STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

Real Madrid na Ronaldo wao wazamishwa 4-0

Saul Niguez doubles Atletico's lead with a superb overhead kick just four minuted after the first goal 
Saul Niguez akifunga bao la pili la Atletico kwa tiktak
Mario Mandzukic akifunga bao la nne la Atletico Madrid
Cristiano Ronaldo looks dejected after Real Madrid concede two goals inside the opening 20 minutes of the game 
Kachokaaa! Ronaldo akiwa hoi timu yake ikitunguliwa ugenini
Former Bayern Munich midfielder Toni Kroos controls the ball while his old team-mate Mario Mandzukic closes him down 
Licha ya juhudi Real Madrid haikufua dafu kwa wapinzani wao wa jadi
MABINGWA wa Ulaya, Real Madrid licha ya kuwa na nahodha wake Cristiano Ronaldo wamepokea kipigo cha aibu cha mabao 4-0 toka kwa wapinzani wao wa jadi, Atletico Madrid katika pambano la La Liga lililochezwa kwenye uwanja wa Vincente Calderon.
Atletico ambao ndiyo watetezi la La Liga walianza kuwaadabisha wapinzani wao kwa kuandika bao la kwanza katika dakika ya 14 kupitia kwa Tiago kabla ya Saul Niguez kuongeza la pili dakika nne baadaye.
Mabao mengine yaliyendeleza ubabe wa Atletico Madrid dhidi ya wapinzani wao yalifungwa na Antoine Griezmann kwa shuti kali dakika ya 67kabla ya Mario Mandzukic kumalizia udhia kwa kufunga kwa kichwa dakika ya 89.Ligi hiyo itaendelea tena kwa michezo mingine mitatu ambapo hivi punde Villarreal ikiwa nyumbani imepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Granada.


No comments:

Post a Comment