STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 8, 2014

PSG yatetea taji Ufaransa licha ya kipigo nyubani

Wanafurahia ubingwa kinyonge
LICHA ya kipigo cha mabao 2-1 ilichopewa nyumbani kwake na Rennes, klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) imefanikiwa kutangazwa kuwa mabingwa tena nchini Ufaransa, baada ya wapinzani wao wa karibu Monaco kulazimishwa sare ya 1-1 na timu inayopigana kushuka daraja la Guingamp.
Kipigo hicho kimeifanya PSG kusaliwa na pointi zao 83 ambazo haziwezi kufikiwa na Monaco kwani kwa sare hiyo imewafanya wafikishe pointi 76 na kusaliwa na mechi mbili ambazo wakishinda zote watafikisha pointi 82 tu.
PSG imetetea taji hilo iliyokuwa ikilishikilia na ni ubingwa wake wa pili msimu huu baada ya hivi karibuni kunyakua Kombe la Ligi kwa kuicharaza Olympique Lyon kwa mabao Edinson Cavani waliposhinda mabao 2-1.
Wenyeji PSG walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Ezequiel Lavezzi katika dakika ya tatu akimalizia kazi nzuri ya Cavani, kabla ya wageni kucharuka na kurejesha bao hilo dakika ya 23 kupitia kwa Foued Kadir na  Paul Ntep kufunga la ushindi dakika nne baadaye.

No comments:

Post a Comment