STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 8, 2014

Said Ndemla awatuliza Simba, adai yupo sana Msimbazi

KIUNGO nyota chipukizi wa Simba, Said Ndemla amezitahadharisha klabu ambazo zinamnyemelea kutopoteza muda wao kwa vile hana mpango wa kutimka klabuni hapo.
Akizungumza na MICHARAZO, Ndemla alisema bado yupo sana Msimbazi, klabu iliyosaidia kukuza kipaji chake.
Ndemla anayemudu nafasi zote za kati, alisema kwa sasa akili yake ni kujipanga kwa msimu ujao kuhakikisha Simba inakuwa na mafanikio makubwa baada ya msimu huu kupepesuka na kumaliza kwenye nafasi ya nne baada ya kipindi kirefu.
"Bado nipo sana Msimbazi, wanaonimezea mate wasipoteze muda wao kwani sina mpango wowote wa kiondoka kwa sasa Simba, nafikiria jinsi ya kuisaidia kwa msimu ujao ili turejeshe heshima mjini," alisema.
Kiungo huyo aliyejijengea jina kubwa hasa katika pambano la watani wa jadi la duru la kwanza lililoisha kwa sare ya 3-3 baada ya kuingia dimbani na kufanikiwa kubadilisha matokeo ya timu yake kulala mabao 3-0 na kumaliza kwa sare.
Ndemla na William Lucian 'Gallas' waliingizwa dimbani kipindi cha pili kuchukua nafasi za Abdulhalim Humud 'Gaucho' na Haruna Chanongo na kufanikiwa kuwadhibiti Yanga na kurudisha maabao matatu kupitia kwa Joseph Owino, Gilbert Kaze na Betram Mombeki.
Kauli ya Ndemla ya kudai ataendelea kusalia Simba imekuwa kukiwa na tetesi kwamba kiungo huyo anatolewa macho na baadhi ya klabu za Ligi Kuu kwa ajili ya kunasa saini yake ili kuzichezea msimu ujao.

No comments:

Post a Comment