TIMU
ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania imefanikiwa kuingia nusu fainali ya
mashindano ya Kombe la Dunia yanayofanyika Rio de Janeiro nchini Brazil
baada ya jana kuifunga Indonesia kwa jumla ya mabao 5-3.
Hadi
muda wa kawaida wa mchezo huo unamalizika timu hizo zilikuwa
zimefungana mabao 2-2 ndipo ikatumia mikwaju ya penalti kuamua mshindi.
Tanzania ilipata penalti tatu dhidi ya moja ya wapinzani wao.
Timu nyingine zilizoingia nusu fainali na mechi zake zinachezwa leo (Aprili 5 mwaka huu) ni Burundi itakayocheza na Pakistan.
Katika mechi zilizopita, Tanzania ilitoka sare ya mabao 2-2 na Burundi, ikaitandika Argentina mabao 3-0 ikailaza Nicaragua mabao 2-0 na ikafungwa na Philippines mabao 2-0.
No comments:
Post a Comment