STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 21, 2013

Chelsea, Mourinho wapumua, Liverpool ikifa nyumbani EPL

Oscar
Oscar akishangilia bao lake jioni hii
Beki Lavren akiitungua Liverpool kwa kichwa

VIJOGOO vya England, Liverpool leo wamejikuta wakiiangukia pua wakiwa uwanja wao wa nyumbani wa Anfield baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 toka kwa Southampton, na kuipisha Chelsea iliyozinduka leo kwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya mahasimu wao wa Fulham kukaa kileleni mwa msimamo.
Liverpool iliyokuwa haijaonja chungu ya kipigo katika mechi nne zilizopita za Ligi Kuu ya England ilitunguliwa bao hilo lililofungwa na Dejan Lavren katika dakika ya 53 na kuzima ubabe wake wa kuwafunga wenzake.
Nayo Newcastle United ikiwa nayo nyumbani ilicharazwa mabao 3-2 na Hull City, licha ya kuongoza hadi mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1.
Chelsea muda mchache uliopita imetoka kupata ushindi kwa kuilaza Fulham kwa mabao 2-0, mabao yaliyofungwa na Oscar katika dakika ya 52 na Obi Mikel aliyefunga la pili dakika sita kabla ya pambano hilo lililochezwa Stanford Bridge kumalizika na kumpa afueni kocha Jose Mourinho.
Mechi nyingine za ligi hiyo ya England, Everton ikiwa ugenini imeisulubu West Ham kwa mabao 3-2 nayo Sundeland ikiwa ugenini imetandikwa mabao 3-0 na West Brom na Aston Villa ikiizima Norwich City ikiwa kwake kwa bao 1-0.
Kipute cha ligi hiyo kinatarajiwa kuendelea kesho kwa michezo nne, Arsenal itakuwa ikiufukuzia uongozi wa ligi hiyo baada ya kuenguliwa wiki iliyopita na Liverpool itaikaribisha Stoke City, Manchester City itakuwa nyumbani kuialika Manchester United, Tottenham Hotspur watasafiri hadi nyumbani kwa Cardiff City na Crystal Palace wataikaribisha Swansea City.

Mbeya City yapunguza kasi Msimbazi, Tambwe aendelee kufumania nyavu, Ashanti yaendelea kuwa mdebwedo


Mbeya City wakiomba dua
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi003q9axgmcyEwn769yPSk0p-qvp7iBWnxb70zu3q8AEvcVy2CrW_ALBPLt_ui4VS13-PzWbTpfaDxDBACnTatNnxlIyckN4u5SXDOATdaTiRtWevZ5goB1IekVocBA9ddoiZP-GkDw90/s400/kikosi1.JPG
Kikosi cha Simba

LILE 'fupa' lililowashinda Yanga kulitafuta, Mbeya City imedhihirisha wapo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kikazi baada ya jioni ya leo kuibana mbavu Simba na kwenda nao sare ya mabao 2-2 kwenye uwanja wa Taifa, huku mshambuliaji nyota toka Burundi, Tambwe Amissi akiendeleza libeneke lake kwa kufumania nyavu.
Simba ambayo hata hivyo inaendelea kukalia uongozi wa msimamo wa ligi hiyo ilishindwa kulinda mabao yake mawili yaliyofungwa na Tambwe katika kipindi cha kwanza na kuwapa mwanya 'wageni' Mbeya City kuyarejesha na kupata ponti yake ya pili ugenini.
Tambwe alifunga bao la kwanza dakika ya 22 kabla ya kuongeza jingine dakika ya 33 na kumfganya afikishe jumla ya mabao sita na kuwaacha mbali wafungaji wenzake wanaomfukuzia kwenye orodha ya wafumania nyavu.
Hata hivyo Mbeya inayonolewa na kocha mzoefu, Juma Mwambusi ilijipatia bao la kwanza dakika nne baada ya kufungwa bao la pili na Simba kupitia Paul Nonga na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe 2-1.
Kipindi cha pili kilishuhudiwa kosa za hapa na pale kwa timu zote na hasa Mbeya kuonyesha kucharuka na katika dakika ya 69, Richard Peter aliisawazishia timu yake bao la pili na kuifanya Simba ipoteze umakini wake na kama siyo papara za washambuliaji wa Mbeya huenda wangeweza kuibuka na ushindi leo Taifa.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Mgambo JKT ikiwa uwanja wa Mkwakwani ililazimishwa sare ya bao 1-1 na maafande wenzao wa Rhino Rangers ya Tabora. Bao la wenyeji lilifungwa na Mwalimu Musuku dakika ya 60 kabla ya Rhino kuchomoa dakika za jioni kupitia Hamis Msafiri.
Nayo timu ya Prisons Mbeya imeendelea kujikongoja baada ya kuambulia sare ya pili mfululizo dhidi ya Mtibwa Sugar, mechi iliyochezwa uwanja wa Sokoine Mbeya, wageni wakianza kupata bao kupitia nahodha Shaaban Nditti aliyefunga kwa kichwa dakika ya 26 akiiunganisha mpira wa adhabu ndogo iliyopigwa na Said Mkopi kabla ya wenyeji kuchomoa bao dakika ya 58 kupityia kwa Peter Michael.
Kagera Sugar ikiwa uwanja wake wa Kaitaba, Bukoba iliishindilia bila huruma 'vibonde' wa ligi hiyo Ashanti United ya Dar kwa mabao 3-0. Mabao ya washindi yalitupiwa kimiani na Daud Jumanne, Seleman Kibuta na Clement Douglas.
 Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea kesho kwa mechi tatu zitakzaochezwa viwanja vitatu tofauti jijini Dar mabingwa watetezi watapimana ubavu na Azam watakaokuwa wenyeji, huku mjini Tanga Coastal Union itapepetana na Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mkwakwani na JKT Ruvu itawalika Oljoro JKT.

Simba, Mbeya City nini bwana, ngoma kesho Yanga vs Azam

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPnNutozTJ6LUNDdmv05v7BvLNYLIQ6dp4CQ2ET3L3oazDgFevrgY8oyJQYiRwp0q85aEDxXie6rSVYqBOkl6hngu5QSM5xh24P58eJEep1bVkTQhE8P0a20N1ChhRt5YTQlf4pHuVo4dH/s1600/MWAIKIMBA.jpg
Wachezaji Azam wakishangilia mabao yao

WAKATI Mbeya City ikiwa na kibarua kigumu mbele ya vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba, macho na masikio ya mashabiki yapo kwenye pambano la kesho kati ya mabingwa watetezi Yanga na makamu bingwa, Azam zitakazopepetana kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Yanga wakishangilia moja ya mabao yao
Simba na Mbeya zinaumana leo pia kwenye uwanja huo katika mfululizo wa ligi hiyo utakaoshuhudiwa pia mechi nyingine tatu katika miji tofauti.
Hata hivyo mashabiki wa soka watakuwa na hamu kubwa ya kushuhudia pambano la Yanga na Azama ambazo zote zimeshindwa kuonyesha makeke katika mechi zake mbili zilizopita.
baada ya kubanwa mbavu jijini Mbeya ikilazimishwa sare mbili mfululizo dhidi ya wenyeji wao Mbeya City na Prisons, Yanga kesho inarejea katika dimba lake la nyumbani kujaribu bahati yake tena kwa Azam.Azam nao kama ilivyo kwa Yanga imetoka kuambulia sare mbili dhidi ya Kagera Sugar na Ashanti na kujikusanyia pointi sita sawa na ilizonazo Yanga, Mbeya City na Coastal Union.
Pambano hilo la Yanga na Azam ni kati ya mechi tatu zitakazochezwa kesho katika ligi hiyo iliyoingia raundi ya tano, michezo mingine ikiwa ni maafande wa JKT Ruvu na Oljoro JKT zitakazopepetana kwenye dimba la Chamazi, Mbagala Dar es Salaam na ile ya 'Wagosi wa Kaya' Coastal Union itakyokuwa nyumbani uwanja wa Mkwakwani, Tanga kuumana na Ruvu Shooting.
Hata hivyo pamoja na mechi hizo nyingine kuwa na mvuto wake, pambano la Yanga na Azam ndilo linaloangaliwa kwa ukaribu na mashabiki wa soka nchini kutokana na upinzani uliopo baina ya timu hizo kila zinapokutana.
Timu hizo zenye pointi sita kila mmoja zikitofautiana uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa zitakutana katika pambano lao la 11 la Ligi Kuu tangu 'Wana Lambalamba' wapande daraja mnamo mwaka 2008.
Klabu hizo zimeshakutana katika michuano kadhaa ikiwamo ya Kombe la Mapinduzi, Kombe la Kagame na Ngao ya Hisani ambayo mara ya mwisho walivaana Agosti 17 na Yanga kuitambia Azam kwa bao 1-0, lakini katika mechi za ligi kuu huwa na matokeo mengi ya kushangaza.
Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo tangu mwaka 2008 Yanga na Azam zimekutana mara 10 katika Ligi Kuu na Yanga kushinda mechi tano na Azam ikishinda mechi tatu huku michezo yao miwili ikiishia kwa sare.
Hivyo katika pambano hilo klabu hizo zitakuwa zikifukuzia nafasi ya kuvuna pointi tatu na wakati huo huo kulinda au kuboresha rekodi yao dhidi ya mwenzake, huku wadau wa soka wakitaka kuona kama wafungaji bora wa msimu uliopita nani anatayemfunika mwenzake.
Kipre Tchetche wa Azam ndiye aliyeongoza orodha ya wafungaji bora kwa kufunga mabao 17 na amezinduka majuzi baada ya kufunga bao lake la kwanza, huku aliyeyemfuata msimu uliopita, Didier Kavumbagu tayari akiwa na mabao mawili kibindoni mpaka sasa.
Kadhalika ni mechi itakayokuwa ikishindanisha makocha wawili wa kigeni wenye rekodi nzuri kwa msimu uliopita, Ernie Brandts wa Yanga aliyeiongoza Yanga kwa mechi zaidi ya 24 bila kufungwa tangu walipolala bao 1-0 toka kwa Kagera Sugar msimu uliopita.
Kocha wa Azam, Muingereza, Stewart John Hall, yeye naye atataka kulipa kisasi kwa mpinzani wake ambaye amemtambia kwa msimu uliopita katika mechi zote za ligi na majuzi kwenye ngao ya Hisani.
Je ni Yanga au Azam itakayocheka au Kipre Tchetche atakayemtambia Didier Kavumbagu ama ni kocha Brandts kuendelea kumfunika Stewart? Tusubuiri tuone.
Rekodi za Yanga na Azam katika Ligi tangu 2008:
Oktoba 15, 2008
Yanga 3-1 Azam
Aprili 8, 2009
Azam 3-2 Yanga
Oktoba 17, 2009
Azam 1-1 Yanga
Machi 7, 2010
Yanga 2-1 Azam
Oktoba 24, 2010
Yanga 0-0 Azam
Machi 30, 2011
Yanga 2-1 Azam
Septemba 18, 2011
Azam 1-0 Yanga
Machi 10, 2012
Azam 3-1 Yanga
Novemba 4, 2012
Yanga 2-0 Azam
Februari 23, 2013
Yanga 1-0 Azam
Sept 22, 2013?

Masogange, Melisa waachiwa huru hatimaye

http://api.ning.com/files/It3-odgnrfRW80PWalq53lRwVSPptJtp*DOsLRl-yTPt24Tlnfb-fOv0Dzh6ppWTIjHud9Q--mi-9R3wu5ArUT7KY4Lt9FlD/MASOGANGE.jpg?width=450
Masogange
WATANZANIA wawili Agness Gerard ‘Masogange’ na Melissa Edward wameachiwa huru na Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg baada ya kutakiwa kulipa faini ya Sh 4.8 milioni (Randi 30,000) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumiwa kutengeneza dawa za kulevya.
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai cha Afrika Kusini (hawk) Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya bali kemikali aina ya ephedrine.
Hata hivyo mahakama ilibaini kuwa Melissa hana hatia kwa kuwa ilionekana amemsindikiza Masogange, aliyemuomba amsaidie kubeba mzigo huo.
Mosagange alilipa faini ya Shilingi 2.5 milioni (R15, 000), huku akiahidi kumaliza nusu yake ambayo juhudi zilikuwa zinafanyika amalize kulipa jana Ijumaa.
“Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa tu kusaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini haikuwa mizigo yake. Mizigo yote iliandikwa jina la Agness Masogange na si Melissa,” alisema Kapteni Ramaloko.
Kapteni Ramaloko alisema, Melissa alijitetea kuwa hakuwa amesafiri na Masogange bali walikutana ndani ya ndege na Masogange alimuomba amsaidie mizigo hiyo kwani ilikuwa mikubwa.
Kwa sheria za Afrika Kusini kubeba kemikali zozote ambazo zimepigwa marufuku ni kosa la jinai kisheria hivyo mahakama iliamuru Masogange ahukumiwe kwenda jela miezi 30 (miaka miwili na miezi sita) au alipe faini ya R30, 000(Sh 4.8 milioni).
Hata hivyo alilipa faini na nusu ya fedha hizo ilishalipwa na nyingine ilikuwa inakaribia kulipwa.
Ingawa Kamishana Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa alipoulizwa juzi Alhamisi alisema mzigo walioubeba Masogange na mwenzake haukuwa ni dawa za kulevya bali ni kemikali za dawa za kulevya, lakini Msemaji wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini, (SARS) Marika Muller, alieleza kuwa timu ya SARS ina uhakika kuwa mabegi sita yaliyokamatwa Julai 5, mwaka huu ni methamphetamine.

MWANASPOTI

Amani Simba aanza tambo Ashanti United

Amani Simba
KIPA mpya wa Ashanti United, Amani Simba ametamba kwamba bado muda mfupi tu kabla ya mashabiki wa soka kuikubali timu yao ambayo imeanza vibaya Ligi Kuu Tanzania Bara kiasi cha kuruza mkia katika msimamo wa ligi hiyo.
Aidha kipa huyo alisema ni mapema mno kuanza kuitabiria ligi ya msimu huu kwa sababu anaamini lolote linaweza kubadilika kwa sasa kutpkana na ukweli ligi ndivyo kwanza ipo raundi ya nne kwa sasa.
Simba aliyeidhinishwa hivi karibuni na TFF kuidakia timu hiyo baada ya kuitema timu aliyoipandisha daraja ya Mbeya City, alisema Ashanti inasumbuliwa na ugeni wa ligi, ila kadri siku zinavyosonga mbele wachezaji wataizoea na kutisha.
Kipa huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Moro United, Simba na Taifa Stars alisema ni mapema mno kuanza kuihukumu Ashanti na matokeo iliyopata kwa sasa kwa sababu ligi bado mbichi na wachezaji wao wanaendelea kuizoea ligi hiyo.
"Ni mapema mno kuijadili Ashanti, naamini muda mfupi ujao wanayoibeza wataikubali baada ya kuanza kupata matokeo mazuri, unajua ugeni wa ligi ndiyo tatizo lakini kadri siku zinavyoenda mbele wachezaji wanaondoa woga," alisema.
Simba, aliyewahi pia kuzidakia Lipuli Iringa, Prisons Mbeya na JKT Ruvu, alisema akishirikiana na wenzake watahakikisha Ashanti inafanya vyema katika mechi zilizopo mbele yake.
Ashanti United inayoburuza mkia katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa pointi moja ni kati ya timu tatu zilizopanda Ligi Kuu msimu huu, nyingine zikiwa ni Mbeya City na Rhino Rangers ya Tabora.

Gaucho bado aliota soka la kulipwa

http://api.ning.com/files/Z311HW*8BLsTaHW*p4y9dVjDgbR8cx2tskdyBtk0ZluRwicT9*Nf2fkCQ3unhX6sg*ce5TuwMHaY4TPmDCzkUwHTqR41EqDZ/GLOBALHUMUD.jpg?width=351
Gaucho
KIUNGO nyota wa klabu ya Simba, Abduhalim Humud 'Gaucho' amesema bado hajakata tamaa na mipango ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi hata baada ya mipango ya kwenda nchini Afrika Kusini kukwama.
Akizungumza na MICHARAZO, Gaucho, aliyerejea tena Simba akitokea Azam aliyoichezea msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, alisema japo ametuliza akili zake kuitumia kikamilifu Simba, bado analiwaza soka la kulipwa.
Gaucho, alisema bado ana kiu kubwa ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi na imani yake siku yoyote ataenda nje ksa kuamini ana kipaji na uwezo wa kucheza soka kokote akipata fursa hiyo.
"Sijakata tamaa na soka la kulipwa, bado naamini ipo siku nitaenda nje kwa uwezo wa Muingu kwani yeye ni Muweza na Mpangaji wa kila jambo," alisema Gaucho nyota wa zamani wa Mtibwa Sugar na Taifa Stars.
Hata hivyo Gaucho aliwataka viongozi swa soka nchini kuepukana hali ya kibabaishaji na tabia za kuwawekea kauzibe wachezaji wanapopata nafasi ya kwenda nje ya nchi kusakata kandanda akidai ni faifa kwa taifa.
Mapema mwaka huu Gaucho alifaulu majaribio yake ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Jomo Cosmos ya Afrika Kusini, lakini wakati akiwa katika maandalizi ya kuondoka alitangaza ghafla kutua klabu ya Simba.
Hata hivyo alinukuliwa katika mahojiano na kituo kimoja cha redio kwamba klabu yake ya zamani ya Azam ndiyo iliyomwekea vikwazo kabla ya uongozi wa Azam kukanusha taarifa hizo na kutangaza kuachana naye.

Ile Ile atoa Wazazi akijipanga upya

Msani Ile Ile katika pozi
MSANII anayekuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya, Maishani Ndee 'Ile Ile' ameachia kibao kipya kiitwacho 'Wazazi' ukiwa ni wimbo wake wa tatu tangu atumbukie kwenye fani hiyo miaka minne iliyopita.
Wimbo huo na video yake umeanza kuwa gumzo kwenye vituo vya redio na runinga kutokana na maudhui wake na Ile Ile alisema amefarijika na anajipanga kuandaa kazi nyinginje mbili kwa mpigo.
Ile Ile aliyewahi kukimbiza na nyimbo za 'Ileile' alioutoa mwaka 2010 na 'Bora Twende' wa mwaka jana alisema nyimbo ambazo zitafuata baada ya 'Wazazi' ni 'Amani na Upendo' na 'Sheila'.
"Hizi zimeshakamilika kila kitu na wakati wowote naziingiza studio kuzirekodi ili kuendelea kuwapa burudani mashabiki wangu na muziki kwa ujumla," alisema Ileile anayejishughulisha na biashara za nguo na hasa lebo yake ya Ile Ile Wears.
Msanii huyo mwenyeji wa Kondoa, alisema angetamani kutoa albamu yake ya kwanza, lakini soko la muziki kwa sasa nchini linamtisha na hivyo anaona bora aendelee kurtoa 'singo' moja moja na video zake ili kujitengenezea mazingira mazuri ya kupata shoo zitakazomuingiza pato la kutosha.

Steve Nyerere 'ala shavu' kifo cha Baba wa Taifa


MSANII wa filamu nchini, Steve Mangendela 'Steve Nyerere' amepata shavu la kutangaza kwa kutoa hotuba mbalimbali za baba wa taifa zitakazokuwa zikirushwa hewani na  Luninga ya TBC mpaka siku ya kilele cha kifo cha hayati Baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Hotuba hizo ambazo zilikuwa zikitolewa na baba wa Taifa sasa Steve Nyerere atakuwa akizitoa kwa kuiga sauti hile hile
Msanii huyo aliyejizolea umaarufu kwa kuiga sauti za viongozi mbalimbali nchini na Duniani kwa ujumla amekuwa akipendwa na wengi kutokana na kuiga sauti ya hayati Baba wa Taifa na kufanya kuchukua jina lake moja kwa moja ambapo kwa sasa popote uendapo uwezi kumwita kwa jina la Steve bali lazima useme Steve Nyerere
Kwa sasa ameingiza kazi yake mpya mtaani inayojulikana kwa jina la Before Wedding ambayo ipo mtaani ikisambazwa na kampuni ya Steps Entatainment ya jijini Dae rs salaam

Bendera 'akiuma' sikio' chama cha Pool kuhusu TBL



 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera(wa pili kushoto), Meneja wa wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool Taifa(TAPA), Fred Mushi na Katibu wa chama cha Pool Taifa , Amos Kafwinga wakiwa katika maandamano ya ufunguzi wa fainali za mashindano ya Safari National Pool Championships.
 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera (wa tatu kushoto) akipigiwa makofi mara baada kufungua rasmi fainali za mashindano ya Safari National Pool Championship 2013 Mkoani Morogoro. Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Chama cha Pool Taifa(TAPA), Amos Kafwinga, Makamu Mwenyekiti wa chama cha Pool, Fred Mushin a Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.


 Baadhi ya wachezaji wa Pool kutoka mikoa 17 ikiwakilisha na vilabu 17 nchini wakiwa katika maandamano kuelekea katika Ukumbi wa Tanzanite Morogoro wakati wa ufinguzi wa fainali za kitaifa za Safari National Pool Championships.
 Top Land- Mkoa wa kimichezo wa Kinondoni Dar es Salaam






 Mdhamini Mkuu wa mashindano ya Safari National Pool Championships, Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo(wa tatu kushoto), Mwakilishi wa TBL Morogoro, Julius Ngaga(wa nne kushoto), Mwenyekiti wa chama cha Pool Mkoa wa Iringa, Salum Kisaku (wa pili kushoto) na Mwamuzi wa kike pekee, Vaileth Mrema (kushoto)  na baadhi ya wachezaji wakiwa katika maandamano ya ufunguzi wa fainali za Pool Taifa Mkoani Morogoro.
 Na Mwandishi Wetu.
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, amewaasa chama cha Pool Taifa(TAPA), kumkumbatia mdhamini mkuu  wa mhezo wa Pool Taifa, “Safari Lager” kupitia Kampuni kubwa nchini Tanzania Breweries(TBL).
Bendera aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa fainali za mashindano hayo yanayoyofanyika kitaifa Mkoani Morogoro ambapo yeye alialikwa kuwa mgeni rasmi.
Alisema Bendera, vipo vyama vya michezo vingi vinashindwa hata kufanya mashindano kwa mwaka lakini Pool ni mwaka wa sita sasa mnafanya, vipo vyama vingi vya michezo vinalia kwanini mpira wa miguu peke yake ndio unapata udhamini lakini Pool ni mwaka wa sita sasa mnaye mdhamini na bado mnaendelea nae na baada ya hapa anaipeleka timu ya Taifa kwenye mashindano ya Afrika ya mchezo wa Pool.
Mchezo wowote  ili ukue na kutambulika nchini na Duniani unaanza na mchezaji mwenyewe kuupenda na kuufanya kutoka moyoni kwa kujiheshimu kwanza mwenyewe na kuuheshimu mchezo ndipo hata jamii huudhamini (Self displine and Tactical displine).
Alisema Bendera yeye kama mdao na mzoefu kwenye tasnia ya michezo na mpaka sasa anashikiria sifa kemkem ambazo hazijawahi kutolewa kwenye rekori anauzoefu wa kutosha na maswala ya michezo, siri ya maendeleo katika michezo ni nidhamu pekee na si vinginevyo.
Mtazamo wa mchezo wa Pool katika jamii siku kadhaa hapo nyuma ulionekana kama mchezo wa kihuni lakini leo mmebadilisha taswira hiyo na sasa mko kwenye mikoa 17 ikiwakilisha na vilabu 17 mkiunganisha na mchezo wa Pool mkiwa mkoani Morogoro katika fainali za kitaifa, hongereni sana TAPA.
Mkuu wa Mkoa pia aliipongeza TBL kupita bia ya Safari Lager kwa kuendelea kudhamini mchezo wa Pool na sasa ni mwaka wa sita ambapo aliomba waendelee kudhamini kwani mchezo huu unaunganisha vijana wengi Tanzania kwa hapo walipofikia kwenye mikoa 17,unaepusha mambo mengi maovu ambayo wangekumbana nayo hawa vijana ni zaidi ya vijana 300 wamekutana Mkoa wa Morogoro na kilicho wakutanisha ni mchezo wa Pool.Endeleeni kudhmini mchezo wa Pool kwani kwa sasa michezo ni afya, michezo ni upendo,michezo ni urafiki,michezo ni matangazo na michezo ni afya.
Bendela aliwakaribisha wote Mkoani Morogoro na kuwaomba wawe na amani kwani Morogoro ni shwari kabisa hewa nzuri baridi kiasi.
Nae Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kujitokeza kufungua fainali hizo na kuahidi lengo la Safari Lager na kuufanya mchezo wa Pool kuwa mchezo namba moja kama ilivyo Safari Lager bia namba moja Afrika hivyo wataenelea kudhamini mashindano ya Pool daima.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool Taifa, Fred Mushi alimsukuru mdhamini Safari Lager kuendelea kuwadhamini na pia kumshukuru Mkuu wa mkoa kwa changamoto alizozieleza za kumlinda mdhamini na kuahidi wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wao kuwaweka sawa vijana kuhakikisha mchezo wa Pool unakuwa chezo namba moja nchini na Afrika kama bia ya Safari Lager.


 Katibu wa Chama cha Pool Taifa, Amos Kafwinga akizungumza.
 Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo. akizungumza
 Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool, Fred Mushi akizungumza
 Mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akizungumza

Friday, September 20, 2013

Shafii Dauda achimba mkwara mzito, kisa...!

Shafii Dauda
MCHAMBUZI maarufu wa soka nchini, Shafii Dauda ameuchimba mkwara uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) unaodaiwa kutaka kuendelea kumwekea mizengwe katika kuwania uongozi ndani ya shirikisho hilo.
Dauda, ambaye ni miongoni mwa wagombea waliokuwa wameondolewa kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa TFF utakaofanyika mwezi ujao na kurudishwa na kamati ya Maadili ametema cheche hizo kupitia akaunti ya Facebook.
Mwanamichezo na mtangazaji huyo, amelazimika kuchimba mkwara huo baada ya kusisikia fununu za kutaka kuwekewa zengwe kama ilivyowahi kusikia awali na kujikuta kweli jina lake likitupwa kwa madai ambayo hayakuonekana kama ana hatia.
Dauda ameomba kugombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, ambapo jina lake la wenzake kadhaa yalitemwa kabla ya Kamati ya Maadili ya TFF chini ya Jaji Jesse Mguto kuwarejesha tena kuendelea na mchakato wa uchaguzi huo utakaofanyika Oktoba 27.
Ebu isome mwenyewe ujumbe huo, ingawa kuna baadhi ya sarufi tumezirekebisha ili ziende sawia la lugha fasaha ya kiswahili;
"Siku chache za nyuma nilizisikia njama za baadhi ya viongozi wa TFF kutaka kuondoa jina langu kwenye mchakato wa uchaguzi wa TFF na kulipeleka kwenye kamati ya Maadili eti nili-publish barua ya FIFA kwenye blog yangu bila idhini yao, nikazipuuzia nikidhani ni stori tu za mitaani,muda ulipofika Taarifa ya TFF ikatoka kweli jina langu likapelekwa kwenye kamati ya Maadili kwasababu zile zile nilizozisikia kabla kwa watu,Kamati ya MAADILI ikaniita nikayasikiliza mashitaka ya Secretarieti ya TFF ambayo iliwakilishwa na Afisa Habari ndugu yangu Boniface Wambura ikanihoji namimi nikatoa utetezi wangu na hatimaye kamati ikaonelea sina kesi ya kujibu hivyo basi jina langu likarudishwa kwenye mchakato wa uchaguzi. Kutoka kwenye vyanzo vyangu mbali mbali ndani ya TFF eti sasa wanajipanga kesho kutoa PRESS ya kuliondoa tena jina langu eti kwa kigezo sina UZOEFU,sasa ninachowambia kama ni kweli yanayozungumzwa WASITHUBUTU kufanya hivyo kwani kwa mara nyingine tena watanipa pointi 3 za mezani.IJUMAA KAREEM!

Simba, Mbeya City uso kwa uso, Mtibwa yaifuata Prisons Mbeya, kivumbi za FDL nacho mmh!

Mbeya City
Simba
Na Boniface Wambura

BAADA ya kuifanyia mauaji ya kutisha Mgambo JKT, vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara,Simba kesho itaikaribisha Mbeya City ambayo iliyozidindia Yanga na Mtibwa Sugar katika mechi zake mbili zilizopita.
Simba itaialika Mbeya City iliyopanda daraja msimu huu kwenye dimba la Taifa ikiwa ni muendelezo ya michezo ya ligi kuu (VPL) inayopingia raundi yake ya tano ambapo pia itashuhudiwa michezo mingine mitatu tofauti.

Uwanja wa Mkwakwani, Tanga utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting Stars na Rhino Rangers ya Tabora. Mtibwa Sugar itakuwa mgeni wa Tanzania Prisons katika pambano litakalochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.


Nayo Kagera Sugar itakuwa nyumbani kwenye uwanja wake wa Kaitaba mjini Bukoba kuvaana na Ashanti United ya Dar es Salaam katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo kutoka Mara.


Ligi hiyo itakamilisha mzunguko wa tano keshokutwa (Septemba 22 mwaka huu) kwa mechi tatu ambapo Azam na Yanga zitacheza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam huku JKT Ruvu ikikwaruzana na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Azam Complex.


Ruvu Shooting inayokamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi itakuwa mgeni wa Coastal Union katika mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.


Wakati huo huo, Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inaendelea wikiendi hii kwa mechi kumi na moja. Kundi A kesho (Septemba 21 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Transit Camp na Green Warriors (Uwanja wa Karume, Dar es Salaam), Tessema na African Lyon (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi).


Ndanda itacheza na Villa Squad kwenye Nangwanda Sijaona mjini Mtwara wakati keshokutwa (Septembe 22 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Polisi Dar es Salaam na Friends Rangers katika Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.


Kundi B kesho (Septemba 21 mwaka huu) ni Mkamba Rangers dhidi ya Burkina Faso kwenye Uwanja wa CCM Mkamba, na Mlale JKT itakuwa mwenyeji wa Kurugenzi Mafinga kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea. 
Keshokutwa (Septemba 22 mwaka huu) ni Majimaji na Kimondo katika Uwanja wa Majimaji.


Mechi za kundi C kesho (Septemba 21 mwaka huu) ni Pamba dhidi ya Polisi Dodoma (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Stand United na Polisi Tabora (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga) na Kanembwa JKT itacheza na Mwadui kwenye Uwanja wa Kawawa ulioko Ujiji. 
Keshokutwa (Septemba 22 mwaka huu) Polisi Mara na Toto Africans zitacheza Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

NSSF YAIPIGA JEKI' ROCKY CITY MARATHON 2013

Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini BMT, Dioniz Malinzi akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa mbio za Rocky Marathon.  
Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Juma Kintu akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa mbio za Rocky City Marathon uliofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo NSSF imedhamini mbio hizo kwa kutoa sh.milioni 15. 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Suleima Nyambui.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio za Rocky Marathon 2013 Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, akizindua rasmi mbio za Rocky City Marathon 2013 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Juma Kintu ambao wamedhamini mbio hizo kwa kutoa sh.milioni 15. 
 Baadhi ya wadau.
Picha ya pamoja.
MSIMU wa tano wa mbio za Rock City Marathon umezinduliwa, ambapo mdhamini mkuu Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limetaka kuwepo kwa mgawanyo wa majukumu kwa mbio za umbali tofauti ili kuharakisha uendelezaji wa vipaji vya wanariadha nchini.

Rock City Marathon zinaratibiwa na Kampuni ya Capital Plus International (CPI), ambapo Ofisa Uhusiano wa NSSF inayodhamini mbio hizo kwa mwaka wa nne sasa, Juma Kintu aliliomba Shirikisho la Riadha Tanzania RT kugawana majukumu na wadau.

“Sisi kama NSSF tuko tayari kudhamini na kuchangia maendeleo ya riadha nchini, ndio maana tunasisitiza mgao wa majukumu kwa wakimbiaji wa umbali fulani kusimamiwa na taasisi au kampuni moja, ili kusaidia maendeleo ya haraka na makuzi sahihi ya vipaji,” alisema Kintu.

Pamoja na NSSF, wadhamini wengine wa Rock City Marathon 2013 zitakazofanyika jijini Mwanza Oktoba 27 ni pamoja na PPF, Airtel, African Barrick, Nyanza Bottlers, Sahara Media, Precission Air, Bank M, New Mwanza Hotel na Umoja.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, aliyekuwa mgeni rasmi, alisema mchezo wa riadha nchini unaelekea kuangamia na jitihada za kuunusuru zinahitajika.

“Ni aibu kuwa mchezo wa riadha nchini unaelekea kufa wakati viongozi waliopewa mamlaka ya kuhakikisha unaendelea wanashuhudia. Ni wakati wa kuamka kuunusuru mchezo huu ambao katika miaka ya 1970 mpaka 1980 uliiletea nchi yetu heshima kubwa.

Kwa upande wake, Rais wa RT, Suleiman Nyambui aliwataka waratibu wa marathon kote chini kuhakikisha wanakuwa na mbio fupi za vijana ili kupanua wigo wa kuzalisha vipaji vipya, vitakavyoliletea sifa taifa na kushinda mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Naye Mgurugenzi Mtendaji wa Capital Plus, Ellen Otaru Okoedion, aliishukuru Serikali kwa ahadi ya ushirikiano, lakini akaitaka kuhakikisha inakaa mezani na (kina Nyambui) RT, ili kujadili njia sahihi zitakazofanikisha kupatikana kwa kina ‘Nyambui wapya.’

Aidha, Mratibu wa tukio hilo, Mathew Kasonta alisema kuwa mbio hizo zitajumuisha  kilometa tano kwa wakimbiaji kutoka katika makampuni, kilometa tatu kwa wenye ulemavu, kilometa tatu kwa watu wazima (zaidi ya miaka 55) na kilometa mbili kwa watoto wenye umri kati ya miaka 7 mpaka 10.

Msiba tena! Mwanajeshi mwingine wa Tanzania afariki Congo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdNJZZWb0uOyOr0xkZ4jESmQ2W9lpQ7JqPz7eO55Re1lTPE9x_VB50rB3ip7BdIvmzMXuzfPSrEPHFiXk3c58fxJmXG4R96K8IghFM_XbKsy5ZG0DVK8q3OsuweCkJUla56q1Cf65TPP5V/s640/mwamnyange.jpg
 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamnyange

MSIBA tena! Hizi ni habari za kusikitisha kusikia, ila ni kwamba  shujaa mwingine wa Tanzania amefariki dunia katika harakati za kulinda amani ya waafrika wenzetu. 
Habari zilizotolewa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) zinasema mwanajeshi anayetambulika kwa jina la Private Hugo Munga, ambaye alijeruhiwa kwenye shambulio lilisababisha Meja Khatibu kufariki dunia, naye amefariki.
Mwanajeshi huyo alikuwa nchini South Africa kwa ajili ya matibabu, lakini kwa bahati mbaya Tanzania imempoteza shujaa huyu. 
Mwili wake unatarajiwa kufikishwa hapa nyumbani kesho ukitokea nchini South Africa.
1j
2j

Polisi Dar wapiga marufuku maandamano ya Wapinzani, kisa...!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTqetlsLeH_ScYXsPtt6WO1C0fCX-TowGb2uhPjHn6Tr5y1FeOFQlW2IKA6Gvj_SbkIxEdBwIkNjl_C_wq6S1VMWROlSa0pU8X4P2JHsx_PisWpU2abyDZBphoYSSGa0JX6_sKaf-j_NY/s1600/Kova1%252814%2529.jpg
Kamanda Suleiman Kova
JESHI la Polisi Jijini Dar es Salaam limeyapiga marufuku maandamano ya umoja wa vyama vya CUF, NCCR na CHADEMA yaliyopangwa kufanyika kesho Jumamosi.
Maandamano hayo yaliyokuwa  yamepangwa  kuanzia Tazara hadi Jangwani kisha Mwenge hadi Jangwani na sehemu mbalimbali .

Taarifa  iliyotolewa  na Kamanda Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova kupitia ITV   imeeleza kuwa Polisi wamechunguza na kugundua kwamba  maandamano  hayo  yataleta usumbufu kwa watu wengine na kwamba kwa kuwa lengo ni kufika Jangwani basi Viongozi wa vyama hivyo wawaambie wafuasi wao waende Jangwani bila Maandamano. 

Masogange aanza kufurahia 'uhuru' wa dhamana aliyopewa 'Kwa Mabida'

Mcheki katika picha hizi alizotupia leo mtandaoni



Picha hizi Amezipiga akiwa Gym leo asubuhi zinazidi kutoa ushahidi kuwa yupo Mtaani ...au jela za South Mambo ndio hivi ? We unasemaje?

Waziri Mukangara mgeni rasmi Redd's Miss Tanzania

Vimwana wanaotarajiwa kuchuana kesho kwenye shindano la Redd's Miss Tanzania 2013
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika shindano la urembo la taifa mwaka huu 'Redd's Miss Tanzania 2013' litakalofanyika kesho kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar se Salaam.
Gazeti la kila siku la NIPASHE linalochapishwa na Kampuni ya The Guardian Ltd ni miongoni mwa wadhamini wa shindano hilo litakalotoa mwakilishi wa nchi katika fainali za Urembo za Dunia (Miss World).
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga, alisema jana wanatarajia  kiongozi huyo wa serikali kushuhudia shindano hilo na kwamba amesharidhia kuwa mgeni rasmi.
Lundenga alisema kila kitu kimekamilika na kuwataka wadau wa sanaa ya urembo kusubiri kushuhudia shindano lililo bora zaidi ya miaka iliyopita.
"Maandalizi yamekamilika na kama ni chakula, sasa kinachosubiriwa ni kukila tu," alisema kwa kifupi mratibu huyo ambaye kampuni yake imekuwa ikiandaa shindano hilo tangu 1994.
Alisema shindano hilo litapambwa na burudani kutoka kwa mshindi wa tuzo ya mwanamuziki bora wa kike nchini, Judith Wambura 'Lady Jay Dee' ambaye kwa sasa anatamba na vibao vyake vya Yahaya na Joto Hasira, Mike Rose wa Uganda na kikundi cha ngoma za asili cha Mama Afrika.
Shindano hilo linatarajiwa kushirikisha warembo 30 kutoka sehemu mbalimbali nchini watakaowania taji linaloshikiliwa na Brigitte Alfred, kutoka Kanda ya Kinondoni jijini ambaye kwa sasa yuko Indonea akijiandaa kupanda jukwaani kuwania taji la dunia ifikapo Septemba 28, mwaka huu.
Hata hivyo, warembo watano wameshatinga hatua ya 15 bora baada ya kutwaa mataji madogo yaliyoshindanishwa wakiwa kambini.
Warembo hao ni Severina Lwinga, kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam ambaye ni Redd's Miss Personality, Prisca Clement (Redd's Miss Tanzania Talent), Clara Bayo (Redd's Miss Sports Woman ), Happiness Watimanywa (Redd's Miss Photogenic) na Narietha Boniface ambaye ni Redd's Miss Tanzania Top Model.
Mshindi wa taji hilo mwaka huu atabeba dhamana ya kuiwakilisha nchi katika shindano la urembo la dunia mwakani na zawadi ya Sh. milioni nane pamoja na gari lenye thamani ya Sh. milioni 15.

Homa ya pambano la Man Utd, City yaanza

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/01507/kompany_1507398a.jpg
Vincent Kompany
http://www.independent.co.uk/incoming/article8668976.ece/BINARY/original/wayne-rooney.jpg
Wayne Rooney


KATIKA kile kinachoonekena kama ni kuanza kupanda kwa 'homa ya pambano' baina ya wapinzani wa mji wa Manchester, Manchester United na Manchester City waachezaji wa timu hizo wameanza kutambiana.
Beki nmahiri wa Manchester City, Vincent Kompany amesema anasubiri kwa hamu kucheza dhidi ya Wayne Rooney keshokutwa Jumapili na anatumai kwamba mshambuliaji huyo wa Manchester United atakuwa katika kiwango chake cha juu.
Rooney amefunga magoli matatu katika mechi mbili tangu aliporejea katika kikosi kwa kwanza baada ya kupata jeraha la katika paji la uso lililomweka nje ya uwanja lakini nahodha huyo Man City alipuuza mitazamo kwamba anatamani kuona kiwango cha mshambuliaji huyo kinakuwa chini katika mechi yao ya mahasimu wa mji wa Manchester Jumapili.
"Hapana. Unahitaji kucheza dhidi ya wachezaji walio katika kiwango chao cha juu kabisa," aliwaambia waandishi wa habari. "Hivyo ndivyo ninavyoona. Daima nataka kucheza dhidi ya wachezaji wanaokuwa katika kiwango chao bora kabisa.
"Nina furaha sana kwa Wayne kwamba yuko katika kiwango cha juu. Huu ndiyo utamu wa Ligi kuu ya England, unacheza dhidi ya washambuliaji wakubwa wakati wote, lakini kuna wachezaji wengi wa kuchunga katika timu zote."
David Moyes na Manuel Pellegrini wanaelekea katika mechi yao ya kwanza ya watani wa jadi wa mji wa Manchester wakiwa kama makocha wa timu hizo, ingawa Mscotland huyo alishinda mechi nne mfululizo kwenye Uwanja wa Etihad baina ya mwaka 2008 na 2010 wakati akiifundisha Everton.
Lakini Kompany haamini kama matokeo hayo ya zamani yana mchango wowote katika kitakachotokea Jumapili.
"Ni timu tofauti, ni msimu tofauti na naweza kusema kwamba huwezi kutabiri matokeo ya mechi hii ya watani wa jadi," aliongeza. "Hakuna mtu aliyetabiri kwamba tungeshinda 6-1 kwenye Uwanja wa Old Trafford (katika msimu wa 2011-12), kwamba wangetufunga kwenye Uwanja wa Etihad au kwamba tungeshinda Old Trafford (msimu uliopita). Nadhani hicho ndicho mashabiki wanachopenda. Mechi isiyotabirika.
"Ni mechi ambayo daima unaisubiri. Sidhani kama watu wa mjini Manchester tu bali duniani kote wanajiandaa kufurahia mechi hiyo.
"Ni mechi ambayo inavutia kwa mengi. Sijawahi kuichukulia poa na najiona kubarikiwa kucheza katika mechi hizo. Unafanya kila uwezalo kuhakikisha unacheza vyema katika mechi hizi."
 





Tottenham, Swansea, Fiorentina 'zaua' Ulaya

Goal king: Jermain Defoe scored twice in the first half as Spurs cruised to victory
Defoe akishangilia moja ya mabao yake ya jana
Up and running: Swansea celebrate after Wilfried Bony scored the club's first European goal
Swansea City wakishangia moja ya mabao yao yalioizamisha Valencia
WAKATI Swansea wakishinda ugenini dhidi ya wenyeji wao Valencia ya Hispania, 'Vijogoo' vya Londo ya Kaskazini, Tottenham Hotspur wenyewe wameikandika Tromso kwa mabao 3-0 ikiwa nyumbani katika mechi za Ligi ndogo ya UEFA.
Valencia iliyomaliza mchezo huo ikiwa pungufu baada ya mchezaji wake Adil Rami kutolewa dakika 10 kabla ya pambano kuisha ilijikuta ikilala nyumbani kwa mabao ya Wilfried Bony, Michu na Jonathan de Guzman.
Katika mchezo wa Spurs dhidi ya Tromso, washindi walipata mabao yake kupitia Jermain Defoe aliyefunga mara mbili na jingine la Christian Eriksen.
Mechi nyingine  timu ya St. Gallen iliishinda 2 - 0 dhidi ya Kuban' Krasnodar,        Dinamo Zagreb ikalala nyumbani 2-1 mbele ya Chornomorets kama ilivyokuwa kwa PSV iliyonyukwa mabao 2-0 nyumbani na Ludogorets.
Nayo timu ya Salzburg iliisasambua Elfsborg kwa mabao 4-0, Standard Liège ikalala 2-1 kwa Esbjerg, Zulte-Waregem na Wigan zikatoka suluhu, Maribor ikalala 5-2 kwa Rubin Kazan' na Fiorentina ikashinda nyumbani 3-0 djhidi ya Paços de Ferreira.
Mechi nyingine matokeo yake ni kama ifuatavyo;
Pandurii Târgu Jiu  0-1 Dnipro Dniprop…    
Eintracht Fran…    3-0  Bordeaux    
Maccabi Tel Aviv    0-0  APOEL    
Dynamo Kyiv     0-1  Genk    
Thun     1-0  Rapid Wien    
Freiburg    2-2  Slovan Liberec    
Estoril     1-2  Sevilla    
Real Betis    0-0  Olympique Lyonnais
Vitória Guimarães   4-0  Rijeka    
Apollon     1-2 Trabzonspor    
Lazio     1-0  Legia Warszawa
Sheriff    0-0  Anzhi    
PAOK     2-1  Shakhter Karagandy    
Maccabi Haifa   0-1 AZ      

Thursday, September 19, 2013

Maskini! Watoto wa3 wa familia moja wateketea kwa moto



WATOTO watatu wa familia moja wenye umri kati ya miaka miwili na sita, mmoja wao mwanafunzi wa shule ya awali, wamekufa baada ya nyumba walimokuwa wamelala kuungua moto.

Tukio hilo lililozua simanzi kubwa, lilitokea katika Kijiji cha Lushamba, Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza, saa 5:00 usiku wa kuamkia Septemba 16, mwaka huu.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Careen Yunus, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, ingawa hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi.

Mama mzazi wa watoto hao anadaiwa kuwaacha watoto hao na kwenda kwa rafiki yake, ambaye mahusiano yao hayakutajwa.

Kitendo hicho ambacho kiliwaudhi wanakijiji na kutaka kumvamia, kumshambulia na kumuua mama huyo.

Hata hivyo, mama huyo alinusurika baada ya uongozi wa kata hiyo chini ya Afisa Mtendaji wake, Amos Mabula, kuingilia kati na kutuliza hasira za wananchi hao.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Bulyaheke, Mabula, aliwataja watoto waliofariki dunia katika ajali hiyo kuwa ni Joseph Alfonce (6),  mwanafunzi wa Shule ya Awali Kanyala; sofia Alfonce (4) na Ndeva Alfonce (2).

Mama wa watoto hao, Naomi Kilembi (25), anashikiliwa na polisi kwa mahojiano.

Mumewe, Alfonce Budanda, ambaye walijaliwa kuzaa watoto wanne, akiwamo mwenye umri wa miezi mitano aliyekuwa ametoka na mama yake usiku huo, wakati tukio hilo linatokea alikuwa safarini.

Mabula alisema akiwa mlinzi wa amani katika kata hiyo, baada ya wananchi kukusanyika eneo la tukio wakiwa na hasira, mama wa watoto hao alitokea, huku watoto wakiwa wameshateketea kwa moto.

Alisema kuwa alichukua hatua baada ya mama huyo kukiri mbele yake kuwa alikuwa ametoka usiku na kuwaacha watoto hao.

Awali, Diwani wa Kata hiyo, Bagesi Ngele, akizungumzia tukio hilo, alisema tabia hiyo haiwezi kuruhusiwa kuendelea.

Alisema tukio hilo lingeweza kuzuilika kama hatua zingechukuliwa kunzia kwa familia yenyewe kwani kitendo cha kuwaacha watoto peke yao huku kukiwa moto ni cha hatari ikizingatiwa ilikuwa nyumba