STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 18, 2013

Taifa Stars sasa kukipiga na Zimbambwe kesho ni baada ya Kenya kuchomoa

Stars ikijifua
TIMU ya soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kesho inatarajia kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya timu ya Zimbabwe mchezo utakaofanyika kuanzia saa 10:00 jioni kwenye Uwanja Taifa jijini Dar es Salaam.
Stars itaivaa Zimbabwe badala ya Kenya (Harambee Stars) ambayo ilipangwa hapo awali.
Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Boniface Wambura, alisema tayari Zimbabwe wamethibitisha kuja kucheza na Taifa Stars na wanatarajiwa kuwasili jijini leo saa tatu asubuhi.
Wambura alisema kikosi cha Zimbabwe kitakuja na jumla ya watu 30 na kuongeza kwamba maandalizi ya mchezo huo unaofanyika kwa mujibu ya Kalenda ya Shirikisho la Soka duniani (Fifa) yako katika hatua za mwisho.
"Sasa Stars itacheza na Zimbabwe na wameshathibitisha kukubali mechi hiyo na watatua nchini Jumatatu (leo)," alisema Wambura.
Alisema mchezo huo utachezeshwa na waamuzi kutoka Uganda huku akimtaja Oden Mbaga wa Tanzania kuwa ndiye mwamuzi wa mezani na mwamuzi mstaafu wa Fifa, Mtanzania Leslie Liunda, atakuwa kamishna wa mchezo huo.
Kiingilio cha chini katika mechi hiyo ni Sh. 5,000 na cha juu ni Sh. 20,000 kwa viti vya VIP A.
Wambura alisema uongozi wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) wamesikitika kuikosa mechi dhidi ya Stars ambayo kiufundi timu hizo mbili zilikuwa zimeshajipanga kukutana.
Aliongeza kuwa, baada ya mechi hiyo, kikosi hicho kitaendelea na mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mashindano ya Kombe la Chalenji yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Novemba 27 hadi Desemba 12, mwaka huu jijini Nairobi, Kenya.
Katika mashindano hayo ya kila mwaka yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati, timu ya Tanzania Bara imepangwa Kundi B pamoja na Zambia, Burundi na Somalia huku Kundi A likiwa na wenyeji Kenya, Ethiopia, Zanzibar na Sudan Kusini.
Kundi C linaundwa na mabingwa watetezi Uganda, Rwanda, Sudan na Eritrea.
Wakati huo huo Kocha Mkuu wa Stars, Mdenmark Kim Poulsen amelalamikia kitendo cha FKF kuizuia ghafla Harambee Stars kuja nchini kucheza mechi hiyo.
"Mwanzo tulipanga kambi ya Taifa Stars iwekwe Arusha ili wachezaji wazoe mazingira ya huko kwani kwa kiasi kikubwa yanawiana na mazingira ya Kenya ambako michuano ya Kombe la Chalenji mwaka huu itafanyika. Kenya wakakataa kucheza nasi Arusha kwa madai kwamba uwanja ni mbovu," alisema Poulsen.
"Siku tatu kabla ya mechi wanatuambia hawaji kucheza nasi wakati wametuharibia mipango. Inasikitisha sana."

Cameroon yaungana na Nigeria, Ivory Coast kutangulia Brazili WC 2014

Nahodha Et'oo akiwajibika uwanjani katika mechi ya jana ambapo Cameroon ilishinda mabao 4-1

 
Huku wawakilishi watatu wa Afrika kwenye fainali za FIFA za kombe la dunia wakiwa tayari wamefahamika,timu hizo ni NIgeria, Côte d'Ivoire na Cameroon , kuna dalili zote wawakilishi wa Bara hilo wakatoka ukanda wa Magharibi.
Ghana iliyoifumua Misri mabao 6-1 kesho itaavana na wapinzani wao hao wakiwa na dalili zote za kufuzu sawa na ilivyo kwa Burkina Faso watakaocheza na Algeria 3-2.
Sare zozote za ugenini kwa timu hizo za Afrika Magharibi dhidi ya Waarabu zitafanya wawakilishi wa Afrika kwa mwakani nchini Brazili kuwa za ukanda huo kama ilivyokuwa mwaka 2010 katika fainali za WOZA.
Nigeria ilianza kukata tiketi hiyo juzi kwa kuinyuka Ethiopia kwa mabao 2-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 4-1 baada ya mechi ya kwanza kushinda 2-1.
Mabao ya Victor Moses kwa penati na Victor Obinna yalitodha kuivusha Nigeria katiia fainali hizo, huku kocha wake, Stephen Keshi akiweka rekodi kuwa kocha wa kwanza Muafrika kuzipeleka timu mbili tofauti katika fainali hizo.
Keshi aliipeleka Togo katika fainali za mwaka 2006 nchini Ujerumani na safari hii akiwa na Nigeria, pia mwenyewe akishacheza fainali hizo wakati wa uchezaji wake.
Katika mechi nyingine ya mtoano wa bara la Afrika, Ivory Coast ililazimishwa sare y 1-1 na Segenal, lakini Tembo hao Afrika walifuzu kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya mechi ya kwanza wakiwa nyumbani kushinda mabao 3-1.
Segenal walitangulia kupata bao kupitia kwa Moussa Sow kabla ya Ivory kuepuka kipigo cha mara ya kwanza tangu kwa karibu mwaka na nusu sasa kwa kusawazisha kupitia kwa Salomon Kalou.
Jana Simba Wasiofugika, waliungana na Nigeria na Ivory Coast kutinga fainali hizo za Brazil baada ya kuizamisha Tunisia kwa mabao 4-1.
Mabao ya Cameroon yalifungwa na Pierre Webo, Benjamin Moudandjo na kiungo mkongwe Jean Makoun aliyefunga mabao mawili.

Katika pambano la kwanza timu hizo zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu ya kutofungana.

Golden Bush Veterani yawanyoa wazee wenzao

Kikosi cha Golden Bush Veterani
Benchi la ufundi la timu hiyo
WAKALI wa kandanda kwa timu za maveterani jijini Dar er Salaam, Golden Bush juzi iliwanyoa wazee wenzao wa Kivukon Veterani kwa mabao 3-0 kablka ya jana kupata ushindi mwingine dhidi ya Kijitonyama.
Ushindi wa juzi dhidi ya Kivukoni ulikuwa ni wa kulipa kiasi kwa wakali hao ambao wiki chache za nyuma walifumuliwa na wapinzani wao hao.
Golden Bush ilipata ushindi huo katika uwanja wa Kinesi Ubungo kwa mabao yaliyowekwa kimiani na Abuu Ntiro, Said Sued 'Panucci' na Mgaza Aguero.
Mlezi wa klabu hiyo yenye maskani yake Sinza, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema ushindi huo mfululizo kwa timu yake umewapa faraja.
Ticotico alisema kwa sasa kikosi chao kinajiandaa kwa ajili ya ziara ya kwenda visiwani Zanzibar kuvaana na wazee wa huko katika mehci ya kuadhimisha siku ya Uhuru, Desemba 9.

Saturday, November 16, 2013

Kijogoo: Mwanasoka aliyehamishia makali yake katika uigizaji

Kijogoo katika pozi tofauti
KUVUTIWA kwake na msanii Mohammed Mwikongi 'Frank' kulimfanya Boniface Gilliard 'Kijogoo' au 'Kikoti' kusahau soka, mchezo aliokuwa akiupenda na kuucheza utotoni.
Muigizaji huyo wa kundi la Jakaya Arts linalotamba na michezo yake kupitia kituo cha runinga cha ITV, anasema alikuwa 'kichaa wa soka' akishiriki michezo ya Shule za Msingi na Sekondari na kucheza Ligi Daraja la Nne katika timu ya Burudani kabla ya Frank aliyekuwa Kaole Sanaa kumhamisha na kuwa muigizaji.
"Kipaji cha uigizaji ni cha kuzaliwa nacho, ila Frank ndiye aliyenifanya nibadili  mawazo yangu katika sanaa, ninashukuru ndoto nilizokuwa nazo tangu nijitose kwenye fani hiyo zimeanza kuonekana japo sijaridhika," anasema Kijogoo.
Msanii huyo anasema enzi akicheza soka alimudu nafasi za ushambuliaji kuanza namba 7, 8, 9 na 10 na baadhi ya rafiki zake wanashangaa kukuona kwenye sanaa kwa umahiri aliokuwa nao katika mchezo huo, japo anaendelea ila siyo kama zamani.
Kijogoo anasema aliingia jumla katika uigizaji mwaka 2010 kupitia kundi la Jakaya Arts, igizo lake la kwanza likiwa ni 'Riziki' kabla ya kufuatiwa na 'Barafu la Moto', 'Mapito', 'Donda la Kichwa', 'Ulimbo' na igizo lililoisha hivi karibuni la 'Chekecheo anaoutaja kama mchezo bomba kwake.

Mbali na tamthilia, Kijogoo ambaye ni kocha wa timu ya soka ya kikundi hicho cha Jakaya, anaigiza pia filamu baadhi ya kazi alizocheza ni 'Mahaba Niue', 'Like Father Like Son', 'XXL', 'Best Player' na nyingine.
"Kwa kweli nashukuru sanaa imesaidia kunitambulisha mbele ya jamii, naingiza kipato kinachonisaidia kuendesha maisha yangu pia na mengine ambayo sikutegemea," anasema na kuongeza;
"Hata hivyo sijaridhika hadi nije kutamba kimataifa na kumiliki kampuni yangu binafsi ya kuzalisha filamu na kuwasaidia chipukizi, ambao wamekuwa wakipuuzwa pale wanapohitaji msaada," anasema.


UHASIBU
Kijogoo shabiki mkubwa wa Yanga na Arsenal akiwazimia nyota wa timu hizo, Haruna Niyonzima na Mesut Ozil, mbali na usanii na uanasoka kitaaluma ni Mhasibu aliyesomea fani hiyo Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).
Mkali huyo anayependa kula pilau na kunywa vinywaji mchanganyiko, anasema anafurahi kuhitimu masomo yake hayo akitarajia kutunikiwa shahada yake hivi karibuni na kudai ametimiza ndoto zake za utotoni za kuwa mhasibu.
"Nilikuwa na ndoto za kuja kuwa Mhasibu na ninashukuru ndoto hizo zimetimia baada ya kuhitimu masomo yangu na ninamshukuru kaka yangu Rabson Gilliard aliyenisomesha na kunikazania masomo kwani wazazi wetu wote walishafariki na yeye kubeba jukumu la kutusaidia wadogo zake," anasema.
Msanii huyo anakiri hakuna tukio linalomtoa machozi mpaka leo kama hilo la kuwapoteza wazazi wake wote japo kwa nyakati tofauti kutokana na ukweli wazazi ni kila kitu na nguzo ya maisha ya binadamu yeyote, japo anamshukuru Mungu kwani ni yeye aliyeumba na ni yeye anayetwaa.
Kijogoo anayemzimia kwa sasa Jacob Stephen kwa umahiri wake wa kuigiza nchini, anasema sanaa ya Tanzania imepiga hatua kubwa lakini imekuwa haina manufaa kwa wasanii kutokana na vikwazo mbalimbali ikiwemo wizi na unyonyaji.
Pia anasema fani hiyo ni ngumu tofauti na wengi wanavyoichukulia na hasa msanii anapokuwa mchanga kwa kushindwa kupewa sapoti kwa waliomtangulia.
Kuhusu skendo zinazofanywa na wasanii wachache, Kijogoo anasema hiyo inatokana na ushamba na ujinga walionao baadhi yao kwa kudhani kujihusisha na skendo kutawasaidia kupata umaarufu wa haraka ilihali wanajiharibia mbele ya jamii na kusababisha sanaa nzima kuonekana kama ya wahuni, kitu ambacho sicho.
"Mimi nawaona ni kama wajinga kwa sababu mtu mwenye akili zake hawezi kukubali kila siku kuandikwa kwa mambo ya upuuzi, umaarufu unakuja kwa mtu kuchapa kazi kwa ufanisi, hivyo wasanii wajitambue wao ni kioo cha jamii na kubadilika kwani wanajiharibia pengine tunakosa hata matangazo kwa matendo maovu yanayofanywa na wachache wetu," anasema.

ALIPOTOKA
Boniface Gilliard alizaliwa Machi 16, 1985 jijini Dar es Salaam akiwa ni mtoto wa nane kati ya 9 wa famili yao na alisoma Shule ya Msingi Mwananyamala Kisiwani kabla ya kujiunga na masomo ya Sekondari katika Shule ya Kambangwa  jijini Dar es Salaam na kumalizia Ifunda-Iringa kabla ya kujiunga Chuo cha IFM.
Msanii huyo anayechizishwa na nguo za rangi ya maziwa (cream), anasema wakati akisoma alishiriki kwenye sanaa na michezo akiigiza, kuimba na kucheza soka akishiriki michuano ya UMISHUMTA na ile ya UMISSETA huku akicheza pia Ligi Daraja la Nne wilayani Kinondoni.
Alikuja kuachana na soka alipotua Jakaya Arts na kuhamishia akili zake katika sanaa akishiriki michezo na filamu mbalimbali.
Kijogoo anayefurahishwa na tukio la kuzaliwa kwa mwanae wa pekee aliyenaye sasa Nabri anaiomba serikali iwasaidie wasanii kuondokana na wizi wanaofanyiwa katika jasho lao pamoja na kuwathamini kama inavyowathamini wanapokuwa wakiwatumia katika shughuli zao ikiwamo kampeni na uhamasishaji wa mambo mbalimbali.

"Wasanii unajua tumegeuzwa kama karai la kujengea, hatuthamini mpaka nyumba inapohitaji kukarabatiwa, tuthaminike na kusaidiwa vipindi vyote na siyo wakati wa shughuli maalum tu za kiserikali au kisiasa," anasema.
Msanii huyo anayemshukuru kaka yake na ndugu zake kwa ujumla, kundi zima la Jakaya Arts na rafiki zake wote ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakimpa sapoti.
Kijogoo anasema anapenda kutumia muda wake wa ziada kuangalia soka, muvi na kubadilishana mawazo na watu wengine sambamba na kufanya mazoezi.

Hizi ndizo nasaha za Jonas Mkude kwa viongozi, makocha

Jonas Mkude

KIUNGO chipukizi wa klabu ya Simba, Jonas Mkude amewataka viongozi wa soka na makocha kuthamini na kuwajali wachezaji ili wacheze kwa ufanisi uwanjani na kupata matokeo mazuri.
Mkude, ambaye ni mchezaji wa timu ya taifa, Taifa Stars, aliiambia MICHARAZO katika mahojiano maalum kuwa wachezaji vijana hukatishwa tamaa na baadhi ya mambo yanayofanywa na viongozi wao na makocha mara niyngine.
"Ili soka liweze kusonga mbele, ni lazima viongozi na makocha wabadilike na kuwajali na kuwathamini wachezaji na kuwasaidia pale wanapoonekana kukosea kuliko kuwakatisha tamaa," alisema Mkude bila kufafanua.
Aidha Mkude alisema upo ulazima wa kuwekeza katika soka la vijana kwa ajili ya kutafuta mafanikio kimataifa.
"Soka la vijana ndiyo ukombozi wa kandanda la Tanzania," alisema Mkude na kueleza zaidi kuwa "hata mataifa ya nje yamefika yalipo kwa kuwekeza katika soka la vijana kitu ambacho nasi tunapaswa kuiga kufikia mafanikio ya kweli," alisema.
Mkude aliyesajiliwa na Simba mwaka 2010 akitokea Mwanza United alisema anaamini Tanzania itaacha kuwa msindikizaji katika anga ya kimataifa kama nguvu kubwa zitawekwa kwa vijana na kupewa maandalizi mazuri.

Elias Maguli achekelea kuingia Stars na 'mguu' mzuri

https://fbcdn-sphotos-d-a.akamaihd.net/hphotos-ak-frc3/1461574_230784413749326_1852912229_n.jpg
MSHAMBULIAJI nyota wa Ruvu Shooting aliyeitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha timu B ya taifa, Elias Maguli, amesema anamshukuru Mungu kwa kuanza na mguu mzuri baada ya kufunga bao lililoizamisha Taifa Stars zilipoumana katikati ya wiki katika mechi ya kujipima nguvu.
Maguli ndiye mfungaji namba mbili kwa kupachika mabao mengi kwenye ligi kuu ya Bara iliyofika nusu msimu baada ya kupachika mabao tisa, moja nyuma ya Amisi Tambwe wa Simba na timu ya taifa ya Burundi.
Maguli alifunga bao hilo kwenye uwanja wa Karume kwa kumalizia pasi ya yosso wa Mtibwa Sugar, Juma Luizio ambao wote wamejumuishwa katika kikosi cha awali cha wachezaji 32 wa Taifa Stars inayojiandaa kucheza Kombe la Chalenji.
Mchezaji huyo alisema anamshukuru Mungu kwa kumuongoza katika kila anachofanya na amefurahi kuingia na mguu mzuri Stars.
"Namshukuru Mungu kwa kila jambo (pamoja) na bahati hii niliyoingia nayo katika timu ya taifa ninayochezea kwa mara ya kwanza," alisema Maguli.
Maguli alisema atajibidiisha zaidi ili aendelee kudumu katika timu hiyo.
Stars iliyoanza kambi rasmi ya maandalizi ya Chalenji katikati ya wiki, itacheza pambano la kirafiki dhidi ya Harambee Stars ya Kenya Jumanne kwenye Uwanja wa Taifa.
Baada ya pambano hilo wachezaji kutoka Zanzibar wataondoka katika timu hiyo kwenda kuungana na wenzao wa Zanzibar Heroes na waliobaki wataunda Kilimanjaro Stars itakayocheza Kombe la Chalenji kuanzia mwishoni mwa mwezi huu nchini Kenya.


Cheki Dogo la Sir Juma Nature videoni

Bonyeza hapa kupata uhondo http://youtu.be/aGkgTM11ePg 

Mwili wa Dk Mvungi kuagwa leo Karimjee pichani mwili huo ulipowasilia usiku wa jana toka Afrika Kusini

 
JENEZA LA MWILI WA MAREHEMU DK SENGONDO MVUNGI MARA BAADA YA KUWASILI  KWENYE  UWANJA WA NDEGE WA MWL NYERERE JANA SAA 1:15
VIONGOZI WA SERIKALI WALIOFIKA KUPOKEA MWILI WA MAREHEMU MVUNGI
VIONGOZI WA SERIKALI PAMOJA NA NDUGU WA MAREHEMU DK MVUNGI WAKIUOMBEA
BAADHI YA VIONGOZI WA NCCR WALIOFIKA KUPOKEA MWILI WA MAREHEMU DK MVUNGI
VIJANA WA NCCR WAKIBEBA MWILI WA MAREHEMU DK MVUNGI MARA BAADA YA KUWASILI JANA
VIJANA WA NCCR WAKIBEBA MWILI WA MAREHEMU DK MVUNGI MARA BAADA YA KUWASILI JANA UKIINGIZWA KWENYE GARI 
MWILI WA MAREHEMU DK MVUNGI ULIWASILI JANA UKITOKEA AFRIKA YA KUSINI BAADA YA KUPELEKWA KWA AJILI YA KUTIBIWA BAADA YA KUPIGWA MAPANGA NA MAJAMBAZI LEO JUMAMOSI MWILI WAKE UTAPELEKWA KATIKA VIWAJA VYA KARIMJEE KUANZIA SAA 3 ASUBUHI  KWA AJILI YA KUAGWA NA KUSOMEWA  MISA ITAKAYOSOMWA PAPO HAPO. VIONGOZI NA WANANCHI WOTE WATAUAGA MWILI WA MAREHEMU NA BAADAE MWILI HUO UTAPELEKWA NYUMBANI KWAKE NA KESHO JUMAPILI UTASAFIRISHWA KUPELEKWA KIJIJINI KWAKE  KISANGARA JUU, WILAYANI MWANGA KWA AJILI YA KUZIKWA

Kaseba, Segu wapigwa kwa KO Australia

 http://www.bongocelebrity.com/wp-content/uploads/2012/06/Kaseba.jpg
BINGWA wa taifa wa ngumi za kulipwa nchini, Japhet Kaseba usiku wa kuamkia leo amekumbana na kipigo cha KO ya raundi ya pili toka kwa mwenyeji wake, Jeremy van Diemen katika pambano la kimataifa la uzito wa Light Heavy lililochezwa nchini Australia.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka nchini humo zinasema kuwa, Mtanzania hatua huyo hakuweza kuhimili makali ya mpinzani wake na kukubali kipigo cha KO ya raundi ya pili tu ya mchezo huo uliokuwa uwe wa raundi sita uliochezwa kwenye ukumbi wa Metro City.
Inaelezwa Kaseba anayefahamika kama Champion, alionyesha upinzani katika raundi ya kwanza tu, kabla ya kushindwa kuhimili ngumi nzito za mpinzani wake ambaye katika mapambano saba aliyocheza sasa ameshinda matano manne kati ya hayo ni ya KO).
Kabla ya Kaseba kudundwa, bondia mtanzania mwingine,m Jonas Segu naye alikumbana na kipigo kama hicho cha KO baada ya kunyukwa na Luke Sharp katika pambano la utangulizi uzito wa kati.
Segu alishindwa kuendelea na pambano katika raundi ya 5 raundi moja kabla ya kuhitimisha pambano hilo na kuendeleza unyonge wa mabondia wa Tanzania wanapoenda kucheza nje ya nchi kwa kupigwa kila mara.
Mabondia hao wawili wanatarajiwa kurejea nchini kesho kinyonge.

Kilimanjaro Stars yapangwa mchekea Chalenji Cup 2013



BARAZA la Shirikisho la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) linatarajia kutangaza ratiba rasmi ya michuano ya Kombe la Chalenji itakayofanyika nchini Kenya. tayari makundi ya michuano hiyo yametangazwa.
Tanzania Bara inayowakilishwa na Kilimanjaro Stars yenyewe imepangiwa kundi mchekea la B pamoja na timu za Zambia ambao ni waalikwa, Burundi na Somalia.
Wawakilishi wengine wa Tanzania, Zanzibar Heroes ya Zanzibar yenyewe imepangwa kundi A na wenyeji Kenya, Ethiopia na Sudan Kusini, wakati kundi la kifo ni kile la C lenye timu za Uganda ambao ni mabingwa watetezi , Rwanda, Sudan na Eritrea.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake kuanzia Novemba 27 jijini Nairobi kuwania taji hilo ambalo kwa miaka mingi limetawaliwa na Waganda.
MAKUNDI YALIVYO CHALENJI 2013:
KUNDI A- Kenya, Ethiopia, Zanzibar, South Sudan

KUNDI B- Tanzania, Zambia, Burundi and Somalia

KUNDI C- Uganda, Rwanda, Sudan and Eritrea.

Canal Top wa Akudo Impact adaiwa kunaswa na 'unga' China

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyXwKTiqD1NQX1dRQ4ccZ28HJ9q7zm58W61tukh7SAidumoj5qVSuwfsuAreqzsTfPRfE0qnmcUsx6PhUk13xzIn2mjrVCfUnSoAD86bGeRE4mjXOtUumQwwZfdgf342hY0cU1LBwj54A/s400/DSC02167+%5B800x600%5D.JPG
Canal Top (wa kwanza kulia) alipokuwa akiwajibika Akudo

RAPA mahiri aliyewahi kutamba na bendi ya Akudo Impact, Canal Top amenaswa nchini kwa tuhuma za kukutwa na Dawa za Kulevya.
Inaelezwa kuwa rapa huyo alinaswa nchini hivi karibuni baada ya kuingiza dawa hizo nchini humo.
Hata hivyo taarifa rasmi zinaendelea kufuatiliwa kujua undani wa tukio hilo kama ni kweli mwanamuziki huyo kutoka DR Congo amenaswa kweli na Unga au kwa mambo mengine, japo mashushushu waliopo nchini humo wamedai ni 'sembe' zilizomkamatisha.
Bongoclan

Ureno yaichinja Sweden, Ugiriki yanusa Brazil, Ufaransa Mmh!

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/71150000/jpg/_71150286_71150285.jpg
Ronaldo akipongezwa baada ya kuifungia Ureno baoa pekee jana dhidi ya Sweden
Clash of the titans: Portugal's Cristiano Ronaldo (left) and Sweden's Zlatan Ibrahimovic shake hands before kick off
Ronaldo na Ibrahimovic walipokuwa wakilisimiana kabla ya pambano, wote ni manahodha wa nchi zao
CRISTIANO Ronaldo amethibitisha yeye ni bora kuliko Zlatan Ibrahimovic baada ya usiku wa jana kuiongoza Ureno kupata ushindi kiduchu nyumbani kwao dhidi ya Sweden katika pambano la mkondo wa kwanza wa mtoano wa kuwania kutinga Fainali za Kombe la Dunia kwa timu za Ulaya.
Pambano la pambano la timu hizo mbili, lakini pia kulikuwa na maneno ya chini chini kuwapambanisha wakali hao wawili na Ronaldo alionyesha anaweza kumzima Ibrahimovic anayecheza PSG kwa kufunga bao pekee lililoipa ushindi Ureno, japo bado nchi hiyo haina uhakika wa kwenda Brazil mwakani.
Bao hiulo la Ronaldo alilifunga kwa kichwa dakika ya 82 kuunganisha krosi ya Miguel Veloso na kuifanya Ureno kusubiri matokeo ya mechi ya mkondo wa pili itakayochezwa mapema wiki ijayo ugenini dhidi ya wenyeji wao Sweden ambao wana rekodi nzuri kwenye dimba lao la nyumbani.
Katika mechi nyingine za 'kapu' Ukraine iliizima Ufaransa kwa mabao 2-0 na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kusonga mbele, huku Ugiriki ikiwa nyumbani ikaifyatua Romania mabao 3-1, huku Iclenad na Croatia zikitoshana nguvu kwa kwenda suluhu ya bila kufungana.
Mechi za mkondo wa pili zitakazoamua hatma ya wawakilishi wa mwisho wa Bara Ulaya zitachezwa siku ya Jumanne.

Friday, November 15, 2013

Japhet Kaseba azidunda Australia

 
BINGWA wa Taifa wa Ngumi za Kulipwa, Japhet Kaseba 'Champion' yupo nchini Australia kwa ajili ya kupigana na bondia Jeremy van Dieman wa nchini humo katika pambano la kimataifa.
Pambano hilo la uzito wa Heavy Light  (kilo 79) linatarajiwa kufanyika kwenye Ukumbi wa Metro City, uliopo mjini Northbridge nchini humo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotumwa nchini na Kaseba akiwa Australia, mabondia hao walipimwa uzito jana tayari kwa pambano hilo la leo ambalo litakuwa la kwanza kwake kimataifa tangu aliporejee kwenye ngumi.
"Nipo Australia na tumetoka kupima uzito kwa ajili ya pambano letu la kesho (leo) la kimataifa dhidi ya mwenyeji wangu Jeremy van Dieman ambaye nitapigana naye kwenye Ukumbi wa Metro City, Magharibi mwa Australia," alisema Kaseba.
Kaseba alisema mara baada ya pambano hilo ambalo ametamba kufanya vizuri ili kujitengenezea mazingira ya kuwania ubingwa wa dunia, atarejea nchini siku ya Jumapili majira ya saa nane mchana.
"Nitarejea nchini Jumapili ya Novemba 17 saa nane mchana, nawaomba Watanzania waniombee kila la heri niweze kufanya vema katika mchezo huo wa Ijumaa (leo)," alisema Kaseba, bingwa wa zamani wa Dunia wa Kick Boxing.
Kaseba mwenye rekodi ya kucheza michezo minne akishinda miwili na kupoteza miwili, atavaana na Dieman anayeshikilia nafasi ya tisa nchini mwake kwenye uzito huo wa Heavy Light huku akicheza michezo minne na kutoka sare miwili.