundi, mkurugenzi wa masoko, mkurugenzi wa fedha na zoezi hilo linaendeshwa na kampuni moja ambayo waliipa nafasi ya kuendesha zoezi hilo.
Zoezi likiwa ndani ya mchakato mmoja wa waombaji wa nafasi hizo Patrick Naggi aliwasili makao makuu ya klabu ya Yanga kwa lengo la kutaka kujua mazingira ya ufanyaji kazi yakoje na kufahamu baadhi ya mambo kuhusiana na klabu ndipo kulipotokea kutokuelewana na baadi ya wanachama wakiwemo wazee waliokuwepo eneo la klabu.
Kwa maana hiyo napenda kutoa taarifa kwa umma na wanachama wa Yanga kuwa uongozi bado haujatoa baraka za ajira kwa mtu yoyote katika nafasi hizo, isipokuwa ni muombaji aliwahi kufika makao makuu kabla ya mchakatao wa usahili kukamilika.
Lawrence Mwalusako anaendelea kuwa kaimu katibu mkuu wa Yanga mpaka hapo kutakapokuwa na taarifa nyingine zozote za mabadiliko kwa nafasi zote zilizopo wazi katika idara mbalimbali.
Uongozi unawaaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa soka kuwa kitu kimoja katika kuunga mkono harakati za kimaendeleo ili kuifanya timu iende katika hatua nyingine ya ushindani wa kimatifa.

Fundi Kinyambe fumbafu thana

Kinyambe (kushoto) akiwa na Mzee Jangala

MCHEKESHAJI mahiri nchini James Mohammed 'Kinyambe'  amefyatua filamu tatu binafsi ambazo amepanga kuziachia moja baada ya nyingine hivi karibuni.
Kinyambe anayetamba kwenye kipindi cha vichekesho cha 'Vituko Show' alizitaja filamu hizo kuwa ni 'Fundi Kinyambe', The Twins na ' Fumbafu Thana' kuanzia Novemba mwaka huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Kinyambe alisema filamu hizo amepanga kuziachia moja moja kuanzia Novemba mwaka huu.
Kinyambe alisema filamu hizo za vyumba mbavu ameigiza na wasanii mbalimbali nchini wakiwamo wenzake wanaoigiza nao katika kipindi cha 'Vituko Show'.
"Ni kati ya kazi zinavyomfanya mtazamaji ashikilie mbavu zake mwanzo mwisho, nitaanza kuziachia rasmi Novemba nikianza na 'Fundi Kinyambe' kisha 'The Twins' na kumalizia 'Fumbafu Thana'," alisema Kinyambe.

Afande Sele kuzindua Novemba

Afande Sele

MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Seleman Msindi 'Afande Sele' anatarajia kufanya uzinduzi wa albamu yake mpya iitwayo 'Kingdom wa Amani na Upendo' utakaofanyika Novemba mwaka huu mjini Morogoro na kusindikizwa a  wasanii mbalimbali nyota wa hapa nchini.
Akizungumza na MICHARAZO Afande Sele, alisema kwa sasa ni mapema kuwataja wasanii watakaomsindikiza kwa sababu anaendelea kumalizana na wadhamini wake.
Alisema kwa sasa anajipanga kuitambulisha albamu hiyo kwa kuachia video ya wimbo unaoendelea kutamba wa 'Dini Tumeletewa' alioimba kwa kushirikiana na Belle 9.
Mkongwe huyo alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo 10 na siku za uzinduzi itaachiwa 'audio' na video yake kwa mpigo ili mashabiki wake wapate vitu kamili kwa wakati  mmoja.
Alitaja baadhi ya nyimbo za albamu hiyo ni pamoja na 'Dini Tumelewa', 'Amani na Upendo', 'Soma Ule', 'Mi Sielewi', 'Karibu Moro', 'Sukari na Chai', 'Simba Dume na 'Kingdom'.

Kinondoni yainyuka Pwani 7-0 Copa Coca Cola


MABINGWA mara mbili wa Copa Coca-Cola timu ya Kinondoni imewapa kipigo kikubwa wenyeji timu ya Pwani cha magoli 7-0 katika mashindano yanayoendelea ya vijana chini ya umri wa miaka 15 ya Copa Coca-Cola ngazi ya kanda kwenye uwanja wa Tumbi, Kibaha juzi jioni.
Kinondoni walipata goli lao la kwanza katika dakika ya 4 kupitia kwa Kidanga Hamadi baada ya kuunganisha krosi kutoka upande wa kulia. Hamadi kwa mara ya pili alitikisa nyavu za wapinzani wao katika dakika ya 11 baada ya kuwapiga chenga mabeki wa timu ya Pwani na kupiga shuti lililotinga moja kwa moja wavuni.
Magoli mengine yalifungwa na Alex Milanzi katika dakika ya sita, Oswin Nungu katika dakika ya 20, Ayubu M. Ayubu katika dakika ya 41, Majid Musa katika dakika ya 66 kwa njia ya penati na Aboubakari Mussa alihitimisha karamu ya magoli katika dakika ya 74.
Katika uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba jijini Mwanza, Geita waliifunga Mara 1-0 katika mechi iliyojaa ushindani.
Kigoma hawakuwa na bahati siku ya Jumatano baada ya kupoteza mchezo dhidi ya wenyeji timu ya Mwanza kwa kufungwa  2-1. Beki wa Kigoma, Hashimu Mussa alijifunga mara mbili katika dakika ya kwanza na ya 72. Kigoma walipata goli lao katika dakika ya 36 kupitia kwa Rashidi Bakari.
Mechi nyingine iliyochezwa katika uwanja huo wa chuo cha ualimu Butimba, Tabora waliilaza Simiyu 2-1. Tabora  walipata goli la kwanza katika dakika ya sita kupitia kwa Selemani Husein kwa njia ya penati kabla ya Rashidi Omary kuhitimisha katika dakika ya 54.
Mechi nyingine katika uwanja wa Butimba juzi iliwakutanisha Shinyanga na Kagera ambapo Shinyanga walishinda 3-0. Magoli ya Shinyanga yalipachikwa wavuni na Anwar Amada katika dakika ya 24, Jahid Nuru dakika ya 60 na Felix Rweyemamu dakika ya 74.
Katika uwanja wa Mkokotoni , Zanzibar , Timu ya Kaskazini Pemba na Kusini Unguja walitoka sare ya 3-3 wakati huo huo Tanga na Temeke nao walitoka sare ya 4-4. Na katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Singida  waliilaza Manyara kwa mabao 2-0.
Fainali za Taifa za Copa Coca-Cola zinahusisha timu 16 ambazo zitaanza kuchuana wiki ijayo jijini Dar es Salaam.

Kaliza wa TRA afagilia masumbwi

Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza katikati akiwa na promota na mdau wa masumbwi Mohamedi Bawazir kushoto Bondia Fransic Cheka na Fransic Miyeyusho wakati walipokwenda Dodoma kutembelea bunge la jamuhuri ya muhungano wa Tanzania baada ya Cheka kutwaa ubingwa wa Dunia wa WBF na kualikwa chakula cha jioni na meneja huyo mjini Dodoma
Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia wakigongesheana grass na Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza wakati wa kutakiana heri baada ya wadau hawo wa masumbwi kupewa heshima ya kutembelea bungeni kwa mara ya kwanza 

Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia  wakiwa katika picha ya pamoja na  Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza
Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia wakigongesheana grass na Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza wakati wa kutakiana heri baada ya wadau hawo wa masumbwi kupewa heshima ya kutembelea bungeni kwa mara ya kwanza  na kuarikwa kwa chakula cha jioni na meneja huyo
Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia wakigongesheana grass na Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza wakati wa kutakiana heri baada ya wadau hawo wa masumbwi kupewa heshima ya kutembelea bungeni kwa mara ya kwanza

Wednesday, September 4, 2013

RUKWA YACHACHAFYA COPA COCA-COLA



Na Boniface Wambura
TIMU ya soka ya Rukwa imeanza vizuri michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 baada ya leo kuichapa Katavi mabao 4-0 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Shule ya Sekondari Iyunga jijini Mbeya.

Mabao ya washindi yalitiwa wavuni na Tumaini Boniface dakika ya 13 na 65, Francisco Mkanga akipachika la pili dakika ya 29 wakati la mwisho lilifungwa dakika ya 75 na Innocent Ahombile.

Katika kituo cha Zanzibar, wenyeji Mjini Magharibi imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kaskazini Pemba kwa mabao ya Faisal Salum na Masoud Mohamed.

Mechi ya pili katika kituo hicho ilikuwa kati ya Kusini Pemba na Kusini Unguja. Bao pekee lililofungwa na Othman Abdallah lilitosha kuipa ushindi wa 1-0 timu ya Kusini Pemba.

Tuesday, September 3, 2013

WAFANYAKAZI STRABAG WAFUNGIWA NJE NA UONGOZI KISA....NI WA MRADI WA MABASI YA KWENDA KASI

 Wafanyakazi wa Kampuni ya Ujenzi wa Mradi wa Mabasi yaendayo Kasi Dar es Salaam (DART), ya Strabag, wakiwa nje ya lango kuu la kuingilia makao makuu ya kampuni hiyo, Ubungo, Dar es Salaam asubuhi hii baada ya uongozi wa kampuni hiyo kuwafungia nje, kutokana na mgomo wa kudai maslahi zaidi kufanyika    KAMANDA WA MATUKIO

















KAMANDA WA MATUKIO BLOG

IRINGA YAINYANYASA RUVUMA COPA COCA-COLA


TIMU ya soka ya mkoa wa Iringa imeanza kwa kishindo michuano ya Copa Coca-Cola kwa watoto wenye umri chini ya miaka 15 baada ya leo (Septemba 3 mwaka huu) kuitandika Ruvuma mabao 4-0.

Hadi mapumziko katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Shule ya Sekondari Iyunga jijini Mbeya, washindi walikuwa mbele kwa mabao 2-0 yaliyofungwa dakika ya 14 na Justin Luvanda huku Alphonce Kalinga akifunga la pili dakika ya 43.

Mabao mengine yalifungwa na Juma Rogani katika dakika ya 49 na Luvanda akafumania tena nyavu dakika ya 59.

Hiyo ni mechi ya pili mfululizo kwa Ruvuma kupoteza ambapo ya kwanza ililala mbele ya wenyeji Mbeya kwa mabao 3-0.

Shafii Dauda 'abaniwa' TFF, 40 wapitishwa kugombea

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgIcvtnmCBqRdmOdMhm1xSloe3lPbWzAf6TIuVarRn2iaYfjrLKFDRXaTZ6FP45x6Txkaxu0GTMf-wMLHf1HSRVsPASI__RtseGcbTrbiQW3z11FugVysqBPtfeQt7wvRCaNWIy1qsSQ6I/s1600/shafi+dauda.JPG
Shafii Dauda aliyeenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa TFF
 Na Boniface Wambura
Kamati ya Uchaguzi imepitisha majina ya waombaji 40 kati ya 58 kwa ajili ya uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi Tanzania (TPL Board) utakaofanyika mwezi ujao.

Waliopitishwa katika orodha hiyo ya awali kwa upande wa Bodi ya Ligi ni Hamad Yahya Juma (Mwenyekiti) na Said Muhammad Said Abeid (Makamu Mwenyekiti).

Kwa upande wa Kamati ya Uendeshaji (Management Committee) ni Kazimoto Miraji Muzo na Omar Khatib Mwindadi. Walioondolewa kwa vile si wenyeviti wa klabu za daraja la kwanza kama kanuni zinavyotaka ni Michael Njuweni Kaijage, Salum Seif Rupia na Silas Masui Magunguma.

Kanda namba moja (Kagera na Geita) aliyepitishwa kuwania nafasi ya ujumbe Kamati ya Utendaji ya TFF ni Kaliro Samson wakati Abdallah Hussein Musa ameondolewa kwa kutojaza fomu ya uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi.

Jumbe Oddessa Magati, Mugisha Galibona na Vedastus Lufano wamepitishwa kuwania ujumbe kupitia Kanda namba mbili (Mara na Mwanza). Samwel Nyalla ameondolewa kwa kutojaza kikamilifu fomu namba 1 ya maombi ya kugombea uongozi wa TFF kwa kutoonesha malengo yake.

Waliopitishwa katika Kanda namba tatu (Shinyanga na Simiyu) ni Epaphra Swain a Mbasha Matutu wakati Stanslaus Nyongo ameondolewa kwa kukosa sifa ya uongozi wa angalau uzoefu wa miaka mitano kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi na Katiba ya TFF.

Kanda namba nne (Arusha na Manyara) wamepitishwa wote watatu; ambao ni Ali Mtumwa, Elley Simon Mbise na Omar Walii Ali. Kanda namba tano (Tabora na Kigoma) nao wamepitishwa wote; Ahmed Idd Mgoyi na Yusuf Hamis Kitumbo.

Blassy Kiondo amepitishwa peke yake kuwania ujumbe Kanda namba sita (Katavi na Rukwa) huku Ayoub Nyaulingo aliondolewa kwa kutokuwa na uzoefu uliothibitika wa miaka mitano katika uongozi wa mpira wa miguu.

Naye Nazarius Kilungeja, Kamati ilikataa maombi yake ya kugombea ujumbe kutokana na vitendo vyake visivyo vya kimichezo ambavyo kwa kiasi kikubwa vilisababisha migogoro kwenye Mkoa wa Rukwa, hivyo suala lake litawasilishwa kwa Kamati ya Maadili kwa ajili ya hatua zaidi.

Kanda namba saba (Iringa na Mbeya) waliopitishwa ni David Samson Lugenge, John Exavery Kiteve na Lusekelo Elias Mwanjala. Cyprian Kuyava hakupitishwa kwa vile hana uzoefu wa uongozi kwa mujibu wa Katiba ya TFF huku Ayoub Shaib Nyenzi akiondolewa kwa kushindwa kuthibitisha uraia wake.

Elliud Peter Mvella ameondolewa kwa kushindwa kuheshimu Kanuni za Uwajibikaji wa Pamoja (collective responsibility) baada ya kushiriki kufanya uamuzi ndani ya Kamati ya Utendaji ya TFF bila ya kutaka msimamo wake wa kupinga uwekwe kwenye muhtasari na baadaye kuupinga uamuzi huo akiwa kwenye uongozi wa mkoa. Suala lake limewasilishwa katika Kamati ya Maadili kwa ajili ya hatua zaidi.

Waliopitishwa kuwania ujumbe kupitia Kanda namba nane (Njombe na Ruvuma) ni James Patrick Mhagama na Stanley William Lugenge wakati Kamanga Tambwe ameondolewa kwa vile alipatikana na hatia ya kushiriki kwenye tuhumu za rushwa kwa waamuzi na kufungiwa na TFF.

Kanda namba tisa (Lindi na Mtwara) waombaji wote watatu wameptishwa. Waombaji hao ni Athuman Kingome Kambi, Francis Kumba Ndulane na Zafarani Mzee Damoder. Pia waombaji wote wa Kanda namba kumi (Dodoma na Singida), Hussein Zuberi Mwamba, Stewart Ernest Masima na Charles Komba wamepitishwa.

Waombaji wanne kati ya watano wamepitishwa kwa Kanda namba 11 (Morogoro na Pwani). Waliopitishwa ni Farid Mbarak, Geofrey Nyange, Juma Abbas Pinto na Twahil Twaha Njoki.

Riziki Juma Majala ameondolewa kwa vile akiwa mtendaji mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) alishindwa kusimamia Kanuni za Ligi kwa kuruhusu timu ambayo si mwanachama wa wanachama wa COREFA kucheza ligi, hivyo kusababisha mgogoro mkubwa kiasi cha mwananchi mmoja kufungua kesi ya kusimamisha Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL). Suala lake litawasilishwa Kamati ya Maadili kwa ajili ya hatua zaidi.

Kanda namba 12 (Kilimanjaro na Tanga) wamepitishwa waombaji wote wawili. Waombaji hao ni Davis Elisa Mosha na Khalid Abdallah Mohamed.  Waombaji wawili kati ya watano wamepitishwa kuwania ujumbe kupitia Kanda namba 13 (Dar es Salaam).

Wagombea wawili kati ya watano wamepitishwa kuwania ujumbe kupitia Kanda namba 13 (Dar es Salaam).  Wagombea hao ni Alex Crispine Kamuzelya na Muhsin Said Balhabou.

Walioondolewa ni Omar Isaack Abdulkadir kutokana na vitendo vyake vya kutoheshimu na kutotekeleza maagizo ya TFF kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi na Katiba ya TFF. Atapelekwa katika Kamati ya Maadili kwa hatua zaidi.

Shaffii Kajuna Dauda ameondolewa kwa kutumia nyaraka ya mawasiliano baina ya FIFA na Rais wa TFF bila idhini na kuiweka hadharani kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, hivyo kukiuka maadili kwa kumiliki nyaraka ambazo hazikuwa kwenye mamlaka yake. Suala lake linapelekwa katika Kamati ya Maadili.

Naye Wilfred Kidao ameondolewa kwa kutumia nyaraka za Kamati ya Utendaji ya TFF bila ridhaa ya kamati, hivyo kukosa uadilifu. Suala lake linawasilishwa kwenye Kamati ya Maadili kwa hatua zaidi.

Kwa upande wa nafasi ya Makamu wa Rais, waombaji wote watatu wamepitishwa. Waombaji hao ni Imani Omari Madega, Ramadhan Omari Nassib na Wallace John Karia.

Athuman Jumanne Nyamlani na Jamal Emil Malinzi wamepitishwa kuwania nafasi ya Rais. Omari Mussa Nkwaruro ameondolewa kwa kuwasilisha cheti chenye utata, hivyo kukiuka utashi wa Ibara ya 27(7) ya Katiba ya TFF. Pia aliwasilisha taarifa za uongo kuhusu uzoefu na kukiuka Kanuni za Maadili, hivyo suala lake linapelekwa Kamati ya Maadili.

Naye Richard Julius Rukambula ameondolewa kwa hakukidhi matakwa ya kugombea uongozi kwa mujibu wa Ibara ya 12(2)(e) ya Katiba ya TFF inayokataza masuala ya mpira wa miguu kupelekwa katika mahakama za kawaida. Hivyo naye anapelekwa katika Kamati ya Maadili kwa hatua stahiki.

Tutaitaka nafasi ya pili kwa Gambia-Kim

Kocha Kim Poulsen
Na Boniface Wambura
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amesema wanaipa umuhimu mkubwa mechi ya mwisho ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Gambia kwa lengo ni kuhakikisha wanamaliza wakiwa wa pili katika kundi hilo.

Mechi hiyo itachezwa Septemba 7 mwaka huu jijini Banjul, Gambia ambapo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premiem Lager itaondoka kesho (Septemba 4 mwaka huu) saa 11 alfajiri kwa ndege ya Kenya Airways kupitia Dakar, Senegal.

Kim amesema wanataka kushinda ugenini, kwani licha ya kuwa wameshatolewa lakini ushindi utawaongezea pointi kwa ajili ya viwango (rankings) vya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na pia kuepuka kuanzia ngazi ya awali ya mechi za mchujo za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) kwa fainali za 2015.

“Tunacheza mechi hii tukiwa katika mazingira magumu, kwani wengi wa wachezaji wa kikosi cha kwanza ni majeruhi. Sijawahi kukutana na hali hii tangu nilipoanza kuifundisha Taifa Stars, lakini tumejipanga kuhakikisha tunafanya vizuri,” amesema Kim.

Amesema kwa mipango ya timu yake mechi hiyo ni muhimu tofauti na wengi wanavyofikiria, na uamuzi wake wa kumwita beki Henry Joseph amezingatia mambo mengi ya kiufundi ikiwemo nafasi anayocheza na uzoefu wa mchezaji aliyekuwa akicheza nchini Norway katika klabu ya Kongsvinger IL.

Wachezaji majeruhi katika kikosi hicho ni Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Aggrey Morris, Salum Abubakar, Athuman Idd na John Bocco.

Vilevile wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu hawatakuwemo kwenye safari baada ya klabu yao ya TP Mazembe kutuma taarifa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo mchana ikidai ni wagonjwa.
Wachezaji wanaoondoka kwenda Banjul ni Juma Kaseja, Mwadini Ali, Ali Mustafa, Amri Kiemba, David Luhende, David Mwantika, Erasto Nyoni, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Henry Joseph, Jonas Mkude, Juma Liuzio, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa, Nadir Haroub, Said Dilunga, Simon Msuva na Vincent Barnabas.