STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 8, 2014

Brazili yaanika kikosi chake, Kaka, Robinho, Coutinho watemwa

KOCHA wa timu ya taifa ya Brazil, Luis Felipe Scolari amebainisha kuwa ilikuwa kazi rahisi kuchagua kikosi chake kwa ajili ya Kombe la Dunia baada ya kutangaza majina ya wachezaji 23.
Kocha huyo amewatema mastaa kibao wa taifa hilo katika kikosi alichotangaza baadhi yao wakiwa ni Kaka, Robinho na Lucas Moura.
Pia nyota wa Atletico Madrid Filipe Luis na Miranda pia hawapo, sambamba na mchezaji wa Bayern Munich Rafinha na kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho. 
Scolari ambaye aliiongoza Brazil kushinda Kombe la Dunia mwaka 2002 amesema ilikuwa vigumu kufanya kazi kama hiyo miaka 12 iliyopita kuliko ilivyo sasa, na kudai kuwa kutakuwa na baadhi ya wachezaji hawatafurahishwa kwa majina yao kukatwa. 
Kocha huyo amesema ilikuwa kazi ngumu mwaka 2002 kutangaza kikosi kwasababu kulikuwa na kelele nyingi sana mpaka ikabidi abadilishe hoteli ambayo hakuna mtu aliyekuwa akifahamu lakini safari haikuwa hivyo. 
Brazil inatarajia kuanza kampeni zake kwa kucheza mchezo wa fungua dimba dhidi ya Croatia Juni 12 mwaka huu kabla ya kuzivaa Mexico na Cameroon zilizopo katika kundi A.

Kikosi kamili cha Brazil ni hiki hapa:

Makipa: Jefferson (Botafogo), Julio Cesar (Toronto FC), Victor (Atletico MG).

Mabeki: Dante (Bayern Munich) David Luiz (Chelsea), Henrique (Napoli), Thiago Silva (PSG) Dani Alves (Barcelona), Maicon (Roma) Marcelo (Real Madrid), Maxwell (PSG).

Viungo: Fernandinho (Manchester City) Hernanes (Inter) Luiz Gustavo (Wolfsburg) Oscar (Chelsea) Paulinho (Tottenham Hotspur), Ramires (Chelsea), Willian (Chelsea).

Washambuliaji: Bernard (Shakhtar Donetsk), Fred (Fluminense) Hulk (Zenit) Jo (Atletico MG), Neymar (Barcelona).

No comments:

Post a Comment