STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 7, 2015

Everton, Liverpool hakuna mbabe, zashindwa kutambiana

Utemi na kutunishiana kifua ulikuwapo katika pambano hilo
Raheem Sterling akichuana na Aaron Lennon
Nahodha Steven Gerrard akijaribu kufunga mbele ya lango la Everton bila mafanikio
WAPINZANI wa jadi wa Merseyside, Everton na Liverpool zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu katika pambano kali lililomalizika hivi punde.
Licha ya kushambuliana kwa zamu na kuwepo kwa kosa kosa za hapa na pale katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Everton wa Goodison timu hizo zilimaliza dakika 90 zikiwa 0-0 na kugawana pointi moja moja.
Katika pambano hilo Liverpool ilipata pigo mapema baada ya kiungo wak Lucas Leiva kuumia katika dakika ya 15 na nafasi yake kuchukuliwa na Joe Allen, huku Aaron Lennon akishuhudiwa akishuka dimbani kwa mara ya kwanza akiwa na jezi za Everton akitokea Spurs.

No comments:

Post a Comment