STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 8, 2014

Real Madrid yajiweka pabaya Hispania, Ronaldo shakani

KLABU ya Real Madrid imejiweka katika nafasi finyu ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania baada ya usiku wa kuamkia leo kulazimishwa sare ya 1-1 na timu ya Real Vallodolid.
Sare hiyo imeifanya timu hiyo kucheza mechi 36 na kufikisha pointi 84, nne zaidi ya vinara wa ligi hiyo Atletico Madrid ambao watakutana nao kwenye mechi ya Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itakayochezwa mjini Lisbon Ureno, Mei 24.
Atletico wana pointi 88 tatu zaidi na ilizonazo watetezi Barcelona huku ligi ikisaliwa na raundi tatu kabla ya kukamilishwa kwa msimu huu.
Wageni, Real Madrid walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa beki wake, Sergio Ramos katika dakika ya 35 kabla ya Humberto Osorio kusawazisha dakika tano kabla ya pambano hilo kumalizika na kuzifanya timu hizo kugawana pointi moja moja.
Katika pambano hilo nyota wa Real, Cristiano Ronaldo alitolewa uwanjani huku ikielezwa kuwa alichezeshwa akiwa na maumivu ya nyama ya paja  na kuifanya klabu hiyo kuingiwa na hofu ya kumkosa kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa.

No comments:

Post a Comment