STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 8, 2014

Jerry Santo ndiyo basi tena Coastal Union

NAHODHA wa zamani wa klabu ya Coastal Union. Mkenya  Jerry Santo amewaaga mashabiki wa timu hiyo kwa kuweka bayana kuwa, hatakuwa na kikosi hicho kwa msimu ujao.
Kiungo mkabaji huyo aliyewahi kung'ara Simba kabla ya kutua Coastal, aliiambia MICHARAZO kuwa, ameachana na klabu hiyo baada ya kumalizika kwa mkataba wake.
Santo alisema kwa sasa amerejea nchini kwao Kenya akifanya mipango ya kujiunga na klabu nyingine kwa msimu ujao iwe ndani au nje ya nchi yao.
Mkenya huyo, aliyekuwa mmoja wa wafungaji wa mabao ya Coastal katika misimu miwili ya timu hiyo kwenye Ligi Kuu, alisema ni mapema mno kusema kama atarejea Tanzania.
"Sintakuwa na Coastal kwa msimu ujao, naendelea kutafuta timu ya kuichezea iwe hapa Kenya au nje ya nchi, sidhani kama nitarejea Tanzania, ngoja tuone," alisema.
Nyota huyo aliyekuwa akiichezea Tusker ya Kenya kabla ya kuja nchini kuichezea Simba, alipoteza cheo chake cha unahodha katika duru la pili kwa beki Juma Said 'Nyosso.
Badiliko hilo lilifanywa na kocha Mkenya, Yusuph Chipo aliyeichukua timu hiyo mikononi mwa Hemed Morocco.

No comments:

Post a Comment