STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 30, 2013

Matokeo Mapya ya Kidato cha Nne haya hapa



Waziri wa Elimu na Ufundi Stadi, Dk Shukuru Kawambwa aliyetangaza matokeo hayo leo

  JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
   

TAARIFA YA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)  ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012








1.0          UTANGULIZI


MtihaniwaKidatochaNne, 2012ulifanyikanchinikotekuanziatarehe8/10-25/10/2012. Baraza la Mitihani la Tanzaniakatikakikaochakecha 94 kilichofanyikatarehe 30 Mei, 2013 liliidhinishamatokeo haya





2.0          USAJILI NA MAHUDHURIO


Jumlayavituo5,058vilitumikakatikakufanyamtihanihuoikilinganishwa na vituo4,795vilivyotumikamwaka 2011.





2.1          TaarifazaWatahiniwa





Jumlayawatahiniwa480,029  walisajiliwakufanyaMtihaniwaKidatochaNne 2012 wakiwemowasichana217,587sawa na asilimia45.33 na wavulana262,442sawa na asilimia54.67.WatahiniwawaliofanyamtihaniwaKidatochaNne 2012  ni 458,139sawa na asilimia95.44.Watahiniwa21,890 sawa na asilimia4.56yawatahiniwawotewaliosajiliwa, hawakufanyamtihani.



2.2          WatahiniwawaShule


Watahiniwawashulewaliosajiliwa ni  411,225 wakiwemowasichana182,982sawa na asilimia44.50 na wavulana228,243sawa na asilimia55.50.Watahiniwawashulewaliofanyamtihaniwalikuwa397,138sawa na asilimia96.57. Aidha, watahiniwa14,087sawa na asilimia3.43 hawakufanyamtihanikutokana na sababumbalimbalizikiwemoutoro, ugonjwa na vifo.





2.3          WatahiniwawaKujitegemea


Watahiniwawakujitegemeawaliosajiliwawalikuwa ni 68,804wakiwemowasichana34,605 sawa na asilimia50.30 na wavulana34,199sawa na asilimia49.70.Watahiniwa61,001 wakiwemowasichana 30,918 nawavulana 30,083  wamefanyamtihaniwakatiwatahiniwa7,803 sawa na asilimia 11.34 hawakufanyamtihani.








3.0          MATOKEO YA MTIHANI





3.1          Maandaliziyamatokeo


MatokeoyaMtihaniwaKidatochaNnemwaka 2012 yalitangazwatarehe 18 Februari 2013 na kufutwaMachi 2013 kutokana na sababuzakitaalamukatikamatumiziyataratibuzakuchakatamatokeo. MatokeoyaliyofutwayalikuwayamechakatwakwakutumiautaratibuwaFixed Grade Ranges. MatokeoyanayotangazwasasayamechakatwakwautaratibuhuohuolakiniyamefanyiwaStandalization.


Kimataifakunaainakuumbilizakuchakatamatokeoyamtihani : Flexible ‘Grade Ranges na Fixed Grade Ranges’.


‘Flexible Grade Ranges’ hutumiaviwangotofautikuchakatamatokeoyawatahiniwakwakuzingatiakiwangochaufauluchasomohusikakwakilamwaka. Hivyoviwangovyakuchakatamatokeohubadilikakilamwakakulingana na ufauluwawatahiniwakwakilasomohusika.


Katikamfumowa ‘Fixed Grade Ranges’ viwangovyaainamojahutumikakuchakatamatokeokwamasomoyote bila kujalikiwangochakufaulukwasomohusika. Viwangovyakuchakatamatokeohutumikahivyohivyokilamwaka bila mabadiliko.


KwamiakamingiBaraza la Mitihani la Tanzanialimekuwalikitumiamfumowa ‘Flexible Grade Ranges’. Mwaka 2012, mfumowa ‘Fixed Grade Ranges’ ulitumikakuchakatamatokeokwamaraya kwanza


Mabadilikohayoyalitokana na maoniyawadauyaliyotokana na utafitiuliofanywa na Wizaramwaka 2010 kufuatiakushukakwaufauluwamtihaniwaKidatochaNnemwakahuo. Pia kwakuzingatiamaelekezoyaTumemaalumiliyochunguzadosarizilizojitokezakwenyematokeoyamtihaniwaKidatocha Sita mwaka 2012 katikasomo la IslamicKnowledge.





3.2 MatokeoyaWatahiniwawaShule


Jumlayawatahiniwawashule159,609katiyawatahiniwa397,138


waliofanyaMtihaniwaKidato cha Nne 2012 wamefaulu. Wasichanawalikuwani60,751nawavulanawalikuwani98,858.








3.3 MatokeoyaWatahiniwawaKujitegemea





Idadiyawatahiniwawakujitegemeawaliofaulumtihanini26,191 katiyawatahiniwa61,001 waliofanyamtihani. Wasichanawaliofauluni11,581nawavulanani14,910.





4.0          UBORA WA UFAULU KWA MADARAJA NA JINSI





Uborawaufaulukwakuangaliamadarajawaliyopatawatahiniwawashuleunaoneshakuwajumlayawatahiniwa35,349wamefaulukatikamadaraja I – III ambapokatiyaowasichanani10,924 nawavulanani24,425.





 MchanganuowaufaulukwakiladarajakwajinsikwaWatahiniwawaShulemwaka 2012 nikamaifuatavyo:







Wavulana
Wasichana
Jumla
Idadi
Asilimia
Idadi
Asilimia
Idadi
Asilimia
I
2,179
1.07
1,063
0.64
3,242
0.88
II
7,267
3.58
3,088
1.85
10,355
2.8
III
14,979
7.37
6,773
4.05
21,752
5.87
I-III
24,425
12.02
10,924
6.54
35,349
9.55
IV
74,433
36.65
49,827
29.78
124,260
33.54
I-IV
98,968
48.66
60,779
36.30
159,747
43.08
0
104,259
51.33
106,587
53.7
210,846
56.92








5.0      SHULE KUMI BORA NA SHULE KUMI ZA MWISHO





Uborawashuleumepangwakwakutumiakigezo cha “Grade Point Average” (GPA) kuanzia A = 1 na F = 5.  Shulezimegawanywakatikamakundimawilikulingananaidadiyawatahiniwakamaifuatavyo:


(i)            Shulezenyewatahiniwa40 na zaidi  (Jumlani 3,396)


(ii)           Shulezenyewatahiniwapungufuya 40 (Jumlani  753).





5.1     Shule Kumi bora katikakundi la shulezenyewatahiniwa 40 na zaidi





Shulezifuatazozimepangwakwakuanzanaya kwanza hadiyakumikatikakundi la shulezenyewatahiniwa40nazaidi.








NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
RANK
CENTRE NAME
REGISTERED
REGION
1
ST. FRANCIS GIRLS  S  S
90
MBEYA
2
MARIAN BOYS'  S S
75
PWANI
3
FEZA BOYS' S S
69
DAR ES SALAAM
4
MARIAN GIRLS S  S
88
PWANI
5
CANOSSA S S
66
DAR ES SALAAM
6
FEZA GIRLS' S S
50
DAR ES SALAAM
7
ROSMINI S S
78
TANGA
8
ANWARITE GIRLS  S S
49
KILIMANJARO
9
ST. MARY'S MAZINDE JUU S S
83
TANGA
10
JUDE MOSHONO SS
51
ARUSHA








5.2     ShuleKumizamwishozenyewatahiniwa 40 nazaidi





Shulezifuatazozimepangwakwakuanzanaya kwanza hadiyakumikutokamwisho.


NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
1
MIBUYUNI  S  S
40
LINDI
2
MAMNDIMKONGO S  S
63
PWANI
3
CHITEKETE  S  S
57
MTWARA
4
KIKALE   S  S
60
PWANI
5
ZIRAI   S S
41
TANGA
6
MATANDA SECONDARY SCHOOL
53
LINDI
7
KWAMNDOLWA   S  S
89
TANGA
8
CHUNO   S.  S
143
MTWARA
9
MBEMBALEO S  S
56
MTWARA
10
MAENDELEO S  S
103
DAR ES SALAAM





5.3          ShuleKumi bora katikakundi la shulezenyewatahiniwachiniya 40





Shulezifuatazozimepangwakwakuanzanaya kwanza hadiyakumikatikakundi la shulezenyewatahiniwa 40 nazaidi.





NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
1
THOMAS MORE MACHRINA SS  S
20
DAR ES SALAAM
2
QUEEN OF APOSTLES-USHIROMBO SEMINARY
24
SHINYANGA
3
BETHELSABS GIRLS   S  S
33
IRINGA
4
PRECIOUS BLOOD   S  S
34
ARUSHA
5
MAUA SEMINARY
31
KILIMANJARO
6
ST. MARY'S JUNIOR SEMINARY
28
PWANI
7
CARMEL  S    S
36
MOROGORO
8
SANU SEMINARY
37
MANYARA
9
BROOKEBOND  S  S
27
IRINGA
10
ST.CAROLUS SECONDARY   S  S
37
SINGIDA








5.4     Shulekumi (10) zamwishozenyewatahiniwachiniya 40





Shulezifuatazozimepangwakwakuanzanaya kwanza hadiyakumikutokamwisho.


NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
1
DODEANI TECH.    S  S
10
PEMBA
2
KALAMBA    S  S
11
DODOMA
3
HURUI    S   S
12
DODOMA
4
USUNGA    S   S
13
TABORA
5
MANDWANGA    S  S
13
LINDI
6
BETTY MITCHEL  S   S
17
MOROGORO
7
CHONGOLEANI   S  S
17
TANGA
8
MMULUNGA   S   S
17
MTWARA
9
NYUAT    S   S
20
ARUSHA
10
MWAKIJEMBE    S   S
13
TANGA








6.0.      HITIMISHO


KuanziasasamatokeoyamithaniyakidatochaNne na Sita yatachakatwakwakutumiaFixed Grade Range na Standardisation. Natoawitokwawadauwotewaelimukutoaushirikianotuwezekuboreshaelimunchini.








7.0.        KUANGALIA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012





MatokeoyaMtihaniwaKidatochaNne (CSEE), 2012 yanapatikanakatikatuvutizifuatazo :


·         www.matokeo.necta.go.tz


·         www.necta.go.tz


·         www.udsm.edu.ac.tz, au


·         www.moe.go.tz


  


Mhe. Dkt. ShukuruKawambwa (Mb)


WaziriwaElimu na MafunzoyaUfundi



30/5/2013
******************************************
MATOKEO YA AWALI YALIYOFUTWA YALIKUWA HIVI

TAARIFA YA MATOKEO YA MITIHANI YA MAARIFA (QT) NA KIDATO CHA NNE (CSEE)

ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012


1.0                 UTANGULIZI

Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) kwa mwaka 2012 ilifanyika nchini kote kuanzia tarehe 8-25 Oktoba 2012.  Napenda kuchukua nafasi hii kutangaza rasmi matokeo ya mitihani hiyo kama ifuatavyo :


2.0                 MTIHANI WA MAARIFA (QT)

2.1           Usajili na Mahudhurio

Katika Mtihani wa Maarifa 2012 watahiniwa waliosajiliwa ni 21,310 ambapo wasichana walikuwa ni 13,134 na wavulana ni 8,176

Jumla ya watahiniwa 17,137 sawa na asilimia 80.42 ya waliosajiliwa wamefanya Mtihani. 


2.2          Matokeo ya Mtihani wa Maarifa (QT)

Watahiniwa 5,984 kati ya 17,137 waliofanya mtihani wamefaulu Mtihani wa Maarifa (QT).


3.0                 MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012

Jumla ya vituo 5,058 vilitumika katika kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 ambapo vituo 4,155 vilikuwa vya watahiniwa wa shule na vituo 903 vilikuwa ni vya watahiniwa wa kujitegemea.


3.1                 Usajili na Mahudhurio ya Watahiniwa

(a)           Watahiniwa Wote

Jumla ya watahiniwa 480,036 walisajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wakiwemo wasichana 217,583 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,453 sawa na asilimia 54.67.  Watahiniwa waliofanya mtihani wa Kidato cha Nne 2012  ni 456,137 sawa na asilimia 95.44. Watahiniwa 21,820 sawa na asilimia 4.55 ya watahiniwa wote waliosajiliwa hawakufanya mtihani.


(b)            Watahiniwa wa Shule

Watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 411,230 wakiwemo wasichana 182,978 sawa na asilimia 44.50 na wavulana 228,252 sawa na asilimia 55.50.  Watahiniwa wa shule waliofanya mtihani walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57. Aidha, watahiniwa 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo utoro,  ugonjwa na vifo.

(c)             Watahiniwa wa Kujitegemea

Watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa walikuwa ni 68,806 wakiwemo wasichana 34,605 sawa na asilimia 50.29 na wavulana 34,201 sawa na asilimia 49.71. Watahiniwa 61,001 wakiwemo wasichana 30,917 na wavulana 30,084  wamefanya mtihani wakati watahiniwa 7,730 sawa na asilimia 11.23  hawakufanya mtihani.


4.0                 MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE


(a)                 Watahiniwa wa Shule

Jumla ya watahiniwa wa shule 126,847 kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 46,161 na wavulana ni 80,686.


(b)                Watahiniwa wa Kujitegemea

Idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 16,112 kati ya watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani.  Wasichana waliofaulu ni 6,751 na wavulana ni 9,361. 



5.0                 UBORA WA UFAULU KWA MADARAJA NA JINSI

Ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 23,520 wamefaulu katika madaraja I – III ambapo kati yao wasichana ni 7,178 na wavulana ni 16,342.


Mchanganuo wa ufaulu kwa kila Daraja kwa jinsi kwa Watahiniwa wa Shule mwaka 2012 ni kama ifuatavyo:



Idadi ya Wavulana
Idadi ya Wasichana
Jumla
I
1,073
568
1,641
II
4,456
1,997
6,453
III
10,813
4,613
15,426
I-III
16,342
7,178
23,520
IV
64,344
38,983
103,327
0
120,664
120,239
240,903


6.0        SHULE ISHIRINI ZILIZOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI

Ubora wa ufaulu wa shule umepangwa kwa kutumia kigezo cha “Grade Point Average” (GPA) kuanzia A = 1 hadi F = 5.  Shule zenye watahiniwa 40 na zaidi ziko 3,391. Shule ya kwanza hadi ya ishirini zimeainishwa kwenye Jedwali lifuatalo :

NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI YA WATAHINIWA
MKOA
1
ST. FRANCIS GIRLS
90
MBEYA
2
MARIAN BOYS S.S
75
PWANI
3
FEZA BOYS S.S
69
DAR ES SALAAM
4
MARIAN GIRLS S.S
88
PWANI
5
ROSMINI  S S
78
TANGA
6
CANOSSA S.S
66
DAR ES SALAAM
7
JUDE MOSHONO S S
51
ARUSHA
8
ST. MARY’S  MAZINDE JUU
83
TANGA
9
ANWARITE GIRLS S S
49
KILIMANJARO
10
KIFUNGILO  GIRLS S S
86
TANGA
11
FEZA GIRLS
49
DAR ES SALAAM
12
KANDOTO SAYANSI GIRLS SS
124
KILIMANJARO
13
DON BOSCO SEMINARY SS
43
IRINGA
14
ST.JOSEPH MILLENIUM
133
DAR ES SALAAM
15
ST.JOSEPH’S ITERAMBOGO SS
64
KIGOMA
16
ST.JAMES SEMINARY SS
44
KILIMANJARO
17
MZUMBE SS
104
MOROGORO
18
KIBAHA SS
108
PWANI
19
NYEGEZI SEMINARY SS
68
MWANZA
20
TENGERU BOYS SS
76
ARUSHA


7.0        SHULE KUMI AMBAZO HAZIKUFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI

NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI YA WATAHINIWA
MKOA
1
MIBUYUNI S.S
40
 LINDI
2
NDAME  S.S
41
UNGUJA
3
MAMNDIMKONGO S.S
63
PWANI
4
CHITEKETE S.S
57
MTWARA
5
MAENDELEO S.S
103
DAR ES SALAAM
6
KWAMNDOLWA S.S
89
TANGA
7
UNGULU S.S
62
MOROGORO
8
KIKALE S.S
60
PWANI
9
NKUMBA S.S
152
TANGA
10
TONGONI S.S
56
TANGA


8.0           TATHMINI YA UFAULU WA WATAHINIWA WA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012

8.1           Tathmini ya awali iliyofanyika kuhusu ufaulu wa watahiniwa katika shule mbalimbali inaonesha kuwa shule zilizofanya vizuri zaidi ni zile ambazo zina mahitaji yote ya msingi ikiwemo walimu wa kutosha, miundombinu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia.  Aidha, shule zenye ufaulu wa chini ni zile ambazo zina changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na:

(i)         Baadhi ya shule za vijijini hazina kabisa walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati na pia zina upungufu mkubwa wa walimu wa masomo mengine;

(ii)        Kutokuwepo kwa maabara kwa shule zenye mikondo ya sayansi na pia kutokuwepo kwa maktaba kwa ajili ya kujisomea; na

(iii)       Upungufu mkubwa wa vitabu vya kiada na ziada. Katika baadhi ya shule uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ni 1:10.

8.2           Mkakati wa Serikali ni kuendelea kupunguza changamoto hizo kila mwaka ikiwa ni pamoja na kufanya mambo yafuatayo:

(i)             Kuajiri walimu kila mwaka ili kuondoa upungufu uliopo katika shule zetu. Mwaka 2011/2012 Serikali iliajiri walimu wa sekodari 13,246 na mwaka huu wa fedha 2012/2013 imeajiri walimu 12,973 ambao wamepangwa katika shule zenye upungufu mkubwa wa walimu. Ajira ya walimu wapya mwaka huu umetuwezesha kuwa na wastani wa walimu 2-3 kwa shule.  Hali hii itaendelea kuboreka kadri tunavyoendela kuajiri walimu.

(ii)            Kuboresha miundombinu iliyoko katika shule zetu ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba za walimu, madarasa na maabara. Mwaka 2012/2013 Serikali imepanga kuboresha miundombinu katika shule 264 zilizopo katika mazingira magumu ikiwemo miundombinu ya maabara na nyumba za walimu.

(iii)           Kuendelea kutoa ruzuku ya Tsh 25,000 kwa mwanafunzi kwa mwaka, ambapo asilimia 50 ya fedha hizo ni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia ili kuziwezesha shule kununua vitabu pamoja na vifaa vingine muhimu kitaaluma.

(iv)           Wizara kuendelea kuzishauri Halmashauri kuweka mgawanyo mzuri wa walimu waliopo baina ya shule na shule.

(v)            Wizara itaendelea kuimarisha Idara ya Ukaguzi wa Shule pamoja na kuwawezesha Waratibu Elimu Kata na Wakuu wa Shule kufanya ukaguzi wa ndani katika Shule za Sekondari zilizo katika maeneo yao.


9.0           MATOKEO YA MITIHANI YALIYOZUIWA


Baraza la Mitihani la Tanzania limezuia kutoa matokeo ya:

(a)           Watahiniwa 28,582 wa Shule ambao hawajalipa ada ya Mtihani hadi watakapolipa ada wanayodaiwa pamoja na faini; na ikiwa hawatalipa katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.

(b)           Watahiniwa 65 wa kujitegemea na 71 waliofanya Mtihani wa Maarifa (QT) mwaka 2012 bila ya kulipa ada ya Mtihani hadi watakapolipa ada pamoja na faini. Ikiwa hawatalipa ada hiyo katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.


10.0        MATOKEO YA MITIHANI  YALIYOFUTWA


10.1              Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Udanganyifu


Jumla ya watahiniwa 789 wamefutiwa matokeo yao yote ya mtihani kwa mujibu wa kifungu Na.52(b) cha Kanuni za Mitihani baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu katika mitihani ya Oktoba 2012. Kati yao, watahiniwa wa shule ni 624 na watahiniwa wa kujitegema ni 148 na watahiniwa wa Mtihani wa Maarifa (QT) ni 17.


Aina ya udanganyifu uliobainika na idadi ya watahiniwa husika ni kama ifuatavyo:



S/N
AINA YA UDANGANYIFU
IDADI YA WATAHINIWA
(i)        
Watahiniwa kubainika kuwa na skripti zenye miandiko tofauti au kuwa na miandiko tofauti katika skripti ya somo moja au zaidi ya moja.
04
(ii)       
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi ndani ya chumba cha mtihani wakiwa na ‘notes.’
170
(iii)      
Watahiniwa kubainika kuwa na mfanano usio wa kawaida wa majibu.
590
(iv)      
Watu kukamatwa wakiwafanyia watahiniwa wengine mtihani ‘impersonation”.
04
(v)       
Watahiniwa kukamatwa na simu ndani ya chumba cha mtihani.
06
(vi)      
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi wakibadilisha karatasi za maswali au skripti kwa lengo la kufanya udanganyifu.
15

JUMLA
789


10.2              Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Watahiniwa Kuandika Matusi Katika Skripti Zao

(i)          Jumla ya watahiniwa 24 waliandika matusi kwenye skripti zao za masomo mbalimbali. Kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kifungu 5(13) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka:

Written responses to any examination question which carry words, drawings or pictures connected to sex or abusive language in such a way that it becomes offensive shall consitute an examination offence and a candidate who commits such an offence shall be punished by the Council.”


Kutokana na kosa hilo Baraza la Mitihani limefuta matokeo  yao yote kwa mujibu wa Kifungu cha 6(2)(a) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka: 

“A candidate found to have committed an examination offence shall - (a) have his examination results nullified”

(ii)         Kitendo cha kuandika matusi kwenye karatasi za majibu (skripti) kinaonesha utovu wa nidhamu wa hali ya juu. Serikali haitaweza kuwavumilia hata kidogo watahiniwa wa aina hiyo. Hivyo, Serikali itaangalia hatua zaidi za kisheria za kuchukua dhidi ya watahiniwa wote walioandika matusi.

Kwa mujibu wa kifungu Na. 6(2)(b) cha Kanuni za Mitihani, watahiniwa wote waliobainika kufanya udanganyifu katika mitihani au kuandika matusi katika skripti zao hawataruhusiwa kufanya mitihani inayoendeshwa na Baraza la Mitihani la Tanzania  kwa kipindi cha mwaka mmoja (01) kuanzia tarehe ya kutangazwa kwa matokeo.


11.0        KUANGALIA MATOKEO YA MTIHANI WA CSEE na QT, 2012


(a)           Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT), 2012  yanapatikana katika tovuti zifuatazo: 

·               www.matokeo.necta.go.tz,

·               www.necta.go.tz,     

·               www.udsm.edu.ac.tz, au

·               www.moe.go.tz


(b)           Matokeo yanaweza kupatikana pia kwa njia ya  ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwenda namba 15311. Jinsi ya kutuma ujumbe andika:


MATOKEOXNAMBA YA KITUOXNAMBA YA MTAHINIWA

(Mfano : matokeoxS0101x0503)




Dkt.  Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb)


WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

18 Februari 2013

Kamati ya Usajili Simba yafagiliwa

Haruna Shamte wakipashaa misuli na mchezaji mwenzake

King Kibadeni akiwa makini kwenye mazoezi ya Simba

Mwaka huu watatukoma: Baadhi ya viongozi wa Simba wakifuatilia mazoezi ya timu yao. (wa pili kushoto) ni Katibu Mkuu, Evodius Mtawala

Baba Ubaya akionyesha 'ubaya' wake mazoezini

Vikosi vyetu vya kupima ubavu vitakuwa hivi: Makocha wasaidizi wa Simba, Julio na Kisaka wakijadiliana leo asubuhi wakati wa mazoezi ya timu yao

Samuel Ngassa naye yumo mazoezni Simba

Messi aliyeipa kamera mgongo na mwenzake

Yule mrefu anatufaa: Julio na Kisaka pamoja na Amri said (6) makocha wasaidizi wa Simba wakiwa kazini

Rukeni hivi:Kibadeni akiwaelekeza kwa mfano wachezaji wake

Mtanikoma! Messi kutoka Coastal akionyesha balaa mazoezini

Lazima mtunyakue tu mtake msitake

Kila mmoja anaonyesha makeke yake, huyu ni Haruna Shamte

Messi akiongoza wenzake

Shamte na mwenzake wakifanya mazoezi ya viungo

BAADHI ya wanachama wa klabu ya Simba wameifagilia Kamati ya Usajili ya klabu hiyo chini ya Mwenyekiti wake, Zakaria Hanspope kwa kufanya usajili mzuro waliodai unawapa matumaini ya kufanye vyema kwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu ujao na hata kwenye michuano ya Kagame.
Pia kamati hiyo imefagiliwa zaidi kwa kuepuka kusajili wachezaji wanaotoka kwa mahasimu wao Yanga, kwa kudai watasaidia kujenga timu yenye nidhamu na mipango itakayoweza kurejesha heshima ya klabu yao.
Mmoja wa wanachama hao, Onesmo Waziri 'Ticotico' aliyewahi kuwa Katibu wa Kamati ya Fedha na Mipango chini ya uongozi wa sasa, alisema amefurahishwa mno na namna usajili wa Simba unavyofanyika.
Waziri alisema ni vyema kamati yao ya usajili ikaendelea na mwenendo huo huo wa kusajili kwa umakini mkubwa na kuepuka kuchukua mchezaji yeyote kutoka Yanga ili waijenge timu katika nidhamu moja itakayoinufaisha timu yao kwa michuano itakayoshiriki.
"Nafurahi sana kuona Simba wanafanya usajili wenye akili kuliko ule uchafu tulioufanya msimu uliopita, lakini niwapongeze zaidi kamati kwa kuachana na tabia ya kusajili wachezaji kutoka Yanga," alisema.
Aliongeza;."Unasajili wachezaji wenye upeo mdogo kama (jina kapuni) maana yake ni kutafuta matatizo napenda wasonge mbele tupate wachezaji wengine wenye viwango vipya na mawazo mapya. Simba tunaweza sana tena sana."
Mwanachama mwingine aliyejitambulisha kama Bakar Ally wa Tawi la Ubungo, alisema kwa mwenendo wanaoenda nao uongozi wao kwa kusajili kwa umakini wanawapa matumaini ya kurejesha heshima yao hasa ikizingatiwa timu ipo chini ya King Abdallah Kibadeni mmoja wa makocha wenye mafanikio nchini.
Pongezi hizo za wanachama hao wa Simba zimekuja wakati kamati hiyo ikitangaza baadhi ya wachezaji iliyowanyakua mpaka sasa ikiwamo Mganda Mosse Oloya, Ibrahim Twaha 'Messi', Issa Rashid 'Baba Ubaya' na kipa kutoka Kagera Sugar.

Phares Magesa aahidi kuendelea kuwalipia yatima wa New Hope Family

Rais wa TPN, Phares magesa (mwenye suti)

RAIS wa Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN) na Mlezi wa kituo cha kulelea yatima cha New Hope Family Group kilichopo Kigamboni, Phares Magesa ameahidi kuendelea kuwalipia ada za shule watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaolelewa na kituo hicho.
Magesa alitoa ahadi hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa mgeni rasmi katika sherehe ya kuwaaga wanafunzi wa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambao ni Wanachama wa Jumuiya ya Umoja wamataifa (YUNA MNMA) mahafali yaliyofanyika kituo hapo, jijini Dar es Salaam.  
Alisema amekuwa akisaidia watoto wa kituo hicho kwa muda mrefu hivyo alidaia aendelea ila aliwataka watoto hao kuongeza juhudi katika masomo ili wasirudishe nyuma juhudi zake za kuwasaidia.
Magesa aliwataka watoto hao kuwa watulivu na kuongeza juhudi ili siku moja wafikie walipofikia wenzao waliowatembelea waliokuwa wakihitimu elimu ya juu akidai ndio njia sahihi ya kujikwamua kimaisha.
 “Naahidi  kuendelea kuwasaidia kwani ni wajibu wangu kama mwananchi ila naomba watu wengine wenye uwezo kujitokeza kama mlivyoamua leo kufanya sherehe yenu kwa kula na watoto hao kwani wanahitaji jamii tofauti nao ili kupunguza msongo wa mawazo”, alisema.
Magesa. alitumia pia alitumia nafasi hiyo kuwaasa wanafunzi wanaomaliza chuo cha Mwalimu Nyerere kuwa waadilifu na wenye maadili pindi watakapopata fursa ya kupaja ajira kokote.
Alisema kumekuwa na tabii ya vijana kukosa uadilifu kwa siku za karibu jambo ambalo linashusha heshima ya vijana ambao wamekuwa wakimaliza masomo katika kwa sasa.
Alisema uadilifu ndio jambo muhimu kwa kijana yoyote ambaye anahitaji kusaidia maendeleo ya nchi yake kwani kuenda kinyume kutarudisha maendeleo na kuathiri jamii moja kwa moja.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa tawi la (YUNA MNMA) Fredirick Semainda ambaye ameingia madarakani hivi karibuni alisema wao kama vijana waliamua kufanya sherehe ya kuwaaga kaka na dada zao kwa kutembelea kituo hicho ili waweze kutoa mchango wao kwa watoto hao.
Alisema wao katika mikakati yao ya mwaka wamejipangia kufanya shughuli mbalimbali za kijamii hivyo hii ya kutembelea kituo hicho ni moja ya utekelezaji wa mipango yao.
Semainda alisema katika mahafali hayo ya pili tangu kuanzishwa kwa YUNA MNMA wahitimu 52 wametunikiwa vyeti jambo ambalo wanaliona kuwa ni la mafanikio makubwa.
Mwenyekiti huyo alisema wataendelea kufanya shughuli za kijamii kama hiyo waliofanya mwishoni mwa wiki ambapo walishiriki kuandaa chakula cha mchana na watoto hao na kula nao pamoja na kuwapatia zawadi mbalimbali ikiwemo mchele kilo 40, mafuta, sabuni, madaftari, kalamu na nguo.
Aidha alisema katika sherehe hiyo wanafunzi wanachama wa YUNA MNMA walichangisha shilingi 43,000 kwa ajili ya kuwapatia madawa watoto ambao wanaishi katika kituo hicho.

Simba waendelea kujifua Mzimbabwe naye ajitokeza kuomba namba Msimbazi


Kocha Kibadeni akiwaonyesha wachezaji wake kipi cha kufanya katika mazoezi ya leo asubuhi

Kocha msaidizi, Amri Said, akionyesha cha kufanya kwa wachezaji wake

King Kibadeni achaneni naye yupo 'serious' mazoezini si mchezo

Beki mpya wa Simba, Issa Rashid 'baba Ubaya' akijifua na wenzake

Wachezaji wa Simba wakijifua huku kocha wao, Amri Said (6) akiwaangalia

Hussein Ibrahim Twaha 'Messi' yuko kikazi zaidi licha ya kusumbuliwa na kifua

mchezaji anayedaiwa kutoka Zimbabwe, Tinash akijifua na wenzake leo asubuhi

KLABU ya soka ya Simba inaendelea kujifua kwenye uwanja wa Kinesi kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Kombe la Kagame itakayofanyika nchini Sudan, huku idadi ya wachezaji wanaojitokeza kuomba kupata nafasi ya kusajiliwa ikizidi kuongezeka wakiwamo wageni, ambapo Wanigeria na Mzimbabwe ni kati yao.
Wanigeria wanaojifua katika mazoezi hayo yanayosimamiwa na jopo la makocha watano wakiongozwa na King Abdallah Kibadeni akisaidiwa na Jamhuri Kihwelu 'Julio' Njames Kisaka, Amri Said na Seleman Matola ni pamoja na Modebe Izze na Samuel Okey wakati Mzimbabwe ni Tinash Motenence.
Wachezaji hao wanashindana na Wakongo wanne waliojitokeza tangu siku ya kwanza ya utambulisho wa Kibadeni kwa wachezaji hao na wanaendelea kupimwa na makocha hao kwa ajili ya mmoja wao kusajiliwa kuziba nafasi ya mchezaji mmoja wa kigeni iliyosalia Msimbazi.
Kocha msaidizi wa Simba, Julio alisema kwa sasa wamesaliwa na nafasi moja tu ya mchezaji wa kigeni na hivyo wataangalia mwenye uwezo wa kubebeshwa nafasi hiyo akisema wanamhitaji zaidi kiungo.
Julio alisema mpaka sasa bado hawana la kusema kuhusu wachezaji hao kwa vile ndiyo kwanza wanaanza kuwapima, lakini alisema miongoni mwa waliojitokeza wapo wenye uwezo mkubwa na kuwapa matumaini ya kupata kikosi imara kitakachoungana na wale walioichezea timu hiyo msimu huu ili kuweza kushiriki vyema Kagame na ligi ya msimu ujao.

Miss Tabata 2013 kufanyika kesho, Twanga Pepeta kunogesha burudani


 
Warembo wa Miss Tabata wakiwa katika pozi walipokuwa wakielekea Mikumi

Warembo wa Miss Tabata

Vimwana wa Miss Tabara 2013

SHINDANO la kumsaka Miss Tabata 2013 linafanyika kesho katika ukumbi wa Dar West Park Tabata, ambapo bendi ya Twanga Pepeta inatarajiwa kuwasindikiza warembo hao kwa kutumbuiza.
Warembo 20 watachuana kutaka kumrithi Noela Michael ambaye anashikilia taji hilo kwa sasa. Noela pia ndiye anashikiria taji la Miss Ilala.
Mbali ya kuwakilisha Miss Tabata kwenye shindano la Miss Ilala baadaye mwaka huu, mshindi huyo pia atazawadiwa Sh.600,000 pamoja na king’amuzi kutoka Multichoice ambacho kimelipiwa tayari kwa miezi mitatu kikiwa na thamani ya  Sh.400,000.
Mshindi pili atapata Sh. 300,000,  wa nne Sh.200,000 na wa tano  atazawadiwa Sh.150,000.
Warembo wengine watakaofanikiwa kuingia 10 bora, watazawadiwa Sh.100,000 kila mmoja wakati waliosalia watapata kifuta jasho cha Sh.50,000 kila mmoja.
Warembo wanaoshiriki kinyang’anyiro hicho mwaka huu ni Madgalena Bhoke (21), Kabula Juma Kibogoti (20), Upendo Dickson Lema (22), Hidaya David Mwenda (22), Aneth Ndumbaro (19),  Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Musa Kitereja (19),  Rehema Kihinja (20),  Pasilida Mandali (21), Brath Chambia (23), Joaniter Kabunga (21), Recho Mushi (20),Caroline Sadiki (20) na  Suzan Daniel (18).
Wadhamini wa shindano hilo ni Dodoma Wine, Redd’s Original, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito Entertainment, Integrated Communications Limited, CXC Africa, Brake Point na Saluti5.
Miss Tabata 2013 imeandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts.

Mwili wa Ngwair kuwasili nchini J'mosi, kuagwa J'2 kabla ya kuzikwa Moro J3

http://blog.greatlakesmix.com/wp-content/uploads/2013/02/ngwair-400x600.jpg
Ngwair enzi za uhai wake
MWILI wa marehemu Albert Mwangwea 'Ngwair' unatarajiwa kutua nchini siku ya Jumamosi jioni na kuagwa rasmi Jumapili kutwa nzima kabla ya kusafrishwa kwenye Morogoro kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika Jumatatu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamati ya Mazishi ya msanii huyo aliyefariki juzi nchini Afrika Kusini taratibu zote za kurejeshwa kwa mwili wa Ngwair zinaendelea vyema na kwamba kamati hiyo inaomba watu wajitokeza kuichangia kamati hiyo kutokana na ukweli kuna gharama kubwa zinazohitajika kufanikisha mambo.
Msemaji wa kamati hiyo Adam Juma, alisema mchana huu kuwa kila kitu kinaenda sawa na kwamba mwili ya marehemu Ngwair utawasili nchini jioni ya Jumamosi na Jumapili kuanzia saa 2 mpaka saa 10 wananchi watauaga mwili huo kabla ya kusafirishwa kwenda Morogoro kwa mazishi.
Juma alisema mazishi ya Ngwair yafanyika Jumatatu na kwamba kamati yao inayoongozwa na Kaka wa Marehemu Kenneth Mangwair inaratibu kila kitu kwa sasa kwa ufanisi mkubwa, ila aliwaomba mashabiki wa muziki na watanzania kwa ujumla kujitolea kwa hali na mali kuwezesha mipango ya mazishi ya Ngwair.
Mkali huyo wa miondoko ya hip hip aliyetamba na vibao mbalimbalio vikali, alifariki nchini humo alipoenda kufanya maonyesho ya muziki akiwa na msanii mwenzake, M to the P ambaye alikuwa amezimika chumbani walimokuwa wanakaa na kwa sasa inaelezwa hali yake inaendelea vyema jambo linalotoa matumaini.

Balozi Biswaro awapa changamoto Stars

Balozi Biswaro

Kikosi cha Stars
Na Boniface Wambura, Addis Ababa
BALOZIi wa Tanzania nchini Ethiopia, Joram Biswaro amewataka wachezaji wa Taifa Stars kuhakikisha wanaipeleka timu hiyo kwenye fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.

Ametoa changamoto hiyo wakati alipotembelea mazoezi ya timu hiyo jana (Mei 29 mwaka huu). Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imepiga kambi nchini Ethiopia na inafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Addis Ababa.

“Watanzania tunafurahi kutokana na uwezo mnaouonyesha, hasa baada ya kuifunga Morocco mabao 3-1. Kama mliwafunga nyumbani hata kwao mnaweza kuwafunga. Tunataka kuwaona Maracana (Brazil) mwakani, mimi tayari ninayo tiketi mtanikuta kule,” amesema Balozi Biswaro ambaye enzi zake aliwahi kuichezea timu ya Yanga.

Taifa Stars ambayo iko Addis Ababa tangu Jumatatu (Mei 27 mwaka huu) imeweka kambi katika hoteli ya Hilton ambapo Jumapili (Juni 2 mwaka huu) itacheza mechi ya kirafiki na Sudan (Nile Crocodile) kwenye Uwanja wa Addis Ababa.

Balozi Biswaro ameikaribisha Taifa Stars ubalozini Addis Ababa mara baada ya mechi dhidi ya Sudan ambapo itakutana na baadhi ya Watanzania wanaoishi Ethiopia kabla ya kuondoka alfajiri kwenda Marrakech, Morocco kwa kupitia Cairo, Misri.

Kocha Kim Poulsen amesema kikosi chake kinaendelea na mazoezi vizuri na kitaimarika zaidi baada ya wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kujiunga nacho Juni 3 mwaka huu jijini Marrakech kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu.

Wachezaji walioko katika kikosi cha Stars jijini Addis Ababa ni Juma Kaseja, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi.

Wednesday, May 29, 2013

Yathibitika M2P hajafa, ila bado yu mahututi

ASUBUHI zilizagaa taarifa nchini kwamba msanii aliyekuwa na marehemu Albert Mangwea 'Ngweair', M to the P aliyekutwa amezimia kwamba naye alikuwa amefariki dunia, ukweli ni kwamba msanii huyo bado yu hai ingawa hali yake inaelezwa kuwa bado si nzuri kwani anaendelea kupumulia gesi.
Kwa mujibu wa Mtangazaji wa kituo cha radio cha Clouds Fm, Millard Ayo, aliyekuwa akizungumza moja kwa moja kutoka Afrika Kusini alipoenda, alisema kuwa M2P bado yu hai, ingawa bado amelazwa na anapumua kwa kutumia mashine maalum.
Ayo alisema M2P aliyekuwa sambamba na Ngweair katika chumba kimoja, alionekana na baadhi ya marafiki zake akiwamo msanii Bushoke akinyanyuka mara aalipowaona wameenda kumjulia hali na kuthibitisha kuwa yu hai tofauti na taarifa za mapema asubuhi kwamba msanii huyo naye aliaga dunia.
Aidha mtangazaji huyo anayeendesha kipindi cha Amplifaya, alisema mwili wa marehemu Ngweair ulihamishw atoka hospitali ya Helen Joseph na kupelekwa hospitali ya serikali ukisubiri taratibu za kuusafirisha kuurejesha Tanzania kwa ajili ya mazishi.

Jide, aungana na MwanaFA, Kalapina kufuta onyesho


 
Judith Wambura Mbibo 'Jide' a.k.a Anaconda
MWANADADA mkali wa miondoko ya muziki wa kizazi kipya nchini, Lady Jaydee ameamua kufuta onyesho lake la miaka 13 tangu awe katika fani hiyo lililokuwa lifanyike Ijumaa kupisha msiba wa Albert Mwangwea 'Ngwair'.
Hatua ya Jide imekuja huku wakali wengine wa muziki huo nchini MwanaFA na Karama Masoud 'Kalapina' ambao nao walikuwa wafanye maonyesho yao Mei 31 jijini dar katika kundi tofauyti.
Jide, ambaye hivi karibuni aliingia kwenye mzozo na kituo cha radio cha Clouds, kiasi cha kufikishwa mahakamani, alinukuliwa akisema kuwa onyesho hilo halitafanyika tena kesho mpaka msiba wa Ngwair utakapomalizika.
Akihojiwa na kipindi cha Super Mix kinachorushwa na kituo cha EA Radio, Jide maarufu kama Komandoo a.k.a Binti Machozi au ukipenda Anaconda, mkongwe alikuwa na wakati mgumu alipoulizwa unamuelezeaje msanii Mangwear.
Jide aliyekuwa mwenye huzuni akijibu huku akilia kuwa, Tanzania imempoteza nyota. Juu ya shoo yake Jide alisema imebidi aisogeze mbele kidogo mpaka msiba huu upite kwanza ndipo atasema tarehe rasmi.
Ngwair alifariki jana nchini Afrika Kusini kwa kile kilichoelezwa kuwa kala kitu chenye sumu, taarifa nyingine zikidai alijidunga dawa na kuzimika yeye na rafikie M to the P aliyeripotiwa kulazwa hospitalini akiwa hoi mjini  Johannesburg.

Familia ya Ngwair watoa taarifa ya mazishi na jinsi mwili utakavyoletwa Bongo

http://3.bp.blogspot.com/-WhLAsO1Z0Cg/TftKo0GeYeI/AAAAAAAAAkY/Z6SKc0_7gz0/s1600/NgweaWEB.jpg
Ngwair enzi za uhai wake
BABA Mdogo wa 'Membaz' wa kundi la Chember Squad, Albert Mangwea 'Ngwair', Mzee Mangweha ambaye yuko Mbinga Songea kikazi, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa yaani baba mkubwa wa Ngwair, David Mangweha ambaye naye yuko Songea kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na pia mapokezi yatafanyika hapa Dar es salaam Mbezi Beach. 
  

Baba huyo mdogo alisema kuwa kesho ndo watarudi Dar es Salaam pamoja na kaka yake yaani baba mkubwa wa marehemu. 
 
Kuhusu mwili kuletwa hapa Tanzania kutoka Afrika Kusini baba mdogo amesema kuwa mpaka sasa hawajajua jinsi gani mwili huo utafika hapa lakini kuna ndugu zao ambao tayari washaanza kufanya taratibu za kuwasiliana na ubalozi wa Afrika Kusini ili kujua ni jinsi gani mwili huo utafika hapa.

Kama kutakuwa na mabadiliko yeyote watakapowasili kesho baba mdogo na baba mkubwa baada ya kikao cha familia watatoa taarifa.
Lakini asuibuhi mmoja wa ndugu wa marehemu kutoka mkoa wa Mara alisema kuwa mwili wa msanii huyo aliyekuwa mkali wa Hip hop utakapowasili nchini utazikwa mjini Morogoro ambapo tayari kuna msiba umewekwa na mama yake.
Ndugu huyo alikuwa akihojiwa moja kwa moja na kituo kimoja cha redio na kusema wana ndugu wamekubaliana Ngwair akazikwe Morogoro alipohifadhiwa baba yake.
Ngwair, aliyefahamika baada ya kutoa kibao cha Ghetto Langu mwaka 2003 kabla ya kupakua albamu ya Mimi na kisha kufuatiwa na Nge, alifariki jana nchini Afrika Kusini kwa kile kilichoelezwa kujidunga dawa za kulevya, ingawa bado haijathibitishwa kidaktari alipoenda kufanya shoo na msanii mwenzake M2P. 

WASIFU WA MAREHEMU NGWAIR


 MAREHEMU Albert Kenneth Mangwea alizaliwa Novemba 16, 1982 mjini Mbeya akiwa ni mtoto wa mwisho kati ya watoto 10 wa baba yake na wa sita kwa mama.
Kiasili Ngwair alikuwa mwenyeji wa mkoa wa Ruvuma kabila la Kingoni, ingawa amekuwa mjini Morogoro na mkoa wa Dodoma.
Shule ya Msingi aliisoma Shule ya Bungo mjini Morogoro alikohamia akiwa na miaka mitano kabla ya kuhamia Dodoma kulamizia darasa la saba toka la tano alilohama nalo Shule ya Mlimwa.
Sekondari aliisoma Mazengo Sec kabla ya kuendelea Chuo cha Ufundi cha Mazengo pia mjini Dodoma alipoanza kujihusisha na muziki kabla ya kutua kundi la Chamber Squad lililoundwa na Jafarah, Jay Mo, Noorah, Mez B, Mchizi Mox na Dark Master.
Amewahi kunyakua tuzo ya Kili Music Award kupitia kipengele cha muziki bora wa Hiphop, huku nyimbo kadhaa zilimtambulisha vyema kwa mashabiki baadhi ikiwa ni  Ghetto Langu, Mikasi na nyingine za kushirikishwa na wasanii mbalimbali.
Katika maisha yake ya muziki aliwahi kutoa albamu mbili za Mimi ya mwaka 2005 na Nge ya mwaka juzi ambayo hata hivyo haikufanya vyema sokoni kama ile ya awali.