STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 4, 2015

TFF yaijibu Yanga kuhusu kinda la Simba

http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/01/Jerry-Muro.jpg
Jerry Muro
BAADA ya uongozi wa Yanga kudai kuhujumiwa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), bodi hiyo imewajibu wanajangwa kwamba 'Mkuki kwa Nguruwe, kwa binadamu mchungu'. Mapema leo, uongozi wa Yanga umetishia kutoingiza timu uwanjani katika mechi yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya JKT Ruvu Stars iliyopangwa kuchezwa Uwanja wa Taifa Machi 11, kutokana na kile ulichodai kutoshirikishwa katika uamuzi wa mabadiliko ya ratiba.
Jerry Muro, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, amesema jijini hapa leo kuwa uongozi wa Yanga ulikuwa unatambua kwamba kikosi chake kingecheza dhidi ya JKT Ruvu leo kabla ya kuivaa Simba SC Jumapili, lakini kimeshangaa baada ya kusoma kwenye mitandao kwamba mechi yao dhidi ya JKT Ruvu Stars haipo.
Hata hivyo, Fatma Shibo, Kaimu Ofisa Mtendaji wa TPLB, amesema mabadiliko ya ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara hayajafanywa kwa siri na yametokea kutokana na ushiriki wa timu nne za ligi hiyo, Azam FC, Mtibwa Sugar FC, Simba SC na Yanga katika michuano ya Kombe la Mapinduzi mapema mwaka huu. Fatma amekanusha madai ya Yanga kwamba mechi yao dhidi ya JKT Ruvu Stars wanayodai ilipangwa kuchezwa leo kwamba yamefanywa kwa siri, kwa vile uongozi wa wanajangwani ulitaarifiwa tangu Febuari 16 juu ya mabadiliko ya ratiba ya ligi.
"Mabadiliko ya ratiba ya ligi kuu yametokea kutokana na ushiriki wa timu nne za Tanzania Bara katika michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar Januari mwaka huu," Fatma amesema.
"Hili la pili la Yanga kudai hatukuwashirikisha katika kupangua mechi yao dhidi ya JKT Ruvu si kweli kwa sababu tuliwasiliana na uongozi wa Yanga tangu Februari 16. Labda wawe na tatizo la kutofungua email, lakini Katibu Mkuu wao (Jonas Tiboroha) alisema aliona email yetu kuhusu suala hilo," amesema zaidi Fatma.
Ofisa huyo amesema bodi haina njama zozote za kuihujumu Yanga katika mechi zake kwani waliibeba pia katika kuilazimisha Tanzania Prisons irejeec Mbeya kutoka Dar es Salaam kucheza dhidi yao mechi waliyoshinda 3-0 jijini Mbeya juzi.
"Kama ni watu wa kulalamika, walipaswa kulalamika Prisons kwa sababu walikuwa hapa Dar es Salaam, lakini tukawaambia warejee kwao Mbeya kucheza dhidi ya Yanga baada ya uongozi wa Yanga kutuomba wacheze mechi zao zote zsa Mbeya kabla ya kwenda Botswana. "Mpaka sasa bodi inadaiwa pesa ya gharama za usaffiri na timu ya Prisons kwa sababu tuliwafanya wasafiri mara mbili kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya na kurudi tena hapa Dar es Salaam," amesema zaidi Fatma.
Katika hoja zake, Muro amedai TPLB ni janga la kitaifa na kwamba kusogezwa mbele kwa mechi hiyo dhidi ya kikosi cha Felix Minziro cha JKT Ruvu, ni hujuma dhidi ya Yanga  kwa kuwa timu hiyo ya Jangwani jijini hapa itakuwa na siku mbili tu za kupumzika baada ya kucheza dhidi ya maafande hao kabla ya kuivaa Platinum ya Zimbabwe katika mechi yao ya kwanza ya raundi ya kwanza ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika Jumamosi.
Huku akihoji kiwango cha elimu cha Kaimu Ofisa Mtendaji wa TPLB, Fatma na watendaji wengine wa bodi hiyo, Muro amesema tayari uongozi wa Yanga umewasilisha barua TFF tangu jana kusaka ufafanuzi wa mabadiliko ya ratiba hiyo.
“Kwa sasa mpinzani wetu ni Azam FC na siyo Simba, mechi dhidi ya Simba kwetu ni kwa sasa kama bonanza, siyo kipaumbele chetu, sisi tunawasubiri siku hiyo ifike tucheze nao, lakini hawana jipya kwa tunawazidi pointi nyingi,”ametamba Muro.
"Azam kesho na keshokutwa tunamwacha mbali maana mpaka sasa tuko mbele yake kwa pointi nne katika msimamo wa ligi, sisi wapinzani wetu na klabu ambazo unaweza kuzilinganisha na sisi ni Kaizer Chief ya Afrika Kusini au TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambazo zinacheza michuano ya kimataifa," amesema zaidi Muro

Pep Guardiola hana mpango wa kuhama Bayern

http://www.predapublishing.com/the-sportist/wp-content/uploads/2014/10/pg-68-garside-pa.jpgKOCHA wa klabu ya Bayern Munich, Pep Guardiola amesema hana mpango wowote wa kuikacha timu hiyo mwishoni mwa msimu kufuatia kuzuka tetesi kuwa anataka kuhamia Manchester City.
Mkataba wa Guardiola na mabingwa hao wa Bundesliga unatarajiwa kumalizika majira ya kiangazi mwaka 2016 lakini mazungumzo ya mkataba mpya yamesimamishwa hatua iliyozua minong’ono ya kuondoka.
Hata hivyo, Guardiola ameweka wazi kuwa bado anataka kuendelea kuinoa Bayern na hajafanya mazungumzo na klabu nyingine yeyote.
Akihojiwa Guardiola amesema hajapokea ofa yeyote kutoka kwa City kwa klabu nyingine kwani matumaini yake ni kubakia Bayern kwa kipindi kirefu.
Guardiola aliendelea kudai kuwa kwa sasa bado ana mkataba na Bayern na anapenda kuheshimu hilo mpaka hapo watakapokaa tena na kuzungumza juu ya mkataba mpya.

Air Jordan nouma! awafuka wanamichezo wote duniani

https://usatftw.files.wordpress.com/2014/09/ap_britain_ryder_cup_golf_67543664.jpg?w=1000&h=736MCHEZAJI mkongwe wa mpira wa kikapu nchini Marekani, Michael Jordan 'Air Jordan' ameendelea kuweka rekodi katika vitabu hata baada ya kustaafu mchezo huo baada ya kutajwa kama mwanamichezo pekee aliyechomoza katika orodha ya mabilionea ulimwenguni.
Wakati akicheza kikapu katika ligi maarufu nchini Marekani NBA, Jordan aliweka rekodi mbalimbali kutokana na umahiri pindi anapokuwa uwanjani lakini hali hiyo imebadilika kwani hivi sasa ameonyesha kuwa mahiri kibiashara pia.
Jordan mwenye umri wa miaka 52 ametajwa kushika nafasi ya 1,741 katika orodha ya watu matajiri duniani ambayo hutolewa na jarida la Forbes kila mwaka akiwa mwanamichezo pekee kuchomoza katika orodha hiyo.
Nguli amepata utajiri mkubwa kutokana na kuingia mkataba na kampuni ya vifaa vya michezo ya Nike ambao ulimuingizia zaidi ya dola bilioni 2.25 mwaka 2013 pamoja na kumiliki hisa asilimia 89 zenye thamani ya dola milioni 700 katika timu ya Charlotte Hornets.

Prisons yamfurusha Mwamaja, Makatta amrithi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjaJrEavPqz6tdbaPJoZmvtYQffdUBf8ZB4pv78v6DDUEKBlffZJyhLOcc-KGwJFL0hn5CO0P6O5Fj_T_zQU8jrYulHMFe7oQSEzt6e49kVAVtP6uu4macHTa9l2xDasmWECDTPulRIcOs/s1600/mwamaja.JPG
Kocha David Mwamaja aliyesitishiwa mkataba wake na Prisons-Mbeya
KLABU ya Prisons Mbeya imemtimua aliyekuwa Kocha wao mkuu, David Mwamaja na nafasi yake imechukuliwa na Mbwana Makatta aliyewahi kuinoa timu hiyo siku za nyuma.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Prisons, Hassain Yusuph alithibitisha kusitishiwa mkataba kwa kocha Mwamaja na kunyakuliwa kwa Makatta aliyekuwa akiinoa timu ya Ligi Daraja la Kwanza, Oljoro JKT.
Timu hiyo ndiyo inayoburuza mkia katika msimamo wa ligi hiyo wakikusanya pointi 14 tu baada ya jioni ya leo kulazimisha sare ya 0-0 na JKT Ruvu kwenye mchezo uliochez a kwenye uwanja wa Chamazi.
Hassain alisema kuwa mabadiliko hayo yamefanywa kutokana na kocha Mwamaja kushindwa kuiweka pazuri timu hiyo na kocha mpya atainoa timu hiyo kwa kipindi chote kilichofuata cha kumalizia ligi.

Mtibwa Sugar yazinduka, Ndanda yaiua Ruvu

Mtibwa Sugar waliozinduka
Polisi Moro waliokubali kichapo mbele ya Mtibwa leo
TIMU ya Mtibwa Sugar wametakata kwenye uwanja wa nyumbani baada ya kuicharaza Polisi Moro kwa mabao 2-1 katika pambano lililochezwa uwanja wa Manungu Complex
Mtibwa ambao kwa muda mrefu walikuwa hawajashinda walipata mabao yake kupitia kwa Ally Shomari na Said Mkopi baada ya awali wageni wao kuitangulia kufunga bao kwa mkwaju wa penati kupitia Said Bahanuzi.
Kwa ushindi huo Mtibwa wamepanda hadi katika nafasi ya tano wakifikisha pointi 22.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Ndanda Fc ya Mtwara iliitambia nyumbani Ruvu Shooting kwa kuilaza mabao 2-1 katika pambano kali lililochezwa uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani.
Ndanda walianza kuandika bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza kabla ya kuongeza jingine kupitia kwa Omega Seme na wenyeji Ruvu walijipatia bao la kufutia machozi dakika za lala salama.
Bao hilo lilifungwa na Yahya Tumbo na kuifanya Ndanda kufikisha pointi 19 wakati Ruvu wakiswaliwa na pointi 21.
Ligi hiyo itaendelea tena siku ya Jumamosi na Jumapili kutakapochezwa pambano la watani wa jadi Simba na Yanga.

Tuesday, March 3, 2015

'Mauro Icardi hang'oki Inter Milan ng'o'

http://gilabola.com/wp-content/uploads/2015/03/icardi.gifMKURUGENZI wa michezo wa Inter Milan, Piero Ausilio amesisitiza kuwa hata Euro Mil. 40 hazitarajiwa kutosha kumng’oa Mauro Icardi katika klabu hiyo.
Icardi mwenye umri wa miaka 22 amekuwa katika kiwango kizuri msimu huu akiwa amefunga mabao 14 katika mechi 24 za Serie A walizocheza.
Hata hivyo, pamoja na vilabu mbalimbali kuanza kumuwinda nyota huyo, Inter inamuona kama mchezaji muhimu kwao na hawana mpango wowote wakumuuza hivi sasa.
Ausilio amesema kwasasa wanatengeneza timu ambayo itadumu kwa kipindi kirefu hivyo hawana mpango wa kuuza wachezaji wao muhimu wanaochipukia.
Strika huyo wa kimataifa wa Argentina ambaye amewahi pia kucheza katika timu za Sampdoria na Barcelona ana mkataba na Inter unapomalizika Juni mwaka 2018.

Shamsa Ford ataka ubunifu zaidi Bongo Movie

WASANII waigizaji nchini wameaswa kuwa wabunifu na kuumiza vichwa kutengeneza kazi za kipekee ili kujitofautisha na pia kulenga kujitangaza kimataifa.
Wito huo umetolewa na muigizaji nyota nchini Shamsa Ford ambaye amesema bila ubunifu na kutoa kazi za kipekee ni vigumu wasanii watanzania kujitangaza katika anga la kimataifa.
Shamsa alisema hata yeye alifikiria na kujaribu kuibuka kivyake vyake katika simulizi la 'Chausiku' ambayo imemjengea jina hata kwa wale ambao siyo mashabiki wa filamu.
"Ubunifu ndiyo siri ya mafanikio, hata mimi niliumiza kichwa kuja na filamu ya 'Chausiku' kwa nia ya kujitofautisha na ninashukuru kazi ilipokelewa vema kiasi kwamba kwa sasa nimepata changamoto ya kutoa kazi nyingine itakayovutia kama hiyo au zaidi," alisema.
Shamsa alisema kwa kuonyesha hakubahatisha kwa sasa yupo katika maandalizi ya kuja na filamu ya 'Mama Muuza' ambayo imebeba uhalisia wa maisha ya uswahili yaliyozoeleka.
"Hakuna njia ya mkato katika mafanikio na hata soko la kimataifa ni ubunifu na kutoa kazi ya kipekee, ili hata zikishindanishwa ijitofautishe," alisema Shamsa.

Nahodha John Terry kuzeekea Chelsea

http://static.goal.com/87600/87660.jpg
John  Terry
NAHODHA wa Chelsea, John Terry amesisitiza amebakisha miaka michache katika timu hiyo huku akidai hana mpango wa kucheza popote baada ya hapo.
Beki huyo wa kati wa vinara hao wa Ligi Kuu ya England ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu, alifunga bao la kwanza katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata katika mchezo wa fainali ya Kombe la Ligi dhidi ya Tottenham Hotspurs Jumapili iliyopita.
Terry amesema kama huu ndio utakuwa mwaka wake wa mwisho katika soka anataka kuumaliza kwa mafanikio.
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa klabu ndio itakayoamua juu ya mustakabali wake kama aendelee au la, lakini hana mpango wa kwenda popote kwingine.
Chelsea inayoongoza msimamo wa Ligi Kuu kwa tofauti ya alama tano wanasafiri kuifuata West Ham United kesho katika moja ya mapambano yatakayochezwa leo, ingawa kwa leo kuna michezo mingine mitatu itachezwa usiku katika mfululizo wa ligi hiyo inayozii kushika kasi.

Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin

Staa wa Sunderland matatani kwa ngono

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Adam+Johnson+Sunderland+v+Carlisle+United+ccdTvhuGA5Tl.jpg
MCHEZAJI wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Sunderland, Adam Johnson amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kufanya ngono na msichana wa umri wa miaka 15.
Katika taarifa ya polisi , Johnson mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa kwa tuhuma hizo za kujihusisha kimapenzi na msichana mwenye umri chini ya miaka 16 lakini ameachiwa kwa dhamana.
Klabu hiyo imedai kuwa kwasasa wamemsimamisha mchezaji huyo ili kupisha uchunguzi wa polisi unaoendelea.
Johnson aliibuka kutoka katka shule ya soka ya klabu ya Middlesbrough akiwa na umri wa miaka 17 mwaka 2005 katika mchezo wa Kombe la UEFA.
Kabla ya kujiunga na Sunderland mwaka 2012 Johnson alikuwa ametokea kwa mabingwa wa Ligi Kuu Manchester City.

Ujenzi Rukwa, Volcano zashushwa daraja

TIMU za Ujenzi Rukwa na Volcano FC ya Morogoro zimeshushwa madaraja mawili hadi ligi za wilaya baada ya kushindwa kufika uwanjani kwenye mechi zao za Ligi Daraja la Pili (SDL).
Uamuzi huo umefanya na Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za matukio mbalimbali ya ligi hiyo.
Ujenzi Rukwa ilishindwa kwenda Kigoma kuikabili Mvuvumwa FC ya huko wakati Volcano FC haikutokea kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya ambapo ilitakiwa kucheza na Wenda FC.
Uamuzi wa Kamati ya Mashindano umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 27 ya SDL ambapo mbali ya kushushwa madaraja mawili, lakini pia timu hizo zimepigwa faini ya sh. milioni moja kila moja. Vilevile matokeo yote ya mechi zao kwenye Ligi hiyo yamefutwa.
Nayo Singida United imepewa ushindi wa pointi tatu na mabao matatu baada ya Ujenzi Rukwa kubainika kumchezesha mchezaji asiyestahili (non qualified) kwenye mechi iliofanyika Februari 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mandela mjini Sumbawanga na timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.
Mchezaji Emmanuel Elias Mseja wa Mbao FC amepigwa faini ya sh. 100,000 na kufungiwa mechi tatu baada ya kukojoa uwanjani kwenye mechi dhidi ya AFC iliyochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha.
Pia viongozi wa Mbao FC, Abdallah Chuma (Daktari) na Meneja Yasin Abdul wamefungiwa miezi sita na faini ya sh. 100,000 kila mmoja kwa kumtukana na kumtishia maisha Kamishna wa mechi hiyo.
Nayo klabu ya AFC imepigwa faini ya sh. 300,000 kutokana na washabiki wake kuifanyia vurugu timu ya Bulyanhulu FC kwenye mechi yao iliyofanyika Februari 7 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Timu ya Magereza Iringa imepigwa faini ya jumla ya sh. 200,000 kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting), na uwanjani kwenye mchezo wao na Njombe Mji uliochezwa Februari 21 mwaka huu. 

Naye mchezaji wa timu Amasha Mlowasa amefungiwa mechi tatu na faini ya sh. 100,000 kwa kumtukana mchezaji mwenzake kwenye mechi hiyo.

Monday, March 2, 2015

El Merreikh yamfukuzisha kazi kocha wa Azam

http://jamboleo.co.tz/wp-content/uploads/2014/12/OMOG.jpg
MABINGWA wa soka nchini, Azam imemtimua kocha wake, Joseph Omog na msaidizi wake Ibrahim Shikanda na baadhi ya watendaji baada ya klabu hiyo kuondolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Katibu Mkuu wa Azam, Idrissa Nassor 'Father' ameweka bayana maamuzi hayo akisema imetokana na makubaliano waliyowekeana na Mcameroon huyo wakati wakiingia naye mkataba.
Father alisema kuwa, wakati wanaingia mkataba na Omog walikubaliana kuivusha mahali ilipo Azam ikiwamo kufanya vema kwenye michuano ya kimataifa, lakini kwa miaka miwili kocha huyo ameshindwa.
"Kwa hali hiyo tumeamua kuachana kwa wema na yeye mwenyewe analifahamu hilo, na hajatoka pekee yake bali na msaidizi namba mbili Ibrahim Shikanda na baadhi ya watendaji wa benchi la ufundi,"alisema.
Aliongeza kuwa kwa sasa timu itakuwa chini ya Kocha msaidizi  kutoka Uganda, George Nsimbe ambaye atakaimua nafasi hiyo mpaka watakapopata kocha mkuu katika mchakato utakaoendeshwa na klabu yao.

GUINEA YAZIGOMEA CAF, FIFA AFCON 2023

https://athlet.org/jdd/public/documents/athlet/football/competitions/200x300/can2023.png

http://www.ghanasoccernet.com/wp-content/uploads/2015/03/AFCONtrophy.jpeg 
WENYEJI wa Fainali za Afrika za 2023, Guinea imeweka bayana kwamba hatakubali kuhamisha michuano hiyo toka mwanzoni mwa mwaka na kufanyika katikati ya mwaka  kama FUIFA inavyotaka.
Wenyeji hao wamesema kuwahawakubaliani na fainali za Mataifa ya Afrika za mwaka 2023 kuchezwa mwezi Juni ili kuziwezesha fainali za Kombe la Dunia kufanyika Qatar, alisema waziri wao wa michezo.
Domani Dore alipingana na taarifa ya Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) Jerome Valcke, ambaye wiki iliyopita alisema kuwa, fainali za Mataifa ya Afrika 2023 zinatakuwa kusogezwa mbele kwa miezi sita hadi Juni kutoka katika muda wake wa kawaida wa mwezi Januari.
Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2022 zimepangwa kufanyika Novemba na Desemba, kufuatia mapendekezo ya kamati ya maandalizi.
Valcke alisema kuandaa fainali za Kombe la Dunia mwezi mmoja baadae ni jambo lisilowezekana, na aliongeza kuwa anakubaliana na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) kuhamisha fainali hizo zinazoshirikisha jumla ya timu 16 baadae mwaka huo.
Hatahivyo, Guinea, imesema kuwa itapinga tarehe hizo mpya.
"hatuwezi kuandaa fainali za Mataifa ya Afrika mwezi Juni, ni kipindi cha mvua, “’alisema Dore alipozungunza na televisheni ya Guinea.
"Caf walitakiwa kusikiliza ushauri wa Guinea kuwa kama sisi ni taifa tunatakiwa kuamua tarehe gani zifanyike. Tunaelewa matatizo yanayolizunguka Kombe la dunia na kugongana na fainali za Mataifa ya Afrika.
"Lakini Caf walitakiwa kusikilisha maoni yetu. Mwezi juni , haiwezekani, " aliongeza Dore.
Shirikisho hilo la Soka la Afrika limesisitiza kuhusu fainali Mataifa ya Afrika 2023 nchini Guinea, likisema kuwa "Uamuzi kuhusu Afcon 2023 utatolewa na Kamati ya Utendaji ya CAF, na sio mtu mwingine, wakati utakapofika."

MALI YAWEKA REKODI AFRIKA YATWAA UBINGWA U17

http://www.foot224.net/wp-content/uploads/2015/03/mali.jpghttp://www.fiba.com/images.fiba.com/Graphic/e7176210/86bb/4e9b/af1c/5e20b580e6d4.jpg?v=20140930135344693MALI imetawazwa kuwa mabingwa wa Afrika kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 17 baada ya kuifunga Afrika Kusini kwa bao 2-0 katika fainali iliyofanyika jijini hapa.
Mabao ya kipindi cha pili yaliyowekwa kimiania na Siaka Bagayoko na Aly Malle yaliiwezesha Mali kutwaa taji hilo.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Mali timu yake ya vijana inayojulikana kama Eaglets kushinda taji la mashindano ya vijana.
Awali, nchi hiyo ilikaribia kushinda taji mwaka 1997, wakati ilipomaliza ya pili nyuma ya washindi Botswana.
Timu zote Mali na Afrika Kusini zilienda katika fainali hiyo ya Jumapili zikiwa tayari zimewahi kukutana katika hatua ya makundi ya mashindano hayo, wakati Afrika Kusini ikiwa nyuma kwa bao 2-0 na kulazimisha sare ya 2-2.
Hatahivyo, Mali haikuruhusu hilo utokea tena, na kuhakikisha inaweka ulinzi mkali baada ya kupata bao la kuongoza na kuhakikisha inaibuka na ushindi.
Bao lao la kwanza lilipatikana baada ya dakika 67 wakati Bagayoko alipofunga kwa kichwa mpira wa kona.
The Eaglets waliongeza bao la pili zikiwa zimebaki dakika 12 kufuatia juhudi binafsi ya Aly Malle. 
Bao hilo alilifunga kutoka umbali wa kama mita 20 kutoka nje ya boksi na kuibua furaha kwa mashabiki wao.
Afrika Kusini walifikiri wangeweza kupata bao la kufutia machozi wakati Khanyisa Eric Mayo alipokaribia kufunga, lakini alijikuta akiwa ameotea.

Jose Mourinho ataka mataji zaidi Stanford Bridge


Mourinhio akilia kwa furaha
Mourinho akikia kwa furaha baada ya kuiwezesha Chelsea kutwaa taji la kwanza msimu huu la Capital One
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedhamiria kutafuta mataji zaidi baada ya kunyakuwa taji la Kombe la Ligi  (Capital One) jana ikiwa ni la kwanza kwa kocha huyo toka achukue mikoba ya kuinoa timu hiyo kwa mara ya pili.
Mabao yaliyofungwa na John Terry na lingine la kujifunga la Kyle Walker yalitosha kuipa ushindi wa mabao 2-0 Chelsea dhidi ya Tottenham Hotspurs katika mchezo wa fainali uliofanyika katika Uwanja wa Wembley. Taji hilo linakuwa la 21 kwa Mourinho toka aanze kufundisha soka.
Akihojiwa Mourinho amesema anajiona kama mtoto aliyeshinda kwa mara ya kwanza kwani mara zote imekuwa ngumu kwake kuishi bila mataji.
Mourinho ambaye kwa mara ya kwanza amewahi kuinoa Chelsea mwaka 2004 hadi 2007 kabla ya kurejea tena mwaka 2013, hilo linakuwa taji lake la saba akiwa timu hiyo na pia kuisaidia Chelsea kulipa kisasi kwa Spurs ambao waliwatungua mabao 2-1 katika fainali za michuano hiyo zilifanyika mwaka 2008.
Kwa furaha kocha huyo alijikuta akimwaga chozi kabla ya baadaye kujumuika na wachezaji wake kushangilia mafanikio hayo yaliyokuja wakati Chelsea ikiongoza msimamo wa Ligi Kuu ya England na pia ikiwa kwenye hatuia nzuri ya kufuzu Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

TAIFA STARS KUPASHA MISULI MOTO COSAFA CUP

TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imethibitisha kushiriki michuano ya kombe la COSAFA nchini Afrika Kusini kufuatia mwaliko wa Baraza la vyama vya soka Kusini mwa Afrika (COSAFA).

Michuano ya kombe la COSAFA inatrajiwa kuanza kutimua vumbi katikati ya mwezi Mei mwaka huu nchini Afrika Kusini, na ratiba ya hatua ya awali ya makundi inatarajiwa kutangazwa leo jioni saa 1:00 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki moja kwa moja na kituo cha runinga cha Supersport 4.

Taifa Stars itakuwa juu (seeded) katika hatua ya makundi, ambapo nchi nane zitagawanya katika makundi mawili na washindi wa kila kundi wataingia hatua ya robo fainali, nchi  nyingine zitakazoanzia kwenye makundi ni Lesotho, Madagascar, Marutius, Namibia, Seychelles, Swaziland.
 
Katika kila kundi, timu zote zitacheza michezo mitatu na mshindi wa kila kundi ataingia katika hatua inayofuata ya robo fainali itakayozijumuisha nchi za  Afrika Kusini, Botswana, Ghana, Malawi, Msumbuji na Zambia ambazo zimeingia katika hatua ya pili kutokana na nafasi zao kwenye msimamo wa viwango vya FIFA.

Kombe la COSAFA lilianza mwaka 1997 linajumuishaa nchi 16 wanchama kutoka Kusini mwa Bara la Afrika, limekua likifanyika kwa kushirikisha nchi wanachama waliopo Kusini mwa bara la Afrika.
Nchi wanachama wa COSAFA ni Afrika Kusini, Angola, Botswana, Comoros, Lesotho, Madagascar, Malawi, Maurtius, Mayotte, Msumbuji, Namibia, Reunion, Sychelles, Swaziland, Zambia na Zimbabwe
.

BASATA LAMLILIA CAPT JOHN KOMBA

Mwili wa Kapteni Komba ukiwasilia Karimjee mapema leo kwa ajili ya kuagwa kabla ya kusafirishwa kwenda kuzikwa kijijini kwao Lutuhi, Nyasa, wilayani Mbinga.
Kapteni John Komba enzi za uhai wake katika picha tofauti akiwajibika katika sanaa yake ya uimbaji wa kwaya
Na Rahim Junior
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limetuma salamu za rambirambi kumlilia Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba aliyefarikia wikiendi iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa yake BASATA imekielezea kifo cha Komba kama pigo kubwa katika tasnia ya sanaa.
Taarifa ya BASATA inasomeka hivi;
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa kifo cha Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Captain John Damian Komba kilichotokea jioni ya Jumamosi ya tarehe 28/02/2015.
Captain John Damian Komba ni msanii na mdau wa muda mrefu wa sekta ya Sanaa nchini. Amekuwa ni taa na nuru ambayo katika kipindi chote cha uhai wake imeangaza na kutoa mwanga angavu kwenye sekta ya Sanaa.
Mchango wake katika muziki wa dansi, kwaya na ule wa kiweledi katika kuandaa na kukuza wasanii mbalimbali nchini hautasahaulika kamwe. Ni mdau aliyeacha alama kuu katika muziki wa bendi, kwaya na taarabu na amejitolea kwa kiasi kikubwa katika kuufikisha muziki wa dansi na kwaya mahali ulipo leo.
Aidha, pamoja na kujiunga na siasa na hatimaye kuwa Mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi, Mheshimiwa Komba hakukoma kuendelea kuipigania sekta ya Sanaa kwani alikuwa ni mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii ambayo kwa mujibu wa kanuni za Bunge ndiyo inayoisimamia na kuishauri Serikali katika masuala yote yahusuyo sekta ya Sanaa na Utamaduni.
Baraza, wasanii na wadau wote wa Sanaa hatuna budi kuendelea kuenzi mema yote aliyotuachia marehemu John Komba hasa katika kutunga nyimbo za hamasa na ujumbe makini na wenye mashiko kwa jamii yote ya Watanzania.
Hakika pengo lililoachwa na Marehemu haliwezi kuzibika, kwani imekuwa ni kama mshumaa uliyozimika ghafla wakati tukiingia kwenye giza.
Baraza linatoa pole kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Anne Makinda, wabunge na wadau wote wa Sanaa hususan wasanii kwa msiba huu. Ni matumaini ya Baraza kwamba, tutaendelea kuenzi mema yote yaliyotendwa na Marehemu, hasa kudumisha upendo na amani katika tasnia yetu ya Sanaa na taifa kwa ujumla.
Bwana ametoa na  Bwana ametwaa, Amen
Godfrey Mngereza
KATIBU MTENDAJI

HII NDIYO NGOMA MPYA YA ALI KIBA-CHEKECHA CHEKETUA

http://api.ning.com/files/3A8rUyA9jKO74o0hv92PLkY4cX5Pc5NkU5Zpw0YYfLFhqQS2Bf6-S-SDS87ET40281CaSxj2VQO9q9KxkyAfyCDor8nBaOVv/IMG_0128.jpg
Baada ya Mwana, Ali Kiba amekuja kivingine na Chekecha Cheketua ebu isikilize hapo chini;

KICHUPA KIPYA CHA ZOLA D FT LATINHO.- I DON'T CARE.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg7q5SJ6OOxchU55rwY3vDndEaHcOnbUOFr39NqBXqkID26wQDFrz9-ALJq1nF84wlrE7ikUfF8CBUSSztJ9iU-jbHvzB2MaIa1ewh5SeXh2jnVFik3CQJSYaNPJEz7e2kT2MH0n6wenu8/s1600/Zola+D2.JPG
Zola D King aliyeachia video ya wimbo wake wa I Don't Care

Sunday, March 1, 2015

CHELSEA, SPURS KATIKA FAINALI YA KISASI

KLABU za Chelsea na Tottenham Hotspur zinatarajiwa kuvaana leo katika pambano la kisasi la fainali za Kombe la Ligi (Capital One).
Pambano hilo litakalochezwa kwenye uwanja wa Wembley linarejesha mchezo wa fainali za mwaka 2008 ilizozikutanisha timu hizo kwenye uwanja huo na Spurs kuitambia Chelsea kwa mabao 2-1.
Katika pambano hilo lililochezwa Februari 24, 2008, Spurs ilinyakua taji hilo katika muda wa nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika kwa timu hizo kufungana bao 1-1 Chelsea wakitangulia kabla ya Spurs kurejesha.
Kadhalika pambano hilo la Fainali hizo za Kombe la Ligi limekuja ikiwa ni wiki kadhaa tangu Spurs walipoitoa nishai Chelsea kwa kuichapa mabao 5-3 katika pambano la marudiano ya Ligi Kuu ya England.
Awali Spurs ilicharazwa mabao 3-0 nyumbani kwa Chelsea mwaka uliopita na waliporudiana White Hart Lane waliwashughulikia Chelsea jambo linalofanya mechi ya leo kujaa visasi vitupu.
Chelsea chini ya Jose Mourinho itawakosa baadhi ya nyota wake akiwamo Nimanja Matic aliyefungiwa mechi mbili baada ya kupungiwa adhabu na FA kwa kadi nyekundu aliyoipata wiki iliyopita.
Hata hivyo timu hiyo inapewa nafasi kubwa ya kuwatambia wapinzani wao ambao wanauguza machungu ya kung'olewa kwenye michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europa League) na Fiorentina ya Italia.
Ikiwa na wakali kama Ces Fabrigas, Diego Costa, Eden Hazard, Willian na wengine, Chelsea itapenda kutwaa taji hilo ili kuweka hazina kwa msimu huu baada ya awali kutolewa katika Kombe la FA.
Vinara hao wa Ligi Kuu wanapaswa kuwa makini na kinda linalotisha Harry Kane ambaye amekuwa wakiwaliza makipa hodari kama alivyoonya kipa wa Chelsea, Thibaut Courtois.
Rekodi zinaonyesha kuwa timu hizo zimeshakutana mara 134, Chelsea ikishinda mara 57 na wapinzani wao mara 44 na mechi 33 zikiisha kwa sare na pambano la leo litakuwa la 135 kwao katika michuano yote.
Je, ni Chelsea au Spurs atakayecheka leo katika uwanja wa Wembley? Bila shaka ni suala la kusubiri kuona ila kwa hakika ni bonge la mechi.