STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 15, 2013

EID MUBARAKA WASOMAJI WOTE WA MICHARAZO MITUPU




BLOGU HII INAWATAKIA EID MUBARAKA WAUMINI WOTE WA KIISLAM NA WATANZANIA KWA UJUMLA AMBAO WANAISHEREHEKEA SIKUKUU HIYO LEO, BAADA YA JANA KUFUNGA ARAFA KUWAUNGA MKONO MAHUJAJI WALIOKUWA KATIKA KISIMAMO CHA ARAFA KATIKA HIJJA YAO.

JAMBO LA MUHIMU TUNAWAKUMBUSHA WAUMINI HAO WAISHEREHEKEE SIKUKUU HIYO BILA KUMUASI MUNGU KADHALIKA KUBWA KWA VIONGOZI WA DINI HIYO HASA WA TANZANIA WAMCHE MUNGU NA WAKUMBUKE WAO NI WACHUNGA NA WATAKUJA KUULIZWA KWA KILE WALICHOKICHUNGA.
TUNAMAANISHA WAMCHE MUNGU NA KUFANYA YALE YALIYO KATIKA MUONGOZO WA ALLAH (SW) NA MAFUNDISHO YA MTUME MUHAMMAD (SAW) BADALA YA UTASHI WA NAFSI ZAO NA KUIKUMBATIA DUNIA KIASI CHA KUWAYUMBISHA WAUMINI WAO. KADHALIKA WAUMINI WAKUMBUKE UISLAM NI MWEPESI ILA UNATIWA UGUMU NA WAO WENYEWE KWA KUTOPENDA KUJIFUNZA NA KUISHIA KUBURUZWA. 
WASWAHILI WA MSEMO WAO KUWA, KAMA KUSOMA HUJUI BASI  HATA PICHA UNASHINDWA KUITAMBUA? ALLAH SW ATUZINDUE...! MAHUJAJI JANA WALIONEKANA 'LIVE" WAKIWA WAMESIMAMA ARAFA JE, FUNGA INAYOFUNGWA LEO NI YA NINI WAKATI MAHUJAJI LEO WANACHINJA?! ALLAH SW ATUPE TAHFIF NA KUTUZINDUA!

Monday, October 14, 2013

Mashauzi kutambulisha mpya Da West Tabata

 
Isha Mashauzi
KUNDI la muziki wa taarab ya Mashauzi Classic inatarajiwa kutambulisha nyimbo zao mpya kwenye onyesho maalum ya kusherehekea sikukuu ya Idd el Hajj katika ukumbi wa Dar West Park, Tabata.
Onyesho hilo ambalo linajulikana kama ‘Usiku wa Isha Mashauzi’, imeandaliwa na Keen Arts na  Bob Entertainment chini ya udhamini wa kinywaji cha Konyagi, Straika, Kwetu Mbambabay  na Saluti5.
Mratibu wa onyesho hilo, Joseph Kapinga amesema kuwa onyesho litakuwa la kipekee na maalum kwa kusherehekea sikukuu ya Idd El Hajj.
Amesema katika onyesho hilo, Mashauzi atatambulisha albamu yake mpya ijulikanayo kama “Asiyekujua Hakuthamini” ambayo ina nyimbo kama “Mimi Bonge la Bwana,” utunzi wake Hashim Said, “Ropokeni Yanayoyahusu” ( Saida Ramadhani) na “Haya ni Mapenzi Tu” (Zubeda Malik).
Zawadi mbalimabli zitatolewa kwa mashabiki wa bendi hiyo inayojulikana kama Wakali wa Kujiachia.
“Tumeandaa zawadi mbalimbali kwa mashabiki wetu. Pia bendi ya Mashauzi Classic watatumia onyesho hilo kutambulisha nyimbo zao mpya,” Kapinga alisema.
“Mashauzi Classic watapiga albamu zao zote. Matumaini yetu ni kuwa watu watapata burudani ya kutosha kuliko siku zingine zote,” alisema Kapinga.
Nyimbo zingine zitakazopigwa ni  “Viwavijeshi” (Issa Ramadhani), “Sitasahau Yaliyonikuta” (Abdul Malik), “La Mungu Halima Mwamuzi” (Zubeda Malik) na “Sijamuona Kati Yenu” (Rukia Juma).
Naye mkurugenzi wa bendi hiyo, Isha Mashauzi, alisema kuwa onyesho la Da West litakuwa la kihistoria na kutaka watu wajitokeze kwa wingi ili historia isiwapite.
“Kwa kweli bendi iko fiti,” alisema Mashauzi.

Linnah Kessy kusimamia Kombe la Dunia

Linna Kessy
 SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Mtanzania Lina Kessy kuwa kamishna wa mechi ya Kombe la Dunia Kanda ya Afrika kwa wanawake chini ya umri wa miaka 20 kati ya Botswana na Afrika Kusini.

Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza itachezwa nchini Botswana kati ya Oktoba 25 na 27 mwaka huu. Waamuzi kutoka Zimbabwe ndiyo watakaochezesha mechi hiyo namba tisa.

Waamuzi hao wataongozwa na Pamela Majo atakayepuliza filimbi wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Rudo Nhananga, namba mbili ni Stellah Ruvinga na mezani atakuwepo Tambudzi Tavengwa.

Kituo cha IDYDCC chafunguliwa Iringa



Na Boniface Wambura
KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Juma Ali Amir amefungua kituo cha kwanza cha Football for Hope kilicho mkoani Iringa kwa kuwataka wananchi kukituia vizuri ili wanufaike na huruma za kijamii zinazotolewa na taasisi ya IDYDC pamoja na kuendeleza mpira wa miguu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo hicho jana (Oktoba 13 mwaka huu), kiongozi huyo amesema taasisi ya IDYDC (Iringa Development of Youth, Disabled and Child Care) wamefanya vizuri kuamua kutumia mpira wa miguu kusaidia jamii kwa kuelimisha juu ya mambo mbalimbali kama ugonjwa wa ukimwi, kusaidia walemavu, haki za watoto na afya ya jamii.
Naye Mwakilishi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Patrick Onyango amesema amefurahishwa na kukamilika kwa kituo ambacho kitasaidia jamii.
Amesema idadi kubwa ya watu waliofika kwenye uzinduzi huo inadhihirisha ni kiasi gani kituo hicho kitakuwa na matokeo mazuri kwa jamii.
Onyango alisema hicho ni kituo cha 14 kukamilika kati ya 20 vinavyojengwa barani Afrika ikiwa ni mpango wa FIFA kurudisha kwa jamii mafanikio iliyopata kwenye fainali za kwanza za Kombe la Dunia barani Afrika.

Kituo hicho kina uwanja mdogo wa mita 20 kwa 40 uliowekwa nyasi bandia, jengo lenye ukumbi wa mikutano kwa ajili ya semina, chumba cha kupimia ukimwi, chumba cha ushauri nasaha, maktaba na ofisi.
Zaidi ya dola 270,000 za Marekani zimetumika kukamilisha ujenzi wa kituo hicho kilicho eneo la Mtwivila, Iringa mjini.

Kamati ya Rufaa ya Maadili yafanya mapitio

Na Boniface Wambura
KAMATI ya Rufani ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana jana (Oktoba 13 mwaka huu) kusikiliza maombi ya mapitio (revision) na mwongozo ya uamuzi wa Kamati ya Maadili.

Sekretarieti ya TFF iliwasilisha maombi ya mapitio kwa Kamati hiyo ya juu kabisa ya masuala ya maadili kutokana na ugumu wa utekelezaji wa uamuzi wa Kamati ya Maadili juu ya mashauri nane yaliyowasilishwa mbele yake.

Kamati ya Rufani ya Maadili itaendelea na kikao chake kesho (Oktoba 15 mwaka huu), na baadaye itakutana na waandishi wa habari (saa 10 jioni) kwa ajili ya kutangaza uamuzi wake juu ya mwongozo ulioombwa na Sekretarieti ya TFF.

Sunday, October 13, 2013

Azam yaiengua Yanga, Mbeya City moto chini, Mtibwa yaua, Abdalla Juma apiga Hat Trick, Maguri naye kama kawa

Mbeya City

Azam Fc
MABINGWA watetezi Yanga imeenguliwa kwenye  nafasi ya pili na kuporomoka hadi nafasi ya nne kufuatia jioni hii timu za Azam na Mbeya City kupata ushindi katika mechi zao za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Azam iliisasambua JKT Ruvu kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa Chamazi, huku Mbeya City wakipata pointi tatu katika uwanja wa Mkwakwani kwa kuizabua Mgambo JKT kwa bao 1-0.
Ushindi wa timu hizo umezifanya Azam kurejea kwenye nafasi ya pili ikiwa na pointi 17 sawa na za Mbeya City inayokamata nafasi ya tatu ila inawazidi uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Azam ilipata ushindi wake kwa mabao ya Humphrey Mieno katika dakika 12 kabla ya Erasto Nyoni kufunga bao la pili kwa kichwa dakika ya 32 mabao yhaliyodumu hadi kipindi cha kwanza kilipoisha.
Bao la tatu lililowanyong'onyesha JKT lilifungwa na kiungo Salum Abubakar Sure Boy dakika ya 90.
Katika mechi nyingine zilizochezwa leo, Elias Maguri aliendeleza kasi yake ya kufumania nyavu baada ya kuifungia Ruvu Shooting bao pekee katika pambano lao dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi.
Maguri alifunga bao hilo kwa mkwaju wa penati baada ya Aypoub Kitala kurangushwa kwenye lango la Rhino na mfungaji huyo kufunga penati. Hata hivyo Ruvu ilipata pigo baada ya kiungo wake Juma Seif 'Kijiko' kulimwa kadi nyekundu.
Nayo Mtibwa Sugar ikiwa kwenye uwanja wa Manungu iliisambaratisha Oljoro JKT kwa kuifunga mabao 5-2, huku Abdsalla Juma akitupia kimiani mabaop matatu (hat Trick) na kuweka rekodi.
Maao mengi ya Mtibwa yalifungwa na Juma Luizio na kumfanya afikishe jumla ya mabao matano mpaka sasa.
Mabao ya kufutia machozi ya Oljoro yalifungwa na Saidi Nayoka na Amir Omar.

MECHI YA SIMBA, PRISONS YAINGIZA MIL 60/-

Na Boniface Wambura
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya wenyeji Simba na Tanzania Prisons kutoka Mbeya iliyochezwa jana (Oktoba 12 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 60,521,000.

Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 katika mechi hiyo namba 55 na kushuhudiwa na watazamaji 10,494 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

Kila klabu ilipata mgawo wa sh. 14,191,002.55 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,232,016.95.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,215,763.96, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,329,458.37, Kamati ya Ligi sh. 4,329,458.37, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,164,729.19 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,683,678.26.

Mbunge Kigamboni ateta na wapiga kura wake


MBUNGE wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndugulile akihutubia wananchi wa Kijichi wakati wa ziara yake ya kuelezea utekelezaji wa ilani ya chama chake cha CCM katika kipindi cha uongozi wake. Pia alipata nafasi ya kupokea kero mbalimbali za wananchi.

Mauaji!: Mtangazaj ITV/Radio One apigwa risasi, ampoteza mama mzazi

Ufoo Saro (kulia) aliyepatwa na mkasa hivi punde
HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema mtangazaji wa kituo cha ITV, Ufoo Saro amejeruhiwa vibaya kwa risasi, huku mama yake mzazi akipoteza maisha baada ya mtu anayedakiwa kuwa mchumba wake au mumewe kuwafyatulia risasi katika ugomvi wa kimapenzi.

Taarifa zinasema kuwa mchumba wa mtangazaji huyo aliyetajwa kwa jina la Ansel aliyekuwa nchini Sudan kikazi alitua nchini jana na kufikia kwa Ufoo lakini kukatokea mzozo ambao haukupata suluhisho.

Hivyo wawili hao waliongozana hadi kwa mama wa mtangazaji huyo kutafuta suluhu, asubuhi hii na kwa bahati mbaya hali ilikuwa tete na ndipo kijana huyo alipotoa bastola aliyokuwa nayo na kumtwanga mama mtu risasi ya kichwa iliyomuua papo hapo.

Kama hiyo haikutosha inaelezwa jamaa huyo alimtwanga risasi Ufoo kifuani na nyingine mguuni na kudhani amemuua kabla ya yeye mwenyewe kujilipua mwenyewe kwa risasi ya kidevuni na kumuua.

Tayari miili ya watu hao wawili yaani mama yake Ufoo na jamaa huyo imepelekwa Muhimbili sambamba na mtangazaji huyo anayeelezwa yupo katika hali mbaya kwa ajili ya kuhifadhiwa na matibabu zaidi.

Haifahamiki chanzo cha mauaji hayo licha ya kudaiwa huenda ni ugomvi wa kimapenzi na haifahamiki jamaa huyo huko Sudan anakodaiwa kuwa alikuwa akifanya kazi UN alikuwa kama nani japo inaelezwa huenda alikuwa mwanajeshi ambapo kabla ya kwenda huko aliwahi kuwa mpiga picha wa ITV na kufanya kazi Mahakama ya Kimataifa ya Arusha kabla ya kuomba kazi UN.
MICHARAZO inaendelea kufuatia kwa kina taarifa hii na itawafahamisha. Pia inamuombea kila la heri na salama mtangazaji huyo aweze kupona katika mkasa uliopata na kumpoa pole kwa msiba uliompata kwa kumpoteza mama yake mzazi.

Drogba aibeba Ivory Coast, waifyatua Senegal 3-1 WCQ

drog
MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya taifa Ivory Coast, Didier Drogba alirejea kwa kishindo katika timu hiyo baada ya kuiongoza kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Senegal katika pambano la kwanza la mtoano wa kuwania nafasi tano za kutinga Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.
Drogba aliitwa tena katika kikosi hicho baada ya awali kuwekwa kando na kusaidia kufunga bao la penati kabla ya Solomon Kalou kufunga la tatu huku la pili wageni wao wakijifunga wenyewe.
Ivory Coast 'The Elephants' sasa imeingia mguu mmoja ndani kwenye fainali hizo za Kombe la Dunia ikihitaji sare yoyote katika mechi ya marudiano baadaye kukihakikisha kucheza fainali hizo kubwa duniani.
Mlinzi wa Senegal Ludovic Sane aliizawadia wenyeji bao kabla ya Kalou kufunga bao la tatu na dakika za lala salama Papiss Demba Cisse aliifungia Senegal bao la kufutia machozi ambalo linaweza kuwa msaada kama Senegal itaenda kushinda nyumbani mabao 2-0 katika mechi ya marudiano. Katika pambano jingine Burkina Faso wakiwa kwenye uwanja wao wa Agosti 4 waliwafunga Algeria 3-2 katika mchezo uliokuwa na upinzani wa aina yake .
Mabao ya Burkinabe yalifungwa na Jonathan Pitroipa , Aristide Bance na Djakaridja Kone huku Algeria wakifunga kupitia kwa Soufiane Feghouli na Carl Medjani. Bukinabe sasa wanahitaji sare yoyote katika mechi ya marudiano itakayofanyika ugenini kufuzu fainali hizo ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwao.
Michezo hiyo ya kuwania fainali hizo za Kombe la Dunia hatua ya mwisho kwa nchi za Afrika zitaendelea tena leo kwa mabingwa wa Afrika Nigeria kuwa ugenini mjini Addis Ababa kupepetana na wenyeji wao Ethiopia, wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) huku timu iliyopenya baada ya Cape Verde kuenguliwa kwa udanganyifu Tunisia itaialika Cameroon na keshokutwa Jumanne Ghana watakuwa wenyeji wa Misri.

Ashanti United yaona mwezi, yailaza Coastal Union 2-1

 
MABAO mawili yaliyofungwa na Tumba Sued moja likiwa la penati liliisaidia Ashanti United kupata ushindi wake wa kwanza katika Ligi Kuu Tanzania Bara na kujinasua mkiani wakiiachia Mgambo JKT ya Tanga.
Ashanti iliipata ushindi huo kwenye uwanja wa Chamazi kwa kuicharaza Coastal Union ya Tanga mabao 2-1, bao la ushindi likifungwa dakika za jioni na kulalamikiwa na Wagosi wa Kaya.
Tumba Sued beki wa kati mmoja wa wachezaji chipukizi wanaotoka ukoo wa wanasoka kaka zake wakiwa ni Said Swued 'Panucci' na Salum Sued 'Kussi' alifunga bao la kwanza kabla ya Coastal Union kusawazisha kwa mkwaju wa penati kupitia nahodha, Jerry Santo.
Mchezaji huyo mrefu aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nchini China, aliiongezea Ashanti bao la pili dakika za lala salama kwa mkwaju wa penati na kuifanya Ashanti ifikishe pointi 5 sawa na Mgambo JKT, ambayo leo inashuka dimbani kuvaana na Mbeya City mjini Tanga.
Hata hivyo Ashanti wapo juu ikishika nafasi ya 13 kutokana na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa na kuiacha Mgambo ikiburuza mkia kwa sasa.
Matokeo ya mechi za jana pia zilibadilisha msimamo wa ligi kuu ambapo Yanga ilikwea hadi nafasi ya pili ikiwapumulia watani zao watakaovaana nao Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, huku Coastal ikijikuta ikiporomoka kwa nafasi moja hadi nafasi ya nane ikiiachia nafasi Ruvu Shooting ambaye hata hivyo jana haikushuka dimbani kwa leo leo itapepetana na Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Mabatini.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                        P  W  D  L    F  A  GD  PTS

1.  Simba                    8    5   3   0   17  5  12  18
2.  Yanga                    8    4   3   1   15   8   7   15
3.  Azam                     8    3   5   0   11   6   5   14
4.  Mbeya City            8    3   5   0   11   7   4   14
5.  JKT Ruvu              8    4   0   4    9    7   2   12
6.  Kagera Sugar         8    3   2   3    9    7   2   11
7.  Ruvu Shooting        8    3   2   3    9    7   2   11
8.  Coastal Union        8    2    5   1    7    5   2   11
9.  Mtibwa Sugar        8    2    4   2    7    9  -2  10
10.Rhino Rangers        8    1    4   3    8   11 -3   7
11.Prisons                   8    1    4   3    4   10 -6   7
12. Oljoro                   8    1    3   4    6   10 -4    6
13.Ashanti                   8    1    2   5    6   16 -10  5
14.Mgambo                 8    1    2   5     2   13 -11  5

Wafungaji:
8-
Tambwe Amisi (Simba
4-
Didier Kavumbagu (Yanga), Peter Michael (Prisons), Kipre Tchetche (Azam), Elias Maguri (Ruvu Shooting)
3- Jerry Tegete, Hamis Kiiza (Yanga), Haruna Chanongo, Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Themi Felix (Kagera), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Jerry Santo (Coastal Union), Tumba Sued (Ashanti Utd)
2- Haruna Moshi (Coastal Union), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Mwagani Yeya (Mbeya City), Mrisho Ngassa (Yanga), Godfrey Wambura (Kagera Sugar)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla,(Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki, Ramadhani Singano (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku, Kamana Salum, Hussein Abdallah (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris,  John Bocco, Joseph Kimwaga, Faridi Maliki (Azam), Steven Mazanda, Richard Peter, Peter Mapunda (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Shaaban Susan, Jerome Lembeli, Cosmas Ader, Said Dilunga (Ruvu Shooting), Masoud Ally, Shaaban Nditti, Shaaban Kisiga (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu, Paul Maono(OG) (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa, Expedito Kidulo, Nurdin Mohammed, Fikiri Mohammed (Oljoro JKT)

Ratiba za Ligi Kuu

Leo
Ruvu Shooting vs Rhino Rangers (-)
Mgambo JKT vs Mbeya City (-)
Azam vs JKT Ruvu (-)
Mtibwa Sugar vs Oljoro JKT (-)

Okt 16, 2013

Ashanti Utd vs Prisons (-)

Okt 19, 2013

Kagera Sugar vs Coastal Union (-)
Oljoro JKT vs Azam (-)
Mtibwa Sugar vs Mgambo JKT (-)
Mbeya City vs JKT Ruvu (-)
Ashanti Utd vs Ruvu Shooting

Okt 20, 2013
Simba vs Yanga

Saturday, October 12, 2013

Simba yaendelea kung'ang'ania kileleni, Yanga yalipa kisasi Kaitaba


Simba walioshinda jijini Dar
Yanga iliyotakata mjini Bukoba kwa kuilaza Kagera Sugar
BAO la kipindi cha pili lililofungwa na kiungo mkabaji, Jonas Mkude limeiwezesha Simba kuendelea kung'ang'ania kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomaliza raundi ya nane.
Simba ilipata ushindi wa bao 1-0 katika pambano kali lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam dhidi ya maafande wa Magereza, Prisons-Mbeya na kufikisha jumla ya pointi 18.
Kiti cha Simba kilikuwa hatarini siku ya leo iwapo kama ingeteleza na matokeo iliyopata watani zao wa jadi mjini Bukoba, baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji wao Kagera Sugar.
Mkude alifunga bao hilo katika dakika ya 61 na kuiokoa timu yake kugawana pointi na Prisons iliyoonyesha upinzani mkubwa katika pambano hilo.
Bao hilo ambalo ni la tatu kwa Mkude katika orodha ya wafungaji mabao, lilikuwa likusubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Simba ambao dakika 45 za kwanza walikuwa wanyonge na hasa walipokuwa wakipata matokeo ya pambano la mjini Bukoba.
Kwa ushindi huo Simba imesalia kileleni na kufuatiwa na Yanga ambao walipata mabao yake kupitia kwa Mrisho Ngassa aliyefunga kwa kichwa  dakika moja tu baada ya pambano hilo kuanza bao lilidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha kilianza kwa wenyeji Kagera Sugar kusawazisha bao dakika mbili baada ya kuanza kwa kipindi hicho, lakini Yanga ilidhihirisha kuwa ilipania kuilipa kisasi na kufuta unyonge wake mbele ya Kagera kila wanapokutana Kaitaba kwa kuongeza bao la pili.
Mganda Hamis Kiiza 'Diego' alifunga bao hilo katika dakika ya 57, goli linalomfanya afikishe jumla ya mabao matatu mpaka sasa katika ligi ya msimu huu, ikiwa ni wiki moja kabla ya timu yake ya Yanga kukabiliana na Simba katika pambano la watani wa jadi litakalochezwa Okt. 20.
Ushindi huo wa Yanga umeifanya mabingwa watetezi hao kufikisha pointi 15, tatu nyuma ya Simba na iwapo itafanikiwa kushinda katika mechi yao ya Jumapili ijayo, huenda vijana hao wa Jangwani wakakikalia kiti cha uongozi baada ya kuenguliwa walipoyumba katika ligi hiyo.

Golden Bush, Pugu Veterani kuvaana kesho Kinesi

Ticotico (kushoto) katika moja ya mechi zao za maveterani

WAKALI wa soka la maveterani jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani kesho asubuhi inatarajiwa kuvaana na Pugu Veterani katika pambano la kukata na shoka la kirafiki litakalochezwa kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa Golden Bush inayoundwa na wakali za zamani wa Simba na Yanga, mechi hiyo ni ya kumaliza mzizi wa fitina baada ya tambo za muda mrefu, huku wakali hao wa soka la jiji wakiwatisha Pugu kwamba wajiandae kupokea kipigo kikali hiyo kesho.
Taarifa ya Golden Bush kupitia Msemaji na mlezi wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' inasomeka hivi:

Wadau,
 
Kutokana na vipigo vya mfululizo kutoka kwa wapinzani wetu wakiwepo Pugu Veterans, na tambo nyingi kutoka kwa wapinzani wetu hapa jijini, Golden bush tumelazimika kuomba mechi ya kirafiki ya marudiano na Pugu Veterans, game itapigwa uwanja wa Kinesi maarufu kama St James Park siku ya jumapili asubuhi.  Kwakutambua umuhimu ya game hii, uongozi wetu umeitisha kikao cha dharula kesho baada ya mazoezi asubuhi ili kuweka mikakati kabambe ya kurudisha heshima ya timu yetu ambayo mpaka sasa inatambulika kama mabingwa wa jiji la Dar es Salaam. Timu yetu imekamilika kabisa hakuna majeruhi hakuna mgonjwa hakuna mgogoro, uwanja uko sawa kamati ya ufundi inamaalizia kazi yake kwa kushirikiana na Walimu wetu. Tumejiwekea lengo la kufunga magoli mengi iwezekanavyo ili kuvunja rekodi ya kufunga magoli.
 
Aidha ningependa kutoa taarifa kwamba timu yetu imeimarika zaidi  mara baada ya Juma Kaseja, Said Swedi ,Mwarami Mohamed na Shadrack Nsajigwa  kurejea kwenye timu yetu.  karibuni mje muone soka la hali ya juu sana huku likihanikizwa na ufundi wa vijana wa zamani chini ya kocha wetu Madaraka Selemani “Mzee wa kiminyio”
 
Baada ya game ya jumapili, timu itakuwa kwenye maandalizi ya mwisho kabisa kwenda kucheza mechi za kirafiki visiwani Zanzibar.
 
Asanteni kwa kunisikiliza.
Onesmo Waziri “Ticotico” Mchezaji Mwandamizi

Mimi ndiye niyeyaruhusu Rai, Mwananchi-Waziri Makalla

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Amos Makalla 'Mtu wa Watu'
 SIKU moja tu baada ya serikali kuyaonya magazeti ya Mwananchi kwa kukiuka adhabu ya kufungiwa na kuamua kutoa habari kwa njia ya mtandao huku gazeti la Mtanzania, kutumia gazeti la wiki la Rai kuchapishwa kila siku , Naibu Waziri Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Amosi Makala ameibuka na kusema ndiye aliyeyaruhusu kufanya hivyo.

Katika habari iliyochapishwa jana na gazeti moja la kila siku (siyo NIPASHE), lilinukuu agizo la serikali likionya mmiliki wa Mtanzania kuzingatia ratiba ya kutoa gazeti lao kila siku ya Alhamisi, la Rai na mmiliki wa Mwananchi, kuacha kuchapisha gazeti lao katika mtandao kama amri ya kufungiwa ilivyoainishwa.

Hata hivyo, wakati kauli za Waziri na Naibu wake, Makala, zikitofautiana, gazeti la Mwananchi limemaliza adhabu yake jana ya kufungiwa kwa siku 14.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Naibu waziri Makala, alisema yeye ndiye aliruhusu Gazeti la Mwananchi kuendelea na utoaji wa taarifa/habari kwenye tovuti yake, pia Gazeti la Rai kutoka kila siku.

“Ninalazimika kutoa ufafanuzi kwa njia ya maandishi kutokana na kupigiwa simu nyingi na waandishi wa habari kuhusiana na tamko jipya la Mkurugenzi wa Habari – Maelezo, Assah Mwambene kuhoji uhalali wa Gazeti la Mwananchi kuwa online na Gazeti la Rai kutoka kila siku, badala ya mara moja kwa wiki (Alhamisi),” alisema.

Makala alisema Oktoba 4, alifanya mazungumzo na viongozi wa Kampuni ya Mwananchi Communication Ltd (MCL) na New Habari Corporation (2006) Ltd kwa upande mmoja na msajili wa magazeti kwa upande mwingine.

Alisema katika kikao hicho cha pamoja na viongozi wa Magazeti ya Mwananchi na Mtanzania waliomba waziri apitie upya adhabu iliyotolewa kwa magazeti hayo, ambapo yeye (Makala) aliwaambia kwamba mwenye mamlaka juu ya suala hilo ni waziri mwenye dhamana na masuala ya habari pekee.

Kuhusu ombi la Mwananchi kuwa online na Gazeti la Rai kutoka kila siku badala ya kutoka siku ya Alhamisi, alisema New Habari walieleza kuwa siku zilizopita waliwahi kuomba kwa maandishi kwamba gazeti la Rai litoke kila siku. Maelezo ya Naibu Msajili wa Magazeti katika kikao hicho yalikuwa kwamba, kulikuwa na tatizo la kiufundi katika kurejea maombi hayo na akakiri kuwa hakuna kinachozuia gazeti la Rai kutoka kila siku. Kutokana na maelezo hayo mimi niliridhia gazeti hilo sasa liruhusiwe kutoka kila siku.

Aidha, alisema kuhusu gazeti la Mwananchi kuwa online, Naibu Msajili alisema hakuna sheria yoyote inayoweza kuzuia gazeti hilo kuwa online ila aliwataka lisionekane gazeti zima kama lilivyo, pia wabadili nembo (Master Head) kwa kuweka ya MCL na siyo ya gazeti husika ambalo limefungiwa. “Pia baada ya maelezo hayo niliridhia gazeti hilo liwe mtandaoni kwa kuzingatia angalizo lililotolewa na Naibu Msajili wa Magazeti,” alisema.

Alisema hoja ya tatu ilikuwa ni ile ya Serikali kupitia Idara ya Habari - Maelezo kuwa na uhusiano mzuri na vyombo vya habari, ili kuepuka misuguano isiyo ya lazima, ambapo pendekezo hilo alilipokea na kuliwasilisha kwa Waziri wa Habari kwa hatua zaidi, likiwamo suala la kupitia upya adhabu na ushauri wa kujenga uhusiano na vyombo vya habari.

Aliongeza kuwa masuala ya gazeti la Mwananchi kuwa online na Rai kutoka kila siku, alilitolea uamuzi siku hiyo hiyo. “Na uamuzi ni kwamba niliwaruhusu baada ya kuridhika kwamba hakukuwa na ukiukwaji wa sheria yoyote uliofanywa na waombaji.”

“Nimeamua kuweka sawa jambo hili kutokana na taarifa ya Mkurugenzi wa Maelezo ambayo ninaamini kwamba kutolewa na kusambazwa kwake ni kukosekana kwa mawasiliano kati yake kwa upande mmoja na Mhe. Waziri, Naibu waziri na Naibu Msajili wa Magazeti kwa upande mwingine.

“Hivyo aliyeruhusu Gazeti la Mwananchi kuwa online na Rai ni mimi na ndiyo maana kuanzia tarehe 5/10/2013 Gazeti la Rai lilianza kuchapwa kila siku na kusambazwa, na Gazeti la Mwananchi likaanza kuwa mtandaoni kwa kuzingatia maelekezo ya Naibu Msajili wa Magazeti,” alisema katika taarifa hiyo.

CHANZO: NIPASHE

Kivumbi cha FDL kuendelea wikiendi hii


KIVUMBI cha Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote matatu kinatarajiwa kuendelea wikiendi hii ambapo kundi B litakuwa na mechi moja tu kati ya Lipuli na Mlale JKT itakayochezwa kesho (Oktoba 12 mwaka huu) katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa.

Transit Camp itakwaruzana na Tessema katika Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi wakati Polisi Dar itaumana na African Lyon kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam katika mechi za kundi A zitakazochezwa kesho (Oktoba 12 mwaka huu).

Mechi nyingine ya kundi hilo itachezwa keshokutwa (Oktoba 13 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kwa kuzikutanisha Friends Rangers na Villa Squad.

Timu zote nane za kundi C zinashuka viwanjani kesho (Oktoba 12 mwaka huu) kusaka pointi tatu. Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Polisi Dodoma na JKT Kanembwa ya Kigoma.

Pamba na Mwadui zitacheza katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, Polisi Tabora itaikaribisha Toto Africans kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati uga wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma utatumika kwa mechi kati ya Polisi Mara na Stand United ya Shinyanga.

Simba, Yanga vitani Ligi Kuu Tanzania Bara

* Yanga yaapa kisasi Kaitaba, Prisons kuishusha Simba kileleni?

Simba itakayokuwa Taifa kuilika Prisons Mbeya
Yanga watakaokuwepo Kagera ili kulipa kisasi kwa Kagera Sugar
Kagera Sugar watakubali 'kufa' nyumbani Kaitaba?
 Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inakamilisha raundi ya nane kesho (Oktoba 12 mwaka huu) kwa mechi tatu zitakazochezwa Dar es Salaam na Bukoba mkoani Kagera.

Simba ina fursa ya kuendelea kukamata usukani wa ligi hiyo iwapo itaishinda Tanzania Prisons ya Mbeya katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni. Tanzania Prisons inayofundishwa na Jumanne Chale inashika nafasi ya kumi na moja katika msimamo wa ligi hiyo.

Ili iendelee kupanda katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo iliyoanza Agosti 24 mwaka huu, Tanzania Prisons ambayo katika mechi yake iliyopita ugenini ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mgambo Shooting inalazimika kuifunga Simba.

Licha ya sare ya bao 1-1 katika mechi yake iliyopita dhidi ya Ruvu Shooting, Simba inayoongoza kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya Azam na Mbeya City matokeo mazuri katika mchezo huo ni muhimu kwao kama ilivyo kwa wapinzani wao Tanzania Prisons.

Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 ambapo tiketi zitauzwa uwanjani kwenye magari maalumu kuanzia saa 4 kamili asubuhi.

Mabingwa watetezi Yanga wao watakuwa mjini Bukoba kwenye Uwanja wa Kaitaba kuwakabili wenyeji Kagera Sugar wanaofundishwa na Mganda Jackson Mayanja akisaidiwa na Mrage Kabage.

Kagera ambayo inapishana na Yanga kwa tofauti ya pointi moja ilipoteza mechi iliyopita dhidi ya JKT Ruvu baada ya kulala kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Azam Complex. Wakati Yanga ikiwa katika nafasi ya nne kwa pointi 12, Kagera Sugar ni ya sita kwa pointi kumi na moja.

Iwapo Kocha Ernst Brandts atawaongoza vijana wake wa Yanga kuibuka na ushindi katika mechi hiyo na Simba kufanya vibaya kwenye mechi dhidi ya Tanzania Prisons huenda akakamata uongozi wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14.

Mwamuzi Zakaria Jacob wa Pwani ndiye atakayechezesha mechi kati ya Ashanti United na Coastal Union itakayopigwa Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.

Raundi ya tisa ya ligi hiyo inaanza keshokutwa Jumapili (Oktoba 13 mwaka huu) kwa mechi kati ya Ruvu Shooting na Rhino Rangers (Mabatini, Mlandizi), Mgambo Shooting na Mbeya City (Mkwakwani, Tanga), Azam na JKT Ruvu (Azam Complex, Dar es Salaam) na Mtibwa Sugar na Oljoro JKT (Manungu, Turiani).

Mechi zitakazooneshwa moja kwa moja (live) na Azam TV kupitia TBC1 wikiendi hii ni kati ya Simba na Tanzania Prisons itakayochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na ile kati ya Azam na JKT Ruvu itakayofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Nyalla wenzake wapeta TFF, washinda rufaa zao

KAMATI ya Rufani ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imewarejesha warufani wote watatu katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa Kamati mpya ya Utendaji ya TFF utakaofanyika Oktoba 27 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Samwel Nyalla, Ayubu Nyaulingo na Ayoub Nyenzi walikata rufani mbele ya Kamati hiyo inayoongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Bernard Luanda kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF kuwaondoa katika uchaguzi huo ambapo wote wanagombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji kuwakilisha kanda mbalimbali.

Akisoma uamuzi wao leo (Oktoba 11 mwaka huu) mbele ya Waandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF, Jaji Luanda amesema baada ya kusikiliza hoja za Mrufani Nyalla walipitia Kanuni za Uchaguzi za TFF na kugundua yafuatayo;

Ibara ya 10(3) imeweka masharti makuu mawili ya ujazaji wa fomu za kugombea uongozi. Fomu hiyo ni lazima iwe na saini ya mgombea na ni lazima ithibitishwe na viongozi wa shirikisho.

Kamati imepitia Kanuni za Uchaguzi haijaona sehemu fomu hiyo ya uongozi imeambatanishwa ili kuifanya kuwa Kanuni ya Uchaguzi. Ni maoni ya Kamati kuwa ni vizuri fomu za kugombea zikawa ni sehemu ya Kanuni za Uchaguzi.

Kwa vile Kanuni za Uchaguzi za TFF za 2013 pia hazijaainisha nini adhabu kwa mgombea aliyekosea kujaza Fomu namba 1 ya kugombea uongozi, Kamati inaona itakuwa si haki kumnyima mgombea nafasi ya kushiriki katika uchaguzi kwa vile tu fomu yake haijajazwa vipengele vyote.

Nyalla aliondolewa kwenye uchaguzi na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa maelezo kuwa si mtu makini anayeweza kutekeleza majukumu yake kikamilifu baada ya kushindwa kujaza Fomu namba 1 kipengele cha 15 kinachohusu malengo ya mgombea uongozi.

Kwa upande wa Nyaulingo ambaye aliondolewa kwa kukosa uzoefu uliothibitika kulingana na Ibara ya 29(3) ya Katiba ya TFF na Kanuni ya 9(3) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF, Kamati ya Rufani imeamua ifuatavyo;

Kamati ya Rufani ya Uchaguzi imepokea sababu za rufani na imepata fursa ya kusikiliza hoja na maelezo kutoka kwa Mrufani juu ya sababu zake alizozitoa kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi.

Mrufani alifafanua historia yake katika masuala ya michezo kuanzia alipokuwa anasema Chuo Kikuu kuanzia 2005-2009 na pia ushiriki wake kama mchezaji wa Rukwa United iliyowahi kushiriki Ligi ya Mkoa wa Rukwa na ligi nyingine za kitaifa.

Kwa kusoma maana ya ‘Familia ya TFF’ iliyoko kwenye utangulizi wa Katiba ya TFF, pamoja na Ibara ya 29(3) na 29(6) ya Katiba hiyo, Kamati imejiridhisha kuwa Mrufani ana sifa za kugombea uongozi wa Shirikisho na amekidhi kigezo cha sifa za ugombea.

Ameshiriki kwenye mchezo wa mpira wa miguu kama mchezaji na mtawala, hivyo kutimiza kigezo kilichohitajika cha ushiriki katika uongozi na utawala wa mchezo wa mpira wa miguu kwa muda usiopungua miaka mitano.

Kwa kuzingatia hayo, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi inaruhusu rufani ya Mrufani. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi umetenguliwa na Mrufani anapewa nafasi ya kushiriki katika uchaguzi.

Kuhusu Ayubu Nyenzi aliyeondolewa kwa kukosa uzoefu kwa mujibu wa Ibara ya 29(3) ya Katiba ya TFF na Kanuni ya 9(3) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF, na pia kushindwa kuthibitisha uraia wake mbele ya Kamati ya Uchaguzi, Kamati ya Rufani katika uamuzi wake imesema;

Imepokea sababu za rufani na imepata fursa ya kusikiliza hoja na maelezo kutoka kwa Mrufani juu ya sababu zake alizozitoa kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi.

Baada ya uchambuzi wa kina, Kamati imeona kuwa kulingana na maelezo yaliyotolewa na Mrufani na viambatanisho vilivyowasilishwa, Kamati haina shaka kuhusu uraia wake. Uthibitisho wa uraia unapaswa kufanywa kwa umakini na taasisi yenye mamlaka ya kiserikali kufanya hivyo.

Kamati pia imejiridhisha kupitia Fomu namba 1 iliyojazwa na kusainiwa na Mrufani kuwa kuanzia mwaka 2004 mpaka 2010, Nyenzi ameshika nyadhifa za utawala wa mpira wa miguu na hasa katika klabu ya Yanga, uzoefu unaomfanya kuwa na sifa ya kugombea nafasi ya uongozi katika TFF kulingana na Ibara ya 29(3) ikisomwa pamoja na Ibara ya 29(6).

Kwa kuzingatia hayo, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi inaruhusu rufani ya Mrufani. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi umetenguliwa na Mrufani atashiriki katika uchaguzi wa TFF kwa nafasi anayogombea.

Wakati huo huo, Kamati ya Rufani ya Maadili ya TFF inakutana keshokutwa (Oktoba 13 mwaka huu), kufanyia mapitio (revision) ya uamuzi wa Kamati ya Maadili kwa waombaji uongozi wanane kama ilivyoombwa na Sekretarieti ili kutoa mwongozo wa utekelezaji wa uamuzi huo.

Wanahabari wakumbushwa kuomba vitambulisho WC 2014

http://www.cambury.edu.br/blog/marketingepp/files/2011/11/logo-copa-2014.jpg
MAOMBI ya vitambulisho kwa waandishi wa habari (Accreditation) wanaotaka kuripoti Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil kwa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) yataanza kupokelewa kwa mtandao Desemba 7 mwaka huu kupitia akaunti ya FIFA Media Channel.

Mwisho wa kupokea maombi hayo itakuwa Januari 31 mwakani, hivyo kwa waandishi wanaotaka kupata vitambulisho hivyo ni lazima wawe na akaunti ya FIFA Media Channel pamoja na utambulisho wa mtumiaji wa akaunti hiyo (user ID).

Kwa mujibu wa FIFA, kila nchi itapewa idadi maalumu ya nafasi kwa waandishi (waandishi wa kawaida pamoja na wapiga picha) baada ya mechi za mchujo za Kombe la Dunia kumalizika ambapo vigezo mbalimbali vitazingatiwa ikiwemo nchi kufuzu kwa fainali hizo.

Hivyo, nchi ambayo itakuwa imefuzu itakuwa na nafasi zaidi kulinganisha na zile ambazo hazitakuwa na timu katika fainali hizo za Brazil.

Mgawanyo wa nafasi zitakazotolewa kwa Tanzania utapangwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kulingana na maombi yatakayokuwa yamewasilishwa FIFA kupitia FIFA Media Channel.

TFF inatoa mwito kwa waandishi wa habari za mpira wa miguu ambao hawana akaunti FIFA Media Channel kuhakikisha wanakuwa nayo mapema ili waweze kutuma maombi yao.

Filama ya Dasmila karibuni kutoka hadharani

FILAMU  mpya ya Dasmila inatarajia kuingia sokoni mwishoni mwa mwezi huu. Akizungumza jijini Dar, Mkurugenzi wa  DJ Marketing & Promotion ambao ndio wasambazaji wa kazi hiyo, Haulle Daniel amesema kazi hiyo ime kamilika kwa asilimia zote hivyo wapenzi wa filamu wakae mkao wa kula kwani imewashirikisha wasanii wengi akiwemo Shamsa Frod,Jack Pentzel, Elias Mkali, Shaban Dicosta na wasanii wengine wanaotamba katika anga za filamu nchini. Filamu hiyo ya mapenzi ambayo kuna mambo mbalimbali ya kuelimisha jamii ya kitanzania ambapo Dasmila aliyeuawa kipindi cha nyuma kidogo, arudi tena kama mzimu, na mengi yanatokea. Fuatilia.. Familia, vichekesho na vimbwanga, mapenzi, kukosa uaminifu, visa na mikasa kibao  ambayo yatapatikana katika filamu hiyo, ambayo imetengenezwa kwa ubora wa ali ya juu na itakayokuwa ikisambazwa na kampuni ya kizalendo ya DJ Marketing ya jijini Dar es salaam.

Friday, October 11, 2013

SHANGWE ZA EID KUPAMBWA NA MASHAUZI CLASSIC


Kocha Wailes ampaisha Gareth Bale

http://www.scaryfootball.com/wp-content/uploads/2013/05/gareth-bale-and-ronaldo-real-madrid-transfer-2013-zidane.png
bale akiwa amebebwa na Ronaldo
KOCHA wa timu ya taifa ya Wales, John Toshack alizungumza na kituo cha radio cha 'La Xarxa' cha Hispania kuhusu mchezaji wake Gareth Bale na akasema kwamba nyota huyohayuko mbali sana na ubora walionao Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.
Alisema: "Sitaki kuingia katika mijadala kuhusu thamani yake, lakini ninaloweza kusema sasa ni kwamba Bale hayuko mbali sana na matawi aliyopo Cristiano Ronaldo na Messi."
Toshack pia alisema winga huyo wa zamani wa Tottenham hahusiki kwa lolote katika kiwango kikubwa cha pesa kilicholipwa ili kumhamishia Real Madrid, akisema: "Mchezaji si wa kulaumiwa kwa ada ya euro milioni 100 iliyolipwa ili kumsajili. Kama klabu mbili husika zimeafikiana bei hiyo, hayo ni makosa yao."
Pia aliwataka watu wawe wavumilivu kwa nyota huyo ili azoee mazingira mapya. "Alikuwa na bahati mbaya hakujifua katika kipindi cha kujiandaa na msimu, kutokatana na mvutano uliokuwapo baina ya Tottenham na Real Madrid, lakini Bale ni mchezaji mzuri. Hakuna sababu yoyote ya kutilia shaka uwezo wa Gareth Bale, nawahakikishia," alisema kwa kujiamini.
Kocha huyo wa Wales pia alizungumzia hali ya vipaji vinavyoibukia Real. "Kwa mfano watu kama Illarramendi, Isco au wachezaji yosso wa El Castilla (Real Madrid B), kama wakiangalia benchi la Ancelotti na Zidane linaleta matumaini. Kwa sasa ni wakati mgumu kwao kwa sababu Barcelona wanafanya vyema, huku Madrid wakiwa nyuma yao kwenye msimamo, lakini wanahitaji kupewa muda,” alisema kocha huyo Wales.