STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 12, 2013

Diamond, Lady Jay dee watajwa kama vibopa Bongo kwa wasanii

When it comes to money, Bongo music is one of the most lucrative but you’d never tell that listening to the artistes pour their hearts out for their loved ones. Bongo Flavour acts rake in the money in truck loads and they don’t spend it on bling only, they invest their money. Sylvia Ambani and Herieth Makwetta looked at some of the richest acts in Tanzania.





NASEEB ABDUL (DIAMOND)

He stayed in the shadows for long looking for a break but now that the limelight has been trained on him, he has proved that he belongs at the top of the music charts. He finally made a debut in 2009 with his hit song “Kamwambie”.

He is one of the most expensive musicians not just in Tanzania but the region and this does not seem to put promoters off as he is on the stage on a weekly basis. Want him for a show, you will have to pay him $4000 (Sh350,000). And that’s after a bargain.

This has enabled him to make a fortune for himself in a very short period of time. He owns mansions in Tanzania, acres of land, cars and shops.



JUDITH WAMBURA (LADY JAY DEE)



She started her music career at the end of the 1999. She is one of the most respected Tanzanian artistes and has remained humble through her success. She is very hard working and this has led her to accumulate a good fortune to her name.



Her garage pays homage to a Nissan Murano, a Toyota Coaster minibus, Toyota Prado among others. She of course can’t own all those and rent. She owns a mansion. She also invests heavily and owns a band by the name Machozi.




JOSEPH HAULE (PROFESSOR JAY)

He began his music career in 1990 with a group called the Hard Blasters. It is this band that started the music style known as ‘muziki wa kizazi kipya’. The artiste has acquired his wealth through the many shows he does internationally.

He owns a beachfront mansion which has an in-built studio, drives a modest Toyota Spacio but don’t let that fool you, it’s not that he can’t afford fuel because he makes good money from his music and owns several parcels of land and is also a serious investor.



JUMA NATURE (KIROBOTO)

He is one of the long timers who are still relevant in the music scene. He has been able to make a name for himself since his days in the male group artists TMK when he was under Mkubwa Fela. He later left and formed his own group called ‘Wanaume Halisi’.

He owns a fleet of taxis that operate in Dar es Salaam; he owns acres of land and a home.



AMBWENE YESAYA (AY)

He started his music career back in 2000 with the group East Coast. The group later split and he continued to do his solo music together with his close friend Hamisi Mwinjuma (Mwana FA). They are still close friends and have been friends for more than ten years.

AY likes to keep his personal life private and stays away as much as he can from the cameras. All the camera shyness may fool you but he is one of the richest artistes in Tanzania. He has derived his wealth from the many shows he does and the international events that pay him handsomely. He has a collection of cars, a clothing line with his name and several boutiques.

He is the owner of Unity Entertainment Company which produces programmes like the famous ‘Mkasi’ which is broadcasted on East Africa Television. He recently did a collabo with Lil Romeo that got some good reception across the continent.

Source: Kenya’s The Nation via wavuti

Uchaguzi wa FRAT upo palepale Siku ya Wapendanao

Na Boniface Wambura
UCHAGUZI Mkuu wa viongozi wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) unafanyika Februari 14 mwaka huu mjini Morogoro kama ulivyopangwa, tofauti na taarifa wanazopewa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa chama hicho.

Kwa mujibu wa Katibu wa Kamati ya Uchaguzi ya FRAT, Damas Ndumbaro, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa FRAT wanatakiwa kufika Morogoro keshokutwa (Februari 12 mwaka huu) . Pia wapiga kura na wagombea wanatakiwa kulipia ada za uanachama kwa mwaka 2013 kabla ya uchaguzi.

Wagombea ni Army Sentimea na Said Nassoro (uenyekiti) wakati wanaoomba nafasi ya Makamu Mwenyekiti ni Juma Chaponda, Juma Mpuya na Tifika Kambimtoni.

Abdallah Mitole, Charles Ndagala na Hamis Kisiwa wanawania ukatibu mkuu, nafasi ya Mhazini inagombewa na Jovin Ndimbo. Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ni Kamwaga Tambwe wakati nafasi ya uwakilishi wanawake yupo Isabela Kapera.

Wagombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni Emmanuel Chaula na Samson Mkotya.

Kampeni za uchaguzi TFF zasitishwa kisa,,,

TAARIFA KWA UMMA

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA NA TANZANIA PREMIER LEAGUE BOARD (TPL)



KUSITISHA ZOEZI LA KAMPENI

12/02/2013



1. Kamati ya Uchaguzi, kwa mamlaka iliyonayo kupitia Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 3(1), 6(1) (g) na (l), 10(5), 11(6) inayosomeka pamoja na Ibara ya 14(1) na (2) na pia Ibara ya 26(5) na (6), imesitisha zoezi la kampeni za uchaguzi wa TFF na TPL Board lililokuwa lianze kesho tarehe 13/02/2013 hadi hapo itakapowatangazia, ili kuhakikisha kuwa mchakato wa uchaguzi unakidhi kikamilifu matakwa ya Kanuni za Uchaguzi na Katiba ya TFF.



2. Tarehe za Uchaguzi Mkuu wa TFF na TPL Board zinabaki kama zilivyopangwa.



3. Taarifa hii inazingatia pia Ibara ya 2(4) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF inayoagiza uongozi uliopo madarakani kuendelea na kutekeleza majukumu ya Shirikisho hadi hapo mchakato wa uchaguzi utakapokamilika.



Deogratias Lyatto

MWENYEKITI

KAMATI YA UCHAGUZI TFF

YANGA KUSAKA POINTI ZA KUIACHA AZAM KWA LYON KESHO

Kikosi cha Yanga

Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inamaliza raundi ya 16 kesho kwa mechi kati ya wenyeji African Lyon dhidi ya Yanga itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro inakutanisha timu zenye mazingira tofauti. Wakati Yanga wakiwa ndiyo vinara wa ligi hiyo kwa pointi 33, African Lyon ambayo sasa inanolewa na Salum Bausi inakamata mkia ikiwa na pointi tisa tu.
Nayo Toto Africans iliyopo katika nafasi ya 12 itaikaribisha Polisi ya Morogoro kwenye Uwanja wa CCM Kirumba-Mwanza katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo wa Musoma. Katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000 utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting na Oljoro JKT.
Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime ambaye sasa ni kocha wa Mtibwa Sugar ataiongoza timu yake hiyo katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani, Morogoro. Ni kwenye uwanja huo huo ambapo Mtibwa Sugar katika mechi yao iliyopita walichapwa mabao 4-1 na Azam.

Shaa wa Wakilisha achia mpya akiapa raha kwa mashabiki


Msanii Shaa katika pozi

MWANADADA mkali wa muziki wa kizazi kipya, Sarah Kais 'Shaa', aliyekuwa kimya kwa kitambo, ameibuka na 'ngoma' mpya iitwayo 'Promise', akiapa kuwapa raha zaidi mashabiki wake.
Shaa, mkali aliyeibuliwa na shindano la Coca Cola Pop Star na kuja kuunda kundi la pamoja na wakali wenzake wawili, Langa na Witness lililoitwa 'Wakilisha', alisema wimbo huo mpya ni salamu kwa mashabiki wake 2013.
Msanii huyo alisema baada ya kimya tangu aachie wimbo wake uitwao 'Siri ya Penzi', amefyatua ngoma hiyo mpya akiwa mbioni kuendelea kufyatua moja moja ili kuwapa raha mashabiki wake.
"Hizi ni salamu zangu za 2013, nimeachia 'Promise' na kwa sasa najipanga kwa ajili ya vitu vingine vikali ili kuonyesha kuwa 'Shaa' bado nipo na ukali wangu ni ule ule," alisema Shaa.
Msanii huyo alisema kwa sasa anafanya kazi chini ya usimamizi wa Babu Tale na umeneja wa Master J na kwamba mashabiki wake waliomiss kitambo watarajie makubwa zaidi kuliko ilivyokuwa siku za nyuma.

TFF YAOMBA MASHABIKI KUZISAPOTI SIMBA, AZAM KIMATAIFA

Tanzania Football Federation
Affiliated to FIFA, CAF and CECAFA
Karume Memorial Stadium, Uhuru/Shaurimoyo Road
P.O. Box 1574, Dar es Salaam, Tanzania
. Telefax: + 255-22-2861815
E-mail:
tfftz@yahoo.com . Website: www.tff.or.tz
 
 
 

 
 
 
Release No. 026
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 12, 2013
WASHABIKI WAZIUNGE MKONO AZAM, SIMBAShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaka washabiki wa mpira wa miguu kujitokeza kwa wingi wikiendi hii kuzishangilia timu za Azam na Simba zitakazocheza mechi za mashindano ya Afrika jijini Dar es Salaam.
Nguvu ya washabiki ni muhimu katika kuziweza timu hizo kufanya vizuri katika mechi hizo za nyumbani dhidi ya Al Nasir Juba ya Sudan Kusini na Club Libolo ya Angola.
Azam itacheza Jumamosi (Februari 16 mwaka huu) dhidi ya Al Nasir katika mechi ya Kombe la Shirikisho wakati Simba itaikabili Club Libolo kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayofanyika Jumapili. Mechi zote zitachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
LYON, YANGA KUUMANA UWANJA WA TAIFALigi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inamaliza raundi ya 16 kesho (Februari 13 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji African Lyon dhidi ya Yanga itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo itakayochezshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro inakutanisha timu zenye mazingira tofauti. Wakati Yanga wakiwa ndiyo vinara wa ligi hiyo kwa pointi 33, African Lyon ambayo sasa inanolewa na Salum Bausi inakamata mkia ikiwa na pointi tisa tu.
Nayo Toto Africans itaikaribisha Polisi ya Morogoro kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo kutoka Musoma. Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000 utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting na Oljoro JKT.
Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime ambaye sasa ni kocha wa Mtibwa Sugar ataiongoza timu yake hiyo katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani, Morogoro. Ni kwenye uwanja huo huo ambapo Mtibwa Sugar katika mechi yao iliyopita walichapwa mabao 4-1 na Azam.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Baby Madaha kutega videoni kidigitali

Baby Madaha katika pozi

LICHA ya kulia na mfumo wa digitali akidai unawalaza kwa kazi zao kutotangazika kama zamani, msanii mahiri wa muziki na filamu nchini, Baby Madaha, ameachia video ya wimbo mpya uitwao 'Nitege'.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby alisema video hiyo iliyotengenezwa na watalaam Tudd Thomas na Nash Disigner, siku yoyote anatarajia kuisambaza ili irushwe hewani na vituo vya runinga.
Alisema ameona haja jinsi zaidi ya kutoa video hiyo, kutokana na ukweli ilikuwa imeshakamilika wakati Tanzania ikiingia kwenye digitali.
"Katika muziki nimetoa video ya Nitege, lakini shaka na namna itakavyotangazika ukilinganisha na kazi zangu za nyuma kutokana na mfumo mpya wa urushwaji wa matangazo ya kidigitali,"alisema Madaha.
Alisema mashabiki wao wameshindwa kumudu kununua ving'amuzi, hivyo anakuwa na mashaka na kazi yake itatangazika vipi, ingawa ameamua kukomaa hivyo hivyo.

KIVUMBI LIGI YA MABINGWA ULAYA KUANZA KUTIMKA LEO

Ronaldo akishangilia moja ya mabao yake ambapo kesho atakivaa kikosi chake za zamani Manchester United

KIVUMBI cha hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kinaanza leo kwa kushuhudiwa timu nne kuanza kusaka tiketi ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo.
Celtic ya Uskochi itakuwa uwanja wa nyumbani kuwakaribisha mabingwa wa Italia, Juventus, huku Valencia watamenyana na vinawa wa Ligi ya Ufaransa Paris Saint Germani.
Mechi zote hizo zitachezwa kuanza saa 4;45 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, kabla ya kesho mashabiki wa soka ulimwengu kuishuhudia dunia 'ikisimama' kwa muda kupisha pambano la Real Madrid ya Hispania dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester United.
Pambano hilo linasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa timu zote kutokana na uwepo wa Criastian Ronaldo aliyewahi kuichezea na kuipa mafanikio Manchester United ambapo leo atakuwa akiiongoza Real kusaka ushindi kabla ya mechi ya marudiano mwezi ujao.
Pambano jingine la leo litazikutanisha timu za Shakhtar Domestic dhidi ya Borrusia Dortmund ya Ujerumani.

Maskini Malinzi atupwa uchaguzi wa TFF


KATIBU Mkuu wa zamani wa Yanga na aliyeekuwa mgombea wa nafasi ya Urais katika Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi ametupwa katika kinyang'anyiro hicho kinachoitarajiwa kufanyika Februari 24.

Kuenguliwa kwa Malinzi, kunaifanya nafasi hiyo ya kusaka mrithi wa Rais wa sasa wa TFF, Leodger Tenga kusaliwa na mgombea mmoja pekee ambaye ni Makamu wa Rais, Athuman Nyamlani.
Malinzi (kulia) alipokuwa akirejesha fomu za kuwania urais wa TFF
Uamuzi wa kumuengua Malinzi umetolewa jana na Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya shirikisho hilo iliyokuwa ikipitria pingamizi mbalimbali ambapo Nyamlani alisalimika baada ya kuonekana kuwa utumishi wake serikalini haumzuii kuwa mgombea.
Wengine walioenguliwa ni Michael Wambura aliyekuwa akigowania nafasi ya Makamu wa Rais na Ahmed Yahya aliyekuwa akiwania nafasi ya uenuekiti wa Bodi ya Ligi.
Imeelezwa kuwa Malinzi ameenguliwa kwa sababu ya kukosa uzoefu katika uongozi.
Akizungumza jana baada ya kupata taarifa hiyo, Malinzi alisema kuwa amechoshwa na vikwazo.
Malinzi ambaye katika uchaguzi wa mwaka 2008 alipitishwa kuwa mgombea akichuana na rais wa sasa anayemaliza muda wake, Leodgar Tenga, alinukuliwa jana akisema amechoshwa na pingamizi na vikwazo ambavyo amewekewa kuhusiana na mchakato huo wa kuwania cheo hicho cha juu.
Alisema mapema jana kabla ya kutangazwa rasmi kwa maamuzi hayo kuwa ataheshimu maamuzi yatakayotolewa na kamati hiyo kwa sababu lengo lake la kuwania uongozi TFF ni kutaka kutoa mchango wake katika kuendeleza soka la Tanzania ambalo bado wadau wana kiu ya kupata mafanikio.
"Nimechoka na hali inavyoendeshwa, mimi siendi kuomba kazi, siendi kuomba ajira, siendi kufanya biashara, lengo langu ni kutoa mchango wangu katika kusukuma soka letu," Malinzi ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Mkoa wa Kagera (KRFA) alisema.
Alisema kwamba moja ya sababu zilizomfanya awanie nafasi hiyo ni kutokana na uzoefu alionao.
Malinzi aliwekewa pingamizi na baadaye kukatiwa rufaa na Agape Fue dhidi ya Kamati ya Uchaguzi TFF kupinga kumpitisha akisema kwamba kiongozi huyo hana uzoefu.
John Bocco 'Adebayor' aliyerejea toka kwenye majeruhi

TIMU ya soka ya Azam imesema ipo tayari kuwavaa Al Nasir Juba ya Sudan Kusini, hasa baada ya kurejea dimbani kwa washambuliaji wake waliokuwa majeruhi, Kipre Tchetche na John Bocco 'Adebayor'.
Azam na Al Nasir wanatarajiwa kuvaana Jumamosi kwenye uwanja wa Chamazi, likiwa ni pambano la awali la michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Afisa Habari wa Azam, Jaffer Idd Maganga aliiambia MICHARAZO jana kuwa, kikosi chao kimeshaingia kambini tangu jana asubuhi baada ya kutoka Morogoro ilipotoka kuiadhibu Mtibwa Sugar kwa kuilaza mabao 4-1 katika mechi ya Ligi Kuu.
Jaffer, alisema maandalizi waliyofanya wakati wakijiandaa na duru la pili la Ligi Kuu kwa kucheza michuano ya Mapinduzi na kusafiri katika nchi za DR Congo na Kenya yameiivisha Azam kimataifa.
Alisema kinachowapa faraja zaidi ni kupona kwa washambuliaji wao nyota, Kipre Tchetche ambaye Jumapili aliifungia Azam mabao mawili kati ya manne yaliyoizamisha Mtibwa, huku Bocco akiwa ameanza kufanya mazoezi mepesi na wenzake.
"Kwa kweli Azam tupo kamili gado kukabiliana na wageni wetu Al Nasir Juba, furaha zaidi ni kurejea kwa nyota wetu waliokuwa majeruhi kadhalika kikosi kina ari kubwa kwa ajili ya mechi hiyo ya Kombe la Shirikisho," alisema Jaffer.
Aliongeza japo Bocco ameanza kujifua mazoezi na wenzake bado hawajajua kama ataweza kucheza katika pambano hilo,  kwa madai inategemea maamuzi ya kocha wao John Stewart Hall.
Azam inashiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya msimu uliopita kushika nafasi ya pili kwen ye Ligi Kuu Tanzania Bara nyuma ya Simba ambao watashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba wenyewe watashuka dimbani Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, kuumana na Libolo ya Angola kabla ya kurudiana nao wiki mbili zijazo ugenini nchini Angola.
Kikosi cha Azam kitakachoshuka dimbani Jumamosi kuivaa Al Nasir Juba


Monday, February 11, 2013

ALIYEPIGWA RISASI NA ASKARI POLISI AKATWA MGUU

      
 Na  Antony Sollo  -  Kishapu.

HALI si shwari katika mgodi wa mwadui,wananchi wamezidi kuuawa na kujeruhiwa kwa risasi huku Serikali ikiwa haina majibu kuhusu kashfa zinazotokea katika  mgodi huo jambo ambalo hadio sasa wananchi wana mpango wa kuvamia mgodi huo kwa lengo la kuharibu mali za mgodi huo.
 
Kufuatia hali hiyo,wananchi wa vijiji vinavyozunguka eneo la mgodi huo wanajipanga kufanya vurugu kubwa katika mgodi huo ili kulipiza kisasi kufuatia kushambuliwa kwa vijana watano ambao waliingia mgodini humo hivi karibuni kama ilivyoripotiwa na Tanzania daima na hatimaye kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za miili yao huku mmoja wa vijana hao bwana Geroge Joseph akikatwa mguu.
Hali hii ni mwendelezo wa taarifa nyingi za kuuawa na kujeruhiwa kwa raia  lakini hakuna ufuatiliaji wowote kutoka kwa viongozi wa Serikali hususani vyombo vya ulinzi na usalama kama jeshi la polisi jambo ambalo kwa siku chache zijazo kama hali hii haitarekebishwa watanzania tukashuhudia mapigano makubwa kati ya walinzi wa mgodi na wananchi.
Matukio haya yamegubikwa na usiri mkubwa huku Viongozi mbalimbali wakiendelea kutupiana mpira na kushindwa kueleza bayana juu ya ukweli wa matukio haya na kibaya zaidi majeruhi aliyepata ulemavu huo bwana George Joseph akiwatuhumu viongozi hao akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kishapu kwa kushindwa kufika kwa muda muafaka kumuona na kumuombea ruhusa kwa uongozi wa mgodi ili aende kupata matibabu.
 
Hali hii inatokana na kwamba mgonjwa majeruhi huyo alikuwa akishikiliwa na uongozi wa mgodi huo kwa tuhuma za kuingia mgodini isivyo halali jambo lililosababisha kumchelewesha kwenda kupata matibabu hivyo kuharibika kwa mguu wake na hatimaye kukatwa.
Kijana huyo alilazwa katika hospitali ya mgodi wa mwadui tangu tarehe 9/01/2013 huku akiwa chini ya ulinzi wa askari wa mgodi huo lakini kukiwa hakuna huduma zilizokuwa zikitolewa jambo lililosababisha aombe kupewa rufaa bila mafanikio ambapo na hatimaye ndugu walifanikiwa kumuondoa hospitalini hapo kwa kutumia nguvu na kumpeleka hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza ambako amelazwa hadi sasa.
Akilalamikia viongozi wa Serikali mgonjwa huyo Bwana George Joseph anasema”ndugu mwandishi,Mkuu wa Wilaya ya Kishapu ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya alikuwa ni mtu wa kwanza kumjulisha juu ya tukio hili na aliahidi kufika hospitalini lakini hakufanya hivyo hadi sasa nimethirika na kuwa mlemavu kwa kukatwa mguu wangu.
Kuhusu kauli ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga kuwa hana taarifa,inashangaza na inasikitisha sana kwani askari waliokuwa wamekuja hapa kwa ajili ya kufanya operesheni walitoka mkoani Shinyanga.
Askari waliofika  kunichukua maelezo nao pia walitoka ofisi ya upelelezi ya Mkoa wa Shinyanga hata operesheni hii huandaliwa na Mkoa,je haya madai kwamba hana na taarifa yana lengo gani kama si kuficha ukweli wa jambo hili? na anafanya hivyo kwa faida ya nani amehoji bwana George.
Wakiongea na Tanzania daima wananchi waliozungumzia tukio hili walisema ndugu mwandishi, kwa kweli kuna idadi kubwa sana ya watu waliouawa na kujeruhiwa katika mgodi huu lakini hatuoni viongozi wetu wakifuatilia masuala haya sijui hawana uchungu na wananchi ambao ndiyo rasrimali ya taifa hili.
Kwa sasa tukio hili limetupa hofu kubwa na sasa tunaiomba Serikali ijiandae kuona machafuko makubwa kwa vile tumechoshwa na vitendo hivi katika maeneo yetu.
tuna mpango wa kwenda kuvamia mgodi na kuchoma ofisi mbalimbali pamoja na kufanya uharibifu mkubwaili kuibua na kuweka wazi manyanyaso tunayofanyiwa na mawekezaji wa mgodi wa Williamson mwadui maana kuna usiri mkubwa mno kuhusu matukio ya unyanyasaji wa wananchi wa Maganzo na vitongoji vyake. 
Akiongea na waandishi wa habari waliotembelea Ofisi za SHILEMA zilizopo katika mji mdogo wa Maganzo, Katibu Msaidizi wa SHILEMA bwana Hamza Yusuph amesema watu wengi wamepoteza maisha na viungo vyao kwa sababu ya kuingia mgodini mwadui pasipo na uhalali wa kuingia mgodini humo,wote tunajua kuwa kuingia mgodini ni kosa la jinai,lakini pia  hatua za watendaji wa jeshi la Polisi  kujichukulia sheria mkononi zinatokana sheria na mamlaka ipi?
 Kwa nini watu hawa wasikamatwe na kufikishwa mbele ya sheria kuliko kufanya ukiukwaji huu wa sheria na kusababisha wimbi la vijana walemavu kuongezeka! Vitendo hivi havikubaliki kabisa alisema bwana Selemani mkaji wa kitongoji cha majimaji mji mdogo wa Maganzo.
Bwana Yusuph amewalalamikia pia viongozi wa kisiasa wanaotumia mwavuli wa kisiasa katika masuala yanayohusu maisha ya watu ili kujijengea umaarufu katika nyakati za uchaguzi huku akiwalaumu viongozi wa kamati ya mzunguko wa mwadui kwa kujali masilahi yao  binafsi na kusahau kwamba wao ni wawakilishi wa wananchi.
Akizungumzia fedha zinazotolewa mgodini hapo bwana Yusuph amesema haelewi kama fedha hizo zinatolewa kama zawadi  au ni wajibu wa kampuni katika kuihudumia jamii hususani huduma za msingi kama Elimu,Afya,Miundo mbinu,Maji,Umeme naBarabara kama ilivyo katika maeneo mengine.
Bwana Yusuph amelaumu pia Serikali kwa kushindwa kuweka wazi mikataba ya Makampuni ya uchimbaji wa madini nchini kwa kuwa wananchi hadi sasa hawaelewi mambo mbalimbali zikiwemo haki zao dhidi ya makampuni ya uwekezaji katika maeneo yao.
 
Tanzania daima ilibisha hodi katika Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Bwana Justine Sheka na kufanya mahojiano naye ambapo alianza kwa kusema,ndugu mwandishi,sisi kama viongozi wa Serikali Wilayani Kishapu tunashangazwa na uongozi wa mgodi wa Mwadui kwa kuendesha shughuli zake kwa ubabe na usiri katika mapato yanayotokana na mgodi huo.
 
Hadi sasa uingiaji ndani ya mgodi huo una urasimu mkubwa kiasi kwamba hata Mbunge wa Jimbo anapohitaji kuingia na kuangalia utendaji wa shughuli za mgodi huo zinavyofanyika ni shida,unaingia ukiwa chini ya ulinzi mkali na mara nyingine yapo madai kuwa ni lazima utoe taarifa mapema kwa uongozi wa mgodi.
 
Lakini pia amesikitishwa na jinsi Serikali ilivyofanya siri kuhusu uwakilishi wake katika kukagua uzalishaji wa madini na namna ya kupata taarifa mbalimbali ili kuweza kuona kama kweli mali inayopatikana ndiyo inayotolewa taarifa  kama ilivyo katika maeneo mengine yaliyo na migodi.
Inasemekana ni muda mrefu mgodi wa Mwadui umekuwa ukiendesha shughuli za uchimbaji wa madini Wilayani Kishapu bila kuwa na mwakilishi wa Serikali ambaye anafanya ukaguzi jambo linalohofiwa kuporwa kwa madini na kuisababishia Hasara Serikali.
Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga bwana Evarist Mangala alipotafutwa kujibu malalamiko juu ya tuhuma zinazotolewa na mgonjwa aliyekatwa mguu bwana George Joseph alisisitiza kwamba bado hana taarifa lakini akashauri kwamba mgonjwa aandike barua ya malalamiko juu ya tukio hilo ili aweze kulifanyia kazi.
 
CHANZO:Francis Godwin

Hatma ya Milovan Simba leo

Kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic


HATMA ya aliyekuwa kocha wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic, kulipwa fidia yake ya kusitisha mkataba wa kuifundisha timu hiyo huenda ikajulikana leo wakati atakapokutana na viongozi wa klabu hiyo kabla ya kurejea kwao baada ya kupata haki yake.
Hata hivyo, Milovan ambaye ameumizwa na sare ambazo Simba imeendelea kuzipata, alisema jana kwamba yuko tayari kurejea kwenye timu hiyo endapo uongozi utamrejesha.
Milovan anaidai Simba dola za Marekani 24,000 (Sh. milioni 36), ambazo ni malimbikizo ya mishahara yake ya miezi mitatu.
Akizungumza jana, Milovan, alisema kwamba  hadi sasa anafahamu kuwa yeye bado ni kocha halali wa timu hiyo kwani mkataba wake unamalizika Julai Mosi mwaka huu.
Mserbia huyo alisema kwamba ndiyo maana, baada ya kuona viongozi wa klabu hiyo wakikaa kimya, aliamua kuja nchini kufuatilia haki yake na kwamba, hata hoteli anayoishi jijini Dar es Salaam gharama zake zitalipwa na Simba.
"Mimi najua bado ni kocha wa Simba kwa sababu mkataba wangu haujamalizika. Na kama watakuwa tayari kuzungumza na mimi, naweza kurejea kazini. Bila shaka mnajua uwezo wangu na nini nilikifanya katika ligi na mshindano ya kimataifa mwaka jana," alisema kocha huyo.
Aliongeza kwamba kabla ya kukutana leo na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alitarajiwa kukutana jana na katibu mkuu wa timu hiyo, Evodius Mtawala; ambaye ndiye huwasiliana naye mara kwa mara.
"Hata hivyo, naye aliahidi tutakutana leo (jana) asubuhi, lakini sijamuona na alisema kwamba anamsubiri Rage na Kaburu,"  aliongeza Milovan.
Akihojiwa juzi katika kipindi cha michezo cha Radio One, Rage alikiri kocha huyo kuidai Simba lakini akashangazwa na maamuzi yake (Milovan) kufuata malipo yake jijini Dar es Salaam wakati wao walimueleza kuwa watamtumia kwa njia salama za kibenki.
Milovan alitua jijini Jumatano wiki iliyopita na kulieleza gazeti hili kwamba amechukua maamuzi ya kufuata haki yake baada ya kuona ahadi alizopewa kwa njia ya simu hazitekelezwi na kwamba sasa, anafahamu kuwa klabu hiyo inazo fedha baada ya kumuuza kwa klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia aliyekuwa mshambuliaji wao wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi.
 

CHANZO:NIPASHE