STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 14, 2013

Arsenal yang'oka Ulaya, Malaga yaisulubu Porto

Mfungaji wa bao la pili la Arsenal, Laurent Koscielny (kulia) akiwa haamini kama wametoka michuano ya UIaya
 LICHA ya kupata ushindi uliotarajiwa wa mabao 2-0 ugenini nchini Ujerumani, Arsenal ya Uingereza imejikuta ikishindwa kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana.
Arsenal ilikuwa nchini humo kukabiliana na wenyeji wao Bayern Munich ikiwa nyuma ya mabao 3-1 iliyonyukwa katika pambano lao la awali lililochezwa mjini Londoni mwishoni mwa mwezi uliopita.
Ushindi huo uliotokana na mabao ya Olivier Giroud aliyefunga dakika ya tatu tu ya kuanza kwa mchezo huo na lile la kipindi cha pili lililotumbukizwa wavuni na Laurent Kocsielny, ulifanya matokeo ya mwisho kuwa sare ya mabao 3-3, lakini vijana hao wa Arsene Wenger kung'oka kwa faida ya bao ya ugenini.
Tofauti na mechi yao ya London, Arsenal jana walionyesha uhai na kuwafunika wenyeji wao na kuwashutukiza kwa bao hilo la mapema la Giroud lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Arsenal ilisubiri hadi dakika nne kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kuongeza bao la pili kupitia kwa Laurent Koscielny aliyefunga kwa kichwa ambalo hata hivyo halikusaidia kusonga mbele ili kukaribia ndoto zao za kumaliza ukame wa mataji klabuni hapo.
Michuano hiyo ndiyo iliyokuwa tumaini pekee la Arsenal kumaliza ukame huo wa mataji kwani ilishatolewa kwenye michuano ya Kombe la Ligi, Kombe la FA na ndoto za kutwaa ubingwa wa Ligi ya England ni finyu kutokana na ukweli imeachwa mbali kipointi na vinara wa ligi hiyo, Manchester United.
Katiika mechi nyingine ya usiku wa jana katika michuano hiyo ya Ulaya, Malaga ya Hispania ikiwa nyumbani ililipa kisasi cha kunyukwa na Porto ya Ureno bao 1-0 kwa kuilaza wageni wao hao mabao 2-0 na kutinga robo fainali.
Malaga ilipata mabao yake kila kipindi kupitia kwa nyota wake, Isco aliyefunga la kwanza dakika ya 43 na Roque Santa Cruz kuonyesha la pili katika dakika ya 77 na kuifanya timu hiyo sasa kuungana na timu za Barcelona na Real Madrid kutoka Hispania, Borussia Dotmund na Bayern Munich za Ujerumani, PSG ya Ufaransa na Galatasaray ya Uturuki kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo.

Wednesday, March 13, 2013

Silaha 23 za Kim Poulsen kwa Morocco hizi hapa

Kipa wa Mtibwa Husseni Sharrif 'Casillas' akiwajibika uwanjani




Na Boniface Wambura

KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja wachezaji 23 watakaoingia kambini Jumamosi  jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi ya mashindano dhidi ya Morocco, akimjumuisha kipa wa Mtibwa Hussei Sharrif 'Casillas'.

Mechi hiyo ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil itachezwa Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kocha Kim, wachezaji wa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager wanatakiwa kuripoti kambini katika hoteli ya Tansoma, Machi 17 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni makipa Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha wa Stars, Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba) na Shomari Kapombe (Simba).

Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Mbali ya Kim, benchi la ufundi la Taifa Stars linaundwa na Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi), Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).

SEMINA ELEKEZI COPA COCA COLA KUFANYIKA MACHI 19


Na Boniface Wambura

SEMINA elekezi kwa ajili ya michuano ya Copa Coca-Cola 2013 itafanyika Machi 19 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Washiriki wa semina hiyo wanatakiwa kuripoti Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) siku moja kabla (Machi 18 mwaka huu).

Washiriki hao ni makatibu wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar. Pia waratibu wa mikoa wa mashindano ya Umoja wa Michezo wa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA).

Barua za mwaliko kwa ajili ya semina hiyo tayari zimetumwa kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa.

FIFA yaionya Tanzania kuingiza siasa TFF

Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Velcke
BERNE, (Reuters)
TANZANIA has been warned by soccer's governing body FIFA over alleged government interference in the country's football federation.

"We can confirm that FIFA secretary general Jerome Valcke has sent a letter to the president of the Tanzanian Football Federation, Leodegar Tenga, concerning alleged governmental interference in the internal affairs of the TFF," said FIFA in a statement sent to Reuters.

"FIFA is in contact with the TFF president who is optimistic that the matter can be sorted out between TFF, FIFA and the Tanzanian authorities.

"Furthermore, we can confirm that FIFA is also planning to send a mission to assess the situation with regard to the electoral process as soon as the current matter of alleged interference has been clarified."

Tanzanian media said that the government has declared the TFF's new statutes illegal and told it to use the old ones for upcoming elections.

FIFA statutes state that its member associations must remain independent of their respective national governments and routinely suspends those who break the rules.

Suspension for Tanzania would mean that they would be excluded from the World Cup qualifiers and their clubs would be kicked out of African competitions.

Tanzania, who have never qualified for the World Cup, are second in African qualifying Group C with three points from two games, one behind leaders Ivory Coast.

BARCELONA YAFANYA MAANGAMIZI ULAYA

 

'Mchawi Mweupe' Lionel Messi akishangilia moja ya mabao yake mawili usiku wa jana.

NI Maangamizi! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya vinara wa Ligi Kuu ya Hispania, Barcelona usiku wa kuamkia leo kuifumua bila huruma AC Milan ya Italia na kutinga robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya bila kutarajiwa.
Mabao mawili ya 'Mchawi Mweupe' Lionel Messi na mengi ya David Villa na Jordi Alba, imeifanya Barca kutinga hatua hiyo kwa kuitupa nje AC Milan kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya mechi ya awali kuchezea kipigo cha mabao 2-0 ugenini.
Messi aliendelea kuimarisha rekodi yake ya mabao katika michuano ya msimu huu kwa kufunga bao la kwanza dakika ya tano akimalizia kazi nzuri ya Xavi, kabla ya kuiongeza jingine dakika tano kabla ya mapumziko kwa shuti kali kwa pasi murua ya Iniesta na kuifanya Barca iende mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili, AC Milan wakiingia wakitafuta mbinu za kuweza kudhibiti mashambulizi ya wenyeji wao, lakini wakajikuta wakitungulia bao la tatu kupitia kwa Villa aliyemegewa pande tamu na Xavi na kufunga dakika ya 55.
Bao lililoikata maini AC Milan ambayo kupitia nyota wake Robinho, Kevin Prince Boateng, Sule Muntari walijaribu kufurukuta bila mafanikio, lilitumbukizwa kimiani na Alba dakika za nyongeza pambano hilo na kuifanya Barca kuweka historia kwa timu iliyonyukwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza kusonga mbele katika michuano hiyo ya Ulaya.
Katika mechi nyingine ya michuano hiyo iliyochezwa usiku wa jana, wenyeji Schalke 04 walijikuta wakinyukwa nyumbani na wageni wao Galatasaray kwa mabao 3-2 na kung'oka kwenye michuano hiyo.

Kikosi cha Galatasaray kilichokuwa na Didier Drogba kilishtukizwa kwa kufungwa bao la dakika ya 18 kupitia Roman Neustadter kabla ya Hamit Altintop kusawazisha katika dakika ya 37 na Burak Yilmaz kuiongezea wageni bao la pili katika dakika ya 42.
Michael Bastos aliipatia Schalke bao la kusawazisha katika kipindi cha pili kwenye dakika ya 63 na wengi kuamini mechi hiyo ingeisha kwa sare hivyo ambapo jumla ya matokeo yalikuwa yakisomeka 3-3 kutokana na sare ya baoa 1-1 waliyopata timu hizo katika mechi ya ya kwanza, Galatasaray walipata bao la tatu.
Bao hilo lililwekwa kiminia kwenye dakika za nyongeza za pambano hilo kupitia kwa Umut Bulut na kuivusha timu yake hadi robo fainali ya michuano hiyo mkubwa kwa ngazi za klabu barani Ulaya.

Tuesday, March 12, 2013

Kim Poulsen kuanika silaha za kuivaa Morocco

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen
Na Boniface Wambura
KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Kim Poulsen kesho anatarajia kuanika kikosi cha timu yake kitakachovaana na Morroco katika pambano la kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2014.
Kim atazungumza na wanahabari kesho majira ya saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na Morocco kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Machi 24 mwaka huu katika mechi ya kundi C ikiwa sambamba na Ivory Coast na Gambia.
Mpaka sasa Stars inashika nafasi ya pili katika msimamo wa kundi lake ikiwa na pointi 3 moja nyuma ya ilizonazo Ivory Coast wanaoongoza msimamo na ambao wikiendi hii nao watashuka dimbani kucheza na Gambia.
Stars inahitaji ushindi katika mechi hiyo ili kuweka hai matumaini yta kufuzu fainali hizo za Kombe la Dunia ambazo zitafanyika mwakani nchini Brazili.
Msimamo wa kundi walilo Stars ni kama ifuatavyo:

                                   P  W  D  L   F  A  GD PTS
1. Ivory Coast             2   1   1   0   4   2    2   4
2. Tanzania                  2   1   0   1   2   3   -1   3
3. Morocco                 2   0   2   0   3   3    0   2
4. Gambia                    2   0   1   1   2   3  -1   1

Pambano la Simba, Coastal laingiza Mil 37



Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya mabingwa watetezi, Simba dhidi ya Coastal Union iliyochezwa juzi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 36,820,000 kutoka na watazamaji 6,284.

Viingilio katika mechi hiyo namba 138 iliyomalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 8,265,752.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 5,616,610.17.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 4,202,924.97, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 2,521,754.98, Kamati ya Ligi sh. 2,521,754.98, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,260,877.49 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 980,682.49.

Uchaguzi TAFCA kufanyika Morogoro



Na Boniface Wambura

UCHAGUZI Mkuu wa viongozi wa Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) utafanyika Jumamosi (Machi 16 mwaka huu) mjini Dodoma ambapo wajumbe wanatakiwa kuripoti siku moja kabla ya uchaguzi.

Wagombea waliopitishwa kuwania uongozi na Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA chini ya uenyekiti wa Ramadhan Mambosasa ni Oscar Don Koroso (Mwenyekiti), Lister Manyara (Makamu Mwenyekiti) na Katibu (Michael Bundala).

Wengine ni Gabriel Gunda (Katibu Msaidizi), Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania- TFF (Wilfred Kidao) wakati wagombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni Jemedali Saidi, George Komba na Magoma Rugora.

Kivumbi cha Ligi Kuu kuendelea J'mosi, Yanga kunusa ubingwa?



Wachezaji wa Yanga wakifurahia moja ya mabao yao ya Ligi kuu

Na Boniface Wambura

KIVUMBI cha Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) kinatarajiwa kuendelea tena Jumamosi kwa mechi tatu kupigwa viwanja vya mikoa mitatu tofauti ya Mwanza, Dar es Salaam na Morogoro.
Timu inayopigana kuepuka kushuka daraja, Toto Africans itakuwa dimba la nyumbani la CCM Kirumba jijini Mwanza kuvaana na Mgambo JKT katika moja ya pambano linalosubiriwa kwa hamu wikiendi hii.
Toto walio nafasi ya pili kutoka mkiani wakiwa na pointi 15 na ikiuguza kipigo cha 'kaka' zao Yanga itakuwa na kiu ya kupata ushindi ili kuweza kujinasua mkiani na kujiweka katika nafasi za kuepuka kushuka daraja.
Pambano jingine la mwishoni mwa wiki ni kati ya vinara wa ligi hiyo, Yanga watakaokuwa dimba la Taifa jijini Dar es Salaam kuwakaribisha maafande wa Ruvu Shooting, mechi ambayo itatoa taswira ya mbio za ubingwa kwa Yanga ambao msimu huu wameonekana wapo tofauti wakiwa na kiu ya kutwaa taji.
Mpaka sasa Yanga inaoongoza msimamo wa Ligi ikiwa na pointi 45 kutokana na mechi 19 ilizocheza ikifuatiwa na Azam waliopo nafasi ya pili na pointi zao 37 kisha Simba wanaokamata nafasi ya tatu wakiwa na pointi 34 wote pia wakiwa wamecheza mechi 19 kila mmoja.
Mtanange mwingine wa Jumamosi utazikutanisha timu zinazolingana pointi na kutofautiana uwiano wa mabo ya kufunga na kufungwa, Coastal Union ya Tanga watakaokuwa wageni wa Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Manungu, Morogoro.
Mshindi yoyote wa mechi hiyo wataweza kufikisha pointi 34 na hivyo kuwakamata mabingwa watetezi ambao wenyewe watashuka dimbani siku ya Jumapili.

DRFA yaunda kamati mbalimbali wakongwe waula


 
KAMATI ya Utendaji ya Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam kwa mamlaka iliyonayo imeteua kamati mbali mbali zitakazoshirikiana na Kamati ya Utendaji katika kukabiliana na changamoto mbali mbali za mpira wa miguu katika Mkoa wake ili kuweza kufikia malengo yake waliyojiwekea. Wafuatao ni watu na kamati mbali mbali walioteuliwa/zilizoteuliwa na Kamati ya Utendaji ya Chama Cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam:
 
Bw. Joseph Kanakamfumo                     Mkurugenzi wa Ufundi
Bw. Saidi Pambalelo                              Afisa Tawala
Bw. Mohamedi Muharizo                       Afisa Habari
Bw. Hashim Abdallah                             Afisa Usalama
 
KAMATI YA FEDHA NA MIPANGO
1.       Bw. Meba Ramadhani               Mwenyekiti
2.       Bw. Iddi Msonga                       Makamu Mwenyekiti
3.       Bw. Ali Hassani                                                  
4.       Bw. Ramadhani Kilemile
5.       Bw. Isack Mazwile
 
KAMATI YA UFUNDI NA MASHINDANO
1.       Bw. Kenny Mwaisabula              Mwenyekiti
2.       Bw. Shabani Mohamedi              Makamu Mwenyekiti
3.       Bw. Hugo Seseme
4.       Bw. Daudi Kanuti
5.       Bw. Kassim Mustapha
6.       Bw. Abeid Mziba
7.       Bw. Bakari Mtumwa
 
KAMATI YA MAENDELEO YA SOKA LA VIJANA NA WANAWAKE
1.       Bw. Benny Kisaka                     Mwenyekiti
2.       Bw. Muhsin Balhabou                Makamu Mwenyekiti
3.       Dr. Sesy Makafu
4.       Bw. Emmanuel Kazimoto
5.       Dr.  Maneno Tamba
6.       Bw. Edwin Mloka
7.       Bw. Sande Mwanahewa
8.       Bw. Richard Shayo
 
KAMATI YA WAAMUZI
1.       Bw. Jovin Ndimbo                     Mwenyekiti
2.       Bw. Sijali Mzeru                        Makamu Mwenyekiti
3.       Bw. Saidi Mbwana
4.       Bw. Benny Mtula
5.       Bw. Abdallah Mitole
 
KAMATI YA NIDHAMU NA USULUHISHI
1.       Mheshimiwa Roman Masumbuko            Mwenyekiti
2.       Bw. Fahadi Faraji Kayuga                       Makamu Mwenyekiti
3.       Bw. Mohamedi Mpili
4.       Bw. Peter Nkwera
5.       Bw. Jimmy Mhango
 
KAMATI YA RUFAA
1.       Mheshimiwa Salehe Njaa                       Mwenyekiti
2.       Bw. Saidi Engo                                      Makamu Mwenyekiti
3.       Bw. Abasi Kuka
4.       Bw. Yusuph Macho
5.       Bw. Boi Risasi
 
Pia Kamati ya Utendaji ya Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam inapenda kuwafahamisha wanachama wake, wadau na mashabiki wa mpira wa miguu Tanzania dhamira yao ya kuendeleza mpira wa miguu katika Mkoa wa Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.
 
Kwa kuanzia Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam kipo kwenye mchakato wa kukamilisha DRFA Strategic Plan 2013 - 2016 (Mpango Mkakati Kazi) kwa kipindi cha miaka minne pamoja na kuboresha Financial Regulations zake ili kiweze kuwa na dira ya kuwahudumia wadau wake kwa ufanisi na uwazi zaidi. Lakini pia Kamati ya Utendaji imeona haja ya Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam kuwa na Website yake kwa ajili ya kuwapa habari wadau wake na Watanzania kwa ujumla.
 
Mwisho Kamati ya Utendaji ya Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam kinaomba ushirikiano na wadau wote wa mpira hususani Serikali, TFF, Vyama vya Mikoa, Walimu, Waamuzi, Madaktari, Vilabu, Makampuni na Waandishi wa habari na Vyombo vya habari katika kuendeleza mpira wa miguu katika mkoa wa Dar es Salaam na hatimaye mikoa yote ya Tanzania. “Kwani Pamoja Tunaweza”
 
Ahsanteni,
 
Almasi Kasongo
Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)

Arteta aitaka bodi Arsena ivunje benki kujiimarisha

Kiungo wa Arsenal, Mikel Arteta


KIUNGO nyota wa Arsenal, Mikel Arteta anaamini kwamba umefika wakati wa Arsenal kuwekeza vya kutosha kuimarisha timu iwapo inahitaji kurejesha heshima yake katika soka la Ulaya.
Mchezaji huyo ametoa maoni yake hayo baada ya kuishuhudia timu yake iking'olewa kwenye michuano ya nyumbani na timu za Bradford City na Blackburn Rovers, huku ikiwa imepoteza mechi ya mkondo wa kwanza wa 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mabao 3-1 dhidi ya Bayern Munich.
Arsenal kwa miaka nane sasa haijawahi kutwaa taji lolote, hali inayompa hofu mchezaji huyo hasa akiangalia pengo lililopo baina yao na wanaoongoza Ligi Kuu ya Engalnd, Mancester United.
Arteta alisema kuwa pamoja na misingi mzuri ya kukuza vipaji vya wachezaji ndani ya Arsenal na falsafa iliyopo na wachezaji iliyonayo, lazima klabu ifanye manunuzi wa wachezaji wakali zaidi iwapo inapata mafanikio zaidi.
Alisema kusalia kwao kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya kunahitaji miujiza, sawa na kukata tamaa ya kutwaa ubingwa wa Ligi ya England.
Hata hivyo alisema ni vema Arsenal ikaanza kujipanga kwa msimu ujao kwa kununua nyota watakaoweza kuijenga upya timu hiyo kuweza kukata kiu ya misimu karibu nane bila taji lolote.
"Tunatakwa kuwa bora na msimu ujao tuhahitaji kupata pointi nyingi zaidi kwa maana ya kutaka kushinda kila mchezo. Nadhani bodi inajua hili na tumaini letu msimu ujao watafanya kila jambo ili kufikia malengo hayo," alinukuliwa kiungo.
Kiungo alieleza pia sababu yake yua kuihama Everton na kutua Arsenal lengo likiwa ni kucheza Ligi ya Mabingwa na kwake ilikuwa na maana kubwa.
Juu ya pambano lao la kesho la Ligi ya Mabingwa Ulaya, Arteta alikiri ni kazi kutokana ukweli wapinzani wao Bayern Munich kuwa wazuri msimu huu na walionyesha hivyo hata katika mechi ya mkondo wa kwanza walipoibuka na ushindi wa mabao 3-1.

Mwandi yahimiza wachezaji kuchangamkia African Youth

Moja ya timu za vijana ya Yosso United ya Arusha
WACHEZAJI wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara na Zanzibar wenye umri kati ya miaka 18 na 21 wametakiwa kuchangamkia fursa ya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa Barani Ulaya, Asia na Afrika wakiwa nyumbani Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Mwandi, Teonas Aswile, waandaaji wa Michuano ya African Youth Football Tournament amesema kuwa katika michuano hiyo wachezaji 11 bora watatafutiwa timu moja kwa moja katika mataifa nane barani Ulaya (Ufaransa, Ureno, Uholanzi, Denmark, Norway, Sweden, Ubelgiji na Switzerland), Asia na Afrika.

Bwana Teonas Aswile amesema kuwa wachezaji wa Tanzania bado hawajaonesha muamko mkubwa licha ya kiwango cha chini cha kushiriki ambacho wamewekewa ikilinganishwa na wachezaji wa kigeni, ambao licha ya kuwekewa USD 500 bado wamezidi kumiminika.

“Mpaka sasa kuna mawakala wawili ambao tumezungumza nao na wamethibitisha kuleta wachezaji wao zaidi ya 20 kushiriki kwenye michuano.”

“Hii ni mbali ya wachezaji mmoja mmoja ambao tunaowasiliana nao ambao wanataka kuja, wakiwa zaidi ya watano. Kwahiyo wachezaji wetu waamke na kuitumia fursa hii ambayo haipo katika nchi nyingine ya Afrika kwa wachezaji kufanya majaribio nchini mwao.”

Aidha Aswile ameviomba vilabu mbalimbali ambavyo vinaweza kuwalipia wachezaji wake ada ya shilingi laki tatu (Tsh 300, 000) ambayo inahitajika kwa mchezaji ili aweze kushiriki kwenye michuano ya African Youth Football Tournament kufanya hivyo kwani mchezaji huyo atakapouzwa klabu husika ndiyo itakayokubaliana na klabu itakayomchukua na si Kampuni ya Tanzania Mwandi.

“Sisi tunachokifanya ni kumuwezesha mchezaji aone njia za kufikia malengo yake. Kwa hiyo akishafanikiwa na amepata timu ya kuchezea iwe Ulaya, Asia au Afrika, klabu yake ndio itakayokubaliana na timu ya huko sisi hatutachukua chochote”, Teonas alisema.

Mkurugenzi huyo akitaja idadi ya wachezaji wa Tanzania ambao tayari wamethibitisha kushiriki amesema kuwa ni wachezaji watatu jambo ambalo bado linaonyesha mwamko umekuwa mdogo.

Michuano ya African Youth Football Tournament itafanyika Tanzania katika uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 10 hadi 14 mwezi wa sita mwaka huu na kuwashirikisha wachezaji wenye umri wa miaka 18 hadi 21 ambapo watafundishwa na makocha watatu kutoka nje ya nchi na wawili wa Tanzania.

Pia michuano hiyo itashirikisha mawakala kutoka nchi nane za barani Ulaya, Asia na Afrika ambao wanahitaji wachezaji kwaajili ya klabu wanazoziwakilisha kati yao wakiwa ni Budak Johan, Cabrera Oliver, Dag Larsson, Phillip Mwakikosa na Dahlin Martin huku wakala wa kimataifa wa Tanzania Dr Damas Ndumbaro akiwa miongoni mwa mawakala wa Tanzania watakaoshiriki katika michuano kusaka vipaji kwaajili ya klabu mbalimbali.

“Tuna maombi ya mawakala wawili ambao wanataka wachezaji mabeki, washambuliaji na viungo kwaajili ya klabu zao Kuwait, Qatar, Libya na sehemu nyingine kwa hiyo hii ndio fursa ya wachezaji wetu kwenda kucheza soka la kulipwa na lenye maslahi zaidi kwao.”

Yanga yaipigia hesabu Ruvu Shooting

 
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga inaendelea kujifua kwa mazoezi makali kwa ajili ya pambano lake lijalo dhidi ya maafande wa Ruvu Shooting litakalochezwa Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar.
Yanga inayoongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 45 na mabao 36 ya kufunga na mabao 12 ya kufunga, inahitaji ushindi katika mechi hiyo ijayo ili kuzidi kujiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa amnbao unashikiliwa kwa sasa na Siumba iliyopo nafasi ya tatu ikiwa  na pointi 34, tatu nyuma ya Azam.
Baada ya kupata ushindi wa nne mfululizo kwa kuilaza Toto Africans, vijana hao wa Ernest Brandts wapo katika mazoezi makali katika uwanja wa Mabatini Kijitonyama ikiwa maandilizi ya mechi hiyo ya Jumamosi.
Katika mazoezi ya jana kikosi hicho kiliwakosa nyota wake Kelvin Yondani na Said Bahanuzi ambao ni majeruhi.
Yondani anasumbulia na maumivu ya dole gumba aliloumia kwenye mchezo dhidi ya Toto Africans na Bahanuzi alishtua msuli wa kisigino na kwa mujibu wa daktari wa timu Dk Nassoro Matuzya wachezaji hao wanaendelea vizuri na huenda leo wakajumuika na wenzao kuendelea na mazoezi.
Pia Dk Matuzya alisema mchezaji Ladislaus Mbogo anatazamiwa kufanyiwa upasuaji wa uvimbe (shavuni) leo.
Mbogo atafanyiwa upasuaji huyo baada ya klabu ya Yanga kuridhia kufuatia  uchunguzi uliofanywa na madaktari juu ya uvimbe huo na kwa maana hiyo mchezaji huyo atakosa mechi kadhaa za timu yake.

Golden Bush Fc yazidi kugawa dozi Ligi ya TFF-Kinondoni



LICHA ya kushiriki michuano ya Ligi kwa mara ya kwanza, timu ya soka ya Golden Bush Fc ya Sinza imeendelea kugawa 'dozi' wa wapinzani wao, baada ya juzi kuifumua Makumbusho Talents kwa mabao 3-1 katika mfululizo wa Ligi Daraja la Nne Wilaya ya Kinondoni.
Vijana hao wanaonolewa na nyota wa zamani wa timu za Kagera Sugar na Moro United, Shija Katina huyo ni ushindi wao wa pili mfululizo kwani katika mechi yao ya fungua dimba la michuano hiyo, iliifanyia 'mauaji ya sharubella' timu ya Victoria ya Kijitonyama kwa kuinyuka mabao 6-1.
Ushindi huo umewapa faraja viongozi wa timu hiyo wakiamini ni mwanzo mwema wa ndoto zao za kuwa kufika mbali katika soka la Tanzania wakitamani kufuata nyayo za Azam Fc inayotamba Ligi Kuu Tanzania Bara ikiqwa timu inayomilikiwa na mtu binafsi kuzitetemesha Simba na Yanga na kung'ara kimataifa.

Monday, March 11, 2013

Simba yakana kuwasimamisha wachezaji wake




Na Ezekiel Kamwaga 
JANA na leo, zimetolewa habari tofauti kuhusiana na klabu ya Simba ambazo uongozi umeona ni vema uzitolee ufafanuzi kwa lengo la kuweka rekodi sawa. Ufuatao ndiyo ufafanuzi wa taarifa hizo.

1. SIMBA KUZUIWA HOTELINI
SAA mbili kabla ya mechi ya jana baina ya Simba na Coastal Union ya Tanga, mmiliki wa Saphire Court Hotel alitoa taarifa kwa uongozi wa Simba kwamba ataizuia timu isiondoke hotelini kwa vile anaidai Sh milioni 25 na anataka alipwe zote jana.

Ikumbukwe kwamba Simba imekuwa ikikaa hotelini hapo kwa muda mrefu sasa wakati inapoweka kambi. Pia, wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba walifanya mkutano na wachezaji wote wa Simba katika hoteli hiyo usiku wa kuamkia jana.
Wamiliki wa hoteli hiyo hawakutoa taarifa yoyote kwa uongozi wakati huo juu ya dhamira yao hiyo.Wamiliki hao hawakutoa taarifa asubuhi ya mechi na walisubiri mpaka wakati timu inataka kuondoka ndiyo wakachukua hatua hiyo.
Kwa uongozi wa Simba, hatua hiyo ilikuwa ya ghafla mno. Ifahamike kwamba kabla ya hatua hiyo, uongozi wa Simba ulikuwa umemlipa mmiliki huyo kiasi cha zaidi ya Sh milioni 30 katika kipindi cha miezi 10 iliyopita.
Mara baada ya mechi dhidi ya Libolo ya Angola, Saphire walilipwa Sh milioni 15 na Simba. Hii maana yake ni kwamba klabu yetu ina utaratibu wa kulipa madeni yake na si watu wasiolipa kama hatua hiyo ya wamiliki wa Saphire inavyotaka kueleza.
Uongozi wa Simba tayari ulitoa ahadi ya kumaliza deni lote inalodaiwa baada ya kulipwa fedha zake inazodai zinazotakiwa kulipwa wakati wowote mwezi huu au ujao.
Simba inadai zaidi ya Sh milioni 500 kwa wadai wake wawili (Etoile du Sahel ya Tunisia na Push Mobile) na inataraji kulipwa fedha hizo. Itakapolipwa fedha zake hizo, Simba itakuwa na uwezo wa kulipa madeni yake yote inayodaiwa na watu binafsi na makampuni bado ikabaki na fedha za kufanya mambo mengine ya kimaendeleo.
Wakati ikisubiri ilipwe fedha zake inazodai, Simba itaendelea kulipa madeni yake taratibu kwa kadri itakavyoweza. Ifahamike kwamba kwa sasa chanzo kikuu cha mapato ya klabu ni fedha za mapato ya milangoni na za udhamini wa bia ya KILIMANJARO ambazo hazikidhi mahitaji yote ya timu.
Kwa kuzingatia nakisi hii ya mapato na matumizi, Simba SC imeanza mchakato wa kutafuta wafadhili na wadhamini kokote walipo duniani ili kuongeza mapato yake.
Tayari mawasiliano yameanza na wenzetu wa Sunderland ya England kupitia mradi wao wa Invest in Africa ili Simba nayo ifaidike. Simba SC inaomba pia umma ufahamishwe kwamba klabu ya soka kudaiwa si dhambi.
Iwapo klabu kubwa na tajiri duniani kama vile Manchenster United, Real Madrid na Liverpool zina madeni, inakuaje madeni ya Wekundu wa Msimbazi (tena ambayo klabu ingeweza kuyalipa yote iwapo wadeni wake nayo wangewalipa kwa wakati) yaonekane kama kitu kigeni?
Uongozi unaahidi kwamba utalipa madeni yake yote kwa kadri utakavyojaaliwa. Kwenye lugha ya kibenki, credit worthiness ya mteja inamaanisha mteja ambaye anakopa na kulipa. Simba inapenda kusisitiza kwamba ni taasisi ya kuaminika na yenye heshima kubwa na bado inavutia watu na taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi. Simba ni CREDIT WORTHY INSTITUTION !
Hata hivyo, uongozi wa Simba unafikiria kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wamiliki wa Saphire Court Hotel kwa kitendo chake cha kuwazuia wachezaji na viongozi wa Simba hotelini kabla ya mechi ya jana. Simba inachukulia kitendo kile kama hujuma na kisheria kinaangukia katika kundi la FORCED IMPRISONMENT kwa wamiliki kuwazuia watu kinguvu hotelini kwao.
Wamiliki hawakutoa notisi kwa uongozi au taarifa yoyote ya mdomo au maandishi kabla ya kuchukua hatua hiyo. Lengo lilikuwa ni kuchafua heshima na hadhi ya Simba kwa hoteli ambayo imetoka kulipwa Sh. milioni 15 wiki mbili tu zilizopita.
Uongozi wa Simba SC unaapa kuilinda na kuitetea hadhi ya klabu yetu kwa nguvu zetu zote, akili zetu zote na maarifa yetu yote.

2. WACHEZAJI, BENCHI LA UFUNDI KUFUKUZWA

KUNA taarifa zimeenezwa pia kwamba kuna wachezaji wa Simba wamesimamishwa au kufukuzwa kuchezea Simba.
Habari hizi nazo hazina ukweli wowote Ukweli ni kwamba, uongozi wa Simba umetoa ruksa kwa benchi la ufundi kupanga timu ambayo litaona inafaa kwa mechi husika.
Uongozi hautaingilia, kwa namna,njia au aina yoyote ile utendaji wa benchi la ufundi. Hakuna mchezaji yeyote aliyesimamishwa hadi sasa.
Pia uongozi unakanusha taarifa kuwa Daktari Mkuu wa Klabu, Cosmas Alex Kapinga, kuwa naye ameachia ngazi. Habari hizi hazina ukweli kwani daktari huyo ana ruhusa ya kikazi ya wiki mbili inayojulikana.

HITIMISHO
Katika namna ya kipekee kabisa, uongozi wa Simba unapenda kutoa shukrani za dhati kabisa kwa washabiki wake waliojitokeza Uwanja wa Taifa na kuisapoti timu kwa asilimia 100.
Uongozi unathamini sana mchango wa wanachama wake na unaahidi kufanya kila unachoweza kuwarejeshea tena furaha mioyoni mwao.
Pia unatumia nafasi hii kuwapongeza wachezaji na benchi la ufundi ambao walicheza mechi ya jana katika mazingira magumu. Walicheza bila ya kufanya warm up na wakitoka kuwa wamezuiwa hotelini jambo ambalo lingeweza kuwaondoa mchezoni.

WAMILIKI WA TELEVISHENI WATISHIA KUSIMAMISHA MATANGAZO KISA VING'AMUZI

   Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi

WAMILIKI wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT) wameitaka serikali kuacha mara moja utaratibu wake wa sasa wa kulazimisha matangazo yote ya televisheni nchini kurushwa kwa digitali kupitia ving'amuzi na badala yake irejeshe utaratibu wa zamani kwani hivi sasa wao wamekuwa wakipata hasara kubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo, mwenyekiti wa MOAT, Dk. Reginald Mengi, ambaye aliambatana na wakurugenzi wa Sahara Communications (Star TV) na wa Clouds Media, alisema kuwa utaratibu wa sasa unaowalazimisha wananchi wote kupata matangazo ya televisheni kupitia ving'amuzi umekuwa ukiwakosha wengi matangazo hayo na matokeo yake, wao huathirika kwa kukosa pesa za kuendeshea shughuli zao kupitia matangazo ya kibiashara kama ilivyokuwa zamani.

Wamiliki hao wameitaka serikali kutoa uhuru kwa wananchi wote kupata matangazo kwa njia wanazotaka wenyewe za digitali na analojia (antena za kawaida) kulingana na utashi wao na pia uwezo wao kiuchumi badala ya ilivyo sasa ambapo wengi wamekuwa wakikosa uwezo wa kununua ving'amuzi na kuvilipia kila mwezi, hivyo kukosa matangazo yao na mwishowe kuwaingizia hasara wamiliki wa vituo vya televisheni.

Mengi ameongeza kuwa hadi sasa bado wanaendelea kufanya taratibu za kuisihi serikalini itekeleze yale wanayoomba na kwamba, wataendelea kufanya subira kwa miezi kati ya miwili hadi mitatu kuanzia sasa na wakiona kuwa bado serikali iko kimya, watakachokifanya ni kufunga vituo vyao vyote vya televisheni kwani ni bora waendelee na biashara nyingine kuliko ilivyo sasa ambapo kila uchao wamekuwa wakipata hasara.

Serikali ililazimisha kuanza urushaji wa matangazo kupitia ving'amuzi kuanzia Januari Mosi, 2013 na kuzima kwa awamu matangazo yote ya televisheni kupitia njia iliyokuwa ikitumika awali ya analojia isiyohitaji ving'amuzi bali antena za kawaida.

TFF YAMLILIA ATHUMANI KILAMBO

Athuman Kilambo (wa kwanza kushoto waliosmama) enzi za uhai wake akiwa na kikosi cha Pan African miaka ya 1980

Na Boniface Wambura 
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Yanga, Pan Africans na Taifa Stars, Athuman Kilambo kilichotokea jana usiku jijini Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Kilambo akiwa mchezaji, na baadaye kocha alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezea na kufundisha zikiwemo Pan Africans na Cargo, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Kilambo, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na klabu ya Pan Africans na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Maziko ya kocha huyo aliyeinoa Pan tangu mwaka 1975 hadi 1984 akiisaidia kutwaa ubingwa wa Tanzania mwaka 1982 na kutetesha soka la Afrika yalifanyika jionio ya leo kwenye makaburi ya Kisutu mkoani Dar es Salaam ambapo TFF imetoa ubani wa sh. 100,000.
Marehemu Kilambo amefariki kutokana na kusumbuliwa kwa muda na ugonjwa wa Kansa ya Koo na inaelezwa marehemu ameacha watoto watano, watat wa kiume wakiwemo nyota wa zamani wa Yanga na Reli Ramadhani Kilambo na Athuman Kilambo.
Mungu aiweke roho ya marehemu Kilambo mahali pema peponi. Amina 

FIFA YATISHIA KUIFUNGIA TANZANIA, KISA SERIKALI

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA) limesema litaifungia Tanzania iwapo itabainika kuwa Serikali imekuwa ikiingilia shughuli za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
FIFA imesema kumekuwa na shutuma kupitia taarifa mbalimbali za vyombo vya habari nchini kuwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imeonesha nia ya kuingilia uendeshaji wa TFF.
Kwa mujibu wa barua ya jana (Machi 10 mwaka huu) ya FIFA kwenda kwa Rais wa TFF, Leodegar Tenga, vyombo vya habari vimemkariri Waziri (Dk. Fenella Mukangara) kuwa Serikali imeiagiza TFF kutumia Katiba ya mwaka 2006 katika uchaguzi wakati tayari imeshafanyiwa marekebisho.
“Pia imeelezwa kuwa TFF imetakiwa kufanya Mkutano Mkuu pamoja na ule wa uchaguzi kwa tarehe ambazo zimepangwa na Serikali. Vilevile imeelezwa kuwa Serikali inakusudia kuunda Kamati ya Muda iwapo TFF haitatekeleza maagizo yake,” imesema sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Valke.
FIFA imesema iwapo yaliyoripotiwa na vyombo vya habari yatathibitika kuwa kweli, maana yake huo ni uingiliaji wa wazi wa Serikali kwa shughuli za TFF.
“Tunapenda kuwakumbusha kuwa wanachama wote wa FIFA wanatakiwa kuendesha shughuli zao kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu mwingine kama ilivyoelezwa katika ibara za 13 na 17 za Katiba ya FIFA. “Hivyo kama maagizo hayo yanayodaiwa kutolewa na Serikali yatatekelezwa, suala hili litapelekwa katika mamlaka za juu za FIFA kwa hatua zaidi ikiwemo kuisimamisha Tanzania kama ambavyo inakuwa pale panapokuwa na uingiliaji wa Serikali,” imesema barua hiyo.
Barua hiyo ambayo nakala yake pia imetumwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) imeelezea baadhi ya athari ambazo Tanzania itakumbana nazo endapo itasimamishwa ni timu za taifa pamoja na klabu kutoshiriki mechi za kimataifa kwa mujibu wa Ibara ya 14 ya Katiba ya FIFA.
Vilevile si TFF au wanachama wake na maofisa wengine watakaoweza kunufaika na programu za maendeleo, kozi au mafunzo yanayotolewa na FIFA na CAF.
“Madai ya uamuzi uliofanywa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ni ya kusikitisha kutokana na ukweli kuwa FIFA ilishatangaza itatuma ujumbe wake kuchunguza jinsi hali ilivyo kwa sasa na kutoa mapendekezo yake.
Kutokana na hali hii, ujumbe wa FIFA uliokuwa uje kuchunguza (suala la uchaguzi) itabidi usubiri kwa vile ni muhimu kushughulikia tatizo hili kwanza.
“Katika mazingira haya tunaomba ueleze msimamo huu wa FIFA kwa mamlaka zinazohusika (Serikali) na athari ambazo mpira wa miguu wa Tanzania utakumbana nazo. Tunakushuru na tunatarajia utatufahamisha kila hatua inayoendelea katika suala hili,” imesema barua hiyo.