STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 23, 2013

Huyu ndiye Hussein Javu mkali wa mabao wa Mtibwa Sugar

Javu wa tatu toka kushoto akiwa na kikosi cha Mtibwa Sugar
Jamaa nouma, Ona alivyuowaacha akina Himid katika pambano baina ya timu zao
Hapa akijifua katika timu ya taifa, Taifa Stars
moza
Akiwajibika uwanjani na kikosi cha Stars
Akitokelezea kibrazamen akiwa home
INGAWA anadai amefunga magoli mengi kiasi hakumbuki idadi yake kamili, lakini Husseni Javu anasema mabao aliyowafunga Yanga katika pambano la duru la kwanza la Ligi Kuu msimu uliopita ndiyo matamu asiyoyasahau kwa urahisi.
Katika mechi hiyo iliyochezwa Sept. 19, mwaka jana, mshambuliaji huyo nyota wa Mtibwa Sugar na Taifa Stars, alifunga magoli mawili yaliyotosha kuipa Mtibwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Yanga na kusababisha aliyekuwa kocha wa timu hiyo ya Jangwani, Tom Saintfied kutimuliwa klabuni hapo akiwa na siku 77 tu.
Javu anasema kwa jinsi alivyoyafunga kiufundi na kuzima ngebe za wapinzani wao waliotamba kushinda kabla ya pambano hilo ndiyo inayomfanya asiyasahau.
"Kwa yeyote aliyeyaona atakubaliana nami yalikuwa ya ufundi na kubwa zaidi ni kukata kilimilimi cha Yanga kwa kuwalaza mabao 3-0 licha ya tambo zao kwamba wangetuchapa Jamhuri," anasema.
Javu shabiki mkubwa wa Manchester United na anayemhofia beki wa zamani wa Simba aliyetua Coastal Union, Juma Nyosso anasema hata hivyo pambano gumu kwake lisilofutika kichwani ni lile la Mtibwa na Mgambo JKT.
Anasema anaikumbuka mechi hiyo ya duru la pili lililochezwa Mkwakwani Tanga kwa sababu ya kuchezewa vibaya na beki aliyekabana naye asiyemkumbuka jina kiasi cha kumtia hasira na kulimwa kadi ya njano kabla ya kocha wake Mecky Mexime kumpumzisha ili kumwepusha na kadi nyekundu.
"Sijawahi kukutana na mechi ngumu kama ile ya Mgambo JKT hasa beki yake iliyokuwa inacheza kwa vurugu hadi nikapewa kadi ya njano na kumfanya kocha anitoe nje,"anasema.
Anasema licha ya vurugu hizo anashukuru Mtibwa walishinda bao 1-0 kupitia Salvatory Mtebe.

YANGA
Javu aliyeanza soka tangu akisoma Shule ya Msingi Turiani-Kilimanjaro, Morogoro na chandimu akikipiga Mwembeni Stars, amekuwa akitajwa kutua Yanga kwa msimu ujao, japo mwenyewe ameziruka taarifa hizo.
Mkali huyo ambaye hajaoa japo ana mchumba na watoto wawili kati ya watatu aliyokuwa nao baada ya mmoja kufariki, anakiri Yanga na Simba zilishamfuata kumtaka ajiunge nazo, ila hajasaini kokote.
"Sijasaini kokote kwani Simba na Yanga ziliponifuata nilizieleza nina mkataba na Mtibwa hivyo wazungumze na viongozi ili waafikiane," anasema.
Anadai tangu baada ya hapo hajajulishwa chochote na kushangaa kudaiwa  ameshamwaga wino Jangwani, huku akizushiwa pia ni majeruhi wa kudumu.
"Taarifa hizi zinashangaza wakati ni juzi tu tumemaliza ligi na kuichezea Mtibwa karibu mechi zote sasa majeraha hayo yametoka wapi," anahoji.
Anadai taarifa hizo zimempa usumbufu kwa kocha na daktari wake wakidhani aliumia kwenye 'ndondo' wakati hazina ukweli.
Javu anayependa kula chakula kizuri kwa afya na kunywa juisi , anasema kama Yanga na Mtibwa wamekubaliana juu yake, yeye hajajulishwa.
Hata hivyo anasema kama Yanga imemtaka kweli wamalizane na uongozi wake anaodai anauheshimu kwa kumtoa mbali kisoka tangu alipotua timu ya vijana enzi za kocha anayemsifia 'King' Abdallah Kibadeni.
"Hakuna asiyependa kuzichezea timu kubwa hivyo Yanga wakimalizana na Mtibwa nami nikaridhishwa na masilahi sitakuwa na tatizo lolote, soka ni ajira yangu na kokote nacheza,"anasema.
Javu (kulia) akiwa na jamaa yake Bakar Seblungo 'Beka'

TUZO
Hussein Omar Javu, alizaliwa Februari 16, 1988 Turiani Morogoro akiwa mtoto wa pili kati ya sita wa familia yao na alisoma Shule ya Msingi Turiani Kilimanjaro kabla ya kubobea jumla katika soka.
Anasema wakati akiibuka katika soka alikuwa akiitwa Hussein Masha, bila kujua sababu, ingawa anamkumbuka nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Tanzania aliyewahi kutamba na Pamba, Simba na Taifa Stars.
"Mtaani walikuwa wakiniita Masha, cha ajabu Masha alikuwa kiungo mimi tangu utoto nacheza ushambuliaji ila nililizoea jina hilo,"anasema. 
Anasema wakati akiichezea chandimu aliumia tumboni na kumfanya baba yake amzuie kucheza kwa miaka mitatu kabla ya kubembelezwa wadau wa soka kijijini kwao wakiongozwa na Mzee Hamis Cheza na kurejea tena uwanjani.
"Kama siyo Mzee Hamis sidhani kama ningecheza tena kwani baba hakutaka kusikia habari za soka akihofia ningeumia tena, niliporuhusiwa nilijiunga Kingstone." anasema.
Mkali huyo anayeitaka serikali kuwekeza katika soka la vijana kwa kuboresha shule za michezo hasa kuzisaidia 'academia' zilizopo ili kuibua na kukuza vipaji, anasema baada ya kuichezea Kingstone katika Ligi Daraja la Tatu alihamia kwa mahasimu wao Docks na kuongeza uhamasa mkubwa mpaka sasa.
Alipokuwa Docks alifuatwa na Alphonce Modest kumshawishi ajiunge Mtibwa iliyokuwa ikisaka vijana wa kuunda timu ya vijana ambapo hata hivyo alikataliwa kabla ya Kibadeni kumkingia kifua na kumbakisha akishajiliwa mwaka 2007.
Akiwa na timu ya vijana walishiriki michuano ya Uhai na kufanikiwa kuibuka  Mfungaji Bora akiifungia timu yake iliyomaliza nafasi ya tatu jumla ya mabao 7.
Javu anasema kabla ya tuzo hiyo alishanyakua tuzo nyingine kama hiyo katika michuano kadhaa ya mchangani mjini Morogoro na ameendeleza moto wa mabao hata alipopandishwa timu ya wakubwa ya Mtibwa aliyonayo mpaka sasa.
Anasema japo hajapata mafanikio makubwa katika soka, anashukuru amenunua kiwanja, kutwaa tuzo na mataji kadhaa kama ya Tusker na Mapinduzi akiwa na Mtibwa mbali na kumudu maisha na familia yake.
Ndoto za Javu ni kucheza soka la kulipwa na anasema analizwa na kifo cha mwanae huku akiwataja King Kibadeni, wazazi wake, rafikie Bakari Seblungo na kaka yake Mrisho Javu kama waliomsaidia kufika alipo.
Javu anayewataka wachezaji wenzake kupendana na kuzingatia nidhamu anadai anaimani kubwa Stars kufuzu fainali za CHAN kwa mara ya pili baada ya zile za mwaka 2009.

Rais JK akutana na Tony Blair Ikulu Dar es Salaam

 Rais Jakaya Kikwete akiwa na Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair na mkewe Cherrie Blair alipokutana nao Ikulu jijini Dar es salaam leo. (PICHA NA IKULU)



Majanga: Msafara wa mazishi ya wanajeshi waliouwawa Darfur wapata ajali

 Picha mbali mbali za ajali ya gari iliyokua katika msafara wa maziko ya wanajeshi waliouawa Darfur iliyotokea Mwanakwerekwe sokoni umbali wa mita 300 kutoka Makaburi ya Mwanakwerekwe ambapo ndiko walipozikwa Wanajeshi hao.(Picha na Haroub Hussein).






                                            Gari lililopata ajali

Lililoua mdogo wake kwa mibangi lanaswa na Polisi

JESHI la polisi mkoa wa Singida limefanikiwa kumkamata Elibariki Alphoce (21) mkazi wa kijiji cha Kizega wilaya ya Iramba, anayetuhumiwa kumuua mdogo wake Mariam (9) mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi Kizega.

Elibariki anatuhumiwa kumuua mdogo wake Mariam Julai 16 mwaka huu katika kijiji cha Kizega kwa kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili na kisha kuteganisha kichwa na kiwiliwili.

Ilielezwa kuwa Elibariki ni mtumiaji sugu wa madawa ya kulevya aina ya bangi.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida ACP Geofrey Kamwela, amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa Julai 18 mwaka huu akiwa amejificha kando kando ya mto Ruruma wa kijiji cha Ruruma tarafa ya Kiomboi.

Polisi Dar wayanasa majambazi 8 na silaha 7 lakana Mnyika kukoswa na bomu

IMG_9423
Baadhi ya askari polisi wakionyesha kwa waandishi wa habari silaha zilizokamatwa kutoka kwa watuhumiwa wa matukio ya ujambazi.

IMG_9432
DCP Mlege akitoa taarifa ya mafanikio ya Jeshi hilo kwa waandishi wa habari ambapo akizungumzia suala la Mh. Mnyika amesema askari No. E. 5340 D/CPL Julius aliyekuwa ndani ya gari la polisi PT. 1902 alikuwa anasogeza boksi lenye mabomu ya kutoa machozi ya kurusha kwa mkono, kwa bahati mbaya bomu hilo lililipuka ndani ya gari hilo na halikuleta madhara yeyote kwa askari polisi wala raia waliokuwa eneo la uwanja wa Sahara uliopo Mabibo ambako chama cha CHADEMA kilikuwa kifanye mkutano wa hadhara tarehe 21 Jula 2013 kinyume na utaratibu.

Jeshi la Polisi Kanda maalum Dar es Salaam limefanikiwa kukamata sila 5 ikiwemo SMG moja, Shortgun mbili, Riffle Mark 3 tatu, Pisto moja, Risasi 56, Maganda ya Risasi 17 na Majambazi 8.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Kamishna wa polisi kanda hiyo, DCP A.M. Mlege amesema zoezi hilo lilifanyika Julai 18 mwaka huu katika maeneo ya Magomeni wilaya ya Kinondoni.

Amesema pia Jeshi hilo limeweza kukamata magari ya wizi matano, Injini tatu za magari, Vipande vya magari yaliyokatwa spea na wezi watano wa magari.

Katika hatua nyingine Jeshilo limekanusha habari zilizotolewa katika vyombo vya habari kuwa mbunge wa Jimbo la Ubungo Mh. John Mnyika kukoswa na bomu na kumjeruhi mmoja wa wafuasi wake.

Aidha limeomba siku zingine kabla ya kutoa habari ni vizuri likaulizwa ili kuthibitisha au kukanusha.

DCO Mlege amesema pia Jeshi la polisi Kanda maalum Dar es Salaam limemkamata tapeli hatari anayetumia namba tofauti za mitandao ya simu na majina ya watu maarufu anajulikana kwa jina la Mfaume Omari maarufu kama ‘Mau’.

Chanzo - MOBLOG 

Rais wa Zanzibar aongoza mazishi wa wanajeshi waliouwawa Darfur

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, (wa tatu kulia) akijumuika na Vingozi na Waislamu wengine katika kuwaswalia  Merehemu Sgt. Shaibu Shehe Othman, na Cpl Mohammed Juma Ally katika Msikiti wa Nuru Muhammad, Mombasa mjini Unguja leo. (Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu)
 Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wakibeba Jeneza la mwili wa Marehemu Sgt Shaibu Shehe Othman, baada ya kuwasili mjini Zanzibar akiwa ni miongoni mwa wanajeshi 7 waliouwawa kwa kupigwa risasi Jimbo la Darfur nchini Sudan hivi karibuni.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, akitia udongo katika kaburi la Marehemu Sgt. Shaibu Shehe Othman, aliyezikwa leo katika makaburi ya Mwanakwerekwe mjini Unguja. 
 Baadhi ya Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania na Ndugu na Jamaa wa marehemu Sgt Shaibu Shehe Othman, na  Cpl Mohammed Juma Ally wakishiriki mazishi hayo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, (katikati) na Viongozi na Waislamu, wakiangalia  Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania, walipokuwa wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu Sgt. Shaibu Shehe Othman, wakati wa mazishi yake katika makaburi ya Mwanakwerekwe leo.

SHIWATA watakiwa kuchangia ujenzi wa nyumba Mkuranga

Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Twalib 'Teacher' (kushoto)
Na Mwandishi Wetu
MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) umewataka wanachama wake kuchangia ujenzi wa nyumba zao katika kijiji cha Mwanzega, Mkuranga ili kukamilisha mradi huo.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA), Caasim Taalib alisema jana Dar es Salaam katika mkutano wa wanachama wanaochangia ujenzi ambapo mpaka sasa nyumba 29 zimekamilika na wanachama 220 wamechangia ujenzi na jumla zilizokusanywa ni mil. 82.5.
Alisema SHIWATA haina fedha za kujenga nyumba za wanachama wake wala haina chanzo cha mapato kama si kwa njia ya kuchangishana na baada ya hapo kuwakabidhi wale waliokamilisha uchangiaji wa ujenzi wa nyumba hizo.
‘Ujenzi wa nyumba za wasanii utafanikiwa kwa kila mwanachama kuchangia nyumba yake kwa kujiaminisha kuwa hakuna utapeli wala biashara katika gharama za ujenzi wa nyumba hizo’alisema Taalib.
SHIWATA ambayo inaundwa na wasanii, wanamichezo, wanahabari na vijana wapatao 7,000 ilikuwa ikabidhi nyumba Agosti mwaka huu kwa mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Jellah Mtagwa na wasanii wengine 14 ambao wamekamilisha michango ya ujenzi  wa nyumba zao katika kijiji chao cha Mwanzega Kimbili, Mkuranga.
Wengine watakaokabidhiwa nyumba zao ni msanii maarufu nchini, Lumole Matovola ‘Big’ wa Bongo movie ambaye ni mwanachama wa SHIWATA wangine ni Mwandishi wa Habari, Josephine Moshi, Farida Ndimbo wa Jeshi la Magereza, Flora Kafwembe wa JKT Mgulani na Nyanza Kisadugwa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).  
Mpaka sasa SHIWATA imejenga nyumba 29 kwa ajili ya wasanii katika eneo la hekari 300 na wanajiandaa kulima shamba la hekari 500 walizonazo ili kujikwamua kimaisha.
              

Master Kinyogoli awafua mabondia Idd Mnyeke, Ibrahim Class

 Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kushoto akipambana na Iddy Mnyeke wakati wa mazoezi yanayoendelea katika Kambi ya Ilala Amana CCM mabondia hao wanafanya mazoezi kwa ajili ya mashindano yao yatakayo fanyika baada ya kumarizika mwezi mtukufu wa Ramadhani 


Bondia Iddy Mnyeke  akipambana na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kamba ya Amana CCM Dar es salaam mabondia hao watapanda ulingoni kuwakabili wapinzani wao baada ya kwisha kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani 

Bondia Iddy Mnyeke  akipambana na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kamba ya Amana CCM Dar es salaam mabondia hawo watapanda ulingoni kuwakabili wapinzani wao baada ya kwisha kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani kulia ni kocha Mkongwe Habibu Kinyogoli 'Master' 
Bondia Omari Bai kushoto akisimamiwa kupiga begi na Kocha Kondo Nassoro wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kambi ya Ilala 
Bondia Iddy Mnyeke  akipambana na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kamba ya Amana CCM Dar es salaam mabondia hawo watapanda ulingoni kuwakabili wapinzani wao baada ya kwisha kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani kulia ni kocha Mkongwe Habibu Kinyogoli 'Master' 
BONDIA IDDY MNYEKE AKIWA KATIKA POZI
Bondia Iddy Mnyeke  akipambana na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kamba ya Amana CCM Dar es salaam mabondia hawo watapanda ulingoni kuwakabili wapinzani wao baada ya kwisha kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani Picha na BLOG YA SUPER D
Bondia Iddy Mnyeke  akipambana na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kamba ya Amana CCM Dar es salaam mabondia hawo watapanda ulingoni kuwakabili wapinzani wao baada ya kwisha kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani 
IDDY MNYEKE
BONDIA OMARI BAI AKIPIGA BEGI
Bondia Omari Bai kushoto akisimamiwa kupiga begi na Kocha Kondo Nassoro wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kambi ya Ilala

Kim atamba Stars imjeiva kuwang'oa Uganda The Cranes

Kim Poulsen
 Na Boniface Wambura
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amesema kikosi chake kimejiandaa kuikabili Uganda kwenye mechi ya marudiano ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) itakayochezwa Jumamosi jijini Kampala.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza leo, Kim amesema tangu kikosi chake kimeingia kambini Julai 14 mwaka huu, wachezaji wamekuwa wakifanya vizuri kwenye mazoezi na wako tayari kwa ajili ya mechi hiyo.

“Uganda ni timu bora kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Mechi itakuwa ngumu, tunaamini tunakwenda kufanya vizuri. Tayari tunayo mikakati kwa ajili ya mechi hiyo, tunakwenda kuikamilisha Kampala,” amesema Kim.

Hata hivyo, Kim amesema licha ya mwitikio mzuri wa wachezaji kwenye mazoezi lakini wanakabiliwa na changamoto ya wengi wa wachezaji kuwawamefunga wakati wachezaji wanapokuwa kambini wanatakiwa kula, kunywa na kupumzika.

“Hiki ni kipindi kigumu kwa mpira wa miguu, na suala la kufunga ni la kiimani ambapo hatuwezi kuwazuia wachezaji kufunga. Karibu nusu ya wachezaji wanafunga, hii ni changamoto ambayo tunaiheshimu,” amesema Kim na kuongeza kuwa ni wazi kikosi chake cha kwanza kitakuwa na mabadiliko baada ya beki Shomari Kapombe kwenda kwenye majaribio nchini Uholanzi.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inaondoka Mwanza kesho (Julai 24 mwaka huu) saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir na kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 8.15 mchana.

Wachezaji waliomo kwenye msafara huo ni makipa Juma Kaseja, Mwadini Ali na Ali Mustafa. Mabeki ni Aggrey Morris, David Luhende, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Nadir Haroub na Vincent Barnabas.

Viungo ni Amri Kiemba, Athuman Idd, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Khamis Mcha, Mudhathir Yahya, Salum Abubakar na Simon Msuva. Washambuliaji ni John Boko, Juma Luizio na Mrisho Ngasa.

Kampuni ya Isere Sports yagawa vifaa


Mkurugenzi wa masoko wa Kampuni ya Isere Sports inayoshuhulika na uagizaji na uuzaji wa vifaa vya michezo,Abbas Isere (kulia) akimkabidhi jezi Katibu Mipango wa timu ya Fresh Niga ya Kilwa Masoko ,Maulid Mtika maarufu Milulu zenye thamani ya Sh. 350,000.

Isere sports yatoa jezi kwa timu ya Kilwa Masoko
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Vifaa vya michezo, Isere Sports imetoa jezi seti moja yenye thamani ya sh. 350,000 kwa timu ya Fresh Niga ya Kilwa Masoko inayoshiriki Ligi Daraja la Tatu wilaya ya Kilwa.
Katibu Mipango wa timu ya Fresh Niga, Maulid Mtika akipokea jezi hizo jana alisema msaada huo ni mfano wa kuigwa na wafanyabiashara wengine wenye uwezo wa kusaidia kuibua vipaji vya vijana kwenye soka.

Mtika ambaye ni maarufu kwa jina la Milulu alisema imefika wakati Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) litafute njia ili lishuke mpaka ngazi ya wilaya kujua matatizo yanawakabili timu ili kutafuta vipaji vya wachezaji watakaochukua nafasi ya waliopo Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars).

'Tunao vijana wenye vipaji vya kucheza soka kufikia ngazi ya timu ya taifa, kinachowanyima nafasi ya kuonekana ni vifaa vya michezo tunaomba TFF ishuke mpaka ngazi ya wilaya kuwasaidia vijana kukuza vipaji.
Alitoa wito kwa wadau wa michezo kujitokeza kusaidia timu ambazo hazina wafadhili lakini kuna vijana ambao wako tayari kuonesha vipaji vyao
Mkurugenzi wa Masoko wa Isere Sports, Abbas Isere alisema jana kuwa msaada huo ameutoa ili kukuza vipaji vya soka katika wilaya hiyo ambao wanahitaji misaada kama hiyo ili kuendeleza vipaji.

Monday, July 22, 2013

Hatimaye ratiba Ligi Kuu yatoka, Simba, Yanga kuanza na wageni zenyewe kuumana Okt. 20

http://blog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2013/06/kochaaa.jpg
Yanga itaendelea kubebana kama hivi katika ligi ya msimu huu itakayoanza Agosti 24?
Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 inatarajiwa kuanza  kutimua vumbi rasmi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 kuwa viwanjani katika miji saba tofauti, ambapo mabingwa watetezi Yanga wataanza kibarua dhidi ya Ashanti United, jijini Dar..

Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi ya kufungua msimu (Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga na Makamu bingwa Azam itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mbali na pambano la Yanga na Ashanti litakalopigwa kwenye uwanja wa Taifa, siku hiyo ya ufunguzi wa ligi hiyo, Mtibwa Sugar na Azam zitaonyeshana kazi kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro huku JKT Oljoro na Coastal Union zitapepetana mjini Arusha kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Simba wenyewe wataanzia ugenini mjini Tabora kuumana na 'wageni' Rhino Rangers, kwenye uwanja wa Ally Hassani Mwinyi, wakati  Mgambo Shooting itaialika JKT Ruvu katika Uwanja wa Mkwakwani, mjini Tanga huku wageni wengine wa ligi hiyo Mbeya City watakuwa nyumbani mjini Mbeya kuikaribisha Kagera Sugar katika uwanja wa Soikoine na Ruvu Shooting na Tanzania Prisons zitaumana Mabatini, Mlandizi.

Pambano la watani wa jadi nchini lenyewe kwa raundi ya kwanza litachezwa Oktoba 20 ambapo Simba watakuwa wenyeji kabla ya kurudiana mwakani April 27, katika moja ya mechi za kufungia msimu Yanga wakiwa ndiyo wenyeji wa pambano hilo.

Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Novemba 3 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Aprili 27 mwakani. (Ratiba kamili ya ligi hiyo itatupiwa hapa MICHARAZO muda si mrefu)

Taifa Stars kuifuata Uganda The Cranes keshokutwa

Stars na The Craned walipoumana katika mechi ya kwanza jijini Dar es Salaam
Na Boniface Wambura
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka Mwanza keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.

Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen kesho (Julai 23 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi chake. Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye hoteli ya La Kairo jijini Mwanza.

Pepe Reina kutimkia Napoli kumfuata kocha Rafa Benitez

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02622/pepe_reina_2622933b.jpg
  GOLIKIPA wa klabu ya Liverpool, Pepe Reina anatarajiwa kujiunga na timu ya Napoli ya Italia kwa mkopo wa muda mrefu.
Kocha wa Napoli Rafael Benitez amekuwa akimkufukuzia Mhispania mwenzake huyo ambaye alikuwa nambari moja kipindi chake Anfield, baada ya kushindwa kumnasa mlinda mlango wa QPR Julio Cesar.
Reina mwenye umri wa miaka 30, alitarajiwa kurejea mazoezini katika klabu yake jana Jumapili kwa kujiunga na wachezaji wenzake huko katika ziara ya maandalizi ya msimu.
Liverpool ilimsainisha mlinda mlango Simon Mignolet raia wa Ubelgiji kutoka katika klabu ya Sunderland kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £9 mwezi uliopita.
Reina alijunga na Liverpool akitokea Villarreal mwaka 2005.

JK kuongoza watanzania kuwaaga wanajeshi waliouwawa Darfur


 

RAIS wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwaongoza Watanzania kuiaga miili ya askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
 
Shughuli ya kuiaga miili hiyo iliyowasili nchini juzi, itafanyika leo kwenye viwanja vya makao makuu ya jeshi hilo, Upanga jijini Dar es Salaam.

Miili ya wanajeshi hao iliwasili nchini juzi kwa ndege maalumu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J. K Nyerere, Terminal One na kwenda kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Wanajeshi waliouawa ni Sajenti Shaibu Othuman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Rodney Ndunguru, Peter Werema na Fortunatus Msofe.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya JWTZ, ilieleza kuwa askari hao wataagwa leo na shughuli hiyo itahudhuriwa na familia, makamanda wa jeshi na viongozi wa Serikali.
 

“Shughuli ya kuaga kwa heshima za kijeshi itaanza saa tatu kamili asubuhi katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Upanga na itaendelea mpaka mchana kabla ya kusafirishwa,” ilisema taarifa hiyo.
 

Wanajeshi hao ambao ni miongoni mwa askari wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha Kulinda Amani katika Jimbo la Darfur nchini Sudan, waliuawa kutokana na mashambulizi ya kushtukiza yaliyofanywa na waasi wanaopigana na Serikali, hivyo kuwa ni mara ya kwanza kwa idadi kubwa ya wanajeshi wa Tanzania wanaolinda amani katika nchi mbalimbali kuuawa kwa wakati mmoja.
 

Mwili wa Mr Bomba kuagwa muda huu Muhimbili rariba kamili hiko hivi

REV. John Makanyagana
Msanii John Makanyaga enzi za uhai wake
MWILI wa muigizaji mkongwe nchini, Mchungaji John Makanyaga unatarajiwa kuagwa asubuhi hii katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya saa 8 kufanyiwa misa kwenye Kanisa la Anglicana tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenye kuzikwa kwao Mpwapwa.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa hivi punde na Adam Malele' Swebe', mmoja wa waigizaji wenzake wa zamani wa Kaole Sanaa Group, mwili wa msanii hiyo aliyefahamika zaidi kama Mr Bomba utafanyiwa misa ya maombezi kanisa la Ilala Sharifu Shamba
Swebe alisema baada ya ibada hiyo ya mazishi kanisani hapo, mwili huo utasafirishwa kwenda Mpwapwa Dodoma kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika kesho Jumanne.
Marehemu Mr Bomba alifariki juzi hospitali ya Muhimbi kwa tatizo la uvimbe wa kansa katika ini na enzi za uhai wake alitamba na tamthilia mbalimbali kupitia kituo cha ITV kabla ya kuhamia kwenye filamu.
Pia alikuwa ni mwalimu na Mcghungaji wa kanisa la Anglakana mpaka mauti yalipomkumba, ambapo yamekuja huku watanzania wakiendelea kuuguza machungu ya vifo vya wasanii wengine wa uigizaji na muziki vilivyotokea mfululizo tangu mwaka jana.

Mwakyembe, Maugo kupaa kesho kwenda Russia

Mada Maugo

Benson Mwakyembe (kushoto)
MABONDIA watanzania wanaocheza ngumi za kulipwa, Mada Maugo 'King Maugo Jr' na Benson Mwakyembe wanatarajia kuondoka nchini kesho (Jumanne) kuelekea Russia kwa ajili michezo yao ya kimataifa dhidi ya wenyeji wao.
Wanamasumbwi hao wataondoka majira ya saa 10 jioni na watapanda ulingoni Jumamosi ya wiki hii katika mipambano yao ya uzito wa kati wa Kilo 75 (Super Middle).
Rais wa TPBO-Limited, Yasin Abdallah 'Ustaadh', aliiambia MICHARAZO kuwa, Maugo yeye ataenda kupigana na Movsur Yusupov  wakati Mwakyembe ataonyeshana kazi na Apti Ustarkhanov kwenye michezo itakayochezwa kwenye ukumbi wa Trade &Intertainment uliopo mjini Kasiysk, nchini Russia.
Ustaadh alisema mapambano yote hayo yatakuwa na raundi 8 kila mmoja na kwamba Watanzania hao wataungana na wakala wao kutoka Kenya, Thomas Mutua katika mji wa Dubai.
Rais huyo wa TPBO alisema mpinzani wa Maugo rekodi yake inaonyesha amecheza mapambano matatu na yote ameshindwa moja likiwa kwa KO wakati mpinzani wa Mwakyemba amecheza mechi mbili na kushinda moja na kuchapwa moja.
Hata hivyo, alisema pamoja na rekodi hizo zisizovutia kwa wapinzani wao, bado Maugo na Mwakyembe wanapaswa kwenda nchini humo na tahadhari kubwa kwani Warusi huwa hawaruhusu mabondia wa ngumi za kulipwa kucheza mpaka wawe wamepitia ngumi za ridhaa na kushiriki michezo ya Olimpiki.
Akizungumza safari hiyo, Mwakyembe aliiambia MICHARAZO asubuhi hii kwamba licha ya kutomfahamu vyema mpinzani wake, lakini anawaahidi Watanzania kwenda kuwawakilisha vyema katika mchezo huo wa kimataifa ambao ni wa pili kwake nje ya nchi.
"Naahidi sintowaangusha watanzania katika mechi hiyo ya Jumamosi, naenda nikiwa na imani ya kutaka kuweka rekodi kwa kumtwanga mwenyeji wangu na kurejea nchini kwa heshima zote, najiamini kwa mazoezi niliyofanya," alisema.
Kuhusu safari hiyo, Mwakyembe alisema kila kitu kimekaa vyema na kwamba panapo majaliwa ataondoka na mwenzake (Mada Maugo) kesho saa 10 jioni.

Suarez aitamani Arsenal, apanga kuiambia Liverpool

 http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/58/photos/888000/620x/4888.jpg
MSHAMBULIAJI Luis Suarez anajiandaa kuiambia Liverpool kwamba anataka kuhamia Arsenal.
Gazeti la Sunday Mirror limesema kuwa Liverpool wanamsubiri Suarez aombe rasmi kuondoka ndiyo wamruhusu wakati mshambuliaji huyo wa Uruguay atakapowasili kutoka mapumzikoni mjini Montevideo na kujiunga na kambi ya mazoezi mjini Melbourne.
Arsenal wameongeza matumaini ya kumpata mchezaji huyo na wanatarajiwa kurejea Anfield na ofa nono zaidi baada ya ofa yao ya awali kukataliwa.
Suarez aliweka moyo wake kujiunga na Real Madrid lakini miamba hao wa Hispania hawajajitokeza tena kutaka kumsajili baada ya kuweka wazi kwamba ofa yao ya mwisho wanayoweza kutoa ni paundi milioni 25.
Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers, alisema kuwa thamani ya Suarez ni sawa na ya Muuruguay mwenzake, Edinson Cavani aliyeuzwa kwa paundi milioni 55 kutoka Napoli kwenda PSG. 
Arsenal wameripotiwa kuwa tayari kutoa paundi milioni 40.
Kocha Arsene Wenger anaona Suarez hana shida licha ya kuadhibiwa kwa kumfanyia vitendo vya kibaguzi Patrice Evra na kumng'ata Branislav Ivanovic kwa vile nyota huyo wa Uruguay ni mchapakazi.

Shasta ahairisha kugawa utamu wa penzi

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=ACbkimIAAAlPUdQbXwAAAJWB87w&midoffset=2_0_0_1_35347&partid=2&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=297
Shasta akiwa katika pozi nyumbani kwake

MSANII wa filamu aliyejitosa pia katika muziki, Leah Mussa 'Shasta' amesitisha kwa muda harakati za kusambaza wimbo wake uitwao 'Utamu wa Penzi' ili kupisha mwezi mtukufu wa Ramadhani, imeelezwa.
Akizungumza mwishoni mwa wiki, Shasta alisema kuwa wimbo huo alioimba na H-Mbizo umeshakamilika na kilichobaki ni mambo madogo tu na kwamba, baada ya kumalizika kwa mfungo na sikukuu ya Idd ataendelea na kazi ya kuusambaza.
"Sasa wimbo huu utatoka baada ya Sikukuu ya Idd El Fitri," alisema Shasta ambaye amejitosa katika muziki baada ya kuvutiwa na wimbo 'Majanga' wa shoga yake na msanii mwenzake katika  filamu, Snura Mushi.
Baadhi ya filamu alizoshiriki Shasta ni 'Ong'wana', 'Julia', 'Kisasi za Mzimu', 'Siri za Majini' na 'Deception'.

Golden Bush Fc yazinduka Ligi ya Kinondoni

Vijana wa Golden Bush wakiwa mazoezini na kocha wao Shija Katina (kushoto) wakipeana mikakati ya kusaka ushindi katika Ligi daraja la Nne wanayoicheza kwa mara ya kwanza
BAADA ya wiki iliyopita kutibuiliwa rekodi yake ya ushindi mfululizo kwa kulazwa na Kijitonyama, timu ya Golden Bush Fc jana ilizinduka katika Ligi Daraja la Nne wilayani Kinondoni kwa kufanya 'mauaji' ya kutisha dhidi ya Shein Rangers kwa kuinyuka mabao 4-1.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam lilishuhudia vijana wa Golden Bush inayonolewa na kocha Shija Katina na Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' wakicharuka tangu mwanzo wa mchezo ili kurejesha heshima yake katiika lig hiyo.
Vijana hao walipata mabao yao yaliyotosha kuwafanya wafikishe pointi 15 katika kundi lake baada ya kucheza mechi 6 yalitumbukizwa kimiani na aliyekuwa nyota wa mchezo, Adilu aliyefunga mawili, Said na Kenan.
Timu hiyo inatarajiwa kushuka tena dimbani siku ya alhamis, ambapo uongozi wa timu hiyo umesema vijana wao watashuka wakiwa na lengo moja tu la kuendeleza vipigo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya pili na hatimaye kuipanda Ligi Daraja la Tatu.