STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 15, 2013

Kuziona Yanga na Azam Buku 7 tu

Na Boniface Wambura
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom, Yanga na makamu bingwa Azam wanavaana keshokutwa (Jumamosi) kwenye mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kuashiria uzinduzi wa msimu mpya wa 2013/2014.

Mechi hiyo inayotarajiwa kuwa kivutio kwa wapenzi wa mpira wa miguu nchini itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni ambapo mshindi atakabidhiwa ngao.

Iwapo dakika 90 za mechi hiyo hazitatoa mshindi, timu hizo zitatenganishwa kwa mikwaju ya penalti huku asilimia 10 ya mapato ya mechi hiyo yakienda kwa kituo cha kulelea watoto cha SOS.

Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya kijani na bluu wakati viti vya rangi ya chungwa ni sh. 10,000. Watakaiongia viti vya VIP C watalipa sh. 15,000, viti vya VIP B ni sh. 20,000 wakati VIP A watalipa sh. 30,000.

News Alert; Sheikh Ponda aondolewa hospitali na kupelekwa Segerea?

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda amehamishwa toka hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kupelekea gereza la Segerea.
Habari hizo zinasema askari Polisi wamefika hospitalini hapo na kuondoka na Sheikh Ponda ambaye jana alisomewa mashtaka akiwa kitandani.
Tunafuatilia kujua ukweli wa jambo hili sambamba na kujua kilichosababisha Sheikh huyo kukimbizwa huko wakati akiendelea kupata matibabu ya jehara alilolipata kwa kilichoelezwa kupigwa risasi na Polisi mjini Morogoro mwishoni mwa wiki wakai wa shamrashamra za sikukuu ya Eid el Fitry.

LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA SEPT 14


Na Boniface Wambura
MICHUANO ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoshirikisha timu 24 zilizogawanywa katika makundi matatu msimu huu (2013/2014) itaanza kutimua vumbi Septemba 14 mwaka huu.

Kila timu itakayoongoza kundi lake katika ligi itakayochezwa kwa mikondo miwili (nyumbani na ugenini) ndiyo itakayopanda daraja kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2014/2015.

Mechi za ufunguzi kwa kundi A zitakuwa kati ya Tessema vs Green Warriors (Uwanja wa Karume, Dar es Salaam) wakati Septemba 15 mwaka huu ni Transit Camp vs Polisi Dar (Uwanja wa Mabatini, Pwani), Ndanda vs Friends Rangers (Uwanja wa Nangwanda, Mtwara) wakati Villa Squad vs African Lyon itachezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Kundi B ni Burkina Faso vs Polisi Moro (Uwanja wa Jamhuri, Morogoro), Mkamba Rangers vs Lipuli (Uwanja wa CCM Mkamba, Morogoro), Majimaji vs Mlale JKT (Uwanja wa Majimaji, Songea) wakati Septemba 15 mwaka huu Kimondo SC vs Kurugenzi (Uwanja wa Sokoine, Mbeya).

Mechi za ufunguzi kundi C ni Polisi Mara vs Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT vs Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United vs Mwadui (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga), na Pamba vs Toto Africans (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza).

Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Oktoba 26 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Machi 22 mwakani.

Wednesday, August 14, 2013

Serikali yaingilia kati mzozo wa Yanga na Azam Media

HATIMAYE mkutano ulioitishwa na serikali kupitia wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo kusuluhisha mgogoro wa mkataba wa mauzo ya haki za matangazo ya Television uliowashirikisha kamati ya ligi kuu ya soka Tanzania bara, klabu ya Yanga na Azam Media umemalizika hivi punde huku maamuzi kadhaa yakifikiwa.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari cha mtandao huu, klabu ya Yanga ni kama imeibuka kidedea kwenye madai yake ya kupinga utaratibu mzima wa mkataba huo baina ya kamati ya ligi na Azam Media. 

Hii inakuja baada maamuzi ya mkutano huo kuamuru kwamba vipengele vya mkataba huo kupitiwa upya na klabu ya Yanga na Kamati ya Ligi na vile ambavyo vitaonekana kuwa na matatizo virekebishwe. 

Pia imeamuliwa kwamba Yanga SC itakaa kikao na Azam Media kuzungumzia mambo mbalimbali ambayo Yanga imeonekana kuwa na shaka nayo kuhusu Azam pamoja na maslahi ya Yanga kupitia dili hilo la ununuaji wa haki za matangazo ya TV ya mechi za ligi uliofanywa na Azam Media.  


Shafii Dauda

Ni Mauaji Kila Kona Mbeya


 [DIWANI ATHUMANI   - ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.



WILAYA YA MBOZI – MAUAJI
MNAMO TAREHE 13.08.2013 MAJIRA YA SAA 07:00 HRS UKO KIJIJI CHA NANSAMA KATA YA ISANSA WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA. SIJAONA S/O HAONGA MIAKA 45, MKULIMA, MNYIHA, MKAZI WA NANSAMA ALIKUTWA AKIWA AMEUAWA KWA KUNYONGWA SHINGO KISHA KUTUPWA KATIKA MTO MLOWO NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA. CHANZO CHA MAUAJI HAYO NI MGOGORO WA MASHAMBA KATI YA MAREHEMU NA SHABANI S/O MBWILI PAMOJA NA MAWAZO S/O MBWILI AMBAO WALITOROKA MARA BAADA YA TUKIO HILO.  MAREHEMU ALIVIZIWA WAKATI   AKIVUA SAMAKI NA PEMBENI YA MWILI WAKE KULIKUTWA NDOANO. MWILI WA MAREHEMU UMEFANYIWA UCHUNGUZI NA KUKABIDHIWA NDUGU KWA MAZISHI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA JAMII  KUTOJICHULIA SHERIA MKONONI NA KUITATUA MIGOGORO YAO KWA NJIA YA  MAZUNGUMZO  NA  YEYOTE MWENYE TAARIFA JUU YA  MAHALI WALIPO WATUHUMIWA WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE, VINGINEVYO WAJISALIMISHE MARA MOJA.
WILAYA YA CHUNYA – MAUAJI
MNAMO TAREHE 13.08.2013 MAJIRA YA SAA 00:05 HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA KANGA WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA.  MARIA D/O MARTIN, MIAKA 37, MNYAMWEZI, MKULIMA, MKAZI WA KANGA ALIUAWA KWA KUPIGWA NGUMI KICHWANI NA KUKABWA SHINGONI NA MPENZI WAKE AITWAE LAMECK S/O MSANGAWALE, MIAKA 35, MNYIHA, MKULIMA, MKAZI WA KANGA.  CHANZO NI WIVU WA KIMAPENZI BAADA YA MTUHUMIWA KUMKUTA MAREHEMU AKIWA NA MWANAUME MWINGINE. MTUHUMIWA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUYATATUA MATATIZO YAO YA KIJAMII KWA NJIA YA MEZA YA MAZUNGUMZO ILI KUEPUSHA MATATIZO YANAYOWEZA KUJITOKEZA. PIA ANATOA RAI KWA MTU/WATU WENYE TAARIFA JUU YA MAHALI ALIPO MTUHUMIWA ALIYEHUSIKA NA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI AKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WILAYA YA MBEYA MJINI – KUPATIKANA NA BHANGI.
MNAMO TAREHE 13.08.2013 MAJIRA YA SAA 11:00HRS HUKO MAENEO YA UYOLE JIJI NA MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIMKAMATA IBRAHIMU S/O MATSON ,MIAKA 25,MUWANJI MRISTO NA MKAZI WA IGAWILO   AKIWA NA BHANGI KETE 8 SAWA NA GRAMU  40 NDANI YA  MFUKO WA SURUALI . MTUHUMIWA NI MVUTAJI NA MUUZAJI WA BHANGI HIYO .TARATIBU ZINAFANYWA ILI AFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA  MTUMIAJI.
Imesainiwa na,
 [DIWANI ATHUMANI   - ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Dunia Imeisha! 'Babu' mbaroni kwa kubaka 'vijukuu'


MBAKAJI ERASTO MWAKYOMO (50) ANAYETUHUMIWA KWA UBAKAJI AKIWA KATIKA OFISI YA MWENYEKITI WA MTAA WA MAPELELE KABLA YA KUCHUKULIWA NA MWENYEKITI WA DAWATI LA WATOTO NA UKATILI WA KIJINSIA MARY GUMBO.
WATOTO WALIOKUWA WAKIBAKWA WAKITOA MAELEZO JINSI WALIVYOKUWA WAKITENDEWA
 MWENYEKITI WA MTAA WA MAPELELE CHRISTOPHER MWAKIBETE AKIANDIKA BARUA KWA WAZAZI NA MTUHUMIWA KUPELEKWA POLISI 
 BAADHI YA WAZAZI NA NDUGU WA WATOTO WAKIWA NYUMBANI KWA MWENYEKITI WA MTAA.

***************

Ezekiel Kamanga

ERASTO MWAKYOMA mwenye umri wa miaka hamsini mkazi wa mtaa wa Mapelele Kata ya ILEMI jijini Mbeya anahojiwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuwadhalilisha watoto wawili wa kike wote wakazi wa Mapelele.

Wazazi wa watoto hao baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa watoto hao ambao mmoja ana umri wa miaka minne na mwingine mitano walitoa taarifa kwa Balozi wa mtaa Bwana CASIAN MWEZIMPYA ambapo baada ya kutafakari kwa kina aliamua kulipeleka suala hilo kwa Mwenyekiti wa Mtaa.

Mwenyekiti wa mtaa Bwana CHRISTOPHER MWAKIBETE Aliamua kuwaita wazazi na mtuhumiwa kuwahoji yaliyotukia ambapo nao watoto walipewa nafasi ya kueleza ambao walieza kuwa ERASTO Alikuwa akiwashika sehemu za siri na kuwapaka mafuta kabla ya kufanya nao mapenzi.

Baada ya kusikiliza kwa makini MWAKIBETE aliamuru kuwa suala hilo ni la kisheria na kitaalamu hivyo hawezi kuchukua hatua zozote bali suala hilo analazimika kulipeleka Polisi ambapo Mwenyekiti wa Dawati la watoto na jinsia MARY GUMBO Alimchukua mtuhumiwa hadi kituo cha Polisi kati.

Baada ya mahojiano ya awali GUMBO aliwachuchukua watoto hadi Hospitali ya Rufaa kwa uchunguzi na mtuhumiwa kubaki kituo cha kati kwa mahojiano zaidi,hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa baadhi ya watoto mtaani hapo wamekuwa wakitendewa vitendo vya ukatili lakini vimekuwa vikifumbiwa macho na baadhi ya wazazi wakihisi ni aibu kwa watoto wao.

 Na Mbeya yetu Blog

BREAKING NEWS!! UZEMBE WA TANESCO WASABABISHA KIFO CHA BINTI WA MIAKA 26 JIONI HII MBALIZI MBEYA

 HAPA NDIPO MAREHEMU ALIPOGUSA NA KUKUTWA NA MAUTI

NYAYA ZA UMEME AMBAZO ZIMENING'INIA MITA MOJA KUTOKA USAWA WA ARDHI ZIMESABABISHA KIFO CHA NEEMA B. KIPENYA (26) ALIPOTELEZA NA KUKAMATA NYAYA HIZO KISHA KUFARIKI PAPO HAPO.
 KATI YA NGUZO HADI NGUZO NI UMBALI WA ZAIDI YA MITA 75 MAHALI AMBAPO PALIPASWA KUWA NA NGUZO TATU LAKINI IKAWEKWA NGUZO MOJA , HALI MTEJA WA ENEO HILO ALIKUWA AMELIPIA NGOZO TATU ZAIDI YA MIAKA MIWILI ILIYOPITA .
 HAPA NDIPO ALIPO TELEZA MAREHEMU NEEMA NA KUANGUKIA NGUZO HIZO
 ASKARI AKIPATA MAELEZO KUTOKA KWA MASHUHUDA 
 MWENYEKITI WA KIJIJI CHA MSHIKAMANO BWANA KISMAN MWANGOMALE AMBAYE NDIYE MTEJA WA KWANZA KULIPIA TANESCO NGUZO TATU  NA KUFUNGWA NGUZO MOJA , NA AMETOA TAARIFA MARA KADHAA TANESCO NA HATA KUANDIKA BARUA KWA NIABA YA KIJIJI LAKINI HAKUNA UTEKELEZAJI ULIOFANYIKA HADI MADHARA YAMETOKEA NDIPO TANESCO WAMEFIKA.

MMOJA KATI YA WATUMISHI WA TANESCO AMBAYE ALIFIKA ENEO LA TUKIO NA KUKATA UMEME USILETE MADHARA ENEO HILO , HATA HIVYO ALINUSURIKA KUPIGWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI AMBAO WALIKERWA NA TUKIO HILO.

 MWENYEKITI WA KIJIJI CHA MSHIKAMANO WA KWANZA KUSHOTO NA WATUMISHI WA TANESCO WAKIANGALIA NGUZO ZILIZO ELEMEWA NA UZITO WA NYAYA HIZO NA KUSABABISHA NGUZO KUSHINDWA KUHIMILI UZITO WA NYAYA HIZO. 
 WAOMBOLEZAJI WAKILIA KWA UCHUNGU KWANI MUDA MFUPI ULIOPITA WALIKUWA NA MAREHEMU NYUMBANI HAPO.
 MOJA KATI YA NDUGU AMBAYE ALIZIRAI KATIKA ENEO LA TUKIO
MWILI WA MAREHEMU UKIWA KATIKA CHUMBA CHA MAITI HOSPITALI YA IFISI ILIYOKO WILAYA YA MBEYA UKISUBIRI UCHUNGUZI ZAIDI WA KITABIBU.

PICHA NA EZEKIEL KAMANGA

SHEIKH PONDA ASOMEWA MASHITAKA AKIWA HOSPITALI

Katibu Mkuu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda amesomewa mashitaka ya uchochezi na Mwanasheria wa serikali, akiwa wodini MOI anapoendelea kupata matibabu. Sheikh Ponda arijeruhiwa Jumamosi iliyopita akiwa katika mhadhara wa Kiislamu huko mkoani Morogoro. Baada ya kujeruhiwa Ponda alilazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya kuhamishiwa katika Taasisi ya Mifupa (MOI) aliposomewa mashitaka. Kesi yake itaendelea pindi atakapopata nafuu.

UCHAGUZI TFF SASA KUFANYIKA OKTOBA 18, USAJILI KUPITIWA IJUMAA


Na Boniface Wambura
KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetoa tangazo la uchaguzi wa Kamati ya mpya ya Utendaji ambao utafanyika Oktoba 20 mwaka huu. Pia Kamati hiyo imetoa tangazo za uchaguzi wa Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania (TPL Board) ambao utafanyika Oktoba 18 mwaka huu.

Akitangaza mchakato huo wa uchaguzi leo (Agosti 14 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Hamidu Mbwezeleni amesema nafasi zitakazogombewa kwa upande wa TFF ni Rais, Makamu wa Rais na wajumbe 13 wa Kamati ya Utendaji wakiwakilisha kanda mbalimbali.

Fomu kwa wagombea zitatolewa kuanzia Agosti 16 mwaka huu kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 kamili jioni kwenye ofizi za TFF. Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Agosti 20 mwaka huu. Fomu kwa nafasi ya Rais ni sh. 500,000, Makamu wa Rais ni sh. 300,000 wakati wajumbe ni sh. 200,000.

Mbwezeleni amesema kwa wale ambao walilipia fomu katika mchakato uliofutwa na wanakusudia kugombea nafasi zilezile walizolipia, hawatalipia tena ada ya fomu husika bali watatakiwa kuambatanisha risiti za malipo wakati wa kurudisha fomu za maombi hayo ili kuthibitisha malipo yao.

Kwa upande wa uchaguzi wa TPL Board, fomu zitaanza kutolewa Agosti 16 hadi 20 mwaka huu, na nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti ambapo ada ni sh. 200,000 wakati wajumbe wa Bodi ada ni sh. 100,000.

KAMATI YA SHERIA SASA KUPITIA USAJILI IJUMAA
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji iliyokuwa ikutane jana (Agosti 13 mwaka huu) na leo (Agosti 14 mwaka huu) kupitia usajili wa wachezaji kwa klabu za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza sasa itakutana keshokutwa (Agosti 16 mwaka huu) saa 4 asubuhi.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Alex Mgongolwa amepanga tarehe hiyo mpya baada ya kikao cha jana kushindwa kupata akidi. Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ina wajumbe saba, na ili kikao kiweze kufanyika ni lazima wapatikane wajumbe kuanzia wanne.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Tuesday, August 13, 2013

Rais Kikwete akutana na vijana wachoraji walioacha kutumia dawa kulevya


 Kijana Jimmy Changchuu alieachana na matumizi ya dawa za kulevya akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete picha aliyochora yeye na kijana mwenzake wakati vijana hao walimpomtembelea Rais Ikulu jijini Dar es Salaam leo.Vijana hao wanalelewa katika kituo cha Pilli Missanah Foundation kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam.
 Vijana walioachana na Matumizi ya dawa za kulevya kutoka katika kituo cha Pilli Missanah Foundation kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo.Kulia pembeni ya Rais ni Mwanzilish Kituo hicho Bi.Pilli Missanah na watatu kushoto ni mfadhili mkuu wa kituo hicho Bwana Zacharia Hans Poppe. Picha na Freddy Maro
Picha ya pamoja.

Kumekucha Redd's Miss Ilala 2013, kivumbi kufanyika Ijumaa hii

 Warembo wanaotarajia kushiriki Redd's Miss Ilala, wakiwa wamepozi wakati wa mazoezi kwenye Mgahawa wa Billicanas, Dar es Salaam, tayari kwa mashindano yatakayofanyika Ijumaa kwenye Ukumbi wa Golden Jubilee jijini.
 Warembo wanaotarajia kushiriki Redd's Miss Ilala, wakiwa wamepozi wakati wa mazoezi kwenye Mgahawa wa Billicanas, Dar es Salaam, tayari kwa mashindano yatakayofanyika Ijumaa kwenye Ukumbi wa Golden Jubilee jijini
 Warembo wakiwa katika moja ya miondoko wakati wamazoezi
 Mwalimu wa warembo hao, Akhsas Peter akiwapanga vizuri kabla ya kupigwa picha na wandishi wa habari.
 Warembo wakipita Mtaa wa Makunganya katikati ya Jiji la Dar es Salaam, wakitokea mazoezini katika Mgahawa wa Billicanas.
 Mwandishi Mwandamizi wa Habari za Michezo wa gazeti la Jambo Leo, Asha Kigundula (kulia), akitoa maelezo kuhusu kazi za kila siku za waandishi wa habari kwa warembo wa wanaotarajia kushiriki mashindano ya Redd,s Miss Ilala walipotembelea chumba cha habari cha Jambo Leo
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concepts Tanzania Limited (JCTL), Juma Pinto (aliyekaa kulia), akizungumza na warembo hao waliomtembelea ofisini kwake, Dar es Salaam. Aliyekaa katikati ni Mratibu wa mashindano hayo, Juma Mabakila. JCPL ni wachapishaji wa magazeti ya Jambo Leo, Staa Spoti, Dar Metro na jarida la Jambo Brand Tanzania.

Mchakato wa Uchaguzi Mkuu TFF kuweka hadharani kesho


MCHAKATO wa uchaguzi wa kamati mpya ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unatarajiwa kutangazwa kesho (Agosti 13 mwaka huu).
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Hamidu Mbwezeleni atakutana na Waaandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF saa 6 kamili mchana ambapo mbali ya mchakato utakavyokuwa anatarajia kutangaza tarehe mpya ya uchaguzi huo ambao awali ulitarajiwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu.
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilikutana Jumapili (Agosti 11 mwaka huu) na inatarajia kuwa na kikao kingine leo (Agosti 12 mwaka huu) ambapo pamoja na mambo mengine itazungumzia maandalizi ya uchaguzi huo.
Mbali ya Mbwezeleni, wajumbe wengine wa Kamati hiyo ni Moses Karuwa (Makamu Mwenyekiti), Mohamed Sinani, Chabanga Dyamwale na Kitwana Manara.
MAGORI, LINA WAINGIA KAMATI ZA CAF
Watanzania Crescentius Magori na Lina Kessy wameteuliwa kuwa wajumbe kwenye kamati ndogondogo (standing committees) mpya za Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) zilizotangazwa juzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Hicham El Amrani.
Magori na Lina ambao ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF watakuwa kwenye kamati hizo kwa kipindi cha miaka miwili (2013-2015). Magori ameteuliwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Mpira wa Miguu wa Ufukweni (Beach Soccer) wakati Lina ameingia kwenye Kamati ya Maandalizi ya Mpira wa Miguu kwa Wanawake.
Makamu wa Rais wa TFF, Athuman Nyamlani ameteuliwa tena kuwemo kwenye Bodi ya Rufani ya CAF yenye wajumbe 12 kwa kipindi kingine cha miaka miwili. Nyamlani alikuwepo kwenye bodi iliyopita, na itaendelea kuwa chini ya uenyekiti wa Prosper Abega kutoka Cameroon.
Rais wa TFF, Leodegar Tenga ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya CAF yuko kwenye kamati tano za Shirikisho hilo. Kamati hizo ni Kamati ya Fedha ambayo ni Makamu Mwenyekiti na Kamati ya Maandalizi ya Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).
Kamati nyingine ni Kamati ya Masoko na Televisheni ambayo ni Mwenyekiti, Kamati ya Ufundi na Maendeleo, na Kamati ya Ushauri na Vyama Wanachama wa CAF.
KAMATI YA SHERIA KUPITIA USAJILI
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa inakutana leo jioni (Agosti 13 mwaka huu) na kesho (Agosti 14 mwaka huu) kupitia na kufanyia uamuzi usajili wa wachezaji wenye matatizo.
Hatua ya kwanza ya usajili imeshamalizika wakati hatua ya pili ya usajili inaanza kesho (Agosti 14 mwaka huu) ikihusisha wachezaji ambao watakuwa hawajasajiliwa katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu na wale kutoka nje ya Tanzania.
Hivyo, dirisha la uhamisho kwa wachezaji wa kimataifa litafungwa baada ya hatua ya pili ya usajili kumalizika Agosti 29 mwaka huu.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

CHADEMA yalaani tukio la kupigwa risasi kwa Sheikh Ponda


 
CHAMA cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimeungana na vyama na asasi nyingine kulaani vikali tukio la kupigwa kwa risasi na Polisi kwa Katibu wa Jumuiya ya Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda.
CHADEMA imelaani tukio hilo katika tamko lake iliyolitoa leo kupitia Mjumbe wake wa Kamati Kuu, Prof  Abdallah Safari.

Kagera Sugar yamaliza ziara Uganda kwa kipigo


BAADA ya jana kuinyuka Bunawaya ya Uganda katika mechi zake za kirafiki za kimataifa za kujiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bar, timu ya Kagera Sugar jioni ya leo imemaliza mechi zake nchini humo kwa kucharazwa bao 1-0 na Watoza Ushuru wa URA.
Kagera itakayofungua dimba la ligi kuu Agosti 24 dhidi ya Mbeya City, jana iliitafuna Bunawaya kwa bao 1-0 ikiwa ni mechi yao ya pili baada ya ile ya awali kulazimishwa 0-0, leo ilishindwa kuendeleza ubabe kwa URA ambao waliifunga Simba na kutoka sare ya 2-2 na Yanga kabla ya kulala kwa Coastal Union ilipokuwa nchini Tanzania mwezi uliopita.
Hata hivyo kocha msaidizi wa Kagera, Mrage Kabange amesema wanashukuru mechi hizo zimewasaidia kujiweka vyema na kuwaandaa vizuri wachezaji wao kabla ya kuanza kipute cha ligi msimu mpya.
Msimu uliopita Kagara Sugar ikiwa chini ya kocha King Abdallah Kibadeni, ilimaliza ligi ikiwa nafasi ya nne, ikitanguliwa na vigogo, Yanga, Azam na Simba zilizokuwa kwenye Tatu Bora.

Ashanti wawafuata mabingwa wa Kagame Bunjumbura


KIKOSI cha timu ya Ashanti inaatarajiwa kuondoka mjini Kigoma kesho kuelekea Burundi kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki za kimataifa dhidi ya wenyeji wao, ili kujiandaa na pambano lao la fungua dimba kati yao na Yanga.
Ashanti iliyorejea Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu baada ya awali kushuka mwaka 2007 itapepetana na Yanga Agosti 24 katika moja ya mechi za fungua dimba, mchezo utakaochezwa katika uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Timu huyo ilikimbilia Kigoma kuweka kambi na kesho itaavuka mpaka kuelekea katika mji wa Makamba kuumana na timu ya Daraja la Kwanza nchini Burundi iitwayo Makamba.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Kigoma ni kwamba mechi hiyo itachezwa keshokutwa mjini humo kabla ya Ashanti United kusogea mbele hadi Bunjmbura mwishoni mwa wiki na kuvaana na Mabingwa wa Kombe la Kagame 2013, Vital'O.
Kocha wa timu hiyo Mbaraka Hassain anaamini mechi hizo zitawasaidia kuwaweka vyema kabla ya kuwavaa Yanga ambao Jumamosi itajitupa uwanja wa Taifa kupapatana na Azam katika pambano la Ngao ya Hisani litakalochezwa uwanja wa Taifa.
Azama waliokuwa Afrika Kusini kwa ajili ya kambi yao ya mazoezi na kucheza mechi nne za kirafiki na kushinda moja na kupoteza tatu, imetua leo mchana na tayari imejichimbia katika kambi yao iliyopo Chamazi, nje ya jijini tayari kuwasubiri Yanga Jumamosi.

Haya ndiyo majina ya wanaodaiwa wauza Unga na Bangi nchini



Majina ya watanzania 255 wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya   yamejulikana  na  JAMHURI  imeamua kuyachapisha...
 
Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa kwenye orodha hiyo wapo watu maarufu na baadhi wamekuwa wakitoa misaada ,huku wengine wakijifanya ni wazee  wa kanisa na kushiriki  shughuli mbalimbali za kijamii....
 
Uchunguzi wetu usio na chembe ya shaka  unaonesha kuwa orodha hii ya watu watakaoandikwa hapo chini kwa sasa wapo chini ya uangalizi wa mahakama na polisi..
 
"Ni kweli kuna watu tumewapeleka mahakamani, huko wamewekwa chini ya uangalizi na wanatakiwa kuripoti  kwa  muda wanaopangiwa.Tunafanya hivyo baada ya uchunguzi wetu kubaini kwa ni kweli  wanahusika na biashara hii haramu."Alisema  Nzowa
Nzowa aligoma kuyataja majina hayo, lakini uchunguzi uliofanywa na JAMHURI  kutoka ndani ya jeshi la polisi na  mahakama  umefanikiwa  kuyapata  majina  hayo...
Katika orodha hii, yumo mchungaji aliwekwa chini ya uangalizi , na baada ya kumaliza muda huo, siku tatu baadaye alikamatwa na  dawa nchini Brazil.Pia yumo Sheikh anayetoa misaada mbalimbali,lakini baada ya kukamatwa na dawa kilo 211, eneo la Kunduchi Dar es salaam, kwa sasa  amekimbilia  Afrika kusini....
DAWA ZINAVYOINGIZWA NCHINI:
Hadi sasa kiwango kikubwa cha dawa za kulevya kinaingizwa nchini kwa njia ya meli katika bahari ya Hindi.
Baada ya meli kuwasili Tanzania, wasafirishaji hutumia boti ndogo ziendazo kasi kuchukua dawa hizo.Maeneo yanayotumiwa zaidi kuingiza dawa ni Bagamoyo, Zanzibar, Tanga na Mtwara....
Jijini Dar, boti hizo hutia nanga  katika eneo la  Bagamoyo ambako pia ndiko kwenye njia kuu ya uingizaji  wa bidhaa za magendo  zisizolipiwa kodi...
Biashara  hiyo  haramu  huwahusisha  baadhi  ya  polisi  ambao  mara  kadhaa  wamekuwa  wakiwapa  ulinzi   wahalifu  hao.
Viwanja  vya  ndege   vinavyotumiwa  kuingiza  madawa  ya  kulevya  ni  Julius  Nyerere ( DAR )  na  Abeid  Amani  Karume ( ZANZIBAR)
Taarifa  toka  kitengo  cha  kuzuia  dawa  za  kulevya   zinasema  kuwa  wasafirisha  wanaotumia  ndege  wamekuwa  wakibuni  mbinu  mbali  mbali  zikiwemo  za  kutumia  manukato  kwa  ajili  ya  kuwapumbaza mbwa  wenye  mafunzo  ya  kubaini  madawa  ya  kulevya....
Habari zaidi  zinasema  kuwa  kitengo  kimepata  vifaa  maalumu    vya  kubaini  kama  ndani  ya  mizigo  kuna  madawa  ya  kulevya. Vifaa  hivyo  ni  mfano  wa  sindano  ambayo  huchomwa  kwenye  mizigo  na  kuipitisha  kwenye  ngozi  ya  mwili.
Kama  kuna  dawa, ikigusishwa  kwenye  ngozi  unga  hupukutika  na  kama  mzigo  hauna  dawa  za  kulevya  basi  hakuna  kitakachotokea....
Tayari  vifaa  hivyo  vimeanza  kutumika  katika  uwanja  wa  kimataifa wa  Julius  Nyerere.
Lisake gazeti la Jamhuri utaiona orodha nzima ya majina hayo 250.
 
Source: Gazeti la Jamhuri.

Monday, August 12, 2013

Sheikh Ponda chini ya Ulinzi mkali wa Polisi, MOI

Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda akiwa amelazwa kwenye chumba maalumu katika taasisi ya mifupa Muhimbili (MOI), muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini hapojana. Picha na Venance Nestory.


KATIBU wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda yupo chini ya ulinzi huku akitibiwa majeraha katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Sheikh Ponda alisafirishwa usiku wa manane kutoka Morogoro baada ya juzi kupigwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni mtutu wa bomu saa 12:25 jioni alipokuwa akisind
ikizwa na wafuasi wake kwenda katika Msikiti wa Mungu Mmoja Dini Moja mara baada ya kumaliza kutoa mhadhara katika kongamano mjini hapo.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kongamano hilo, Sheikh Idd Mussa Msema, alidai kuwa Sheikh Ponda alipigwa risasi tatu begani.
Taarifa kutoka ndani ya familia ya Ponda zilisema kwamba baada ya kupata taarifa za kupigwa risasi, baadhi ya masheikh walifunga safari kwenda Morogoro na kumrejesha Dar es Salaam usiku huo huo. Kabla ya kurudishwa Dar es Salaam, imeelezwa kuwa Sheikh Ponda alipelekwa katika Zahanati ya Islamic Foundation.
Mmoja wa wanafamilia alidokeza kwamba Sheikh Ponda alifichwa na alikuwa chini ya ulinzi mkali wa wafuasi wake na hakuna aliyeruhusiwa kumsogelea.
Muhimbili
Hata hivyo, habari zilizopatikana baadaye jana zilisema kuwa alifikishwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Sheikh Ponda alifikishwa Muhimbili jana saa 7:18 mchana na alipelekwa kwenye chumba cha wagonjwa wa dharura na baadaye alitolewa na kupelekwa kwenye chumba cha x-ray kwa ajili ya vipimo. Baadaye alipelekwa chumba cha upasuaji.
Eneo kubwa la hospitali hiyo lilikuwa na idadi kubwa ya askari na mmoja wa askari waliokuwa doria hospitalini hapo alisema walitawanywa kwenye hospitali mbalimbali za Dar es Salaam baada ya kupata taarifa kuwa angeletwa kwa matibabu.
“Nakuambia tuko hapa tangu saa kumi na moja asubuhi, tumetawanywa hospitali mbalimbali baada ya kupata taarifa kuwa analetwa Dar. Bahati nzuri kaletwa hapa Muhimbili... tunasubiri apate matibabu na tutamtia mbaroni,” alisema askari huyo.
Taarifa ya polisi
Msemaji wa Polisi, Advera Senso alisema jana katika taarifa yake kuwa Sheikh Ponda yuko Hospitali ya Muhimbili akitibiwa baada ya kupata majeraha yaliyotokana na purukushani na polisi wakati wafuasi wake walipokuwa wanataka kumtorosha. 
 
MWANANCHI.

Njemba yafia gesti ikifanya mapenzi na demu wake


MFANYABIASHARA wa sokoni Kariakoo jijini Dar ambaye pia ni mkazi wa Kigogo Flesh, Hamad Kiponda (46), amefia nyumba ya kulala wageni akiwa na mpenzi wake Latifa Saidi (25).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi alisema tukio hilo lilitokea juzi saa saba mchana katika nyumba hiyo iitwayo Sansiro iliyoko Kiwalani kwa Gude.

Alisema kuwa kutokana na tukio hilo, Latifa alitoa taarifa polisi kwamba mpenzi wake aliishiwa na nguvu ghafla na kuanza kutokwa povu mdomoni wakati wakifanya mapenzi.

Minangi alieleza kuwa mtoa taarifa huyo aliomba msaada kwa wahudumu wa gesti hiyo, lakini Kiponda alifariki papo hapo kabla ya kupelekwa hospitali.

Chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika, wakati mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi huku Latifa akishikiliwa kwa kuhojiwa.

Wakati huo huo, moto umezuka ghafla katika nyumba ya Matiku Nestori (43) mkazi wa Tuamoyo Kigamboni, yenye vyumba sita na kuteketeza vyumba vinne pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani ambazo bado thamani yake haijajulikana.
Kwa mujibu wa Kamanda Minangi tukio hilo lilitokea juzi saa nane mchana na chanzo cha moto huo inasadikiwa ni hitilafu ya umeme iliyosababisha moto kuanzia kwenye nguzo.

Tanzania One 

Papii Catalogue sasa aamua kuwatetea wanawake

Catalogue akizungumza kueleza
RAPA mahiri wa bendi ya Extra Bongo, Pappy Catalogue ameibuka na wimbo mpya unawaotetea wanawake dhidi ya vitendo vya ukatili na unyanyasaji kutoka kwa wanaume uliotarajiwa kutambulishwa rasmi kwa mashabiki wakati wa Idd.
Catalogue aliutaja wimbo huo ni  'Mwanamke Hapigwi' ambao una mashairi unaohimiza wanaume kuacha kutumia ubabe kwa wanawake kama kuwapiga, kuwanyanyasa na kuwaona hawana maana kwa sababu wanawake wanahitaji kutunzwa na kubembelezwa na kama kupigwa basi hupigwa kwa upande wa khanga.
Rapa na muimbaji huyo alisema wimbo huo ameutunga maalum katika kuwapigania wanawake katika zama hizi za matukio ya unyanyasaji dhidi yao hasa majumbani na katika mapenzi.
Catalogue alisema wanaume wamekuwa na desturi ya kuwapiga na kuwanyanyasa wanawake na wapenzi wao na ikitokea wanawake hao wakachoka na kuamua kuwakimbia kwa wanaume wengine wanaojua kuibembeleza wanaume wa awali huona kama wameonewa na kuanzisha songombingo.
"Huu ni wimbo maalum kwa ajili ya kutetea wanawake ni utatambulishwa sambamba na rapu mpya iitwayo 'Utaishije mjini bila ya kazi'," alisema.
Katika hatua nyingine dansa kiongozi wa bendi hiyo, Hassain Mussa 'Super Nyamwela' ametamba kuwa ujio wa wanenguaji wawili wapya kutoka Kongo, Jolie Kindu 'Mrisho Ngassa' na Grace Kamba 'John Bocco' kutazidi kuipaisha bendi yao huku akiwapiga vijembe wapinzani wao kuwa wataishia 'kukopi na kupesti'.
Nyamwela alisema ukali walionao madansa hao wa kike utaiweka kileleni Extra Bongo na kuthibitisha kuwa wao siku zote ni wa kwanza katika safu ya unenguaji kwa sababu wapo chini ya mwalimu asiyechuja (yaani yeye Nyamwela).