STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 8, 2014

Rose Ndauka, Wastara Juma, Lulu kuchuana kwenye tuzo

Riyama
Rose Ndauka

WAIGIZAJI wa kike nyota wa filamu nchini, Rose Ndauka, Wastara Juma, Elizabeth Michael 'Lulu' na Irene Paul ni kati ya waigizaji wanaowania Tuzo za Filamu za ACVC-2014.
Wasanii hao wanachuana kwenye kipengele cha Msanii Bora wa Kike wakiwa sambamba na waigizaji, Jacklyne Wolper, Irene Uwoya na Riyama Ally.
Kwa mujibu wa waratibu wa tuzo hizo, Ndauka kaingia kwenye kipengele hicho kupitia filamu ya Waiting Soul, Irene Paul (Love& Power), Irene Uwoya (Questions Mark), Lulu (Foolish Age), Wolper (Mahaba Niue), huku Wastara (Mr Mres Sajuki) na Riyama ( The Dream).
Kwa upande wa Msanii Bora wa Kiume tuzo hiyo inawaniwa na Jacob Stephen 'JB', Mohammed Mwikongi 'Frank', Simon Mwampagata 'Rado',Hemed Suleiman 'PHD', Steve Mengere 'Nyerere' na
Salim Ahmed 'Gabo'.
Upande wa vunja mbavu (Comedian) wapo King Majuto, Mboto, Dk Cheni, Kitale na Marehemu Sharo Milionea huku wachekeshaji wa kike tuzo hiyo inawaniwa na Salma Jabu 'Nisha'
Rehema Abdallah 'Bi Rehema' na Chuma Suleiman 'Bi Chau'.
Tuzo nyingine zinazowaniwa na  Wasanii Bora Chipukizi wa Kiume na Kike ambazo zitawaniwa na
Rammy Gallis, Mohammed Mussa, Gerry wa Rhymes, Lukeye Lukamo, Mteme Baga, Wellu Sengo, Janeth Lameck, Najma Dattan, Gertrude Mwita na Khadija Kopa.
Vincent Kigosi 'Ray', Issa Mussa 'Claud 112', John Lister, Jackson Kabirigi, Leah Richard 'Lamata' na Kulwa Kikumba 'Dude' wanawania tuzo ya Muongozaji Bora, huku Filamu Bora inawania na filamu za
Twisted ya RJ Production, Nguvu ya Imani-Timamu Effects, Shikamoo Mzee-Jerusalem Film Production, Tikisa-Nisha Production na Mr & Mrs Sajuki ya Wajey Film Production.
Tuzo nyingine zinazowaniwa ni ya Mhariri Bora wa Filamu, Muigizaji Msaidizi Bora wa Kike na Kiume, Filamu Bora ya Maadili, Filamu Bora ya Kuitangaza Tanzania, Wasambazaji Bora na zoezi la upigaji kura kwa washiriki hao litahusishwa 'code' za kila kipengele na kutumwa katika namba 15678.

No comments:

Post a Comment