STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 8, 2014

Man City yanusa ubingwa England, Sunderland yaendeleza maajabu yake

Dzeko akifunga bao
Dzeko akishangilia moja ya mabao yake na wachezaji wenzake wa Man City
Fabio Borini akishangilia bao lake lililoisaidia Sunderland kunusurika kushuka daraja
WAKATI Sunderland ikijihakikisha kusalia kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kuitwanga West Bromwich kwa mabao 2-0, Manchester City imejiweka katika nafasi nzuri ya kunyakua taji la ligi hiyo baada ya kupata ushindi mnono nyumbani dhidi ya Aston Villa.
Manchester City iliyorejea kileleni ikiitoa Liverpool ilipata ushindi wa mabao 4-0 na kuwafanya wafikishe jumla ya pointi 83, mbili zaidi ya Liverpool huku ligi ikitarajiwa kumalizika mwishoni mwa wiki ambapo itahitaji ushindi kurejesha taji hilo kwenye himaya yao toka kwa wapinzani wao Manchester United waliolitema taji hilo walilowapokonya msimu uliopita.
Ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Etihad, Manchester City ilipata mabao yake kupitia kwa  Edin Dzeko aliyefunga mabao mawili katika dakika za 64 na 72, Stevan Jovetic na Yaya Toure.
Katika mechi nyingine iliyochezwa pia jana, Sunderland ikiwa nyumbani iliweza kupata ushindi wake wanne mfululizo kwa kuilaza West Brom kwa mabao 2-0 na kujinasua kwenye janga la kushuka daraja ikiwaachgia kasheshe wapinzani wao, West Brom, Norwich City na Hull City.
Mabao yaliyoivusha salama Sunderland katika msimu huu baada ya kusota mkiani kwa muda mrefu yalifungwa na Jack Colback katika dakika ya 13 na Fabio Borini dakika ya 31 na kuifanya timu hiyo kufikisha jumla ya pointi 38 ambazo haziwezi kufikiwa na timu ya Norwich iliyopo nafasi ya 18 ikiwa na pointi 33 ligi ikiwa imesaliwa na mzungumzo mmoja tu siku ya Jumamosi.
Msimu wa Ligi Kuu ya England utakamilishwa siku hiyo ya Mei 11 kwa mechi kati ya Cardiff City vs Chelsea, Fulham vs Crystal Palace, Hull City vs Everton, Liverpool vs Newcastle United, Manchester City vs West Ham United, Norwich City vs Arsenal, Southampton vs Manchester United, Sunderland vs Swansea City, Tottenham Hotspur vs Aston Villa na West Bromwich vs Stoke City.
Timu za Fulham na Cardiff City zenyewe tayari zimeshaaga ligi hiyo na inasubiri timu moja ya mwisho za kurudi nao Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao.

No comments:

Post a Comment