STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 18, 2013

Hali ya hewa Arusha yarejea kwenye utulivu

MOTO UNAWAKA BAADA YA KUCHOMWA MATAIRI


HALI ya utulivu imeanza kurejea jijini Arusha baada ya hali kuchafuka kwa Jeshi la Polisi kufyatua mabomu ya machozi dhidi ya wafuasi na viongozi wa CHADEMA baada ya kukusanyika kwenye viwanja vya Soweto ili kujua namna watakavyoshiriki mazishi ya watu waliouwawa kwa Bomu siku ya Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa toka Arusha zinasema kuwa hali imerejea kuwa tulivu baada ya mshikemshike wa Polisi kuwatimua wananchi hao na kuleta kizaazaa cha kutunishiana misuli na kurejea hali ya taharuki jijini humo baada ya hivi karibuni kukumbwa na matukio yaliyosababisha vifo vya watu wasio na hatia.

Msajili wa vyama alaani mlipuko wa bomu Arusha, avinyooshea kidole vyama vya CCM na CHADEMA

Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania, John Tendwa
Na Suleiman Msuya
MSAJILI  wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa amesema ili kuhakikisha kuwa amani inaendelea kudumu ni muhimu kuwepo kwa uvumilivu na kuheshimiana  kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Kauli hiyo ameitoa leo Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku chache baada ya kutokea kwa mlifuko wa bomu kwenye mkutano wa kampeni ya udiwani uliokuwa unaendeshwa na CHADEMA katika viwanja vya Soweto mjini Arusha.
Tendwa alisema kwa muda sasa kumekuwepo kwa msuguano mkubwa baina ya vyama hivyo viwili jambo ambalo linaonyesha dalili za kuhatarisha amani ya nchi na wananchi kwa ujumla.
Msajili huyo alisema vyama hivyo vinaonyesha kukosa  uvumilivu na kuheshimiana kwani kwa kipindi hiki kifupi cha kampeni za udiwani viomekuwa na fujo ambazo kila mmoja anamshutumu mwenzake jambo ambalo sio nzuri katika nchi.
Alisema kutokana na tukio hilo viongozi wao wameibuka na kushutumiana ambapo  Katibu Uenezi wa CCM Nape Mnauye alisikika akiwashutumu CHADEMA kuhusikana wakati Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akisema CCM na Jeshi la Polisi wanahusika.
“Inasikitisha sana kuona watu wanakufa alafu watu wanajitokeza na kuanza kushutumiana kuwa huyu ndiye anahusika mimi nomba wapeleke ushahidi Jeshi la Polisi ili kuweza kusaidia upelelezi,” alisema.
Tendwa alisema katika kuhakikisha kuwa vyama hivyo vinaendelea kuheshimiana na kuvumiliana anatarajia kuita kikao ambacho kitashirkisha ofisi yake, jeshi la polisi na vyama hivyo kwani wanapoelekea ni pabaya.
Alisema iwapo uchaguzi wa Udiwani hali inakuwa hivyo je itakuwakuaje katika uchaguzi wa Serikali za Mitaaa na uchaguzi mkuu watu watarajie nini kwani ni ishara mbaya kwa Taifa ambalo linasifika kwa amani.
Aidha Msajili huyo alipotakiwa kuelezea juu ya ofisi yake kuvifuta vyama hivyo viwili vya CCM na CHADEMA alisema ofisi yake ina mamlaka hayo ila hiyo ni hatua ya mwisho kuchukuliwa iwapo itabidi.
Tendwa alisema uamuzi wa kuvifuta vyama hivyo unaweza kuwa na athari kubwa kwani utahitaji gharama kubwa za kufanyika uchaguzi jambo ambalo sio la kukimbilia.
Alisema ofisi yake inahitaji kukutana na vyama hivyo  kwani ndio njia sahihi ya kufikia muafaka kwa maslahi ya vyama hivyo na wananchi kwa ujumla.
“Ni lazima jamii itakatumbua kuwa maamuzi haya yanahusi CCM ambayo ipo madarakani ambapo matokeo yake ni kuvunja Serikali na kwa CHADEMA ni kuwaondoa wabunge wake hivyo uchaguzi kufanyika tena,”  alisema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini Peter Mziray amevitaka vyama hivyo kutambua kuwa nchi hii iwapo itaingia vitani wao ndio wahusika wakubwa.
Alisema Baraza hilo linatajia kukutana kwa pamoja likishirikisha vyama vyote vya siasa ambapo watatoka na azimio juu ya hali ilivyo hivi sasa kwani inaonyesha dalili za kupotea kwa amani.
Mziray ambaye ni Rais Mtendaji wa Chama cha African Progressive Party Tanzania (APPT Maendeleo alisema hali inayotoke kwa sasa jeshi la Polisi na vyombo vyote vya usalama vinapaswa kushutumiwa kwani vionyesha kutofanya kazi vizuri.
Mwenyekiti huyo alisema hali hiyo inasikitisha sana kutokana na ukweli kuwa watu wasio na hatia kupoteza maisha jambo ambalo halikubaliki.
“Kwa kweli vyama hivi viwili vimekuwa na matukio mbalimbali ambayo kwa muono wangu nadhani vinahitajika kubadilika kwani hali sio shwari ila vyombo vya usalama pia vina mapungufu yao,” alisema

Klabu Thailand yaja kusaka wachezaji wa kulipwa

Nembo ya klabu ya Thai Port FC
Na Boniface Wambura
KLABU ya Thai Port Football ya Thailand inatafuta wachezaji nchini Tanzania kwa ajili ya kucheza mpira wa miguu nchini humo na katika nchi nyingine barani Ulaya.

Kupitia kwa wakala wake, klabu hiyo imetuma taarifa kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikitaka wachezaji wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 28 kwa ajili ya kuwafanyia majaribio ambapo watakaofuzu watacheza nchini humo na katika klabu nyingine za Ulaya ambazo wana ushirikiano nazo.

Wachezaji wenye nia ya kufanya majaribio wanatakiwa kutuma taarifa za wasifu wao (CV) kwa klabu hiyo kwa njia ya emaili, wawe na pasi ya kusafiria pamoja na pasi ya mchezaji (player passport).

Wakala atapitia vitu hivyo, na kwa wachezaji atakaowahitaji atawatumia tiketi za ndege na viza kwa ajili ya kwenda kufanya majaribio nchini humo, na watakaofanikiwa kabla ya kusaini nao mikataba watawasiliana na klabu zao nchini (kwa wale wenye klabu).

Polisi wafafanua sababu ya kulipua mabomu ya machozi leo Arusha


JESHI la Polisi limekipiga marufuku chama cha demokrasia na maendelo(CHADEMA)kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo .


Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas amesema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi.


Kamanda Sabas amedai  kuwa  jeshi la polisi  liliwataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini si kwenye viwanja hivyo.

Hali kwenye viwanja hivyo imekuwa ya pilika pilika tangu juzi kwa wafuasi wa chama hicho kujikusanya tokea asubuhi hadi jioni kwa madai ya kuomboleza ..

Hata hivyo viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo walikaidi agizo hilo na  kuanza  kujikusanya uwanjani hapo pamoja na wafuasi wa CHADEMA, hali iliyoleta  mvutano kati ya viongozi  wa jeshi la polisi na  wafuasi hao.
Wakati mabishano hayo yakiendelea, Askari Polisi mmoja  alijichanganya na kuingia katikati ya wafuasi wa Chadema pembeni mwa uwanja huo ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa na bomu June 15 2013.

Baada ya hapo, wafuasi hao hawakupenda kitendo cha Polisi kujichanganya nao hivyo ikazuka ugomvi huku wakitaka atoke, baada ya dakika kadhaa  mabumu yalianza kusikika.

Baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho waliokuwepo uwanjani haponi mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika,Ezekia Wenje,Tundu lissu, Halima Mdee.

TFF yapongeza mashabiki kuiunga mkono Stars

Stars wakishangilia moja ya mabao yao dhidi ya Ivory Coast

Na Boniface Wambura

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawashukuru washabiki kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Taifa Stars na Ivory Coast (The Elephants) iliyochezwa juzi (Jumapili) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwitikio wa washabiki katika mechi hiyo ilikuwa ni moja ya chachu ya kiwango kilichoonyeshwa na Taifa Stars, kwani walishangilia mwanzo hadi mwisho licha ya kupoteza kwa mabao 4-2.

Ni matarajio utakuwepo mwitikio kama huo huo katika mechi ijayo ya Taifa Stars ya michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Nyumbani (CHAN) dhidi ya Uganda (The Cranes) itakayochezwa Dar es Salaam kati ya Julai 12-14 mwaka huu. Stars itaingia tena kambini Julai 4 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo.

Mbongo kukipiga Yemen, TFF yatoa ITC yake


Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Mtanzania Gossage Mtumwa ili aweze kucheza mpira nchini Yemen.

Mtumwa ambaye anatoka katika kituo cha kukuza na kuendeleza vipaji cha Rollingstone cha Arusha aliombewa hati hiyo na Chama cha Mpira wa Miguu cha Yemen (YFA) kwa ajili ya kucheza nchini humo.

TFF inamtakia kila la kheri Mtumwa katika safari yake ya Yemen, na ni matarajio yetu kuwa atakuwa balozi mzuri wa Tanzania nchini humo ili wachezaji wengine wa Tanzania nao wapate fursa ya kucheza mpira wa miguu nchini Yemen.


Kamishna Alferd Rwiza kuhudhuria Semina CAF

Na Boniface Wambura
KAMISHNA Alfred Kishongole Rwiza ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuhudhuria semina ya makamishna itakayofanyika kuanzia Julai 6-7 mwaka huu katika makao makuu ya shirikisho hilo jijini Cairo, Misri.

Semina hiyo inashirikisha baadhi ya makamishna wa CAF walioko kwenye orodha ya makamishna ya shirikisho hilo kwa mwaka 2012-2014.

Rwiza ni mmoja wa makamishna wa CAF kutoka Tanzania, na mechi ya mwisho kusimamia ilikuwa ya Kombe la Shirikisho iliyochezwa Mei mwaka huu nchini  Msumbiji.

CAF tayari imeshamtumia tiketi Rwiza, na anatarajia kuondoka nchini Julai 4 mwaka huu kwenda Cairo kwa ndege ya EgyptAir.

Mbunge CHADEMA, Mr Sugu atapata ajali akielekea Arusha

Mbuinge wa Mbeya Mjini-CHADEMA, Mhe. Joseph Mbilinyi 'Sugu'
Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi amepata ajali hivi punde katika eneo la kasheki wilayani Hanan'g akielekea Arusha mjini.

Joseph Mbilinyi maarufu Sugu alikuwa akielekea Arusha mjini kuungana na wabunge wengine ktk shughuli ya kuaga marehemu
waliolipukiwa na bomu kwenye mkutano wa Chadema, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika ajali hiyo hakuna mtu yoyote amejeruhiwa, Mbunge huyo yuko salama, gari la Sugu limeharibiwa vibaya baada ya kugongana na basi la abiria.

Kichanga chatafunwa na mbwa baada ya kutupwa kichakani

mbwa kama huyu amemtafuna kitoto kichanga
MTOTO mchanga ameliwa na mbwa na  kubakishwa mguu, baada ya mtu asiyejulikana kukitelekeza kichakani katika eneo la Magole, mtaa wa Kivule, Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam.Tukio hilo la kusikitisha limebainika baada ya mbwa huyo kukibeba kiungo hicho kutoka kilipokuwa na kukifikisha nyumbani anakofugwa majira ya sita mchana juzi.
Mwenye mbwa huyo aliyejitambulisha kwa jina la Maria John, aliiambia NIPASHE kuwa, kabla ya kupelekwa mguu huo, jana yake mbwa huyo alikwenda na utumbo ambao hata hivyo hakuna aliyekuwa  na hofu nao, kwani walidhani ni wa kuku.
 
“Niliona ni kitu cha kawaida tu, mbwa hutembelea maeneo mbalimbali labda ameokota mzoga wa kuku, lakini leo (juzi) nilipoona mguu nilistaajabu na kufahamu kuwa ni kiungo cha binadamu nilitoa taarifa kwa majirani na kupata msaada,” alisema.
 
Alisema lengo la kutoa taarifa kwa majirani zake ni ili waweze kujadiliana na  kutamfuta aliyefanya kitendo hicho cha kikatili kisha baadaye kutoa taarifa kwa mjumbe wa mtaa huo.
 
Mmoja wa majirani waliokusanyika kushuhudia tukio hilo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema hajawahi kushuhudia tukio kama hilo.
 
“Ni tukio la kushangaza na kusikitisha sana kwa mtu kukatisha maisha ya kiumbe kisicho na hatia,kwani huwezi kujua mungu alimpangia nini duniani, hivyo kwa kweli kama mama najisikia uchungu sana,” alisema.
 
Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa eneo hilo, Grace Martin, alisema alipigiwa simu na mdogo wake kuwa, mbwa ameokota kiungo cha mtoto na  kutakiwa kurudi mtaani hapo haraka.
 
“Nilipofika nilihakikisha kuwa kweli ni mguu wa mtoto, niliamua kumpigia simu Mwenyekiti wa Mtaa kwa ajili ya msaada,”alisema.
 
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivule,Joseph Gassaya alisema yeye alipojulishwa alitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kituo cha Stakishari Ukonga nao baada ya muda mfupi walifika eneo la tukio.
 
Alisema askari walitoa amri ya kukizika kiungo hicho katika eneo hilo, huku Jeshi la Polisi likiendelea na upelelezi wa kumsaka mama aliyefanya ukatili huo ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria.
 
Chanzo:Nipashe

Monday, June 17, 2013

KONYAGI YAWAPIGA MSASA WABUNGE KUHUSU BIASHARA VIROBA


 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa, akionesha kinywaji cha Afrika Kusini kilichofungwa kwenye viroba kama ambavyo Konyagi inafanya hapa nchini.Vinywaji kama hivyo vipo karibu nchi nyingi Ulimwenguni.

 Meneja wa Masoko wa Konyagi, Joseph Chibehe akielezea jinsi vinywaji vyao vinavyochangia mapato ta serikali
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo,Maji na Mifugo, Said Nkumba akichangia mada hiyo kwa kuviasa baadhi ya vyombo vya habari kuacha kuandika habari za kudidimiza viwanda vya haba nchini. Kulia ni Idd Azzan Mbunge wa Kinondoni na Dunstan Kitandula ambaye ni Makamu Mwenyekiti was  Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara.
                               Bidhaa mbalimbali zikiwa zimfungwa kwenye viroba
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa () akifafanua jambo katika semina ya wajumbe wa Kamati mbili za Bunge za Uchumi,Viwanda na Biashara  pamoja na Kilimo,Maji na Mifugo kuhusu baadhi ya vyombo vya habari vyenye uhusiano na nchi jirani vinavyotumika kupiga vita viwanda vya ndani kikiwemo cha Konyagi. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amos Makala, akichangia mada katika semina hiyo. Kushoto ni Naibu Waziri wa TAMISEMI, Kassim Majaliwa na Said Nkumba.
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara, Dunstan Kitandula akichangia mada hiyo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa (kushoto) akimkabidhi jezi Idd Azzan kwa ajili ya timu ya Bunge iliyocheza na timu ya Konyagi kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma Jumamosi
 Mgwassa akikabidhi jezi ya timu ya Konyagi kwa Idd Azzan tayari kwa mtanange na timu ya Bunge
 Meneja Masoko wa Konyagi, Joseph Chibehe (kushoto) akimkabidhi W. Zuberi  msaada wa vyerehani, ambavyo alivipokea kwa niaba ya BNaibu Spika wa Bunge, Job Ndugai
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora, George Mkuchika, akisalimiana na timu ya Bunge muda mfupi kabla ya pambano lao na timu ya Konyagi, kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

 George Mkuchika akisalimiana na wachezaji wa timu ya Konyagi
 Wachezaji wa timu ya Bunge wakisalimiana na wachezaji wa Konyagi
 Kikosi cha timu ya Bunge kilichochuana na Konyagi
Kikosi cha timu ya Konyagi kilichomenyana na Timu ya Bunge

CCM yalaani tukio la mlipuko wa bomu Arusha wakiitupia lawama CHADEMA


Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza  na waandishi wa habari leo mjini Dodoma.

CHAMA cha Mapinduzi, CCM kimetoa tamko la kulaani tukio la mlipuko wa bomu uliotokea kwenye mkutano wa CHADEMA, ambapo watu wawili walipoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na blog ya chama hicho ikimnukuu Katibu Mwenezi wake, Nape Nnauye, CCM imesema tukio hilo linasikitisha na tukio hilo huku ikiwatupia lawama viongozi wa CHADEMA kwa kulitumia tukio hilo kisiasa zaidi, huku wakiipongeza serikali.
Ripoti hiyo ya CCM isome mwenyewe hapo chini;
Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na mbili (22)  kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.
 Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.


 Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka. Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.
 Kata nne za jiji la Arusha hazikufanya uchaguzi baada ya kuahirishwa kufuatia tukio la kusikitisha la kulipuka kwa bomu kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema mjini Arusha tarehe 15/06/2013.


 CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu. Tunawapa pole wale wote walioathirika na tukio hilo. Ni vizuri serikali ikalichunguza swala hili kwa kutumia muda mfupi na kuhakikisha waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua zinazostahili.


 Pamoja na kulaani na kuitaka serikali kukomesha vitendo hivi nchini, ni wakati muafaka kwa vyama vya siasa nchini kujitazama upya kwani kuna kila dalili kuwa tukio hili kama alivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari mhe. Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni la kupangwa, inawezekana limepangwa na Chadema wenyewe.
 Hali ya kisiasa jijini Arusha kuelekea uchaguzi huo ilikuwa wazi kuwa wana Arusha walishaamua kuzirudisha kata hizo nne kwa CCM, hasa baada ya kuchoshwa na maandamano na vurugu za kila siku jijini Arusha. Aidha kauli za kukata tamaa za viongozi wa Chadema na vitendo vyao ni dalili tosha kuwa tukio hili lilipangwa na Chadema wenyewe.


 CCM tunaendelea kusisitiza na kulaani juhudi za wenzetu kujaribu kujenga umaarufu wa chama chao juu ya damu za Watanzania. Juhudi hizi zinapaswa kulaaniwa na wazalendo wote ndani na nje ya nchi. Tukumbuke asiyekubali kushindwa, si mshindani. Si busara wala uungwana na ni kinyume na utu kutumia majanga ya kutengeneza kama mtaji wa kisiasa.
 Lakini CCM tunalaani pia kitendo cha viongozi wa Chadema kujaribu kutumia baadhi ya misiba na majeruhi wa tukio hili kisiasa na mwisho wa siku kwenda kuwatelekeza hospitali baadhi yao baada ya kuwaahidi kubeba gharama zote za matibabu na mazishi.Tunaipongeza serikali kwa kuingilia kati na kuwasaidia waathirika hawa na kuhakikisha wanapata huduma inayostahili.


 CCM inarudia kueleza masikitiko yake kwa waathirika wa tukio hili la kinyama na kikatili lisilostahili kuvumiliwa hata kidogo. Kama Chama tumeguswa sana na tukio hili pamoja na kulilaani, tunawasihi watanzania tushindane na kutofautiana bila kupigana na kuvunja tunu ya nchi yetu ya amani na utulivu. Katika demokrasia ya vyama vingi swala la kuvumiliana ni swala la msingi sana katika kufikia ukomavu wa demokrasia hiyo.


 Imetolewa;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi.
17/06/2013
 
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary

PRESIDENT KIKWETE TOURS SUNDERLAND FC 

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete and Chairman and owner of Sunderland Football Club Mr.Ellis Short pose with some students who study football skills at the club’s Academy of Light in Sunderland yestarday afternoon. The Club in collaboration with Symbion Power Tanzania Limited have agreed to build a state of the art football academy in Dar es Salaam at the request of President Kikwete. President Kikwete is London for a three days working visit.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete talks to pupils attending  some lessons on football skills AND HEALTH  at Sunderland’s Association Football Club Academy of Light in Sunderland yestarday afternoon.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with Sunderland’s Association Football Club  Chairman and owner Mr.Ellis Short at the Club’s Stadium of Light in Sunderland yestarday afternoon.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete and his delegation pose with some students who attend football training at Sunderland’s  Association Football Club Stadium of Light Academy yestarday afternoon. Others in picture from left are Symbion’s Power Limited CEO Mr.Paul Hinks(left), Ilala member of parliament Hon. Musa Zungu(Second left), Minister for Information,Youth ,Culture and Sports Dr.Fenella Mukangara(fourth left) and Minister for Land and Human Settlement Prof.Anna Tibaijuka(right).
President  Dr.Jakaya Mrisho Kikwete unveils Sunderland’s Association Football plaque at the club’s Academy of Light yestarday afternoon when the President and his delegation toured the club. On the left, looking on, is the Club’s Chairman and Owner Ellis Short.(photo by Freddy Maro).

LUCY CHARLES NDIYE KISURA WA JIJI LA MWANZA


SHINDANO la kumsaka mrembo wa mkoa wa Mwanza kwa mwaka 2013, kiliteguliwa mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya Lucy Charles, msomi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino kuwabwaga warembo wengine 13 waliojitokeza kuwania taji hilo.

Nyota ya mrembo huyo ilianza kuonekana mapema katika mavazi yote aliyovaa, lakini zaidi aliwapagawisha mashabiki wa urembo waliofurika katika ukumbi wa Yatch club baada ya kujibu swali kwa ustadi lililouliza ni changamoto ipi kubwa walionayo vijana wa leo.

Mshindi wa pili katika shindano hilo alikuwa Judith Josephat na mshindi wa tatu ni Suzan Ikombe.
Washindi hao watauwakilisha mkoa wa Mwanza katika shindano la kanda ya ziwa litakalofanyika mwishoni mwa mwezi huu.

MAREHEMU LANGA KILEO AAGWA LEO, AZIKWA JIONI HII




 Mwili wa marehemu langa ukiwa umeishafika nyumbani kwa ajili ya kuombewa na kuagwa 
 Baadhi ya ndugu na jamaa waliofika kuuaga mwili wa Marehemu langa Nyumbani kwao
<

Mama na Baba wa Marehemu Langa wakiwa na uzuni wakati wa kuagwa kwa mwili wa marehemu Langa leo mchana
 Baadhi ya wananchi waliokuja kumuaga Marehemu Langa nyumbani kwao



 Baadhi ya marafiki na wapenzi wa marehemu Langa wakiwa katika makundi
Mara baada ya zoezi hilo la kuagwa kwa mwili wa Langa, msafara ulianza kuelekea makaburi ya Kinondoni ili kuuhifadhi katika nyuma yake ya milele ambapo muda huu ndiyo anazikwa.

Taifa Stars kuingia tena kambini Julai 4



Na Boniface Wambura
KOCHA wa Taifa Stars, Kim Poulsen ameiita tena kambini timu hiyo Julai 4 mwaka huu kujiandaa kwa mechi ya kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inavunja kambi leo (Juni 17 mwaka huu) baada ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, kundi C Kanda ya Africa dhidi ya Ivory Coast iliyochezwa jana (Juni 16 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kim amesema wachezaji watakaoitwa kambin ni wote walioko kwenye timu hivi sasa isipokuwa Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaocheza mpira nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) katika klabu ya TP Mazembe Englebert.

Wachezaji hao ni Juma Kaseja, Aishi Manula, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi.

Mechi hiyo namba 37 dhidi ya Uganda (The Cranes) itachezwa jijini Dar es Salaa kati ya Julai 12 na 14 mwaka huu wakati ile ya marudiano itafanyika wiki mbili baadaye katika Uwanja wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Jiji la Kampala.

Epiq Open Mic kumekucha Dar

Vijana waliojitokeza wakiwa kwenye foleni. 
 Jopo la washauri likongozwa na Marco Chali (wa pili toka kulia), akifuatiwa na Dknob, Walter na mwisho kulia ni Godzila
 Mmoja wa vijana akiimba mbele ya washauri.
Mmoja wa wasichana akionyesha uwezo wake.

Vijana waliojitokeza wakijiandikisha.


NaMwandishi wetu


Baada ya kuzinduliwa kwa mafanikio wiki mbili zilizopita katika viwanja vya Mwembe Yanga, mamia ya vijana wamejitokeza mwishoni mwa wiki hili katika viwanja ya ofisi za Zantel kuhudhuria usaili wa Epiq Open Mic.
Huku ikiwa imebaki wiki kadhaa kabla ya kuanza kwa msimu mya wa Epiq BSS, Zantel kwa kushirikana na Marco Chali Foundation, wamezindua Epiq Open Mic ili kuwapa vijana nafasi ya kuonyesha vipaji vyao.
Fursa hii, ya Epiq Open Mic, inawapa nafasi vijana wenye vipaji vya muziki fursa ya kusikilizwa na mtayarishaji wa muziki maarufu nchini, Marco Chali pamoja na jopo la wanamuziki kama Godzila na Dknob, ambao wanawashauri mambo kadhaa kuhusiana na muziki wao, na huku wale wenye vipaji zaidi wakipewa nafasi ya kurekodi na Marco Chali.
Akizungumzia Epiq Open Mic, Marco Chali anasema hii ni fursa ya vijana kujifunza misingi ya muziki, lakini pia kuweza kurekodiwa muziki wao.
‘Lengo la Epiq Open Mic ni kuwahamasisha vijana kushiriki katika kukuza vipaji vyao, kuongeza uelewa wa mambo ya muziki pamoja na kuchangamkia fursa zilizopo katika muziki’ alisema Chali.
Marco Chali ambaye pia ni mtunzi na mwimbaji, ametayarisha nyimbo nyngi ambazo zimeshinda tuzo ndani na nje ya nchi za wasanii kama Ms. Trinity kutokea Jamaica, A.Y wa Tanzania, Prezzo wa Kenya, J Martins kutoka Nigeria na wengine wengi.
Kwa upande wake, Afsa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan alisema kampuni ya Zantel inaaminini katika kuwawezesha vijana kufikia ndoto zao.
‘Muziki ni ajira kwa vijana wengi, na kuamini hilo ndio maana kampuni ya Zantel imeamua kuwafikia vijana wote wenye vipaji na kuwapa nafasi ya kuonekana’ alisema Khan.